Member of EVRS

Thursday 27 December 2012

New Year Greetings, of Course from ME!

As we are about to finish the year 2012
  
It is not a bad idea to send the warmest greetings to all
It is good to wish you having the successful coming year of 2013 in all aspect of your life and carrier plans
It is not good to keep quiet without saying sorry for what I made you fail
It is very bad if I keep quiet while I see you are falling apart while I can help.
  
Have a wonderful new year 2013
Just remember, your smile doesn't cost you a thing, but it means a lot to other people to whom they love and trust you so much. Sooo, just shower it this time.....
  
Blessings

Friday 7 December 2012

Timu za Taifa za Tanzania Zimefungwa Nusu Fainali ya Cecafa Tusker Challenge cup 2012

Timu za Tanzania, Zanzibar Heroes na Kilimanjaro stars hazikufanikiwa kuingia fainali ya Cecafa Tusker Challenge cup mwaka huu wa 2012 baada ya kushindwa kwenye michezo yao ya nusu fainali. 
   
Timu ya Zanzibar imetolewa kwa maamuzi ya penati,, baada ya kumaliza kwa sare ya magoli 2 - 2 na timu ya Harambee stars ya Kenya. Zanzibar Heroes walikosa penati mbili za mwanzo.
 Mwisho ushindi ulisomeka kama hivi: Kenya 6 - 4 Zanzibar 
  
Nayo timu ya Tanzania Bara ilifungwa kwa jumla ya magoli 3 - 0 na timu ya Uganda, (the cranes) baada ya kuzidiwa maarifa ya mchezo.  
Timu ya Tanzania ilionekana kushindwa kwenda mbele, na badala yake mipira mingi walikuwa wanarudisha nyuma kuelekea golini kwao badala ya kushambulia mbele.  
  
Magoli ya pili na tatu yaliyofungwa na Uganda, yalitokana na uzembe wa walinzi wa Kilimanjaro stars kutokukaba kwa wakati wakidhani wachezaji wa Timu ya Uganda walikuwa wameotea.  
  
Kwa mantiki hii, Zanzibar na Tanzania bara zitakutana katika mchezo wao wa mwisho kutafuta mshindi wa tatu siku ya jumamosi tarehe 8 Disemba 2012.   Baadaye kwenye uwanja huo huo, Uganda itacheza na Kenya katika Fainali ya kutafuta bingwa wa mwaka 2012/13.

Sunday 18 November 2012

Kujivua Gamba na Kuliacha Likining'inia

Siasaaaa

Siasa kwa kweli ni mchezo wa kujaribu kuvutia na kufanikiwa kuteka fikra za wafuasi na watu wengine.
Pia siasa unaweza kuitafsiri kama ni dhana au mawazo aliyonayo mtu, na kujaribu kuwa aminisha watu wengine, ya kuwa hayo mawazo ya mwanasiasa huyo ni sahihi, na kama yakifutwa kwa makini, basi yatawasogeza watu kutoka sehemu moja kwenda nyingine yenye maendeleo zaidi. 
   
Wakati mwingine, mwanasiasa mwenyewe hana uhakika kama yupo sahihi, lakini anajaribu kuwavutia watu tu ili afanikishe malengo yake.  
  
Miezi kadhaa imepita tangu watu fulani waliposema walikuwa ni kama mfano wa wanyama wanaotambaa na wenye damu baridi, wakaueleza uma ya kuwa wamebadili safu yao na kuanza vita na mafisadi kwa mfumo wa kujivua makoti ya zamani na kubakia na makoti mapya. 
  
Lakini .... naona sina kumbukumbu kama walivua makoti au walinyofoa mifuniko ya makoti yao tu. 
  
Sasa tunasikia tena wamebadili safu na wamekuja na usemi ule ule wa vita tena ile ile..... 
  
Kwa hiyo tusubiri tena mwaka 2014 wakibadili safu za serikali za vijiji, tena tutasikia nini tena!! aaah  
  
Kwangu, nafikiri hakuna sababu ya kuendeea kuwapa nafasi watu wenye ahadi tuuuu au vipi!  
 
Ninachukia siasa za ahadi hewa!  Tubadilike alaaa!!

Thursday 8 November 2012

Romney: Your Time just Collapsed in the last minute

Mitt Romney .... May be your time is not yet



Obama has won re election by scooping minority, women and youths votes.
From African-American he scooped 93%, 71% of Latinos, and Asian origin individuals.
Apart from this, his party obtained 2 extra senate seats, these are Massachusets and Indiana.

Overall he got 303 electoral votes while Romney obtained 206 electoral votes.

Good luck Americans!

Monday 29 October 2012

Kumbe ........



Hata nami, bado nipo nipo tu

Sunday 30 September 2012

Adha na Raha ya Kazi ya Huduma kwa Jamii

Kazi zinahusiana na kutoa huduma kwa jamii zina raha zake na karaha zake.
Kazi hizi ni kama vile za siasa, sekta ya afya, polisi, huduma za hoteli na migahawa, benki na kadhalika.

Wakati wote unahitaji kuwa mchangamfu na unayejali.

Hata pale anapokuja mtumishi wako wa nyumbani, ule ukali wako wooote, unayeyuka anapokuja ofisini kwako kwa ajili ya kupata huduma.

Lakini sina hakika kama watu wote wanakuwa hivi....
Nilikuwa nawatakia wikend njema tu!

Wednesday 12 September 2012

Mfanyakazi Takukuru - Ngara Ajiua kwa Kujipiga Risasi

Mfanyakazi mmoja wa TAKUKURU wilaya ya Ngara, siku chache zilizopita alijiftyatulia risasi na kufa papo hapo kwa sababu ambazo bado hazijafahamika. 
  
Mfanyakazi huyo kazi yake kubwa ilkuwa ni ya masuala ya usalama na utunzaji wa zana za moto (silaha), ambaye pia ni mwenyeji wa mkoa mmojawapo wa nyanda za juu kusini magharibi mwa Tanzania, ambapo mkoa huo hapo awali ulikuwa na sifa ya wenyeji wake kujiua pale wanapoudhiwa kupita kiasi.    
  
Chanzo cha mtu huyo kufikia uamuzi mgumu kama huo hakijajulikana wazi, japo inasemekana alitakiwa kutoka kwenye kikao ambacho kinahisiwa kilitakiwa kukaa na kumjadili yeye. 
  
Alipotoka nje ya kikao, muda mfupi baadaye ulisikika mlio wa risasi, jambo ambalo lilizua taharuki kutoka kwa wajumbe waliokuwa kwenye kikao cha kazi na kuwafanya wakimbie hovyo huku wakisigana kupita kwa kasi ya ajabu kwenye mlango wa kuingilia kwenye chumba hicho cha mkutano.  
  
Habari zaidi zinadai ya kuwa funguo za chumba cha silaha alikuwa amekwisha kuzikabidhi kwa mamlaka husika kazini kwake, na kuna hisia labda alikuwa amekwisha itoa silaha iiyomuua, au alikuwa janja na kutoa nakala ya ufunguo  wa chumba cha kuhifadhia silaha za moto. 
 

Saturday 8 September 2012

Dedicated to You!

Masseter Muscles!

Friday 31 August 2012

UEFA Champions League 2012 /13 Groups


Group A

FC Porto (Portugal)
Dynamo Kiev (Ukraine)
Paris Saint-Germain (France)
Dinamo Zagreb (Croatia)  
 
Group B
Arsenal (England)
Schalke 04 (Germany)
Olympiacos (Greece)
Montpellier (France) 
  
Group C
AC Milan (Italy)
Zenit Saint Petersburg (Russia)
Anderlecht (Belgium)
Malaga (Spain)  
  
Group D
Real Madrid (Spain)
Manchester City (England)
Ajax Amsterdam (Netherlands)
Borussia Dortmund (Germany)  
  
Group E
Chelsea (England)
Shakhtar Donetsk (Ukraine)
Juventus (Italy)
Nordsjaelland (Denmark) 
  
Group F
Bayern Munich (Germany)
Valencia (Spain)
Lille (France)
BATE Borisov (Belarus) 
  
Group G
Barcelona (Spain)
Benfica (Portugal)
Spartak Moscow (Russia)
Celtic (Scotland)  
  
Group H
Manchester United (England)
SC Braga (Portugal)
Galatasaray (Turkey)
CFR-Cluj (Romania)



Group E

Thursday 30 August 2012

Rwanda: Makahaba wauawa na Watu Wasiojulikana

Kumezuka wimbi la mauaji ya wasichana Nchini Rwanda. Mpaka sasa wanaohusika na mauaji hayo hawajajulikana.  
Mauaji hayo yanawalenga wasichana makahaba. Kwa mwezi huu wa Agosti pekee, wasichana 15 wamekwishauawa kwa njia mbali mbali ikiwa ni pamoja na kukatwa katwa kwa vitu vya ncha kali au kunyongwa.  
Jana mchana kuna habari ya kuwa wasichana watatu waliuawa kwa kunyongwa kwenye nyumba moja ambayo ipo sehemu ya makazi ya watu wengi. Mauaji hayo yanahisiwa kufanywa nyakati za mchana.  
Hata majirani walistaajabu kupata habari za vifo hivyo, bila wao kusikia au kuhisi chochote.
Kwa sasa, katika nchi ya Rwanda, masuala ya kuendesha shughuli za ukahaba ni kosa la jinai.  
  
Hakuna shaka mauaji haya hayahusiani na vyombo vya dola, bali kuna uwezekano yanaendeshwa na watu wanaochukia shughuli za ukahaba. 

Tuesday 28 August 2012

Bila Onyo... Mambo hayaendi!


Wakati niliokuwa natembea mitaa ya katikati ya jijini Kampala, Uganda kwenye siku za mwisho wa wiki nilikutana na bango hili. 
Nafikiri nia ni nzuri kuwatishia nyau madereva wasiojali sehemu wanapoegesha magari yao.
  
Lakini naona hilo tozo la adhabu ni dogo, kwani ni sawa na dola 2 tu za kimarekani!  
 
Kilichonkiuna zaidi.... miaka 4 iliyopita, nilipita eneo hili, lilikuwa na uzio kama huu, sasa sijui huko ndani wanajenga nini ambacho kwa miaka 4 hakijaweza kuonekana! 
  
Naendelea kuchanja mbuga!

Saturday 25 August 2012

Rais Kagame Aahidi Kuendelea Kudhamini Kombe la Kagame, Yanga nayo Yapata ushindi Kigali

Rais Paul Kagame akipokea Kombe la Kagame kutoka kwa nahodha Haroub (Kushoto) na Kocha mkuu Saintfiet (Kulia) wa Yanga ambao walifanikiwa kushinda michuano ya Kagame ya Afrika mashariki na kati kwa mwaka 2012
Siku ya Juzi, Rais Kagame wa Rwanda alilipokea kombe ambalo limepewa jina lake kutoka kwa nahodha na kocha wa timu ya mpira wa miguu ya Yanga ya Tanzania.
Mbali ya kulipoke kombe hilo, aliahidi na kupendelea udhamini wake wa kombe hili uendelee hata pale atakapo staafu na mambo ya siasa. 
   
Rais Kagame amekuwa akitoa jumla ya dola za Kimarekani 75,000 kila mwaka kwa Shirikisho la soka la Afrika Mashariki na Kati (CECAFA). Kati ya hizo, dola 60,000 zinaenda kwa washindi wa kwanza hadi wa tatu, na dola 15,000 kuendesha shughuli za michezo hiyo. 

  
Mazoezi ya timu ya Yanga, Kigali

Timu ya Yanga ilienda Kigali, Rwanda kwa mwaliko wa rais Kagame mwenyewe, na imepangiwa kucheza michezo mitatu ya kirafiki, wa kwanza ulikuwa siku ya ijumaa tarehe 24 Agosti 2012 dhidi ya Mabingwa wa soka nchini Rwanda, Rayon sports, ambao wenyeji, yaani Rayon sports, wamefungwa magoli 2 - 0. 
   
Mbali na mwaliko huu walioupata Yanga kutoka kwa Rais wa Rwanda, pia wamepata mwaliko mwingine kutoka kwa Rais wa Tanzania.  
   
Picha na sehemu kubwa ya habari kwa kimombo nimeitoa hapa, na picha na maelezo kiasi ya Rwanda yanapatikana hapa japo yapo kwa lugha ya kinyarwanda!

Sunday 19 August 2012

IDDI NJEMA KWA WOTE!

Blogu ya Hadubini inapenda kuwatakia heri na baraka zote kwa Waislamu popote Duniani katika kusheherekea sikukuu hii ya Iddi. 
  
Wadau wa blogu hii wanaamini katika mfungo wote wa Ramadhan waislamu wote wamekuwa wanaombea amani na utulivu duniani pote. 
 
Tunamuomba Mwenyezi Mungu aziskilize sala zote zilizoombwa wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani na kuzipa baraka zake. 
  
Eid Mubarak!

Rada ya Utata Uwanja wa Ndege Dar es Salaam Imeharibika

Uwanja wa kimataifa wa ndege uliopo jijini Dar es Salaam kwa muda sasa umeshindwa kutoa mawasialiano ya kuongozea ndege kwa kutoa taarifa muhimu za mabadiliko ya hali ya hewa.
Habari hii niliishtukia wakati nilipokuwa naangalia matarajio ya mabadiliko ya hali ya hewa kwa muda wa wiki nzima tunayoianza kupitia mtandao huu, Mtandao huu ulionyesha ya kuwa rada iliyopa kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Dar es Salaam haitoi taarifa yoyote. 
  
Rada hii hutoa vielelezo vyote muhimu vinavyohusiana na hali ya hewa ikiwa ni pamoja na kiasi cha joto, hali ya unyevu, kasi na mwelekeo wa upepo, hali ya mawingu, mvua na radi. Na pia kama kutatokea mabadiliko ya ghafla, basi rada hii hutoa taarifa ili marubani wa ndege waweze kujiandaa au kutoa maamuzi ya mahali pa kutua iwapo hali ya hewa ni mbaya sana. Mbali ya yote hayo, pia rada hii hutoa taarifa ya vyombo vya anga mahali vilipo na upande vinapoelekea ili kuweza kuziongoza ndege na kufika salama sehemu zinapotarajia kutua.

Katika pitapita yangu nikakuta taarifa hii ambayo ikanihakikishia ya kuwa ni kweli rada hiyo imeharibika tangu tarehe 3 August 2012, taarifa hii ilithibitishwa na mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya hali ya hewa, ambaye alidai kuna kifaa kimeharibika ambacho kimesababisha rada hiyo kushindwa kufanya kazi. Kifaa kilichoharibika kitaweza kupatikana sehemu moja tu, kwa wale walioiuzia Tanzania rada hiyo kwa bei ya kuruka, yaani kampuni ya Uingereza (BAE Systems), ambayo ililazimika kurudisha chenji iliyojipatia kiwizi. Lakini kwa sasa, ile chenji ambayo kampuni hii ilirudisha Tanzania, itabidi itumike kwa kurudi tena kwao hao hao waliokuwa wameiibia serikali ya Tanzania ili waweze kutengeneza na kuleta kifaa kilichoharibika! 
  
Kwa sasa marubani wanategemea mawasiliano ya kizamani na kutumia akili yao binafsi hasa kwenye kutua na kuruka, kwani kasi ya upepo na ndege zilizo karibu haziwezi kuonwa na rada hii. 
  
Uwanja wa kimataifa wa ndege wa Dar es Salaam, ni mmoja wa viwanja ambavyo vina ndege nyingi zinazotua na kuruka katika ukanda huu wa Afrika mashariki, kwa hiyo kukaa bila rada kunahatarisha hali ya usalama kwa vyombo vinavyoruka katika anga la Tanzania. Wasiwasi huu umeonyeswa na matangazo ya BBC kupitia idhaa yake ya kiingereza usiku wa jumamosi 18 Agosti 2012.

Sunday 12 August 2012

Dk. Steven Ulimboka Arejea Tanzania

Leo mchana, Dr Steven Ulimboka amerejea nchini akiwa buheri wa afya na nguvu kamili. 
 
Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ghafla ulifurika watu ambao wengi wao hawakutegemea kurudi kwa Dk Ulimboka.
Katika makundi yaliyoenda kumpokea ni pamoja na jopo la madaktari wenzake na wana harakati wa haki za binadamu.

Kwa maneno machache kabisa, Dk Ulimboka amesema ya kuwa ni yeye kwa sasa ni mzima kabisa, na yupo tayari kuwajibika kwa shughuli yoyote ndani ya uwezo wake.  
   
Nao madaktari wenzake, mbali ya kufurahia ujio wake akiwa mzima, wameendelea kusisitiza ya kuwa ni muhimu kwa serikali kuweka vifaa na madawa ya kutosha kuwahudumia wananchi hapa nchini, kwani sio wananchi wote wanaweza kupelekwa nje kwa matibabu ambayo hayapatikani nchini.
 
Neno langu....... sitegemei tena kuwepo na jaribio lingine la kumteka na kumjeruhi mtu huyu. Ni muhimu sana waliolitenda tukio hili wapewe stahiki yao ili kuondoa wingu la uoga na kutokuaminiana. Nina imani jamii ya madaktari na ile ya wanatuhumiwa waliotenda tukio hili wanahitaji kufanya kazi kwa ushirikiano zaidi kuliko hali ya kutokuaminiana iliyopo sasa.

Kila la heri Dk Steven Ulimboka

Uganda wins First 2012 Olympic Medal via Men's Marathon

I do not understand why people they say Ugandan Stephen Kiprotich gold medal win for 2012 London Marathon came unexpectedly! 
  
I am sure this man was determined and he met the qualification standard for participating in the event. Therefore he had an equal chance to clinch the medal like the usual common teams from Kenya and Ethiopia.

Anyway, he fought to the end to clinch the first olympic medal for his country clocking 02:08:11, he was followed by Kenyans Abel Kirui 2:08:27 and Wilson Kipsang 02:09:37 in second and third position respectively. It appears the name beginning with "K" had a lucky chance to clinch a medal!!

Other East African countries marathon athletes could not beat the clock on time as Tanzanian Faustine Mussa finished on 33rd position and Samson Athumani went to the finishing line at 66th position.

The Rwandan fellow Mvuyekure was exhausted, at times he had to walk rather than running, he finished 79th.
The last person to finish olympic for this year was Tsepo Ramonene of Lesotho clocking at 02:55:54 on 85th position.

For full list of men Marathon results click here

Distinguished Medals for "Olympic Veterans"


Just thinking aloud ....... International Olympic Committee should think about giving distinguished medals to countries which are "veteran participants" (Participating for a longer time without winning any medal!)
Probably this will be the stimulant for those countries to wake up....
 

Friday 10 August 2012

Mpaka wa Tanzania na Malawi: Hali ya Wasiwasi Yatanda Malawi

Mara baada ya waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Tanzania, Bernard Membe kutangaza katizo la makampuni yanayofanya utafiti wa mafuta na gesi katika ziwa Nyasa upande wa Tanzania kupitia nchi ya Malawi kuacha kazi hiyo mara moja. Kwa mujibu wa kituo cha runinga cha Taifa cha Msumbiji, kimesema wananchi wa Malawi wanaoishi karibu na Tanzania ikiwa ni pamoja na mji mkuu wa Malawi wa Lilongwe, wameingiwa na hofu ya kutokea vita baina ya nchi yao na Tanzania. 
  
Kwa mujibu wa Kituo cha matangazo ya runinga ya Msumbiji, kauli za Membe na mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya masuala ya usalama na mambo ya nje, Edward Lowasa, zimesababisha baadhi ya wakazi wa maeneo hayo kujiandaa kuhama maeneo yao iwapo mapigano yataanza.  
   
Waziri wa mambo ya nje wa Malawi, Ephraim Chiume, aliwatoa wasiwasi wananchi wa Malawi kwa kusema mazungumzo ya kidiplomasia na Tanzania yamekwisha anza, japo alisisitiza ya kuwa upande wa mashariki wa ziwa nyasa linalopakana na Tanzania ni mali ya Malawi kwa mujibu wa makubaliano ya wakoloni wa kiingereza na Wajerumani unaoitwa Heligoland wa mwaka 1890 ambao Malawi wanadai unatambuliwa na Umoja wa Afrika. 
  
Kwa upande wa Tanzania, hawautambui mkataba huu, ila wao wanafuata ule wa awali kabla ya makubaliano ya wakoloni hawa.
  

Monday 30 July 2012

Watazamaji Wabadili Matokeo ya Waamuzi Kwenye Olimpiki

Kushoto Cho akishangilia alipotangazwa mshindi na picha ya Kulia akiwa na butwaa mara matokeo yalipobatilishwa
 Katika hali isiyo ya kawaida, waamuzi na majaji wa shindano la judo kati ya Cho Jun-Ho wa Korea Kusini na Ebinuma Masashi wa Japan, ilibidi wabadili maamuzi ya kutangaza mshindi pale hapo awali walipomtangaza Cho kuwa mshindi kwa kunyanyua bendera za rangi ya bluu ambayo ndio iliyokuwa inawakilisha mwenye mavazi ya bluu.
Lakini, mashabiki walizomea uamuzi huo, ikabidi majaji na waamuzi wakae tena na kujadili kabla hawajabatilisha matokeo na kumtangaza  Masashi wa Japan kuwa mshindi
Maamuzi yalipobadilishwa

Hali hii inatia wasiwasi ya kuwa majaji hawako makini, au kwa makusudi wanawatoa baadhi ya washindani. Katika angalia yangu, kuna maamuzi waliyotoa kwenye mchezo wa masumbwi hata na mimi yalinipa mashaka.

Habari huu kutoka Euro sport

Sunday 29 July 2012

Yanga Bingwa Kombe la Kagame 2012


Timu ya Yanga ya Dar es Salaam, Tanzania imefanikiwa kutetea kombe lake la Klabu Bingwa Afrika Mashariki ambalo kwa sasa limepewa jina la Kombe la Kagame baada ya kuifunga timu ya Azam ya Dar es Salaam pia kwa jumla ya magoli 2 - 0. 
  
Magoli ya Yanga yalifungwa na Hamis Kiiza katika dakika ya 45 na Said Bahanuzi katika dakika ya 90.
  
Kwa sasa, Yanga imefanikiwa kulichukua kombe hili kwa mara ya tano. 
  
Hapo awali, Timu ya Vita Club, kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ilifanikiwa kuifunga timu ya APR ya Rwanda kwa magoli 2 - 1 na kujiwezesha kushika nafasi ya tatu.  
   
Binafsi, nazipongeza timu zote za Tanzania kufanikiwa kufika katika hatua za mbele na hatimaye fainali kuzikutanisha timu za Tanzania pekee

Friday 27 July 2012

Gharama ya Kuunganishiwa Umeme Kushuka - Waziri wa Nishati na Madini

Waziri Sospeter Muhongo ambaye ana dhamana ya kuongoza wizara ya Nishati na Madini, leo akiwa anawasilisha makadirio na matumizi ya wizara ya Nishati na Madini kwa ajili ya bajeti ya mwaka 2012/13 ametangaza kusudio la serikali kupunguza gharama za kuunganisha umeme kwa maeneo ya mijini na vijijini likiwa na punguzo kati ya asilimia 25 na 70 kutegemea na mahitaji ya vijijini na mijini, huku akizungumzia zaidi kwa njia moja (Single phase). 
  
Hata hivyo, punguzo la gharama hizi litaanza kutumika kuanzia mwezi Januari mwaka 2013. 
  
Katika mambo mengine aliyozungumzia, ni pamoja na kukiri kuwa kuna baadhi ya watendaji wa Tanesco si waaminifu, na wamekuwa wakishiriki katika vitendo vya kulihujumu shirika la hilo la ugavi wa umeme. 
Waziri ameahidi kuwa kuna hatua madhubuti za kuhakikisha umeme utapatikana na polepole suala la mgawo wa umemem litakwisha. 
  
Serikali pia imewekeza katika kumiliki na kutumia njia za kusafirisha gesi asilia ambayo itatumika kuzalisha umeme, na pia kuhakikisha asilimia 0.5 ya faida ya kuzalisha gesi asilia inatumika katika kutoa umeme kwenye maeneo gesi asilia ainapozalishwa na kupitia.  
  
Cha muhimu alichoahidi, ni kuendesha wizara kwa uwazi na watu wote wanakaribishwa kutoa maoni yenye mtazamo chanya au hasi. 

Monday 23 July 2012

War in Eastern DR Congo: Kagame Blasts International Community



President of Rwanda, Paul Kagame today when addressing the Ambassadors, Internationa senior Military officers, Local senior and junior Military Officers and other invited guests to the inauguration of Rwanda Defence Forces Command and Staff College. He expressed his disatisfaction on remarks which has been made by powerful international community by condemning his Government to support Eastern Congo rebels.
He denied all accusations impounded on his Government's shoulders as baseless and infact intriguing more chaos in the region. 
  
He spent some time explaining how the current war started which was engineered by the same Internation community which he did not disclose their identities.  
  
Among the things he said, where his speech was broadcasted live by Rwanda Television, is that he was approached well in advance before the current havoc, that he should give help to the Internation Criminal Court (ICC) to facilitate arrest for some of the Congolese rebellions which were needed by Internation Criminal Court for justice trial regarding crimes against humanity (which he said this organisations-ICC, has been politicised and lost its meaning and intentions). According to him, he was shocked by this act, and he refused to interfere other autonomy state, he gave them clear answer if they want to do that in Congolese territory, let them proceed without involving Rwanda.  
  
He further said, he communicated to DR Congo president on this matter to warn him what has been cooked under the ground, which he realised his neighbour president was aware and actually wanted those rebellions to be handled to his Government rather than being sent to ICC. 
  
President Kagame was puzzled after he realised that the plan was going ahead despite that The Congolese Government had a meeting with rebellions and International community where there was an agreement of certain matters to be solved to maintain the peace. 
  
H. E. Kagame is irked to see the war is getting fiercer, and the International community have shut down their deaf ears to what they know exactly what is happening, while opening their mouth by shouting Rwanda stops ........... He added that, what is happening in Congo now, is what exactly happened during the Rwanda genocide in 1994 where same if not similar people shut down their deaf ears and eyes witnessing shed of innocent blood massively. He actually express that the ICTR which was established by UN to charge the genocide mastermind network, should also charge some members of International Community.

Friday 13 July 2012

Mbunge wa Kigamboni Atolewa Bungeni kwa Kuwatetea Wananchi Wake


Mbunge wa Kigamboni Dr Faustine Ndugulile (CCM) jana tarehe 12 Julai 2012 alitolewa nje ya ukumbi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano ya Tanzania baada ya kulazimishwa kuomba radhi na kufuta kauli ambayo aliitoa juzi kueleza wasiwasi wake wa mazingira ya baadhi ya madiwani wake kukaribishwa bungeni na waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi bila ya yeye kuwa na taarifa, na hasa ukizingatia alikuwa anajua madiwani wake walikuwa katika ziara ya mafunzo katika mkoa mwingine.

Dr Ndugulile ambaye yupo mstari wa mbele kutetea haki na stahiki za wananchi wake, amekuwa mwiba mkali kwa mawaziri ambao wamekuwa wanatumia nguvu na kuvunja sheria dhidi ya wananchi wake.
Nguvu alizonazo, zinasukumwa kwa ukubwa na matakwa ya wananchi wake ambao walimchagua kuwawakilisha katika kutatua matatizo yao mbalimbali.  
  
Mojawapo ya jambo walilomtuma kuwasemea bungeni ni pamoja na kuukataa mpango wa mji mpya wa Kigamboni kwani umegubikwa na utata mwingi na umekiuka sheria nyingi za ardhi pamoja na katiba inayotumika sasa.  
   
Wananchi hapo awali walitaka mpango huo uratibiwe upya kwa kuwashirikisha, lakini wizara husika ilikuwa inapiga chenga na kutoa taarifa ambazo hazikuwa sahihi kwenye baadhi ya vyombo vya habari na vya sheria. 
   
Inaonekana wizara na watendaji wake hawakuwa na habari ya kuwa wananchi walimwita mbunge wao katika kikao chao cha wazi na kumtuma nini akawasemee bungeni, na ndicho hicho alichokisema bungeni ambacho kinaonekana kiliwaudhi baadhi ya watendaji wa serikali na bunge na kuamua kumpa adhabu kali kwa kumkoseha siku 3 za kuhudhuria vikao halali vya bunge.  
   
Mwezi uliopita wananchi hawa hapa chini walitoa dukuduku zao na maazimio kuhusu mji wa Kigamboni

Baadhi ya wananchi wa Kigamboni walipomuita mbunge wao wamueleze dukuduku lao kuhusu mji mpya wa Kigamboni

Mwananchi akichangia mawazo kuhusu mji mpya wa Kigamboni

Mmoja wa wachangiaji aliyekuwa anawakilisha taasis ya kidini

Mwakilishi wa kamati ya wakazi wa Kigamboni akifafanua jambo kuhusu Mji Mpya unaotaka kuletwa

Viongozi wa wananchi wakisikiliza kwa makini

Mbunge akikabidhiwa ripoti ya kamati kuhusu juhudi walizozifuata na maazimio waliyoyapitisha
Katika kuonyesha kutahayari, naibu waziri wa wizara ya ardhi na maendeleo ya makazi, alionekana kwa namna fulani kuwa na kigugumizi alipokuwa akijibu baadhi ya hoja za wabunge, kwani yeye ndiye aliyekuwa mchangiaji wa kwanza baada ya Dk Ndugulile kutolewa nje ya ukumbi wa bunge.  
  
Na kudhihirisha kuwa suala hili halikumpendeza waziri, alitumia karibu theluthi moja ya muda wake wa kujibu hoja za wabunge zaidi ya 150 waliochangia kuzungumzia suala la Kigamboni na mbunge wake. Na kuonyesha ya kuwa hakupendezwa na Mbunge huyo wa Kigamboni, alikataa kumtaja Mbunge wa Kigamboni kama mmoja wa watu waliochangia katika hotuba yake aliyoitoa hapo awali. 
  
Japo waziri Tibaijuka alianza kwa kuisifia demokrasia iliyopo kwa sasa na watu kusema bila uoga, na baadaye alitamka ya kuwa amemsamehe Dr Ndugulile kwa yale aliyoyasema, lakini haikuweza kuficha kutofurahishwa na kauli ya Dr. Ndugulile na wasiwasi wake kuhusu kutekelezwa kwa mradi huo.
Sio siri, Mama Tibaijuka amekuwa mstari wa mbele kwa kutekeleza mambo kisheria, lakini kwa Kigamboni, bado hajapata ufumbuzi wa mpango huu ambao hata yeye ameukuta ukiwa tayari njiani pamoja na kasoro zake nyingi tu.  
   
Kutolewa bungeni kwa Dr Faustine kuliwashtusha wapiga kura wake, na kwa ujumla wamemuona kama shujaa wao kwa kusimama kidete kutetea maazimio yao.  
 
Kama wananchi wa nchi huru na yenye ustaarabu, hatutapenda kuona kunatokea uvunjifu wa amani kwa wana Kigamboni. Tuna imani busara na hekima itatumika kwa kufuata sheria mama za nchi.  

Wednesday 4 July 2012

Rwanda Yaadhimisha Miaka 18 Baada ya Mauaji ya Kimbari ya Mwaka 1994


Siku ya leo tarehe 4 Julai 2012, Rwanda imeadhimisha miaka 18 tangu mauaji ya Kimbari dhidi ya Watutsi yalipomalizika. 
Tarehe kama hii ya leo hapo mwaka 1994, jiji la Kigali lilikombolewa na majeshi ya RPF na hivyo kukomesha mara moja mauaji yaliyokuwa yanaendelea amabyo yalilengwa haswa kwa watutsi, japo na wale wahutu wenye msimamo wa wastani nao walikuwa wakishambuliwa na hata kuuawa. 
  
Siku kama ya leo, watu huwa wanatoa ushuhuda wa matukio yalivyokuwa na kuendelea kutoa msamaha kwa wale waliofanya mauaji na kutesa watu waliokuwa hawana hatia. 
  
Tarehe 4 Julai huwa ni kilele cha maombolezo ambayo huanza tarehe ambayo ni sambamba na wakati mauaji yalipoanza mnamo mwezi wa Februari. 

Kwa mwaka huu wa 2012, wananchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kutoka nchi za Kenya, Tanzania, Uganda na Burundi waliungana kwa pamoja kwenda kutoa heshima kwa wahanga wa mauaji hayo waliozikwa kwenye eneo la Gisozi wakisindikizwa na wanyarwanda ambao wengi wao walikuwa wakiishi Tanzania kama wakimbizi baada ya kukimbia vita na mauaji ya kikatili yaliyokuwa yakiendelea wakati huo nchini Rwanda. 

Tuesday 3 July 2012

Choo na Mgawanyo wa Matumizi

Alaa, kumbe mgawanyo wa matumizi ya choo upo wa aina nyingi!

Nilishazoea kuona mgawanyo wa jinsia ........

Monday 2 July 2012

Euro 2012 Final: Spain 4 - 0 Italy



Italiaaaaaa ...... Last minutes, I thinks their stockings were packed with gravels and stones, they could not fly!
Anyway, they were playing with the best team in the World!

Scorers
Silva - 14'
Jordi Alba - 41'
Torres - 84'
Mata - 88'

Ball possession 50 - 50

Sunday 1 July 2012

Rwanda Yasheherekea Miaka 50 ya Uhuru Wake


Rwanda leo imeadhimisha miaka 50 tangu ilipopata uhuru wake kutoka kwa wabelgiji hapo mwaka 1962.
 
Hadi kufikia miaka 50 ya uhuru, nchi ya Rwanda imepitia mambo mengi, kubwa zaidi ni mauaji makubwa ya kimbari yaliyolengwa kuwaanagamiza watutsi wa Rwanda yaliyofanyika mwaka 1994. 
  
Mbali ya kusherehekea miaka 50 ya uhuru, pia iliadhimisha miaka 18 tangu mauaji ya kimbari yalipomalizika.  
 
Katika hotuba ya Rais wa Rwanda, Paul Kagame, amesema kwa sasa wanaangalia maisha ya baadaye na kusahau yaliyopita. 
 
Kesho Jumatatu itakuwa siku ya mapumziko, kwani leo watu watakesha wakisheherekea sikukuu hii.

Saturday 30 June 2012

Kupaa Mbinguni au Kuokoka?

Mtu anaposema anamuomba Mungu aweze kwenda Mbinguni.....
Basi usifikiri njia ya kwenda huko ni rahisi kama barabara hii  ....
  
Kuomba peke yake pia hakutoshi, bali utafanikiwa kama utaweka mkazo katika mambo mengi ikiwapo na Matendo, Upendo, Uadilifu, Huruma, Kujali, Kusaidia na kuwa Mkweli. 
 
Ni kazi bure kujionyesha ya kuwa wewe ni mcha Mungu, wakati unapokuwa kwenye giza unakuwa mchafu kuliko hata yule unayemdhihaki kila siku ya kuwa anabebwa na Ibilisi.
Mungu unayemuogopa na kujificha, ni mwanadamu mwenzako, lakini unasahau ya kuwa Mweza wa yote hafichwi kitu na anakuona!

Halafu watu wakikuambia wewe Pambaaaf unatudanganya, unatishia ati utawapeleka mahakamani na kudai mabilioni ya kuchafuliwa jina!!!
 
  
Weekend njema kwa wote!

Friday 29 June 2012

Weekend spells

You will never be in Darkness when there is a full Moon. 
  
Impossibles can turn into possibles when you are determined. 
 
Have a lovely weekend!

Euro 2012 Final is Italy Vs Spain

Super Mario scored twice in the first half period to pave way for Italy into Euro 2012 Finals.
Italy won by 2 - 1 goals against Germany.

I bet for Italy to be the new Champions!

Tuesday 29 May 2012

Vurugu za Zanzibar!

Huu Mgogoro au vurugu za Zanzibar ni kweli unahusu kudai majadiliano ya muungano au una malengo tofauti?  
Sijaelewa kwa nini zinazoshambuliwa zaidi ni taasis za kidini!
  
Nawaza kwa maandishi tu.  
 
Nawatakia Jumanne njema

Monday 28 May 2012

Pale Unapokutana na Mtu Usiyemtarajia!

Wiki hii nilipata mwaliko maalumu wa chakula cha usiku kutoka kwa mtu ambaye hatufahamiani.
Habari hizi nililetewa na mtu ambaye tumekwisha fanya kazi pamoja kama mara 3 hivi katika kituo cha kulelea watoto yatima na wenye ulemavu ikiwa ni pamoja na wenye mtindio wa ubongo.  
  
Katika kituo hiki cha kulelea watoto yatima, nilikataa kupokea malipo yoyote kutoka kwa huyu mtu aliyeniomba nije kuwapima watoto hao na kutoa ushauri wa kitaalam. Niliamua kufanya kazi ya ujuzi wangu kwa kujitolea kutokana na mguso nilioupata baada ya kuwaona watoto wenyewe, kwani hapo awali sikudokezwa ya kuwa kuna watoto wenye ulemavu na wengine wana mtindio wa ubongo.
  
Historia niliyoipata ya mahangaiko aliyopata mtu huyu labda nimuite msamaria mwema, alijitahidi kutafuta wataalamu kwa miezi zaidi ya mitatu na walikuwa wanatoa miadi ya kuja lakini baadaye wanajitoa kwa sababu mbalimbali. Kama alivyoniambia, jiwe lake la mwisho ndio hilo alilonirushia mimi, na hakutegemea kama angepata mtu kwani alikuwa anahitaji watoto waonwe kabla ya mwisho wa mwezi huu ili kuagiza chochote kitakachowasaidia.
  
Kwangu bila kujua historia hiyo, aliponipigia simu baada ya kupata taarifa zangu kupitia ofisi za ubalozi wa Marekani hapa Kigali, nilimpa siku ya kwenda kuwaona kwani nilikuwa nina ratiba ngumu sana kwa wiki hiyo. Ilibidi nivunje ratiba yangu ya kazi kwa muda japo kwa shingo upande. Siku na saa niliyoahidi nilifika kwa muda tuliopanga hata yeye hakuwa na imani ya kwamba nitafika kutokana na uzoefu alioupata hapo awali.

Kuhusu mwaliko wa chakula cha usiku, ambao ulifanyika Jumamosi tarehe 26 May 2012 .....Nilikubali kufika kwenye hoteli ambapo nilijulishwa kuwa wameandaa meza maalum kwani ilitolewa oda maalum tangu asubuhi kwa ajili ya chakula hicho. Nilikutana na mtu huyo ambaye ni Mzungu na raia wa Marekani. Alikuja na mkewe ambaye ndio yule nilikutana naye kwenye shughuli ya kuona watoto.
Mwenyeji wangu na mkewe walionekana waungwana sana na wenye heshima. Hata walivyonipokea walionyesha kujali na kuwa waungwana, sikuwa nimezoea hali hii ya kuongozwa na kufunguliwa milango nk.  Pia, wahudumu kuwepo muda wote na kubadili hiki na kile, kama vile tupo kwenye dhifa fulani, kumbe tupo watatu tu! 
  
Tuliongea mambo mengi ya binafsi na maisha yetu hapa Rwanda. Tuligusia kidogo mambo ya uchumi na siasa. Siku ilikuwa nzuri na chakula kizuri pia.


Baadaye nilifahamishwa ya kuwa mwenyeji wangu alikuwa ni mwakilishi mkaazi wa Shirika la Fedha Duniani (IMF) nchini Rwanda! Na alipata habari zangu akapenda kukutana nami kwa ajili ya mazungumzo ya kawaida na kufahamiana. Japo mimi sina taaluma na mambo ya fedha wala uchumi, na shughuli zangu hazihusu masuala hayo. …… Bado ninatafakari ….. kwa nini alipenda kukutana nami, wakati shughuli zilizonikutanisha na watu wengine, taasisi yake haishughuliki moja kwa moja katika uendeshaji wake. 
  
Nimependa tu kuwasiliana nawe msomaji, ujue ya kuwa kuitika wito ni bora, japo unaweza kuichuja habari ulioitiwa au kuikataa.  

Friday 25 May 2012

Jihadhari na Bidhaa Kutoka China

Kwa siku nyingi kumekuwa na malalamiko kutoka nchi zinazoendelea kuhusiana na uduni wa bidhaa kutoka China. 
Serikali ya China ilikuwa inajitetea na kusema inaudha bidhaa zake kutokana na mahitaji ya wateja, maana yake nchi zinazoendelea zilikuwa zina agiza bidhaa za bei nafuu lakini zikiwa na ubora duni. 
Serikali ya Tanzania kupitia mamlaka zake, ilikuwa inazikamata bidhaa bandia na kuziteketeza. Jitihada hizi hazijaweza kuzimaliza bidhaa bandia au feki au zenye ubora wa hali ya chini.  
   
Wiki iliyopita, Serikali ya Marekani ililaumu China kwa kuiuzia vifaa vya ndege za kivita ambavyo takribani asilimia 60 ya vifaa vilivyotumika kutengeneza ndege za kijeshi, vilikuja kugundulika kuwa vilikuwa chini ya kiwango.  
 
Uchunguzi uliofanyika na taasisi za Marekani kwenye bidhaa nyingine zilizoingizwa nchini humo zikiwamo nguo, baiskeli nk umebaini ya kuwa bado wanatengeneza na kuzipeleka bidhaa bandia zenye ubora hafifu wakati mwingine kwa asilimia 90 ya bidhaa zote wanazoziingiza Marekani, japo wanabandika alama au lebo sahihi. Watu wamejikuta wakinunua lebo sahihi huku bidhaa ikiwa bandia.
  
Baadhi ya taasisi zimeshindwa kuyafunga maduka au kuteketeza bidhaa zilizouziwa bidhaa bandia kutoka China kwani wanahofia kuwa kuna mamilioni ya watu watapoteza ajira wakati kuna kiu kubwa ya ajira kwa watu wengi! 
  
Habari zipo nyingi, lakini unaweza kusoma mojawapo hapa

Sunday 20 May 2012

Chelsea: New European Champions - 2012

Drogba was the man of the day for Chelsea. 
He scored an equiliser goal in 88th minute and send the match into extra time. 
  
He gave penalty to Bayern Munich during the extra time while he was trying to defend the goal. But Arjen Robben spot kick was denied by Chelsea goal-keeper Cech. 
  
He scored the the last penalt kick which earn Chelsea the European Champion trophy for the first time in their history. They beat Bayern Munich by 4 - 3 penalties.

Some statistics:             Bayern Munich   vs    Chelsea
Total Shots                           34                        9
Corners                                20                        1
Fouls committed                   11                       26

 
Congratulations Chelsea!

Sunday 13 May 2012

Simba yatolewa Na Al Ahly Shandy kwa Penati 9 - 8



Mabingwa wa mpira wa Miguu Tanzania Simba ya Dar es salaam, usiku wa tarehe 13 May 2012 imeyaaga mashindano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika baada ya kufungwa magoli 3 - 0 na Al-Ahly Shandy ya Sudan kwenye muda wa kawaida. 
  
Magoli yote hayo yalifungwa katika kipindi cha pili, la kwanza likiwa dakika ya kwanza kipindi cha pili, yakifuatiwa na jingine dakika 3 baadaye. La tatu lilifungwa baada ya dakika 10 baada ya goli la pili kwa uzembe wa Victor Costa kwa kutokuwa makini na utoaji wa pasi na hivyo kupoteza mpira huo uliomfikia mchezaji wa Al-Ahly Shandy aliyefunga kwa urahisi. Mwisho wa dakika 90 mabao yalikuwa 3 - 0 dhidi ya Simba, na hivyo kufanya kuwe na jumla ya mabao 3 - 3.  
     
Mshindi alipatikana kwa njia ya penati ambapo jumla ya penati 10 zilipigwa. Juma Kaseja alishindwa kufunga penati ya mwisho kwa Simba na hivyo kuzidiwa bao moja na Al-Ahly Shandy 
  
Simba wanatarajiwa kurudi Dar es Salaam Jumatatu, ili waanze kuganga mashindano mengine.

Man City Made it ... Since 1968


English Premier league 2011/12 season has ended with a dramatic win for Man City over QPR after being trailling by 2 - 1 until the injury time. The heroes were Dzeko and Aguero who scored two vital goals on stoppage time to lift up Man City to the top spot of English Premier League.

It was a great moment for Man City fans who had been seated on hot coal throughout the game.

Manchester United came second after the narrow win 1 - 0 over Sunderland, just beaten by goal difference with arch-rival and Premier Champions, Manchester city. Arsenal came out third when they won against West Bromwich Albion by 3 - 2 goals, and Tottenham clinch the last post for Champions League

Both Arsenal and Manchester united have a good record for Champions League qualiffication. However, for this year they both finished without any title.

Wednesday 9 May 2012

Wakuu wapya wa Wilaya Tanzania Bara

Ifuatayo ndio orodha ya wakuu wapya wa wilaya Tanzania Bara kama walvyiotajwa leo na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Idadi ya wakuu wa wilaya walioachwa ni 51.

Wakuu wa wilaya wapya na sehemu walizopangiwa ni:-


1. Novatus Makunga - Hai

2. Mboni M. Mgaza - Mkinga

3. Hanifa M. Selungu - Sikonge

4. Christine S. Mndeme - Hanang

5. Shaibu I. Ndemanga - Mwanga

6. Chrispin T. Meela - Rungwe

7. Dr. Nasoro Ali Hamidi - Lindi

8. Farida S. Mgomi - Masasi

9. Jeremba D. Munasa - Arumeru

10. Majid Hemed Mwanga - Lushoto

11 Mrisho Gambo - Korogwe

12. Elias C. J. Tarimo - Kilosa

13. Alfred E. Msovella - Kiteto

14. Dkt. Leticia M. Warioba - Iringa

15. Dkt. Michael Yunia Kadeghe - Mbozi

16. Mrs. Karen Yunus - Sengerema

17. Hassan E. Masala - Kilombero

18. Bituni A. Msangi - Nzega

19. Ephraem Mfingi Mmbaga - Liwale

20. Antony J. Mtaka - Mvomero

21. Herman Clement Kapufi - Same

22. Magareth Esther Malenga - Kyela

23. Chande Bakari Nalicho - Tunduru

24. Fatuma H. Toufiq - Manyoni

25. Seleman Liwowa - Kilindi

26. Josephine R. Matiro - Makete

27. Gerald J. Guninita - Kilolo

28. Senyi S. Ngaga - Mbinga

29. Mary Tesha - Ukerewe

30. Rodrick Mpogolo - Chato

31. Christopher Magala - Newala

32. Paza T. Mwamlima - Mpanda

33. Richard Mbeho - Biharamulo

34. Jacqueline Liana - Magu

35. Joshua Mirumbe - Bunda

36. Constantine J. Kanyasu - Ngara

37. Yahya E. Nawanda - Iramba

38. Ulega H. Abadallah - Kilwa

39. Paul Mzindakaya - Busega (mpya)

40. Festo Kiswaga - Nanyumbu

41. Wilman Kapenjama Ndile - Mtwara

42. Joseph Joseph Mkirikiti - Songea

43. Ponsiano Nyami - Tandahimba

44. Elibariki Immanuel Kingu - Kisarawe

45. Suleiman O. Kumchaya - Tabora

46. Dkt. Charles O. F. Mlingwa - Siha

47. Manju Msambya - Ikungi (mpya)

48. Omar S. Kwaangw’ - Kondoa

49. Venance M. Mwamoto - Kibondo

50. Benson Mpesya - Kahama

51. Daudi Felix Ntibenda - Karatu

52. Ramadhani A. Maneno - Kigoma

53. Sauda S. Mtondoo - Rufiji

54. Gulamhusein Kifu - Mbarali

55. Esterina Kilasi - Wanging’ombe (mpya)

56. Subira Mgalu - Muheza

57. Martha Umbula - Kongwa

58. Rosemary Kirigini - Meatu

59. Agness Hokororo - Ruangwa

60. Regina Chonjo - Nachingwea

61. Ahmed R. Kipozi - Bagamoyo

62. Wilson Elisha Nkhambaku - Kishapu

63. Amani K. Mwenegoha - Bukombe

64. Hafsa M. Mtasiwa - Pangani

65. Rosemary Staki Senyamule - Ileje

66. Selemani Mzee Selemani - Kwimba

67. Lt. Col. Ngemela Lubinga - Mlele (Mpya)

68. Iddi Kimanta - Nkasi

69. Muhingo Rweyemamu - Handeni

70. Lucy Mayenga - Uyui

Tuesday 8 May 2012

Makinda: Tanzania Haijawa Tayari Kuridhia Kuondolewa kwa Masharti ya Uhamiaji EAC

Mkutano wa viongozi wa mabunge (National assembly speakers) ya nchi zinazounda Jumuiya ya Afrika Mashariki wanaokutana jijini Kigali, Rwanda walikuwa na mjadala mkali unaohusu kufungulia mipaka na kelegeza masharti ya uhamiaji kati ya nchi wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki.

Habari zinadai ya kuwa mashambulizi mengi yalielekezwa kwa Tanzania kwani bado haijaridhia kufungulia mipaka yake kama nchi nyingine zinavyopenda kuharakisha mkataba huu.
   
Spika wa Bunge la Tanzania, Anne Makinda alisema kwa sasa Tanzania haipo tayari kufanya hivyo kwa kuwa wananchi wa Tanzania wanatakiwa kuulizwa kwanza kama wapo tayari kufanya hivyo ukizingatia ina idadi kubwa ya watu kuliko nchi zote za Afrika Mashariki. Pia aliongeza kusema ya kuwa kumekuwa na wahamiaji haramu wengi wanaoingia Tanzania kutoka nchi mbalimbali hata zilizo nje ya Afrika mashariki ambao huleta vitendo vya uhalifu na uvunjifu wa amani ndani ya Tanzania. Kwa hiyo kuna haja ya kudhibiti hilo kwanza. 
  
Kingine alichoongeza Mama Makinda, ni kuwa Tanzania haina vitambulisho vya taifa, na kwa sasa iko kwenye mpango wa kuvitoa kwa wananchi, na hatarajii zoezi hilo litakwisha mapema, labda litachukua zaidi ya miaka miwili kutoka sasa.

Monday 7 May 2012

Ujumbe Mahsusi Kwa Rais .......

Wananchi wa Uganda wamechoka kupiga kelele kwa maneno.
Sasa wameamua kufanya kwa vitendo!

Sunday 6 May 2012

Yanga Yawapa Ujiko Simba

Pazia la ligi kuu ya Tanzania limemalizika leo.  
   
Moja ya mechi iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu na wapenzi wa soka ilikuwa ni kati ya Bingwa mpya wa msimu 2011/12 Simba ya Dar es Salaam na mabingwa waliopita wa msimu wa 2010/11 Yanga ya Dar es Salaam pia. 
   
Mpira ulipoisha, Yanga walikuwa wamefungwa mabao 5 - 0, huku magoli 3 yakiwa yamefungwa kwa adhabu za penati!  
   
Hivyo Yanga wamemaliza msimu kwa kuwapa ujiko na sifa timu ya Simba ambapo timu zitakazokuja kucheza na Simba zitakuwa zinatishiwa na ushindi huu wa kufungia ligi kuu ya Tanzania Bara.

Saturday 5 May 2012

Tanzania: Baraza Jipya la Mawaziri, May 2012

MAWAZIRI
1. OFISI YA RAIS

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu)
Ndugu Stephen M. Wasira  
   
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Utawala Bora)
Ndugu George Mkuchika  
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (UTUMISHI)
Ndugu Celina Kombani  
  
2. OFISI YA MAKAMU WA RAIS
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MUUNGANO) 
   Ndugu Samia H. Suluhu  
     
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MAZINGIRA)
Dr. Terezya P.L. Huvisa  
  
3. OFISI YA WAZIRI MKUU  
  
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji)
Ndugu Mary M. Nagu 
   
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Hawa Ghasia  
  
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge)
Ndugu William V. Lukuvi  
  
4. WIZARA 
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Ndugu Samuel J. Sitta
   
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
Ndugu Shamsi Vuai Nahodha  
   
Waziri wa Ujenzi  
Dr. John P. Magufuli 
  
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
Dr. Hussein A.H. Mwinyi 
   
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi 
Dr. Shukuru J. Kawambwa 
   
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto  
Ndugu Sophia M. Simba  
  
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Bernard K. Membe  
   
Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Mathias M. Chikawe  
  
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Emmanuel Nchimbi  
   
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Dr. David M. David 
   
Waziri wa Kazi na Ajira
Ndugu Gaudentia M. Kabaka 
   
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Prof. Makame M. Mbarawa 
    
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
Prof. Anna K. Tibaijuka  
 
Waziri wa Maji 
Prof. Jumanne Maghembe 
  
Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum 
Prof. Mark Mwandosya  
   
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
Eng. Christopher Chiza  
   
Waziri wa Uchukuzi
Dr. Harrison Mwakyembe  
    
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Dr. Fenella E. Mukangara 
       
Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Khamis Kagasheki 
  
Waziri wa Viwanda na Biashara
Dr. Abdallah O. Kigoda 
  
Waziri wa Fedha
Dr. William Mgimwa 
  
Waziri wa Nishati na Madini
Prof. Sospeter Muhongo  
  
5. MANAIBU WAZIRI
I. OFISI YA MAKAMU WA RAIS
  
Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais
Ndugu Charles Kitwanga  

II. OFISI YA WAZIRI MKUU

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Majaliwa K. Majaliwa
   
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Aggrey Mwanry 
  
III. WIZARA MBALIMBALI 
  
Naibu Waziri wa Kazi na Ajira
Dr. Makongoro M. Mahanga 
   
Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
Ndugu Adam Malima  
   
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Pereira A. Silima  
   
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara
Ndugu Gregory G. Teu  
   
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Ndugu Benedict N. Ole-Nangoro
  
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Mahadhi J. Maalim  
   
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,
Ndugu Goodluck J. Ole-Medeye  
  
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Ndugu Ummy A. Mwalimu 
   
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Ndugu Philipo A. Mulugo
  
Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dr. Abdulla Juma Abdulla  
  
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Lazaro Nyalandu  
   
Naibu Waziri wa Ujenzi
Ndugu Gerson Lwenge  
    
Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,
Dr. Seif Suleiman Rashid  
    
Naibu Waziri wa Nishati na Madini
Ndugu George Simbachawene  
    
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Ndugu January Makamba   
   
Naibu Waziri wa Uchukuzi
Dr. Charles J. Tizeba  
   
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Ndugu Amos Makala 
  
Naibu Waziri wa Maji
Eng. Dr. Binilith Mahenge 
 
Naibu Waziri Nishati na Madini
Ndugu Stephen Maselle 
 
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Angela Jasmine Kairuki  
  
Naibu Waziri wa Fedha  
Ndugu Janet Mbene 
 
Naibu Waziri wa Fedha
Ndugu Saada Mkuya Salum 

Friday 4 May 2012

Rwanda: Ukatili Bado Unajitokeza Hapa na Pale

Ukatili wa mtu, wakati mwingine upo kwenye damu yake.
Sio lazima iwe kulipiza kisasi.

Kama huyu kijana wa kinyarwanda mwenye umri wa miaka 12 ambaye alirudi nyumbani na kudai apewe chakula, lakini dada yake wa tumbo moja mwenye miaka 10 alimueleza ya kuwa chakula hakijawa tayari.
Huyu kijana kwa hasira zake, akalifuata jembe na kumkata kata dada yake mpaka akafa, hakuishia hapo, akaanza kumkata na mdogo wake wa kiume wa mika 4 na kumjeruhi vibaya kabla hajadhibitiwa.


Msemaji wa polisi, alisema tukio hili linawakumbusha watu ya kuwa wanahitaji kutoa ushauri na nasaha kwa vijana, japo kwa huyu sijaelewa kwa nini alifanya hivi, kwani alizaliwa miaka mingi tu baada ya mauaji ya kimbari!

Katika tukio jingine la ukatili ni la huyu baba asiye na utashi wa kutunza watoto wake, pale alipokodisha muuaji aue watoto wake wawili wa kuzaa tena wakiwa wadogo wa umri wa miaka 6 na 8
Mtu aliyekodishwa kuwaua watoto hao aliahidiwa kupewa kiasi cha faranga za Rwanda 80,000 ambazi ni karibu ya shilingi 200,000 za kitanzania. Muuaji mtarajiwa alikubali kuwaua japo nia yake ilikuwa kuwaokoa kama anavyodai mwenyewe! Kwa hiyo alipopewa kianzio, aliamua kutoa taarifa polisi juu ya tukio hilo ambapo mtuhumiwa alikamatwa.
Baadaye ilikuja kujulikana sbabu ya kutaka kuwaua watoto hao ni Mama wa watoto hao kudai vyombo vya sheria vimshughulikie huyo baba ili atoe fedha za matumizi ya watoto hao na kama hawezi, basi apewe sehemu ya ardhi ili aitumie kuwatunzia watoto hao wawili. Pia ilikuja kujulikana ya kuwa mama wa watoto hao, ni mke mdogo kwa mtuhumiwa huyo!
Huyu jamaa aliona njia nzuri ya kutokuwa muwajibikaji wa kutunza watoto wake ni kuwaua!

Tuesday 1 May 2012

Yaliyo Moyoni mwa JK na Mei Mosi 2012

Mei mosi 2012 ndiyo hiyo inakatika.  

  
Watu walikuwa wanatarajia kusikia neema ya mishahara kuongezwa, na ndio maana katika jiji la Tanga ambapo wafanyakazi walifanya maandamano ya mei mosi walikuwa wamejizatiti kufikisha kiu yao kwa kushika mabango yaliyokuwa na ujumbe wa “Mishahara duni, Mfumuko wa Bei na kupanda kwa gharama za Maisha” ni tatizo kubwa la wafanyakazi. 
 
Rais Kikwete ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi, hakuahidi moja kwa moja ya kuwa mshahara utapanda, bali alitoa ahadi ya kuuboresha kidogo kidogo mpaka lengo litakapofikia, japo haijulikani ni lini. 
  
Mbali ya hayo alizungumzia mjadala mkali ulioibuka mwezi uliopita bungeni juu ya taarifa za ufujaji wa fedha na raslimali za watu. Alieleza ya kuwa huo mjadala aliufurahia sana, kwani uliashiria kuwa wabunge wamekuwa makini katika kutetea mali na raslimali za Tanzania. Alisisitiza ya kuwa ni yeye ndiye aliyeamua taarifa za mkaguzi mkuu wa Serikali awe anaziweka hadharani ili kutoa fursa wabunge wazijadili kwa kina, badala ya mfumo wa zamani ambapo zilikuwa hazpewi muda wa kutosha kipitiwa na kuzijadili wakati zilikuwa na kasoro nyingi. 
  
Pia alionekana kukerwa na wizi na kutowajibika kulikofanywa nabaadhi ya watendaji wa serikali, na pia kusema ya kuwa ameipa nguvu kisheria ofisi ya mkaguzi mkuu wa Serikali kuwafikisha wahalifu wa mali za uma kwenye vyombo vya sheria pale watakapobaini matukio ya wizi hata kama ukaguzi bado unaendelea. 
  
Hakuzungumzia hatua atakazowachukulia mawaziri ambao wametajwa katika taarifa hizo, japo kuna kila dalili ya kuwa atawaondoa kama si kuwafuta kazi kwenye baraza hilo, na pia kuna uwezekano wengine wakashitakiwa kwa makosa ya jinai. 
  
Mfumo madhubuti wa kudhibiti matumizi utaanza na idara za Elimu, Afya na Maji ikiwa ni pamoja na kuweka wazi fedha zitakazokuwa zinatengwa kwa kila idara, na matumizi kutolewa taarifa kwa ngazi zote.
  
Kinachoashiria ya kuwa kuna wengine wanaweza kuwa wamekwishapoteza nyadhifa zao, ni pale mhesh. Omari Nundu alipotambulishwa zaidi ya mara mbili kama Mbunge mwenyeji wa sherehe hizo, na wala hakutajwa kama waziri huku mawaziri na manaibu waziri wengine ambao hawana kashfa walipotajwa kwa nyadhifa zao. 

English Premier League Champion to be Known on the Last Game



The big game between the Manchester Clubs has just ended!

Manchester United today's defeat by 1 - 0 at the hand of Manchester City has left the English premier title open between these two teams. The winner will be known at the closing day of EPL.  The goal for Man City was scored by Kompany in the dying minutes of the first half. 
  
The Manchester City Club has the upper edge to Manchester United just by goal difference, where Man City has an advantage of 8 goals on top of Man United.

Photo from BBC

Monday 30 April 2012

Mei Mosi Isiyo na Matumaini Wala Furaha

Hapo zamani za kale ....... Ilipokuwa inafika siku ya mei mosi, wafanyakazi walikuwa wanaingojea kwa hamu kubwa kwa sababu mbalimbali. Kwani siku hiyo walikuwa wanatarajia :
  1. Kusikia mafanikio yaliyopatikana kitaifa kutokana na mchango wa wafanyakazi katika kulisogeza mbele gurudumu la maendeleo. 
  2. Kujua ni nani amekuwa mfanyakazi bora katika taasisi wanazozifanyia kazi ili kuwapa hamasa ya kufanya kazi zaidi ili na wao waje wapate tunuku hiyo kwa miaka inayokuja
  3. Kujua mipango ya serikali yao katika shughuli zijazo za maendeleo
  4. Kutaka kujua nyongeza ya mishahara itakuwa kiasi gani, na vilevile kujua itapunguza kivipi ukali na gharama za maisha yao ya kila siku.  
  
Lakini kwa mwaka huu, matumaini na tashwishwi imebadilika sana kwani badala ya watu kungojea kwa hamu taarifa ambazo hapo awali ndizo zilizokuwa zikiwapa matumaini wafanyakazi, kwa sasa wanasubiri kudra za Mwenyezi Mungu ili awashushie baraka kimiujiza za kupunguza ukata.  
Cha ziada kwa mwaka huu, wafanyakazi wamekaa mkao wa kusubiri kama kiongozi wa nchi yao atasema chochote kuhusiana na tuhuma nzito za uhujumu uchumi na wizi wa mali za uma unaowahusu wateule wake ambao wengi wao wamekosa dira, kujitambua, sifa za uongozi na uzalendo kwa nchi yao na kugeuka kuwa vichaka vya ubadhirifu, wizi na ubinafsi huku wakiendelea kujisafisha kwa kujipakaa madhambi yao kwenye miili yao na kuonekana kama .... 
  
Ninavyofikiri kwa sasa, ni kwamba kunahitajika mabadiliko makubwa ya mfumo wa utawala, uongozi, na wateule waliopo na kupata utawala mbadala, ambao unaweza kuwafanya watanzania wapime na kuwalinganisha waliopo madarakani kwa sasa na wale watakaokuja. Baada ya hapo, nina imani wateule watawajibika kwa wanachi vyema kwani wananchi watakuwa wameshapima na kujiridhisha ya kuwa hawa wanatufaa, na hawa hawafai....

Huu ni mtazamo wa mtu binafsi. Ameutuma ujumbe huu na kuomba niuchape ili watu waupime na kumuunga mkono au kumkosoa. 
  
Happy May Day!

Series: Natures of Our Universe

Wonders of the Nature! Are everywhere. 
 
Recently, when I was flying ...., while we were air-borne on auto-pilot, I just popped out my eyes out of window to get an impression of the blue sky. 
What attracted me was how the appearance of the clouds..... below our aircraft.
  
I had to recall my science knowledge on the forces which maintain the clouds at their position while figuring out what I was seeing out of them. Well, the journey became shorter, and I was glad to arrive at my final destination without being tired despite hours we spent outer there! 
   
Have a blessed monday!

Monday 23 April 2012

CCM Tunawaimarisha kuja kuwa Wapinzani Madhubuti Kwenye Serikali Ijayo - Mbilinyi

Mbunge wa Mbeya Mjini, mh. Mbilinyi amewapa somo wabunge wa CCM ya kuwa wabunge wa CHADEMA kuwapigia kelele wabunge na Serikali ya CCM ni kuwajenga kuwa wapinzani imara mara pale CHADEMA itakaposhikilia dola kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015. Kwani CHADEMA haitataka kuwa na wapinzani legelege, inahitaji watu wanaoisimamia serikali iliyopo madarakani kwa ushupavu ili wao CHADEMA na serikali yao waende kwenye mstari ulionyooka.


 
Mh. Mbilinyi alikuwa anachangia muswada uliowasilishwa na kamati teule iliyochunguza tukio la kutoroshwa kwa wanayama hai mwaka jana unaohusisha wizara ya Maliasili na Utalii.

  
Taarifa hiyo imejaa kila aina ya takataka utakayoifikiria kutokana na yaliyojiri katika uchunguzi huo.

  
Baadhi ya matatizo yaliyoainishwa ni pamoja na
  • Waziri wa Maliasili na Utalii kujiamulia kutoa vibali kwa makampuni ambayo hayakuomba kibali cha uwindaji
  • Waziri kutoa vibali kwa makampuni ambayo hayakuwa na sifa japo kamati ya ushauri ilimweleza waziri kuwa makampuni hayo hayana sifa
  • Wanyama kusafirishwa wakiwa hai kwenda nje ya nchi bila maombi yoyote kutoka huko nje
  • Raia wa kigeni kupewa kibali cha kukamata wanyama wakati hivyo vibali hutolewa kwa watanzania tu
  • Baadhi ya viongozi wa chama ….. kuingilia shughuli za uhamiaji na kuwapitisha wageni wa shughuli za uwindaji kinyume cha sheria
  • Wanyama kufugwa/kuhifadhiwa kwenye makazi ya watu kwa zaidi ya hata miaka 8 wakati sheria hairuhusu wanyama kukaa sehemu kama hizo au kutunzwa kwa zaidi ya miezi mitatu
  • Vibali vya kukamata wanyama kutolewa kiholela na kwa watu ambao kisheria hawaruhusiwi kuto
  • Vitalu kutolewa bila kufuata sheria zilizopo za uwindaji
  • Kampuni iliyopewa kibali cha kusafirisha wanyama hai ya Jungle International haikuwa imeomba kibali cha kusafirisha wanyama, na pia kimsingi kampuni hiyo ilishabadilishwa jina na kazi miaka mingi na wakati inapewa kibali hicho haikuwapo kwenye daftari la msajiri, kwa maana nyingine ni kampuni hewa.   
Mambo ni mengi na kama una uzalendo na nchi yako unaweza kuivunjilia mbali radio unayosikiliza au runinga unayoitazama.

 

Sunday 22 April 2012

Mnyika Apoza Machungu ya Mh. Omari Nundu

Mh. Omari Nundu

Mijadala ya Bunge letu kwa sasa sio kwamba inaudhi peke yake, bali wakati mwingine inasisimua pia.
Kama watu wengi walivyosikia taarifa ya kamati za Bunge zilizowasilishwa wiki hii, pamoja na taarifa ya mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali ambazo zimeainisha matumizi mabaya ya fedha za uma, pamoja na kila dalili za ufisadi hasa kwa watendaji wengi ambao huwa wanateuliwa na Rais peke yake. 
  
Taarifa hizi zilipokelewa kwa hasira kali na wabunge wote bila kujali itikadi za vyama vyao na hata kufikia maazimio ya kutaka kuleta hoja ya kutokuwa na imani na waziri mkuu iwapo mawaziri waliotajwa kuhusika na kashfa hizo hawatajiuzuru. 
 
Kikao cha Bunge cha jumamosi ya tarehe 21 Aprili 2012, kilidhihirisha mkanganyiko na ugomvi mkubwa uliomo miongoni mwa mawaziri wa serikali iliyopo madarakani, mara baada ya Waziri wa Uchukuzi, Bw. Omari Nundu kueleza bayana ndani ya Bunge ya kuwa hakuwahi kushirikishwa kwa namna yoyote na mkataba unaosemwa upo sasa wa kujenga gati namba 13 na 14 katika bandari ya Dar es Salaam. Alidai ya kwamba kisheria yeye ni mdau muhimu katika kuingia na kuidhinisha mkataba wowote unaohusiana na wizara yake. Kwa maana nyingine inaonekana waziri wa fedha alitumia mamlaka kinyume cha sheria kupitisha mkataba huo bila kumshirikisha Bwana Nundu kama ilivyotakiwa.  
Lakini kwa upande mwingine, naye waziri Nundu, alishindwa kueleza kivipi naye ana mkataba wa "mfukoni" na kampuni nyingine kutoka China, ambapo huo mkataba haujulikani na mtu yeyote isipokuwa yeye peke yake!!!!! 
  
Kikao cha jumamosi kilionekana kuwachanganya watu wote bungeni ikiwa ni pamoja na spika wa Bunge Mama Anne Makinda.

Aliyeokoa jahazi siku ya jana, labda na Taifa kwa ujumla, ni mbunge wa Ubungo, John Mnyika, ambaye alikuja na mapendekezo ya kubadili azimio la kamati inayohusiana na masuala ya uchukuzi ambayo ilitaka gati hilo lianze kujengwa mara moja, ambapo Mnyika alipendekeza upembuzi yakinifu ufanywe na taasisi inayojitegemea. Hii ilitokana na kugundulika ya kuwa mkataba uliopo kwa sasa ulifanywa na kampuni ambayo ndiyo hiyo hiyo ilikuja kupewa tenda ya kujenga gati hilo.
Hali hii ilizusha wasiwasi wa kuwepo na hali ya kuweka makadirio ya juu kupita kiasi na watu kujenga hisia au kuashiria kuwepo na dalili za rushwa ukizingatia makubaliano ya ujenzi hayakuwa na kushindanishwa, ni kama hiyo kampuni ilipewa moja kwa moja tenda ya ujenzi wa magati hayo. 
 
Kilichowafurahisha watazamaji wengi, ni jinsi Bwana Nundu alivyokuwa anashangilia kwa njia ya kibunge baada ya hoja ya Mnyika kuungwa mkono na kupitishwa ambapo ni kinyume kabisa na tulivyozoea kuona kutoka kwa mawaziri ambao mara nyingi hupinga vikali hoja za wabunge wa vyama vya upinzani!

Yaani...... kushangilia kwa mhesh. Nundu......kwangu naona hii ilikuwa ni kama ..... "haya tukose wote"

Tuesday 17 April 2012

Upotoshaji wa Habari za Tanzania

Jana nilikuwa ninasoma jarida la matangazo ya bidhaa za duka kubwa la vitu mchanganyiko (Supermarket) ambalo lilikuwa limenakshiwa kwa picha za kuvutia za bidhaa mbalimbali ambazo ninauzwa katika duka hilo.  
Mbali ya yote hayo, liliongeza baadhi ya habari za nchi za Afrika ya Mashariki ambazo zilijumuisha vivutio mbalimbali vinavyopatikana katika nchi za Afrika Mashariki. 
 
Niliposoma kichwa cha habari kinachohusu Tanzania... nilivutiwa ili nisome makal hiyo.
Kulikuwa na habari nzuri za vivutio kama mlima Kilimanjaro, ziwa Tnaganyika (Lake Tanganyika) na umaarufu wake, pia na bonde la Ngorongoro ambalo ni la kipekee Duniani lilipambwa vizuri.  
 
Tatizo...... 

Nilipoingia kwenye habari za lugha... nilishangaa wakidai ya kuwa lugha ya kigogo ndiyo inayoongewa sana Tanzania ikifuatiwa na kihaya, halafu kiha, tena kimakonde, na wakadai kiswahili hakimo katika lugha zinazo ongewa kwa wingi!!!! 
  
Nilipofika kwenye hoteli na mighahawa maarufu sana ya Tanzania, nilihisi siijui Tanzania....

Nikaona bora niishie hapo na kunywa maji ya baridi, sijui kupoza nini, lakini nilipata nafuu na kuendelea na kazi nyingine. 
 
Kwa anayejua habari sahihi za mambo hayo hapo juu, basi na anifahamishe ili nami niende na wakati!!

Wednesday 11 April 2012

Hofu ya Kutokea Tsunami Yaondolewa


Tetemeko kubwa la ardhi lililotokea leo katika pwani iliyo karibu na Kisiwa cha Sumatra nchini Indonesia ambalo lilikuwa na kipimo cha 8.6 halikuweza kuleta Tsunami kama ilivyobashiriwa hapo awali. 
  
Mawimbi makubwa sana yalikadiriwa kuwa na ukubwa usiozidi meta 1 kutoka usawa wa bahari, na kuna sehemu nyingi walipata mawimbi madogo zaidi na hivyo hayakuleta madhara yoyote zaidi ya usumbufu kwa watu kukimbia na kuingiwa na wasiwasi. 
  
Kufuatia onyo hilo, shughuli nyingi za kwenye bahari ya Hindi zilisitishwa ikiwamo na nchi za ukanda wa pwani ya Afrika Mashariki ambapo ilikadiriwa pwani hii ingeweza kupigwa na mawimbi ya Tsunami hiyo kwenye muda wa kati ya saa 11 jioni hadi saa 2 usiku. 
  
Kutokana na habari zilizotolewa na kituo cha kutoa tahadhari ya Tsunami, ni kwamba Tsunami hiyo haipo tena, na wala watu hawana haja ya kuwa na wasiwasi.

Friday 6 April 2012

Kuenguliwa Kwa Lema, Ndio Mwanzo wa Ukurasa Mpya

Siasaaaaaaaa!
Kuenguliwa Ubunge kwa Godbless Lema kunaashiria mambo mengi, ya kuwa kuna uwezekano wa wabunge wengine nao kun'golewa ikiwa ni pamoja na wale waliopo kwenye baraza la mawaziri la sasa hivi. 
  
Iwapo ukitukana mtu wakati wa kampeni za ubunge wako unaweza kuenguliwa Ubunge hapo baadaye, basi kazi ipo. 
  
Mimi nafikiri tutarajie mengi tu kwenye kesi zinazoendelea. Halafu uchaguzi ukirudiwa, Chama fulani kitashinda.... Wakati huo huo mabilioni ya pesa yatapotea kwenye kampeni, huku dawa na vitendanishi katika hospitali hakuna. 
  
Kweli Bongo akili ipo.
Sitegemei sana mabadiliko ya atakayemrithi Lema, kwani watu wa Arusha hawajabadilika na Serikali yetu tukufu nayo haijabadilika. 
  
Ijumaa Kuu Njema!

Monday 2 April 2012

Matokeo Yasiyo Rasmi: CHADEMA Washinda Arumeru Mashariki

Matokeo yaliohakikiwa na tume ya Taifa ya Uchaguziya katika kata 15 kati ya 17 yameonyesha mgombea wa Chadema, Bw Nassari anaongoza kwa zaidi ya kura 6,000, na matokeo ya kata mbili zizobaki hayatarajiwi kuleta mabadiliko ya ushindi.

Wale waliokokotoa matokeo ya kila kituo, wameshathibitisha ushindi kwa CHADEMA.  
  
Kinachosubiriwa ni kutangazwa mshindi rasmi.  
  
Tahadhari: Haya ni matokeo ya awali.

Matokeo ya Awali ya Uchaguzi wa Ubunge - Arumeru Mashariki

Baada ya kuzuka mvua isiyo ya kawaida ya vurugu na kurushiana mawe imesababisha kucheleweshwa kwa majumuisho ya kura za Arumeru Mashariki, na hivyo kuna uwezekanao matokeo yakatangazwa kukiwa kumekucha tayari.

Fuatilia hapa kura zisizo rasmi za baadhi ya vituo kwa kubofya hapa FK5HA

Friday 30 March 2012

Airtel: Yazindua Huduma zake Rwanda

Kampuni ya huduma za mawasiliano kwa njia ya simu ya Airtel inayomilikiwa na Bharti ya India, leo imezindua huduma zake nchini Rwanda na hivyo kuongeza idadi ya nchi ambazo Airtel inatoa huduma zilizopo barani Afrika kufikia 17. 
  
Nchi ambazo kwa sasa zinafikiwa na huduma za Airtel katika bara la Afrika ni Burkina Faso, Niger, Nigeria, Zambia, Kenya, Tanzania, Uganda, Chad, Malawi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Congo Brazaville, Sierra Leone, Madagascar, Ushelisheli (Seychelles), Ghana na Gabon. 
  
Bharti Airtel Ltd, ina mpango wa kuwekeza kiasi cha dola za Kimarekani milioni 100 katika kipindi cha miaka 3 ijayo. Kati ya hizo, dola milioni 30 zitatumika katika kupata leseni ya uendeshaji!  
  
Pia, kampuni hii inatarajia kutoa zaidi ya ajira 300 kwa wananchi wa Rwanda, nyingine zikiwa ni za moja kwa moja na nyingine si za moja kwa moja.  
 
Inatarajiwa gharama za kutumia simu zitapungua kwa sababu nguvu ya ushindani kwa sasa itaongezeka baada ya makampuni yanayotoa huduma hizo kwa sasa kufikia matatu. Mengine ni TIGO na MTN.