Member of EVRS

Sunday 1 July 2012

Rwanda Yasheherekea Miaka 50 ya Uhuru Wake


Rwanda leo imeadhimisha miaka 50 tangu ilipopata uhuru wake kutoka kwa wabelgiji hapo mwaka 1962.
 
Hadi kufikia miaka 50 ya uhuru, nchi ya Rwanda imepitia mambo mengi, kubwa zaidi ni mauaji makubwa ya kimbari yaliyolengwa kuwaanagamiza watutsi wa Rwanda yaliyofanyika mwaka 1994. 
  
Mbali ya kusherehekea miaka 50 ya uhuru, pia iliadhimisha miaka 18 tangu mauaji ya kimbari yalipomalizika.  
 
Katika hotuba ya Rais wa Rwanda, Paul Kagame, amesema kwa sasa wanaangalia maisha ya baadaye na kusahau yaliyopita. 
 
Kesho Jumatatu itakuwa siku ya mapumziko, kwani leo watu watakesha wakisheherekea sikukuu hii.

No comments: