Member of EVRS

Friday 29 July 2011

Tanzania: Kuanza Kutegemea Mgao wa Mbalamwezi Wakati wa Usiku!

Suala la upatikanaji wa umeme, Watanzania inabidi waendelee kuishi kwa matumaini… 

  
Kampuni inayozalisha gesi asilia kutoka visiwa vya Songosongo, Songas imekiri kuwa haina uwezo wa kuzalisha gesi ya kuendesha mtambo mpya ulionunuliwa na Tanesco wa kuzalisha umeme wa megawati 100 kwa kutumia gesi asilia. 
   
Kampuni hiyo imesema kwa sasa inazalisha gesi kwa kiwango cha ukomo wa juu, na haiwezi kuongeza hadi itakapofanya upanuzi wa mitambo yake ya kuzalisha gesi ikiwa ni pamoja na kubadili bomba la kusafirisha gesi kuelekea Dar es Salaam. Shughuli hii inatarajiwa kukamilika baada ya miaka 2. Kwa maana hiyo, hata hizo megawati za ziada kutoka Tanesco zitapatikana kuanzia mwaka 2013. Hii ina maana huo mtambo ambao Tanesco ilikimbilia kuununua haraka haraka utakaa bila kazi hadi mwaka 2013!!!!! 
 
Hii inanikumbusha hotuba za mbunge wa CHADEMA na waziri kivuli wa Nishati na Madini, John Mnyika. Pia na ile ya mwenyekiti wa kamati ya nishati na madini, January Makamba (CCM), ambao walionyesha shaka kubwa kwa mipango ya Tanesco katika kuzalisha umeme huku wakiwa hawajajipanga kujua ni wapi watapata nyenzo za kuendesha hatua zao za dharura. 
  
Sasa ukweli umeanza kujionyesha kuwa mipango ya hawa wenzetu ni kweli ilikuwa ni ya “zima moto” kwa maana zote mbili za kufanya mambo kidharura ambapo mara nyingi watu hawafikirii sana zaidi ya kuuzima moto haraka kabla haujaharibu zaidi, na pili kufanya mchezo wa kiini macho kuwapumbaza watu kuwa umeme waja hivi karibuni kupunguza moto wa hasira za watu na wabunge kuhusiano na mgao mkubwa giza… 
 
Lakini…. Walikuta wabunge karibu wote bila kujali itikadi zao za kisiasa, walikuwa tayari ni moto usioweza kupozwa kwa mbinu ya ghiliba. 
  
Watanzania endeleeni kuishi kwa matumaini mkitegemea mgao wa mbalamwezi, kwani hata hizo taa za mafuta ya taa mtashindwa kuzitumia baada ya bei ya mafuta ya taa nayo kupandishwa. Siku mkipata umeme kwa siku nzima inabidi mshangae 

Sunday 24 July 2011

Mauaji ya Norway: Ukatili Dhidi ya Haki ya Kuishi

Anders Behring Breivik (Pichani juu), ambaye ni raia wa Norway ameitikisa dunia wiki hii kwa kufanya mauaji ya kikatili ya karibu watu 100 kwa siku moja katika mji mkuu wa Norway, Oslo. 
  
Sababu kubwa za kufanya mauaji hayo bado zipo kwenye uchunguzi mkali unaofanywa na Serikali ya Norway. Mtu huyu alikamatwa siku hiyohiyo aliyofanya mauaji ya kutisha na kinyama, kwani aliwashambulia kwa risasi vijana waliokuwa katika mkutano wa mafunzo ya kisisasa wanaounga mkono chama kinachotawala Norway. Inadaiwa siku ya kufanya shambulio hilo, alikuwa amevaa nguo kama askari.
Mtu huyu, pia anahusishwa na kutega bomu lililolipuka karibu na ofisi kuu za Serikali mjini Oslo. Siku ya tukio hili la kutisha, maiti 7 zilipatikana karibu na eneo lilipolipuka bomu hilo, na ilikuwa inahofiwa kuwa huenda kuna baadhi ya watu wanaweza kuwa wamefukiwa na kifusi cha jengo lililobomoka kutokana na bomu lililolipuka.  
  
Tukio hili linasikitisha sana, na haieleweki huyu jamaa kama alishirikiana na mtu yeyote, japo alipohojiwa alidai yeye akushirikiana na mtu au kikundo chochote kutekeleza azma yake hii mbaya sana.  
  
Tunaombea amani na utulivu katika nchi ya Norway tukiwa na matumaini ya kuwa tukio kama hili halitarudiwa tena!  

Friday 22 July 2011

Friday Humour!

One afternoon a lawyer was riding in his limousine when he saw two men along the roadside eating grass.
Disturbed, he ordered his driver to stop and he got out to investigate.
He asked one man, 'Why are you eating grass?'
'We don't have any money for food,' the poor

man replied. 'We have to eat grass.'
'Well, then, you can come with me to my house and I'll feed you,' the lawyer said.
'But sir, I have a wife and two children with me. They are over there, under that tree.'
'Bring them along,' the lawyer replied.
Turning to the other poor man he stated, 'You come with us, also..'
The second man, in a pitiful voice, then said, 'But Sir, I also have a wife and SIX children with me!'
'Bring them all, as well,' the lawyer answered
They all entered the car, which was no easy task, even for a car as large as the limousine was.
Once underway, one of the poor fellows turned to the lawyer and said, 'Sir, you are too kind.'
'Thank you for taking all of us with you.'
The lawyer replied, 'Glad to do it.
You'll really love my place..

The grass is almost a foot high.'

What do you think now, was he too kind or too exploitant?!!!!

Tuesday 19 July 2011

Mzaha kwa Tanesco!

Utani mwingine bwana.....

Ati kwa sababu nyaya za umeme za Tanzania hazipitishi umeme kwa sababu ya mgao, kwa hiyo kwa sasa hazina la kufanya zaidi ya kujitafutia michezo ili kupitisha muda zikishirikiana na nguzo.

Mojawapo ya michezo inazofanya ambayo ni ya kitoto ni kuruka kamba kama unavyoona katika opicha hiyo hapo juu :-)

Monday 18 July 2011

Give Your Week a Smile

Smile is just a smile. It always increase facial beauties!
It also make your life more meaningful!

Photo from FPs

Japan Beats USA to clinch 2011 Women World Cup

Few minutes ago, USA has proven that today they were not in better shape to score through penalties after missing 3 out of 4 penalty shots and lost the game to Japan who scored 3 out of 4 penalty shots. Therefore Japan were crowned the Queens of 2011 FIFA women world cup winners after winning the final game by penalties 3 - 1 against USA.

Japanese player, Kumagai was the scorer of the winning goal after beating USA goalie Solo.

Up to the end of regular time, the score was 1 - 1, at extra time Japan equalise for the second time in dying minutes of  this period forcing the game winners to be decided by penalties.

Awards given to individual players

Best player Solo - USA
Best Goalie Solo -USA
Golden boot - Sawa - Japan
Golden ball Sawa - Japan

Friday 15 July 2011

Nice Weekend

I have nothing to write... Just wishes you a nice weekend!

Thursday 14 July 2011

Rostam Aziz Kujiuzulu Ubunge na Ujumbe wa NEC: Hotuba Kamili


Rostam Aziz, ambaye ni mbunge wa Igunga, au aliyekuwa mbunge wa Igunga kama amekubaliwa kujiuzulu, jana kwnye muda wa saa 7 mchana alitangaza kujiuzulu nafasi zake zote za kisiasa alizozipata akiwa ndani ya CCM na kubakia kuwa mwanachama wa kawaida.
Alitaja sababu nyingi lakini kubwa ni kuwa amechoka na siasa za uchwara na tuhuma zisizo na ushahidi ambazo zimekuwa zikielekezwa kwake kwa muda mrefu. 
  
Hotuba yake kamili inapatikana hapa 
Mbali ya kutoa sababu hizo, alijivunia mafanikio aliyoyapata kwa kipindi cha miaka 18 aliyokuwa mbunge, mara baada ya kushinda uchaguzi mdogo kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa Igunga Charles Kabeho. 
  
Kuna mabo kadhaa wa kadha yaliyojitokeza katika mkutano huo aliouita wa kuongea na wazee wa Igunga.

Kwangu naona kama alichelewa mno kutoa uamuzi huu, na hivyo kuendelea kupakwa madongo kwa tuhuma mbalimbali alizohusishwa nazo ikiwamo ya kampuni ya kufua umeme ya Richmond na baadaye Dowans (ambayo ilikuwa inasemekana ilikuwa ikitumia anuani ya posta na abarua pepe ya huyu mheshimiwa mstaafu), na pia kuna nyaraka mbalimbali za mawasiliano kati ya Tanesco na Dowans ambazo zilikuwa zinalitaja jina lake katika masuala ya makubaliano katika mktaba tata uliowekwa kati ta ya Tanesco na Dowans. 
  
Ingekuwa busara mheshimiwa huyu angechukua uamuzi wa uwajibikaji kama alivyofanya aliyekuwa mkuu wa IMF au Mzee Mwinyi wakati ule alipokuwa waziri wa mambo ya ndani. 
 
Nina matumaini mwenyekiti wake atakubaliana na uamuzi wa kada huyu ili kujenga imani kwa serikali yake kuwa ni sikivu na inayowajibika kisheria kwa sasa. 
  
Mengi tunawaachia wanasiasa na wanachi waamue....

Wednesday 13 July 2011

Wonders of the World. Parasitic Twin Removed in India


Eight year old Deepak Kumar Paswaan from India will finally have a normal childhood after his “parasitic twin” has been surgically removed. The boy who became known around the world by the nickname “octopus-boy” was born with partially developed legs and arms of his undeveloped twin growing from his chest.  
  
The boy was stigmatized for eight years; by some he was perceived as an incarnation of God, while others thought of him as the devil in the human body. 
   
In order to allow the boy to have a normal life, four-hour operation of removing his undeveloped twin was performed in a hospital Fortis, the Indian city of Bangalore in June this year and boy is recovering successfully and begins to live a normal life.


The boy first appeared in the media in February when the shares started collecting money for an operation that would remove the extra limbs of a boy. 
 
“I’m tired of it to be different from other kids, I just want to live normally,” said Deepak after surgery.







Tuesday 12 July 2011

Mabango Mengine Yanapotosha Maana

   

Kwa kawaida huwa napenda kusoma matangazo na mabango ya biashara yanayobandikwa sehemu ambapo yanaitaji kusomwa. 
Wakati nilipokuwa naliangalia bango lenye tangazo la uvuvi haramu wa kutumia baruti hilo sehemu ya kivuko upande wa Kigamboni, kwani ndilo linalowapokea watu wanaoshuuka katika pantoni nilijikuta najiuliza kama kweli bado ninakikumbuka kiswahili sawasawa. 
  
Nilivyofahamu mimi ni kuwa maandishi mekundu ni kwa kiswahili na ya kijani ni kwa kiingereza, lakini nilipojaribu kutafsiri mwenyewe kila mahali nilijikuta nagonga mwamba. 
  
Hata hilo neno kizazikijazcho sikulielewa, nahisi walitaka kuandika kizazi kijacho, nina wasiwasi hata walioandaa bango hilo walitoa oda maalumu kutoka "China" 
  
Bado najiuliza... hatuna watu wa kuhakiki kinachoandikwa, au wote wamesoma sekondari za kata maarufu kama sekondari za maamuzi magumu!

Sunday 10 July 2011

Yanga Mabingwa wa Cecafa Kagame Cup 2011


Wachezaji wa Yanga wakifurahia ushindi huku wakiwa gizani

Mashabikiwa Yanga wakiwa na furaha baada ya kupata goli

Mashabikiwa Simba wakiwa katika huzuni
 Timu ya mpira wa miguu ya Yanga kutoka Dar es Salaam, Tanzania, imefanikiwa kutwaa ubingwa wa klabu za mpira wa miguu kutoka ukanda wa Afrika Mashariki ambao mwaka huu ulipewa jina la Cecafa Kagame Casttle Cup baada ya kuwalaza wapinzani wao wa jadi Simba SC ya Dar es Salaam pia.
Mpira wa leo ulikuwa mzuri kwa timu zote ukilinganisha na mechi za timu zote mbili wakati zilipocheza nusu fainali, na kila moja kufanikiwa kuingia fainal baada ya kuzitoa timu pinzani zao kwa mikwaju ya penati.
Yanga imepata ushindi wa bao 1 - 0 dhidi ya Simba, bao hili lilifungwa kwa kichwa na mchezajiwa kimataifa kutoka Ghana, Kenneth Asamoah.
Mbali na uzuri wa mechi hii, dosari haikukosekana pale wakati wachezaji wakipewa medali zao, kabla mabingwa wa mwaka huu kupanda jukwaani, umeme ulizimika uwanjani kukawa na giza kabisa, na haukuweza kuwashwa tena. Medali za Yanga zilitolewa kwa msaada wa taa za gari la wagonjwa (Ambulance) ambalo lililazimika kusogea karibu na jukwaa la zawadi ili mgeni rasmi katika pambano hilo atoe medali za dhahabu kwa mabingwa hao wapya wa Cecafa.

Dosari nyingine ilikuwa ni mwandishi wa habari aliyekuwa amevaa fulana ya njano kutimuliwa na polisi asikae karibu na mashabiki wa Simba, na mashabiki wa Yanga walijibu mapigo kwa kuwatimua wahudumu wa msalaba mwekundu waliokuwa wamekaa karibu nao, kwani mavazi yao huwa na rangi nyekendu na nyeupe, ambazo ndizo rangi za klabu ya Simba. Hali hii ikiendelea ni hatari!
Kocha wa Simba Basena alipohojiwa na Supersport, alidai anasikitika kwa timu yake kufungwa na Timu ya kawaida, hii inaashiria ya kuwa Timu ya Simba iliingia kwa kujiamini sana, na matokeo yake ilizidiwa na mwisho kupoteza mchezo.

Picha kutoka Mtaa kwa Mtaa

Friday 8 July 2011

Lovely Weekend!

Life goes on......

Wish you a lovely weekend

Wednesday 6 July 2011

Interesting Attempted Prison Break

A woman was caught trying to smuggle her husband out of a Mexican prison in a suitcase........

Maria del Mar Arjona, 19, was stopped after the guards at the jail in Chetumal saw her acting nervously and struggling with the heavy suitcase on wheels.
They opened the bag and found her husband Edwin Valdemar Artiaga Perez inside - wearing only socks and pants.
The husband was returned to his cell after last week's jailbreak attempt.

Source: B B C