Member of EVRS

Tuesday 29 May 2012

Vurugu za Zanzibar!

Huu Mgogoro au vurugu za Zanzibar ni kweli unahusu kudai majadiliano ya muungano au una malengo tofauti?  
Sijaelewa kwa nini zinazoshambuliwa zaidi ni taasis za kidini!
  
Nawaza kwa maandishi tu.  
 
Nawatakia Jumanne njema

Monday 28 May 2012

Pale Unapokutana na Mtu Usiyemtarajia!

Wiki hii nilipata mwaliko maalumu wa chakula cha usiku kutoka kwa mtu ambaye hatufahamiani.
Habari hizi nililetewa na mtu ambaye tumekwisha fanya kazi pamoja kama mara 3 hivi katika kituo cha kulelea watoto yatima na wenye ulemavu ikiwa ni pamoja na wenye mtindio wa ubongo.  
  
Katika kituo hiki cha kulelea watoto yatima, nilikataa kupokea malipo yoyote kutoka kwa huyu mtu aliyeniomba nije kuwapima watoto hao na kutoa ushauri wa kitaalam. Niliamua kufanya kazi ya ujuzi wangu kwa kujitolea kutokana na mguso nilioupata baada ya kuwaona watoto wenyewe, kwani hapo awali sikudokezwa ya kuwa kuna watoto wenye ulemavu na wengine wana mtindio wa ubongo.
  
Historia niliyoipata ya mahangaiko aliyopata mtu huyu labda nimuite msamaria mwema, alijitahidi kutafuta wataalamu kwa miezi zaidi ya mitatu na walikuwa wanatoa miadi ya kuja lakini baadaye wanajitoa kwa sababu mbalimbali. Kama alivyoniambia, jiwe lake la mwisho ndio hilo alilonirushia mimi, na hakutegemea kama angepata mtu kwani alikuwa anahitaji watoto waonwe kabla ya mwisho wa mwezi huu ili kuagiza chochote kitakachowasaidia.
  
Kwangu bila kujua historia hiyo, aliponipigia simu baada ya kupata taarifa zangu kupitia ofisi za ubalozi wa Marekani hapa Kigali, nilimpa siku ya kwenda kuwaona kwani nilikuwa nina ratiba ngumu sana kwa wiki hiyo. Ilibidi nivunje ratiba yangu ya kazi kwa muda japo kwa shingo upande. Siku na saa niliyoahidi nilifika kwa muda tuliopanga hata yeye hakuwa na imani ya kwamba nitafika kutokana na uzoefu alioupata hapo awali.

Kuhusu mwaliko wa chakula cha usiku, ambao ulifanyika Jumamosi tarehe 26 May 2012 .....Nilikubali kufika kwenye hoteli ambapo nilijulishwa kuwa wameandaa meza maalum kwani ilitolewa oda maalum tangu asubuhi kwa ajili ya chakula hicho. Nilikutana na mtu huyo ambaye ni Mzungu na raia wa Marekani. Alikuja na mkewe ambaye ndio yule nilikutana naye kwenye shughuli ya kuona watoto.
Mwenyeji wangu na mkewe walionekana waungwana sana na wenye heshima. Hata walivyonipokea walionyesha kujali na kuwa waungwana, sikuwa nimezoea hali hii ya kuongozwa na kufunguliwa milango nk.  Pia, wahudumu kuwepo muda wote na kubadili hiki na kile, kama vile tupo kwenye dhifa fulani, kumbe tupo watatu tu! 
  
Tuliongea mambo mengi ya binafsi na maisha yetu hapa Rwanda. Tuligusia kidogo mambo ya uchumi na siasa. Siku ilikuwa nzuri na chakula kizuri pia.


Baadaye nilifahamishwa ya kuwa mwenyeji wangu alikuwa ni mwakilishi mkaazi wa Shirika la Fedha Duniani (IMF) nchini Rwanda! Na alipata habari zangu akapenda kukutana nami kwa ajili ya mazungumzo ya kawaida na kufahamiana. Japo mimi sina taaluma na mambo ya fedha wala uchumi, na shughuli zangu hazihusu masuala hayo. …… Bado ninatafakari ….. kwa nini alipenda kukutana nami, wakati shughuli zilizonikutanisha na watu wengine, taasisi yake haishughuliki moja kwa moja katika uendeshaji wake. 
  
Nimependa tu kuwasiliana nawe msomaji, ujue ya kuwa kuitika wito ni bora, japo unaweza kuichuja habari ulioitiwa au kuikataa.  

Friday 25 May 2012

Jihadhari na Bidhaa Kutoka China

Kwa siku nyingi kumekuwa na malalamiko kutoka nchi zinazoendelea kuhusiana na uduni wa bidhaa kutoka China. 
Serikali ya China ilikuwa inajitetea na kusema inaudha bidhaa zake kutokana na mahitaji ya wateja, maana yake nchi zinazoendelea zilikuwa zina agiza bidhaa za bei nafuu lakini zikiwa na ubora duni. 
Serikali ya Tanzania kupitia mamlaka zake, ilikuwa inazikamata bidhaa bandia na kuziteketeza. Jitihada hizi hazijaweza kuzimaliza bidhaa bandia au feki au zenye ubora wa hali ya chini.  
   
Wiki iliyopita, Serikali ya Marekani ililaumu China kwa kuiuzia vifaa vya ndege za kivita ambavyo takribani asilimia 60 ya vifaa vilivyotumika kutengeneza ndege za kijeshi, vilikuja kugundulika kuwa vilikuwa chini ya kiwango.  
 
Uchunguzi uliofanyika na taasisi za Marekani kwenye bidhaa nyingine zilizoingizwa nchini humo zikiwamo nguo, baiskeli nk umebaini ya kuwa bado wanatengeneza na kuzipeleka bidhaa bandia zenye ubora hafifu wakati mwingine kwa asilimia 90 ya bidhaa zote wanazoziingiza Marekani, japo wanabandika alama au lebo sahihi. Watu wamejikuta wakinunua lebo sahihi huku bidhaa ikiwa bandia.
  
Baadhi ya taasisi zimeshindwa kuyafunga maduka au kuteketeza bidhaa zilizouziwa bidhaa bandia kutoka China kwani wanahofia kuwa kuna mamilioni ya watu watapoteza ajira wakati kuna kiu kubwa ya ajira kwa watu wengi! 
  
Habari zipo nyingi, lakini unaweza kusoma mojawapo hapa

Sunday 20 May 2012

Chelsea: New European Champions - 2012

Drogba was the man of the day for Chelsea. 
He scored an equiliser goal in 88th minute and send the match into extra time. 
  
He gave penalty to Bayern Munich during the extra time while he was trying to defend the goal. But Arjen Robben spot kick was denied by Chelsea goal-keeper Cech. 
  
He scored the the last penalt kick which earn Chelsea the European Champion trophy for the first time in their history. They beat Bayern Munich by 4 - 3 penalties.

Some statistics:             Bayern Munich   vs    Chelsea
Total Shots                           34                        9
Corners                                20                        1
Fouls committed                   11                       26

 
Congratulations Chelsea!

Sunday 13 May 2012

Simba yatolewa Na Al Ahly Shandy kwa Penati 9 - 8



Mabingwa wa mpira wa Miguu Tanzania Simba ya Dar es salaam, usiku wa tarehe 13 May 2012 imeyaaga mashindano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika baada ya kufungwa magoli 3 - 0 na Al-Ahly Shandy ya Sudan kwenye muda wa kawaida. 
  
Magoli yote hayo yalifungwa katika kipindi cha pili, la kwanza likiwa dakika ya kwanza kipindi cha pili, yakifuatiwa na jingine dakika 3 baadaye. La tatu lilifungwa baada ya dakika 10 baada ya goli la pili kwa uzembe wa Victor Costa kwa kutokuwa makini na utoaji wa pasi na hivyo kupoteza mpira huo uliomfikia mchezaji wa Al-Ahly Shandy aliyefunga kwa urahisi. Mwisho wa dakika 90 mabao yalikuwa 3 - 0 dhidi ya Simba, na hivyo kufanya kuwe na jumla ya mabao 3 - 3.  
     
Mshindi alipatikana kwa njia ya penati ambapo jumla ya penati 10 zilipigwa. Juma Kaseja alishindwa kufunga penati ya mwisho kwa Simba na hivyo kuzidiwa bao moja na Al-Ahly Shandy 
  
Simba wanatarajiwa kurudi Dar es Salaam Jumatatu, ili waanze kuganga mashindano mengine.

Man City Made it ... Since 1968


English Premier league 2011/12 season has ended with a dramatic win for Man City over QPR after being trailling by 2 - 1 until the injury time. The heroes were Dzeko and Aguero who scored two vital goals on stoppage time to lift up Man City to the top spot of English Premier League.

It was a great moment for Man City fans who had been seated on hot coal throughout the game.

Manchester United came second after the narrow win 1 - 0 over Sunderland, just beaten by goal difference with arch-rival and Premier Champions, Manchester city. Arsenal came out third when they won against West Bromwich Albion by 3 - 2 goals, and Tottenham clinch the last post for Champions League

Both Arsenal and Manchester united have a good record for Champions League qualiffication. However, for this year they both finished without any title.

Wednesday 9 May 2012

Wakuu wapya wa Wilaya Tanzania Bara

Ifuatayo ndio orodha ya wakuu wapya wa wilaya Tanzania Bara kama walvyiotajwa leo na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Idadi ya wakuu wa wilaya walioachwa ni 51.

Wakuu wa wilaya wapya na sehemu walizopangiwa ni:-


1. Novatus Makunga - Hai

2. Mboni M. Mgaza - Mkinga

3. Hanifa M. Selungu - Sikonge

4. Christine S. Mndeme - Hanang

5. Shaibu I. Ndemanga - Mwanga

6. Chrispin T. Meela - Rungwe

7. Dr. Nasoro Ali Hamidi - Lindi

8. Farida S. Mgomi - Masasi

9. Jeremba D. Munasa - Arumeru

10. Majid Hemed Mwanga - Lushoto

11 Mrisho Gambo - Korogwe

12. Elias C. J. Tarimo - Kilosa

13. Alfred E. Msovella - Kiteto

14. Dkt. Leticia M. Warioba - Iringa

15. Dkt. Michael Yunia Kadeghe - Mbozi

16. Mrs. Karen Yunus - Sengerema

17. Hassan E. Masala - Kilombero

18. Bituni A. Msangi - Nzega

19. Ephraem Mfingi Mmbaga - Liwale

20. Antony J. Mtaka - Mvomero

21. Herman Clement Kapufi - Same

22. Magareth Esther Malenga - Kyela

23. Chande Bakari Nalicho - Tunduru

24. Fatuma H. Toufiq - Manyoni

25. Seleman Liwowa - Kilindi

26. Josephine R. Matiro - Makete

27. Gerald J. Guninita - Kilolo

28. Senyi S. Ngaga - Mbinga

29. Mary Tesha - Ukerewe

30. Rodrick Mpogolo - Chato

31. Christopher Magala - Newala

32. Paza T. Mwamlima - Mpanda

33. Richard Mbeho - Biharamulo

34. Jacqueline Liana - Magu

35. Joshua Mirumbe - Bunda

36. Constantine J. Kanyasu - Ngara

37. Yahya E. Nawanda - Iramba

38. Ulega H. Abadallah - Kilwa

39. Paul Mzindakaya - Busega (mpya)

40. Festo Kiswaga - Nanyumbu

41. Wilman Kapenjama Ndile - Mtwara

42. Joseph Joseph Mkirikiti - Songea

43. Ponsiano Nyami - Tandahimba

44. Elibariki Immanuel Kingu - Kisarawe

45. Suleiman O. Kumchaya - Tabora

46. Dkt. Charles O. F. Mlingwa - Siha

47. Manju Msambya - Ikungi (mpya)

48. Omar S. Kwaangw’ - Kondoa

49. Venance M. Mwamoto - Kibondo

50. Benson Mpesya - Kahama

51. Daudi Felix Ntibenda - Karatu

52. Ramadhani A. Maneno - Kigoma

53. Sauda S. Mtondoo - Rufiji

54. Gulamhusein Kifu - Mbarali

55. Esterina Kilasi - Wanging’ombe (mpya)

56. Subira Mgalu - Muheza

57. Martha Umbula - Kongwa

58. Rosemary Kirigini - Meatu

59. Agness Hokororo - Ruangwa

60. Regina Chonjo - Nachingwea

61. Ahmed R. Kipozi - Bagamoyo

62. Wilson Elisha Nkhambaku - Kishapu

63. Amani K. Mwenegoha - Bukombe

64. Hafsa M. Mtasiwa - Pangani

65. Rosemary Staki Senyamule - Ileje

66. Selemani Mzee Selemani - Kwimba

67. Lt. Col. Ngemela Lubinga - Mlele (Mpya)

68. Iddi Kimanta - Nkasi

69. Muhingo Rweyemamu - Handeni

70. Lucy Mayenga - Uyui

Tuesday 8 May 2012

Makinda: Tanzania Haijawa Tayari Kuridhia Kuondolewa kwa Masharti ya Uhamiaji EAC

Mkutano wa viongozi wa mabunge (National assembly speakers) ya nchi zinazounda Jumuiya ya Afrika Mashariki wanaokutana jijini Kigali, Rwanda walikuwa na mjadala mkali unaohusu kufungulia mipaka na kelegeza masharti ya uhamiaji kati ya nchi wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki.

Habari zinadai ya kuwa mashambulizi mengi yalielekezwa kwa Tanzania kwani bado haijaridhia kufungulia mipaka yake kama nchi nyingine zinavyopenda kuharakisha mkataba huu.
   
Spika wa Bunge la Tanzania, Anne Makinda alisema kwa sasa Tanzania haipo tayari kufanya hivyo kwa kuwa wananchi wa Tanzania wanatakiwa kuulizwa kwanza kama wapo tayari kufanya hivyo ukizingatia ina idadi kubwa ya watu kuliko nchi zote za Afrika Mashariki. Pia aliongeza kusema ya kuwa kumekuwa na wahamiaji haramu wengi wanaoingia Tanzania kutoka nchi mbalimbali hata zilizo nje ya Afrika mashariki ambao huleta vitendo vya uhalifu na uvunjifu wa amani ndani ya Tanzania. Kwa hiyo kuna haja ya kudhibiti hilo kwanza. 
  
Kingine alichoongeza Mama Makinda, ni kuwa Tanzania haina vitambulisho vya taifa, na kwa sasa iko kwenye mpango wa kuvitoa kwa wananchi, na hatarajii zoezi hilo litakwisha mapema, labda litachukua zaidi ya miaka miwili kutoka sasa.

Monday 7 May 2012

Ujumbe Mahsusi Kwa Rais .......

Wananchi wa Uganda wamechoka kupiga kelele kwa maneno.
Sasa wameamua kufanya kwa vitendo!

Sunday 6 May 2012

Yanga Yawapa Ujiko Simba

Pazia la ligi kuu ya Tanzania limemalizika leo.  
   
Moja ya mechi iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu na wapenzi wa soka ilikuwa ni kati ya Bingwa mpya wa msimu 2011/12 Simba ya Dar es Salaam na mabingwa waliopita wa msimu wa 2010/11 Yanga ya Dar es Salaam pia. 
   
Mpira ulipoisha, Yanga walikuwa wamefungwa mabao 5 - 0, huku magoli 3 yakiwa yamefungwa kwa adhabu za penati!  
   
Hivyo Yanga wamemaliza msimu kwa kuwapa ujiko na sifa timu ya Simba ambapo timu zitakazokuja kucheza na Simba zitakuwa zinatishiwa na ushindi huu wa kufungia ligi kuu ya Tanzania Bara.

Saturday 5 May 2012

Tanzania: Baraza Jipya la Mawaziri, May 2012

MAWAZIRI
1. OFISI YA RAIS

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu)
Ndugu Stephen M. Wasira  
   
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Utawala Bora)
Ndugu George Mkuchika  
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (UTUMISHI)
Ndugu Celina Kombani  
  
2. OFISI YA MAKAMU WA RAIS
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MUUNGANO) 
   Ndugu Samia H. Suluhu  
     
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MAZINGIRA)
Dr. Terezya P.L. Huvisa  
  
3. OFISI YA WAZIRI MKUU  
  
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji)
Ndugu Mary M. Nagu 
   
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Hawa Ghasia  
  
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge)
Ndugu William V. Lukuvi  
  
4. WIZARA 
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Ndugu Samuel J. Sitta
   
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
Ndugu Shamsi Vuai Nahodha  
   
Waziri wa Ujenzi  
Dr. John P. Magufuli 
  
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
Dr. Hussein A.H. Mwinyi 
   
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi 
Dr. Shukuru J. Kawambwa 
   
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto  
Ndugu Sophia M. Simba  
  
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Bernard K. Membe  
   
Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Mathias M. Chikawe  
  
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Emmanuel Nchimbi  
   
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Dr. David M. David 
   
Waziri wa Kazi na Ajira
Ndugu Gaudentia M. Kabaka 
   
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Prof. Makame M. Mbarawa 
    
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
Prof. Anna K. Tibaijuka  
 
Waziri wa Maji 
Prof. Jumanne Maghembe 
  
Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum 
Prof. Mark Mwandosya  
   
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
Eng. Christopher Chiza  
   
Waziri wa Uchukuzi
Dr. Harrison Mwakyembe  
    
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Dr. Fenella E. Mukangara 
       
Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Khamis Kagasheki 
  
Waziri wa Viwanda na Biashara
Dr. Abdallah O. Kigoda 
  
Waziri wa Fedha
Dr. William Mgimwa 
  
Waziri wa Nishati na Madini
Prof. Sospeter Muhongo  
  
5. MANAIBU WAZIRI
I. OFISI YA MAKAMU WA RAIS
  
Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais
Ndugu Charles Kitwanga  

II. OFISI YA WAZIRI MKUU

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Majaliwa K. Majaliwa
   
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Aggrey Mwanry 
  
III. WIZARA MBALIMBALI 
  
Naibu Waziri wa Kazi na Ajira
Dr. Makongoro M. Mahanga 
   
Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
Ndugu Adam Malima  
   
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Pereira A. Silima  
   
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara
Ndugu Gregory G. Teu  
   
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Ndugu Benedict N. Ole-Nangoro
  
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Mahadhi J. Maalim  
   
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,
Ndugu Goodluck J. Ole-Medeye  
  
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Ndugu Ummy A. Mwalimu 
   
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Ndugu Philipo A. Mulugo
  
Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dr. Abdulla Juma Abdulla  
  
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Lazaro Nyalandu  
   
Naibu Waziri wa Ujenzi
Ndugu Gerson Lwenge  
    
Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,
Dr. Seif Suleiman Rashid  
    
Naibu Waziri wa Nishati na Madini
Ndugu George Simbachawene  
    
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Ndugu January Makamba   
   
Naibu Waziri wa Uchukuzi
Dr. Charles J. Tizeba  
   
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Ndugu Amos Makala 
  
Naibu Waziri wa Maji
Eng. Dr. Binilith Mahenge 
 
Naibu Waziri Nishati na Madini
Ndugu Stephen Maselle 
 
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Angela Jasmine Kairuki  
  
Naibu Waziri wa Fedha  
Ndugu Janet Mbene 
 
Naibu Waziri wa Fedha
Ndugu Saada Mkuya Salum 

Friday 4 May 2012

Rwanda: Ukatili Bado Unajitokeza Hapa na Pale

Ukatili wa mtu, wakati mwingine upo kwenye damu yake.
Sio lazima iwe kulipiza kisasi.

Kama huyu kijana wa kinyarwanda mwenye umri wa miaka 12 ambaye alirudi nyumbani na kudai apewe chakula, lakini dada yake wa tumbo moja mwenye miaka 10 alimueleza ya kuwa chakula hakijawa tayari.
Huyu kijana kwa hasira zake, akalifuata jembe na kumkata kata dada yake mpaka akafa, hakuishia hapo, akaanza kumkata na mdogo wake wa kiume wa mika 4 na kumjeruhi vibaya kabla hajadhibitiwa.


Msemaji wa polisi, alisema tukio hili linawakumbusha watu ya kuwa wanahitaji kutoa ushauri na nasaha kwa vijana, japo kwa huyu sijaelewa kwa nini alifanya hivi, kwani alizaliwa miaka mingi tu baada ya mauaji ya kimbari!

Katika tukio jingine la ukatili ni la huyu baba asiye na utashi wa kutunza watoto wake, pale alipokodisha muuaji aue watoto wake wawili wa kuzaa tena wakiwa wadogo wa umri wa miaka 6 na 8
Mtu aliyekodishwa kuwaua watoto hao aliahidiwa kupewa kiasi cha faranga za Rwanda 80,000 ambazi ni karibu ya shilingi 200,000 za kitanzania. Muuaji mtarajiwa alikubali kuwaua japo nia yake ilikuwa kuwaokoa kama anavyodai mwenyewe! Kwa hiyo alipopewa kianzio, aliamua kutoa taarifa polisi juu ya tukio hilo ambapo mtuhumiwa alikamatwa.
Baadaye ilikuja kujulikana sbabu ya kutaka kuwaua watoto hao ni Mama wa watoto hao kudai vyombo vya sheria vimshughulikie huyo baba ili atoe fedha za matumizi ya watoto hao na kama hawezi, basi apewe sehemu ya ardhi ili aitumie kuwatunzia watoto hao wawili. Pia ilikuja kujulikana ya kuwa mama wa watoto hao, ni mke mdogo kwa mtuhumiwa huyo!
Huyu jamaa aliona njia nzuri ya kutokuwa muwajibikaji wa kutunza watoto wake ni kuwaua!

Tuesday 1 May 2012

Yaliyo Moyoni mwa JK na Mei Mosi 2012

Mei mosi 2012 ndiyo hiyo inakatika.  

  
Watu walikuwa wanatarajia kusikia neema ya mishahara kuongezwa, na ndio maana katika jiji la Tanga ambapo wafanyakazi walifanya maandamano ya mei mosi walikuwa wamejizatiti kufikisha kiu yao kwa kushika mabango yaliyokuwa na ujumbe wa “Mishahara duni, Mfumuko wa Bei na kupanda kwa gharama za Maisha” ni tatizo kubwa la wafanyakazi. 
 
Rais Kikwete ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi, hakuahidi moja kwa moja ya kuwa mshahara utapanda, bali alitoa ahadi ya kuuboresha kidogo kidogo mpaka lengo litakapofikia, japo haijulikani ni lini. 
  
Mbali ya hayo alizungumzia mjadala mkali ulioibuka mwezi uliopita bungeni juu ya taarifa za ufujaji wa fedha na raslimali za watu. Alieleza ya kuwa huo mjadala aliufurahia sana, kwani uliashiria kuwa wabunge wamekuwa makini katika kutetea mali na raslimali za Tanzania. Alisisitiza ya kuwa ni yeye ndiye aliyeamua taarifa za mkaguzi mkuu wa Serikali awe anaziweka hadharani ili kutoa fursa wabunge wazijadili kwa kina, badala ya mfumo wa zamani ambapo zilikuwa hazpewi muda wa kutosha kipitiwa na kuzijadili wakati zilikuwa na kasoro nyingi. 
  
Pia alionekana kukerwa na wizi na kutowajibika kulikofanywa nabaadhi ya watendaji wa serikali, na pia kusema ya kuwa ameipa nguvu kisheria ofisi ya mkaguzi mkuu wa Serikali kuwafikisha wahalifu wa mali za uma kwenye vyombo vya sheria pale watakapobaini matukio ya wizi hata kama ukaguzi bado unaendelea. 
  
Hakuzungumzia hatua atakazowachukulia mawaziri ambao wametajwa katika taarifa hizo, japo kuna kila dalili ya kuwa atawaondoa kama si kuwafuta kazi kwenye baraza hilo, na pia kuna uwezekano wengine wakashitakiwa kwa makosa ya jinai. 
  
Mfumo madhubuti wa kudhibiti matumizi utaanza na idara za Elimu, Afya na Maji ikiwa ni pamoja na kuweka wazi fedha zitakazokuwa zinatengwa kwa kila idara, na matumizi kutolewa taarifa kwa ngazi zote.
  
Kinachoashiria ya kuwa kuna wengine wanaweza kuwa wamekwishapoteza nyadhifa zao, ni pale mhesh. Omari Nundu alipotambulishwa zaidi ya mara mbili kama Mbunge mwenyeji wa sherehe hizo, na wala hakutajwa kama waziri huku mawaziri na manaibu waziri wengine ambao hawana kashfa walipotajwa kwa nyadhifa zao. 

English Premier League Champion to be Known on the Last Game



The big game between the Manchester Clubs has just ended!

Manchester United today's defeat by 1 - 0 at the hand of Manchester City has left the English premier title open between these two teams. The winner will be known at the closing day of EPL.  The goal for Man City was scored by Kompany in the dying minutes of the first half. 
  
The Manchester City Club has the upper edge to Manchester United just by goal difference, where Man City has an advantage of 8 goals on top of Man United.

Photo from BBC