Member of EVRS

Wednesday 30 November 2011

Mchungaji Arusha Atembezwa Uchi Kwa Kugomea Shughuli za Kimila

Mchungaji mmoja wa kanisa la pentekoste Jijini Arusha na ambaye ni mkazi wa kijiji cha Siwandeti, wilayani Arumeru alikamatwa na kutembezwa uchi baada ya kukataa kuhudhuria kikao cha kimila la kabila la wamasaai kilichohusu mambo ya tohara kwa kuwa aliona hakiendani na imani yake ya kidini.

 
Hatua ya kumtembeza uchi kwa takribani Saa 22 katika vijiji zaidi ya vinne na kuogeshwa kwenye maji ya baridi Saa 11:00 alfajiri kulitokana na yeye kugoma kutekeleza hukumu ya kutoa ng’ombe dume kama adhabu ya kutohudhuria kikao cha mila.
  
Miongoni mwa vijiji alivyotembezwa uchi mchungaji Lukumay ni pamoja na Ngaramtoni, Mringaringa, Kenyaki, Olevelosi, Kiranyi na Elerai. 
  
Habari zaidi kutoka kwenye Mwananchi

Monday 28 November 2011

Ni siku ya Uchaguzi DR Congo na Egypt

Wapinzani wakidhibitiwa na askari wa Congo katika viunga vya jiji la Kinshasa

Leo ni siku ya uchaguzi wa rais na wabunge katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC)
Katika kampeni za kujinadi kwa wagombea, kulikuwa na matukio mengi ya uvunjifu wa amani ambapo polisi walilazimika kutumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya wafuasi wa vyama mbalimbali waliokuwa wanapingana. 
Katika kampeni, lugha mbalimbali zilitumika kama njia ya mawasiliano kutegemea na mahali kampeni za kisiasa zilipokuwa zikifanyaika. Lugha kuu zilizotumika zaidi katika kampeni hizo ni Kilingala, Kifaransa na Kiswahili.  
   
Huu utakuwa ni uchaguzi wa kwanza wa kipekee kwa muda mrefu, kwani gharama za uchaguzi huu zimegharimiwa na nchi ya Kongo yenyewe.


Askari wa Misri karibu na Tahrir square

Wakati huo huo, nchi ya Misri nayo leo inafanya uchaguzi wake wa kuwachagua wabunge wa mabunge mawili ya nchi hiyo.  
Itakumbukwa kwa wiki kadhaa sasa kulikuwa na maandamano ya kuipinga serikali ya Kijeshi inayotawala nchi ya Misri baada ya kiongozi wake wa siku nyingi, Hosni Mubarak kuachia madaraka kufuatia shinikizo la wananchi kumtaka kuondoka madarakani, ambapo alitii baada ya vurugu kubwa kuzidi nje ya uwezo wa utawala wake.  
  
Pia kwa Misri, uchaguzi huu unahesabika kuwa wa uhuru zaidi kwa miaka zaidi 30 iliyopita.
Kulikuwa na matukio ya ucheleweshaji wa makaratasi ya kupigia kura kwenye vituo kadhaa vya Cairo na Alexandria.  
  
Tunawaombea wamalize uchaguzi kwa amani ili waweze kizijenga nchi zao.

DRC Photo from The Telegraph
Egypt photo from Guardian

Wednesday 23 November 2011

Uhamasishaji wa Kujikinga na Ukimwi


Mipira 80,000 ya kinga ya kiume ikiwa imening'nizwa Paris ikiwa ni kuhamasisha kujikinga na janga la UKIMWI.

Picha kutoka TravelNews

Tuesday 22 November 2011

Road slides Towards Sea After Heavy Rainfall


Landslide occured near Los Angeles, CA after heavy downpours over last sunday 20th Nov 2011.
Na casualties were reported to this natural disaster which occured along the coastal road.

Read more here

Monday 21 November 2011

Ugonjwa wa Katiba Mpya Tanzania:Unatibiwa kwa Kidonge cha Rangi Mbili

Siku chache zimepita baada ya Bunge la Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kuridhia muswada wa sheria utakaongoza na kuratibu jinsi ya kukusanya maoni ya katiba mpya. Japo wabunge wa Upinzani kwa idadi kubwa waliususia kabisa kwa kile kinachodaiwa kuletwa na kusomwa huku vipengele kadhaa vya sheria vikiwa vimevunjwa.  
  
Muswada ndio umeshapita, na rais Kikwete alithibitisha pale alipokuwa akiongea na "wazee wa Darisalama" japo kuna wengine hata mimi nilikuwa nawazidi umri japo sina sifa kamili ya kuitwa Mzee, nao walikuwa humo ati kama wazee! Mhesh. Rais aliahidi kuuwekea sahihi muswada uliopitishwa na wabunge (ambao kwa karibu asilimia 80 ya michango yao walikuwa nje kabisa ya muswada wenyewe), ili uwe sheria rasmi na kuanza kutumika mara moja. 
Pia aliwaagiza wabunge wa CCM mara alipokutana nao baada ya kikao cha bunge kilichoupitisha muswada huo kuwahi majimboni kwenda kueleza ujio wa neema na kiu ya katiba mpya kwa wananchi wanaowawakilisha.  
  
Hali hii ilichafuliwa na taarifa ya kamati teule ya bunge iliyoundwa kumchunguza David Jairo (ama vijana wanavyomuita DJ) kuwasilisha taarifa yao ambayo ilikuwa inachafua maana ya maadili ya kiuongozi. Kuna mapendekezo mengi tu yalitolewa ikiwa ni pamoja na kuchukuliwa hatua za kinidhamu ikijumuisha wote waliotajwa kwa makosa ikiwa ni pamoja na waziri Ngeleja akidaiwa alipewa takrima ya sh. 4M ambazo ni kinyume na matumizi ya fedha za uma. 
 
Nahisi wabunge wengi wa CCM watakuwa na wakati mgumu kwenda kuiuza rasimu ya katiba itakayokuja, na mijadala itahamia kwenye pengo la uadilifu lililo onyeshwa na baadhi ya watendaji wa serikali tawala na kuwa kigezo cha kukataa vifungu vitakavyoletwa.
Kuna viashiria ambata kwa sasa kuwa mwaka 2015 utakuwa mgumu sana kwa serikali iliyopo madarakani kukubalika, labda kama kutakuwa na kipengele cha kuchomeka serikali ya umoja wa kitaifa au yaje mabadiliko makubwa sana yatakayofanyika sasa kubadili fikra za watu wanaotaka mabadiliko ya kisiasa kwa mazuri au la, yaani, people they just want a change...   
  
Kuna taarifa zisizo rasmi kwamba katibu mkuu kiongozi anatarajiwa kustaafu mwishoni mwa mwezi ujao mwaka huu, labda itakuwa ni fursa ya kuachia ngazi bila kupoteza haki zake za muda aliolitumikia Taifa, kwa wale mtakaotaka kusema muda Taifa lililomtumikia ni nyie, na wala sio mimi. 
  
Watendaji wengine wa wizara ya nishati na madini inasemekana wameanza kujiandaa kukaa benchi, na pia mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali naye inawezekana hajui nini kitafuata hasa baada ya kumsafisha DJ na baadaye kuonekana kama taarifa yake aliiandikia kwenye kituo cha daladala bila kupitia hesabu kamili ili kubaini kasoro. Pia kuna wingu la shaka kwa sasa liko juu yake kuhusu utendaji wake wa kazi, japo anasifika kwa umakini wa kwenye hesabu za halmashauri za miji na wilaya. 
  
Tunachosubiri ni Kitendawili au bomu?!!

Don' Need a Bridge!

Cheers ha ha haa

Thursday 17 November 2011

Mchakato wa Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba Mpya ya Tanzania

Nimenukuu:
Maoni ya Dk. Faustine Ndugulile (Mbunge wa Kigamboni) kuhusu mchakato na muswada wa sheria ya mabadiliko ya Katiba mpya

Nchi yetu inatimiza miaka tarehe 9.12.2011. Kwa hiyo mjadala wa kufanya mapitio ya katiba yetu umekuja muda muafaka kwa taifa hili. Ni muda mrefu umepita na hivyo ni jambo jema kutafakari tulipotoka kama Taifa, tulipo na tuendako.

Tumekuwa na katiba ya mwaka 1977 ambayo imekuwa ikutuongoza hadi hivi sasa, lakini kama taifa tumeamua kuanza mchakato utakaopelekea kuwepo na katiba mpya itakayodumu vizazi na vizazi vijavyo.

Nashukuru kuwa sehemu ya mchakato wa kupitia muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba ambayo itaongoza mchakato mzima wa kupata katiba mpya.

Kwa babati mbaya sana muswada huu umezua mjadala mkubwa ndani na nje ya Bunge. Baadhi ya wananchi, wanaharakati na wanasiasa wanataka muswada huu usijadiliwe kutokana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kupinga uwasilishwaji kwa mara ya pili, wananchi kutopata fursa ya kuchangia na mamlaka ya Rais kwenye mchakato huu.

Ninaungana na watanzania wote wanaotaka katiba mpya. Ninaungana na watanzania wote wanaotaka katiba nzuri na yenye kuweka maslahi yaTaifa mbele na yenye kulinda haki za msingi za Raia wa nchi.

Sasa hizi tofauti zinatoka wapi? Kwanini kumekuwa na mtazamo tofauti katika suala hili?

Jioni ya leo nimejaribu kuwasiliana na watu mbali mbali kupata mawazo na maoni yao kuhusu muswada huu unaoendelea kwa sasa. Nimegundua yafuatayo:
  1. Baadhi ya watu hawana ufahamu mzuri wa kitu gani kinachoendelea kwa sasa. Baadhi ya watu wanafikiri kuwa ndio tumeshaanza kuandika hiyo katiba mpya pasipo kuwashirikisha wananchi.
  2. Uelewa wa nini kilicho ndani ya muswada bado ni mdogo hata kwa wale wasomi.
Vilevile kuna matatizo mengine. Kuna watu ambao kipato chao cha kuendesha maisha kinatokana na mchakato huu wa Katiba Mpya. Watu hawa wanapata fedha nyingi za wafadhili na baadhi yao wanaleta mkanganyiko wa makusudi ili waendelee kushibisha matumbo yao. Wapo wengine wanaouangalia mchakato huu kwa mtazamo wa kiitikadi, kidini, Uzanzibari na Utanzania Bara. Ukichanganya yote hapo juu na upotoshaji unaendelea kwenye mitandao na vyombo vya habari, unakuta suala hili linazidi kuwachanganya wananchi.

Kimsingi kinachofanyika sasa hivi ni kutengeneza sheria itakayoweka utaratibu wa kuandaa katiba mpya. Binafsi nimeisoma mara kadhaa na ninaona inakidhi mahitaji iliyokusidiwa. Nasema hivyo kwa sababu zifuatazo:
  1. Maboresho yanayozingatia hoja zilizotolewa na wadau wengi zimeongezwa kwenye muswada huu. 
  2. Nchi ya Zanzibar ambayo ni wadau wa Muungano wamepata uwakilishi wa kutosha. Raisi wa Tanzania Bara na Raisi wa Zanzibar watashirikiana katika kila hatua ya mchakato wa katiba hii. Hakuna atakayefanya maamuzi ya peke yake.
  3. Madaraka ya Rais yanayolalamikiwa yamepunguzwa sana kwenye muswada huu. Kwanza, Maraisi wote watashirikiana kutoa maamuzi. Pili, hadidu za rejea zimeshainishwa badala ya Raisi kuja na za kwake. Tatu, sifa na vigezo vya wajumbe wa tume zimeshainishwa.Kwa hiyo majukumu ya Raisi ni machache sana na maamuzi mengi yatafanywa na wananchi.
  4. Ushirikishwaji wa wananchi utakuwa ni mkubwa. Nchi nyingine zimeweza kutengeneza katiba kwa kupitia Bunge la Katiba au chakato wa kura za maoni (Referendum). Sisi Tanzania tumeamua kutumia njia zote mbili. Wananchi watashirikishwa kwa kutoa maoni yao kwenye mikutano ya tume inayosimamia mchakato wa katiba mpya, wananchi watashirikishwa kwenye mabaraza ya mapitio ya katiba, wananchi watashirikishwa kwenye Bunge la Katiba, wananchi watashirikishwa kwenye kura za maoni (Referendum).
Kwa mtazamo wangu ni vyema tukakamilisha muswada huu ili kazi kubwa na ya msingi iliyo mbele yetu iweze kuanza. Kuna mambo ya msingi ambayo kama Taifa tungependa kujadili ikiwa ni pamoja na mambo yafuatayo:
  1. Muundo wa Serikali-Tungependa Serikali iwe kubwa kiasi na ya aina gani, masuala ya Serikali ya Mseto (ikiwa chama kinaongoza uchaguzi kikashindwa kupata zaidi ya nusu ya kura zote), mamlaka na madaraka ya Raisi, uthibitishaji wa Bunge kwa viongozi n.k.
  2. Usimamizi na uthibiti wa Rasilmali zetu kama vile ardhi, madini, gesi na kama tutabahatika kupata mafuta. 
  3. Mfumo wa Bunge tunalotaka
  4. Uwakilishi wa wananchi wasio na vyama (Zaidi ya watanzania millioni 30 si wanachama wa vyama vya siasa) na suala la wagombea binafsi 
  5. Masuala ya uwakilishi wa jinsia na makundi maalumu kwenye sehemu za maamuzi
Tutumie muda mwingi katika hatua zinazofuata ili kujadili mambo ya msingi kama nilivyoainisha baadhi yake hapo juu.

Mchakato wa katiba ni mrefu. Niwasihi watanzania wenzangu tujadili kuhusu katiba tunayotaka pasipo kuweka masuala ya udini, maslahi binafsi, itikadi na sehemu ya Jamhuri tunapotoka. Tufanye hivi pasipo kuweka jazba na fujo. Tukifanya hivi tutafika salama. Wanaharakati watumie fursa hii kuwaelimisha wananchi haki zao na pia kuwapa elimu ya kutosha ili waweze kuchangia kwenye mjadala huu. Wanaharakati wasitumie fursa hii kufanya fujo, kuleta vurugu na kupotosha umma.

Mimi binafsi ningependa kuona tunapata katiba yenye maslahi kwa Taifa letu na vizazi vitakavyokuja baadaye. Tuna deni hilo kwao. Hatma ya Taifa hili iko mikononi mwetu. Hekima na busara zinahitajika sana wakati huu. Tutangulize Utaifa kwanza na maslahi ya nchi hii mbele.

Mungu Ibariki Tanzania

Dk. Faustine Ndugulile-Mbunge Kigamboni

15/11/2011

Dr Faustine angependa kupata maoni yako katika suala hili ili kuweza kumjenga kihoja katika kutambua watanzania wanapenda nini katika suala hilo. Kwa mtizamo chanya au hasi.

Saturday 12 November 2011

Short-cut to Heaven!

 Enjoying the siesta!

 Yesterday... was watching the game till dawn!!!
It doesn't cost a thin' here!!

Ha ha haaa

Friday 11 November 2011

Dr. Hemed Abbas Kilima: Ninavyokukumbuka

Sekta ya Afya ya Tanzania imempoteza Mtaalamu aliyebobea katika fani ya macho, Dr Hemed Abbas Kilima (Pichani juu) aliyefariki jana tarehe 10 Nov 2011 kutokana na ajali mbaya ya gari.

Hayati Dr Kilima alikuwa anasafiri kutoka Mbeya kuelekea Dar es Salaam alipopata ajali hiyo pale gari aliyokuwamo ilipogongwa na basi eneo la Al-Jazeera.  
 
Ni habari ya masikitiko kwa wana-taaluma wa afya hususan upande wa macho.  
  
Dr Kilima, mpaka anapoteza uhai wake akiwa bado ni kijana wa miaka 42 tu, alishapata shahada tatu katika fani ya afya zikiwa ni pamoja na:-
  • Shahada ya udaktari wa binadamu kutoka chuo kikuu cha tiba za Afya na sayansi ya Jamii - Muhimbili
  • Shahada ya uzamili katika fani ya macho kutoka chuo kikuu cha Tumaini
  • Shahada ya afya ya jamii kwa macho kutoka London School of hygiene and tropical medicine

Mbali ya hayo, alikuwa ni
  • Daktari bingwa wa magonjwa ya macho kwa watoto (Fellow- Paediatric Ophthalmology) aliyojifunza CCBRT - Dar es Salaam.
  • Fellow wa Eastern Africa college of Ophthalmology
  • Mwenyekiti msaidizi wa chama cha madaktari na wanataaluma wa Macho Tanzania.  
  
Ninamkumbuka Dr Kilima, kwani kwenye kozi ya shahada ya uzamili kwenye fani ya macho (Master of Medicine - Ophthalmology), tulikuwa darasa moja na tulikuwa wawili tu, mimi na yeye, kwa hiyo tulipitia hatua nyingi kimasomo ikiwa ni pamoja na kusoma, kufanya kazi, kufanya tafiti na kujiandaa kwa mitihani. Mbali na hayo tulikuwa tunasafiri sehemu mbalimbali pamoja ndani na nje ya nchi katika kutekeleza majukumu ya fani yetu. 
  
Tulipeana ushauri wa mambo mengi katika masomo na kujiendeleza kitaaluma, na kama tulikuwa tunafuatana katika kisomo na kujiendeleza kama vile mmoja akibandua mguu mwenzie anafuata, na hata nilipomaliza fellowship yangu naye baadaye alijiunga na kozi kama hiyo kwa fani tofauti kidogo tu, na alihitimu vyema mwaka uliopita.  
  
Na pia ndie niliyemuachia mikoba ya Mwenyekiti msaidizi wa Chama cha madaktari na wanataaluma wa afya macho Tanzania kabla sijapata nafasi zaidi katika shirikisho la taaluma hii kwa Ukanda wa Afrika mashariki (Ophthalmological Society of Eastern Africa).  
 
Mpaka anatutoka, alikuwa ni Daktari anayefanya kazi katika hospitali ya rufaa ya Mbeya, na mratibu wa macho kwa kanda ya kusini na nyanda za juu. Hivyo, Taifa limempoteza mtu muhimu ambaye bado alikuwa na muda mrefu wa kuendeleza huduma ya afya na kuwainua wengine. 
 
Binafsi nimempoteza mwenza na mshirika mkubwa kikazi, na pia nimempoteza rafiki wa karibu ambaye nilitarajia kushirikiana naye sana kuweza kuinua fani ya afya ya macho kwa Tanzania. 
  
Bwana alitoa, bwana ametwaa. 
 
Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi, Amen.

Tuesday 8 November 2011

Vote for Mount Kilimanjaro as one of The New 7 Wonders of the World



Mount Kilimanjaro is located in Northern Tanzania, it lies few degree below the equator line.
It is the highest mountain in African continent, the highest point is at Kibo peak which is 5,895 metres above sea level.
It is an amazing mountain because of its location along the tropic, and its peak is covered by snow through out the year. Everything is natural.  
 
Apart from that, the whole of its basement is occupied by wild animals living freely without causing harm to neighbouring villages. 
  
Visiting and climbing this mountain, you will not only reach the highest point in Africa, but also you will enjoy seing ecological diversity and fresh atmosphere which is almost the same all year round. 
  
Few kilometres from Mount Kilimanjaro, you will be able to see the second highest mountain in Tanzania, mount Meru located in Arusha, and if you move further to north west you may get an opportunity to visit Ngorongoro crater, which is one of great wonders of the world filled again with all diversity you may think in the tropics.  
 
Natural beauties of mount Kilimanjaro has attracted me to vote for this mountain to be among the new seven wonders of the world. What about you? Just follow this link and follow instruction to cast your vote for Mount Kilimanjaro by using telephone or online. 
In Tanzania, you can vote through SMS by sending a message to number 15771 from any telephone network.
Sala pekee hazitoshi, piga kura yako tafadhali!
  
The deadline for voting is on 11th Nov 2011 (11.11.11)

Friday 4 November 2011

Man's Facial Image Seen in Ultrasound


A mystical image or sheer coincidence? Either way, that’s one sad ‘nad.
Doctors in Canada were scanning through ultrasound images of a 45-year-old man with a painful mass in his testicles when they did a doubletake. There was a man's face staring up at them, the mouth grimacing as if he were in agony.
"It looked like a man screaming in pain, which I thought was hilarious considering the clinical picture of the poor guy," Dr. G. Gregory Roberts, School of Medicine at Queen's University, Kingston, Ontario, told msnbc.com

Roberts and urologist Dr. Naji J. Touma reported their amazing discovery -- which ranks right up with the grilled cheese Madonna or pancake Jesus -- in a recent issue of the medical journal Urology.
In the article, "The Face of Testicular Pain: A Surprising Ultrasound Finding," the doctors revealed that, upon spotting the distinctive tumor, a "brief debate ensued on whether the image could have been a sign from a deity (perhaps "Min" the Egyptian god of male virility; however, the consensus deemed it a mere coincidental occurrence rather than a divine proclamation."

Click here for full article

Thursday 3 November 2011

Tuesday 1 November 2011

Joseph Machele: Mtanzania Aliyepata Nishani ya Heshima ya Franklin Nchini Mexico

Joseph with assistant of the Ambassador to the US Embassy in Mexico city  Mr.  John Feeley Deputy Chief of Mission.caption

Joseph na Mkewe Mariana

Rafiki na wafanyakazi wenzake Joseph - Ubalozi wa Marekani Mexico
Joseph Machele, Mtanzania ambaye anaishi Mexico city nchini Mexico, amepata tuzo ya heshima ya Franklin (Franklin Award) ambayo hutolewa kila mwaka kwa wananchi wa Marekani au wanaofanya kazi katika idara za serikali ya Marekani ambao mchango wao kwa Taifa la Marekani katika fani mbalimbali za kazi zao umepita kipimo na kuweza kusababisha ufanisi mkubwa wa kazi au kuleta faida kwa uchumi au hali ya usalama kwa Marekani. 

   
Joseph Machele ambaye ni Mtanzania anayefanya kazi katika ubalozi wa Marekani nchini Mexico, ameweza kupata tuzo hiyo kwa utumishi bora na kuwa mbunifu. Allipata siku ya tarehe 12 Oktoba 2011, baada ya kupewa na naibu balozi wa Marekani nchini Mexico Bw. John Feeley.
Kupitia kujituma kwake na maarifa yake binafsi, aliweza kuokoa zaidi ya dola za kimarekani 115,000 kwa mwaka mmoja ambazo zingetumika kulipia gharama za kusafirisha samani na vifaa vya kukodisha na vitu vingine vidogo vidogo kwa ajili ya makazi ya watumishi wageni wanaoenda kufanya kazi kwenye ubalozi wa Marekani nchini Mexico.  
 
Mbali ya Joseph Machele kupata tuzo ya heshima, pia alijipatia kitita cha dola kama zawadi yake katika juhudi zake binafsi akiwa kazini. Alifanikiwa kuokoa kiasi hicho cha fedha kwa kuwashawishi wanaokodisha vifaa hivyo kutoa usafiri wa bure kusafirisha vifaa hivyo, jambo ambalo maafisa wa ubalozi wa Marekani walikuwa wanadhani ni kitu kisichowezekana kabisa. 
  
Hongera sana mdogo wangu Joseph kwa juhudi zako binafsi. Nakufahamu sana tangu kwenye ujana wako, ni mtu ambaye upo makini sana katika kazi zako. Usiishie hapo tu, bali ongeza bidii zaidi kwani mafanikio yako ni sifa kubwa kwetu sote tunaoishi Bara pevu na lenye utajiri mkubwa.