Member of EVRS

Wednesday 29 December 2010

Vacation!

Umh! I am on Christmas and New Year Vacation.

Visiting blog is altered due to here and there travelling.
I will keep posting whenever I get time.

I wish you a Happy New Year 2011

Friday 24 December 2010

Tanesco! Bado Kabisa!


Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) kwa hivi karibuni limeanza kututumka na kutaka kuonyesha kuwa linawajali na kuwaheshimu wateja wake na kuthamini malipo yao kuwa ndio uha wa Tanesco (kwani ndio linawafanya watendaji waweze kwenda haja).
Kumekuwa na vipindi vingi vya kwenye radio na runinga wakijielezea mikakati yao, kujibu maswali ya wasikilizaji na watazamaji na pia kutoa ushauri kwa wenye malalamiko wapi wataweza kusikilizwa.
Hata siku ya tarehe 23 Desemba 2010, waziri wa nishati na madini Mh. Ngeleja akiwa na watendaji wa Tanesco, alikuwa akitoa maelezo na kujibu maswali ya wasikilizaji/watazamaji moja kwa moja (live bila chenga).
Mbali ya juhudi za uongozi wa juu kujaribu kulisafisha shirika hili la ugavi wa umeme, bado watendaji wa ngazi za chini yao, wana roho zilizosheheni kutu, utukutu wa akili au makusudi na kutowajibika.

Kuna sehemu fulani huko manispaa ya Ilala kuna nguzo imeoza na kuegeme ukuta nyumba kwa zaidi ya miaka 3 sasa. Wenye nyumba walishapiga kelele weee mpaka wakamwachia Mungu awalinde hizo nyaya zisijeangukia watu hususan watoto, basi ndio ikawa mauti tena.



Mpita njia waweza kuona nguzo hiyo ikiwa imeegemea ukuta, na kwa hapo chini utaona ule waya unaoshikilia nguzo ikae wima ukiwa umelegea kabisa, kuashiria ya kuwa hauna kazi tena kama ilivyokusudiwa!

Picha hii chini inaonyesha nguzo ikiwa imekwisha kabisa na kugeuka mahali pa ndege kujikinga na jua la Dar es salaam!
Na hii picha juu ndio hali halisi ya nyaya za umeme zikiwa zimeshuka chini kabisa chini ya usawa wa mabati ya nyumba! 

Kinachoshangaza, wiki chache zilizopita, watu wa Tanesco walikuja kumuunganishia umeme mteja mpya, na wakaweka waya kutoka kwenye nguzo hiyo hiyo iliyooza, na walipotaarifiwa kuhusu ubovu wa mlingoti huo, waliuangalia na kusema wanaenda kutoa taarifa ofisini, na kwa sasa inakaribia miezi 2 na hakuna taarifa wala mtu aliyekuja kuona.

Watendaji wa kweli walipotaarifiwa, wakawapa maelekezo walalamikaji mahali pa kwenda na namba za simu, sasa sijui nicheke au... mhusika alipopatikana kwa simu, alisema yupo likizo na akatoa namba nyingine ya mtu ambaye kwa zaidi ya wiki amefunga simu, na watu wakamshauri mlalamikaji ati asubiri sikukuu zipite ndipo akaulizie tena!!!!!

Hivi hizo nyaya za umeme na nguzo zinajua sikukuuu hizo ambazo Tanesco wanasubiri ziishe kwanza!
Na hao wafanyakazi watafungaje line mpya kwenye nguzo wanayoiona imeoza?!
Likitokea janga ... ni nani wa kulaumiwa.
Hakika watendaji wabovu wa Tanesco wanastahili kuongozwa  na mtu kama Stalin :-(

Tuesday 21 December 2010

Hukumu ya BAE SYSTEMS Kutolewa Leo

Hukumu kesi ya shirika kubwa la kuuza silaha la Uingereza (BAE Systems) itatolewa kesho na Jaji Bean anayesikiliza madai ya kampuni hiyo kujihusisha na rushwa kubwa kwa kuiuzia Tanzania radar ya kijeshi ambayo iliigharimu nchi maskini ya Tanzania zaidi pauni za Uingereza milioni 28 ( Zaidi ya sh.billioni 70 za kitanzania)

Hakimu huyo aliihoji kampuni hiyo kuhusu madai ya kumlipa mfanyabiashara Sailesh Vithlani kiasi cha kama pauni millioni 7.7, katika kujitetea kampuni hiyo ilidai ilitoa pesa kumpa Vithlani kwani walimtumia kama papa mdogo kupenyeza ili waweze kushinda zabuni ya kuiuzia Tanzania rada hiyo kwa bei ya kuruka.
Kampuni ilikiri kuwa na kosa dogo la kuweka vizuri kumbukumbu za mahesabu kwa kudai walimlipa Vithlani kama mshauri wa kiufundi wakati Vithlani mwenyewe hakuwa na ujuzi wowote katika masuala hayo ya ununuzi wa rada.

Jaji hakuridhika na maelezo hayo, na akaendelea kusisistiza kuna kila dalili ya rushwa kwani alihoji kwa nini zaidi ya 97% ya malipo ilipitia  kwenye mikono ya Vithlani!, kiasi kwamba alitaka kutoa uamuzi wa kuita mashahidi kueleza ni vipi pesa alizopewa Vithlani zilivyotumika kabla ya kutoa hukumu yake, lakini baadaye alibadili mawazo yake na kuahidi kutoa ya hukumu dhidi ya BAE System leo siku ya Jumanne.
 
Hapo awali, kampuni hii ilikiri kuwa na makosa ya kuweka vibaya kumbukumbu za pesa, na ilikubali kulipa pauni milioni 3 kama fidia kwa Tanzania na pesa hizo kutumika nchini Tanzania kwa ajili ya shughuli za maendeleo. Lakini ikawa inasisitiza haikutoa mlungula wowote.

Pata maelezo zaidi kwa mwanzilishi wa mjadala huu wa uuzwaji wa rada hii kwa bei isiyo na tija

Monday 20 December 2010

WikiLeaks Cable Hit Tanzania

Today I was reading Subi's Wavuti and came accross this astonishing news about radar scam!

Quoted ......The Tanzanian prosecutor, Edward Hoseah, investigating worldwide misconduct by BAE, Britain's biggest arms company, confided to US diplomats that "his life may be in danger"...

Hoseah met a US diplomat, Purnell Delly, in Dar es Salaam in July 2007, and claimed (unrealistically it turned out) he would be able to prosecute guilty individuals in the BAE case. The US cable reports: "He called the deal 'dirty' and said it involved officials from the Ministry of Defence and at least one or two senior level military officers."

Hoseah spoke gloomily about the prospects for Tanzania's anti-corruption struggle and his original hopes to prosecute the "big fish" of corruption.

"He told us point blank... that cases against the prime minister or the president were off the table ..." The cable then details allegations against former leaders and their inner circles, saying they would be "untouchable".................

Today, is the beginning of the case related to BAE fraud on radar scam. More terrible news are going to be revealed out ....

The Guardian (UK) has more astonishing news

Friday 17 December 2010

Enjoy your Weekend!

Hi Guys, I am still with you.
  
But, I wish christmas will be ten weeks ahead, so that this working under pressure to beat the deadlines will be kept out of our mind and order.  
  
I wish you the nice weekend for those who will have the really weekend.

Wednesday 15 December 2010

Homa ya Harusi ya Prince William Yazidi Kupanda

Baadhi ya makampuni ya kutengeneza zawadi yameanza kuchangamkia tenda ya kutengeneza zawadi ya Harusi ya mjukuu wa malkia wa Uingereza Prince William ambaye anatarajjia kufunga ndoa na Kate Midleton mwishoni mwa mwezi Aprili 2011.

Kampuni hizo zipo Uingereza na China.
Wamiliki wameanza kutengeneza vito vya thamani kama pete na vyombo vingine vikiwa na picha ya mtoto huyo wa kifalme na mchumba wake, kwani wanatarajia soko litakuwa kubwa sana hapo harusi itakapokuwa inakaribia.

Kampuni moja ya China imeanza kutengeneza pete mfano wa ile ya uchumba ambayo Kate amejipatia. Pete hiyo ambayo imetengenezwa kwa almasi za rangi tofauti tofauti ikizunguka kito cha rangi ya sapphire ilikuwa ya Diana. William alisema hakutaka kabisa marehemu Mama yake apitwe na tukio lolote la harusi hiyo, ndio maana alikubali mchumba wake avikwe pete ambayo ilikuwa ya uchumba ya mama yake.

Wachina wamepata haki ya kutengeneza mfano wa pete hiyo, na kwa yeyote anayetaka kununua, Soko lipo wazi sasa.

Harusi hiyo ambayo itaonyeswa moja kwa moja na vyombo vya runinga mbalimbali inatarajiwa kuvunja rekodi ya harusi kuangaliwa na watu wengi duniani.

Gonga hapa kupata habari zaidi

Monday 13 December 2010

Gwiji la Muziki Remmy Mtoro Ongala Afariki Dunia

Mwananmziki mkongwe na maarufu nchini Tanzania, Ramadhani Mtoro Ongala au maarufu kama Dokta Remmy amefariki dunia usiku wa kuamkia leo.  
  
Remmy alikuwa akisumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa kisukari ambao ulisababishwa alazwe mara kadhaa hospitalini ikiwa ni pamoja na hospitali ya taifa ya Muhimbili. Inasemekana amefariki kwa matatizo hayo hayo ya kisukari.  
   
Remmy atakumbukwa kwa mengi ikiwa ni pamoja na kuwa mshindi wa pili kwa sura mbaya Tanzania japo alilalamika ya kuwa kaonewa kwani aliamini ya kuwa yeye ana sura mbaya kuliko watu wote waliokuwa wanaishi Tanzania wakati huo!!!!!  
  
Pia kuna nyimbo kadhaa alizoimba ambazo watu watatzikumbuka ikiwa ni pamoja na wimbo wa KIFO. 
 
Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi

Saturday 11 December 2010

Tanzania Bara Yaingia Fainali ya CECAFA Tusker Challenge Cup 2010

Timu ya mpira wa miguu ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) hapo juu wakishangilia ushindi, jana ilifanikiwa kuingia fainali ya kombe la CECAFA baada ya kuwafunga timu ya Uganda (The Cranes) kwa mikwaju ya penati 5 - 4


Kipa namba moja wa Kilimanjaro Stars, Juma Kaseja kama anavyoonekana hapo juu akiiokoa penati moja ya waganda na hivyo kuifanya Tanzania Bara kuingia fainali.

Fainali itakuwa kesho, ambapo Tanzania Bara itapambana na timu ya Ivory Coast. Hata hivyo ni lazima kombe libaki Tanzania hata kama Ivory Coast itashinda, kwani timu hii ya Afrika Magharibi ilialikwa tu kupasha moto mashindano, na sheria za CECAFA timu mualikwa huwa haipewi kikombe, isipokuwa inapewa zawadi iliyopangwa kwa mshindi wa kwanza, na kikombe huchukuliwa na nchi mwanachama aliyeshika nafasi ya juu.

Kwa maana hiyo, Kilimanjaro Stars ndiyo itakayopewa kombe hilo kwa matokeo ya aina yoyote.

Tuna imani Tanzania Bara itashinda na kuchukua kombe hilo.

Picha kutoka kwa michuzi

Friday 10 December 2010

Nobel Peace Price 2010 Received by a Ghost


The family of Liu Xiaobo who is the Nobel Peace prize winner for 2010 has been banned to attend the prize giving ceremony in Oslo - Norway today.

They were not granted permission to leave China for not clearly known reasons, but every one in the world can guess the main reason.  
  
Xiaobo has been sentenced to jail for 11 years on charges for trying to "westernises" China. 
The wife of Xiaobo has been in house arrest for 2 months now since annoncement of the winner for Nobel Prize. Yesterday the security was even more tighter at the front of her apartment in Beijing with both plain and uniformed security officers.

For another time since 1936, this year ceremony will be conducted without the laureatte or representative to be in Oslo to receive the award.

More info at TVS

Thursday 9 December 2010

Unaelewa Nini Kuhusu Uhuru wa Tanganyika

Leo, watanganyika (hata kama huupendi huu ukweli), wamesheherekea miaka 49 tangu wapate uhuru wao kutoka kwa mkoloni (Uingereza). 
  
Asilimia kubwa ya watu wanaofuatilia uhuru huu, wanaukandia na kuubomoa, na kuona hauna maana kubwa kwa hali halisi ya kiuongozi tulionao na watendaji wengine. 
  
Mkulima wa kijijini, ndio kwanza haelewi hata maana ya uhuru wenyewe.
Kwa wale wanaokenua meno na kushangilia siku ya uhuru, wanapaswa kujiuliza kwa nini watnganyika wengine hawaelewi kabisa maana ya siku na uhuru wenyewe.  
  
Nina hakika uhuru wenye maana kwa wananchi, kila mtu huwa anaguswa na siku hii, lakini kwa watanganyika, naona huwa wanajua kwa kuwa siku hiyo hawatakiwi kwenda kazini, na pia kushuhudia gwaride la kijeshi, baada ya hapo hawajui chochote.

Mchambuzi Fadhy Mtanga, kaeleza mtazamo wake kuhusu uhuru wa Tanganyika, soma makala yake hapa

Wednesday 8 December 2010

Mstaafu ateuliwa kushika Nyadhifa ya Mstaafu

Rais Jakaya Kikwete amemteua Jaji Mstaafu Salome Suzette Kaganda kuwa Kamishna wa Maadili ya Viongozi wa Umma. Uteuzi huo ulianza tangu tarehe 4 Desemba 2010. 
  
Jaji mstaafu Salome amechukua nafasi ya jaji mstaafu Stephen Ihema ambaye amemaliza muda wake.  
Taarifa hizi zimetolewa na Kurugenzi ya mawasiliano Ikulu.
   
Tukumbuke pia kuwa tume ya uchaguzi inaongozwa na Jaji Mstaafu Lewis Makame.  
  
Sielewi vizuri hii dhana ya kuchagua wastaafu kuwarithi wastaafu.
Ningependa kusikia watyu wenye uwezo ambao hawajastaafu wakishikilia nyadhifa hizo na watu wengine wanaochipukia wakibana nafasi za wenzao wanaopanda nyadhifa, na sio kila siku wastaafu ndio wanashika hatamu.
Suala hili lingeenda pia na kwa wakuu wa vyuo vikuu, weneyviti wa bodi mbalimbali kwani wengine wako hoi sana kwa uzee na sioni sababu ya wao kuendelea kukamata nyadhifa hizo.

Tuesday 7 December 2010

Tuwe Waangalifu na Mwisho wa Matumizi ya Bidhaa

Mimi bado nina imani vitu vinavyotengenezwa Bongo, vina uzuri fulani, na kwa kiasi fulani huwa vina ubora unaoridhisha hususan mambo ya vyakula.
Ninaogopa kuvamia hasa vile vinavyotoka Uchina, kwani vingi huwa ni bandia. 
 
Lakini wabongo wanaudhi pale wanapokuwa si makini katika kuangalia mazao yao wanayouza au kununua kama yana vigezo vyote vinavyofaa kwa mlaji kupata taarifa sahihi ya vyakula vyenyewe, kama paketi au gunia limefungwa vizuri, bidhaa iliyomo ndani haijaharibika, na kama lebo inaendana na bidhaa iliyopo. Na cha muhimu zaidi tarehe ya mwisho ya matumizi ya bidhaa yenyewe. Hapo mii ndio hutoa jicho la nguvu. 
  
Nikiwa mitaa yangu ya huku, nikisikia mtu aja kutoka Bongo, ni kawaida yangu kuagiza chochote ali-mradi nafsi yangu itafurahia matunda ya mamaland, hata kama ni vitumbua, wee leta tuu.

Kwa mara nyingine tena nilikutana na lebo hii hapo juu, tarehe ya mwisho wa matumizi, nimeitafuta kwenye kalenda zooooooote sijaipata. 
  
Hivi hao watengenezaji wa vyakula hivyo, huwa hawana elimu ya tarehe za kwenye kalenda, na hao wanaonunua kuuza vyakula kwenye masoko haya ya kisasa hawana wataalamu wa vyakula kukagua kama kila kitu kiko sawa.  
   
Ukisiskia mtu anasema bidhaa za wabongo ni feki sijui utamjia juu au uta.... 
  
Tunahitaji kuwafahamisha wajasiriamali wetu kuwa makini na bidhaa zao kama wanataka mafanikio ya kweli.

Monday 6 December 2010

Nawaza tu


Aina mbali mbali za vimiminika ambavyo kamwe haviozi hata kama vitakaa kwa zaidi ya miaka kumi.

Mimi nimeshapata 6, lakini nataka mpaka idadi ifikie kumi.
Jaribu kufikiria nami na unipe mawazo

Duh! Jumatatu njema

Image from CGA

Saturday 4 December 2010

Vituko vya Marais wa Afrika: Ivory Coast Presidential Results Controversy

I hate people who thinks they were created to be leaders for life, look this man from Ivory Coast!
  
Marais wengi wa Afrika wana kasumba ya kujiona kuwa wao ndio pekee wanaofaa kuongoza nchi kama wafalme, yaani kifo tu ndicho kinaweza kuwaondoa madarakani.

Mifano michache ya ving'ang'anizi ni kama Museveni (Uganda), Mugabe (Zimbabwe), Mubarak (Misri), na hata huyu jamaa wa Angola ambaye kaamua kuwa rais anachaguliwa na wabunge walioshinda katika uchaguzi na sio wananchi tena.

Nguli mwingine ni Laurent Gbagbo wa Ivory Coast (pichani juu) ambaye ametia mpya hivi karibuni ktika uchaguzi huru uliofanyika nchini Ivory Coast. Katika raundi ya mwisho alipokuwa anashindana na mpinzani wake mkuu Allasane Ouattara (pichani chini), alihisi kuelemewa na hivyo kuamuru matokeo yasitishwe kutangazwa, na sehemu iliyokuwa bado kumaliza kutolewa matokeo ilikuwa ni ngome ya mpinzani wake
Hii ilisababisha kuchelewa kutolewa matokeo kwa siku mmoja, hata hivyo tume ya uchaguzi ilimtangaza Ouattara kama mshindi  kwa kupata  54%, na miongoni mwa watu wa kwanza kumpongeza alikuwa Rais Obama wa Marekani.
    
Cha kushangaza, baraza la katiba ambalo ndicho chombo kikuu cha mwisho kuidhinisha matokeo kilipinga matokeo ya tume na kusema tume ilichelewesha kutoa matokeo, na hivyo baraza hili likachakachua matokeo na kumtangaza Gbagbo kuwa kashinda kwa 51.45%.

Kwa sasa jeshi limefunga mipaka yote ya Ivory Coast, na kuzuia vyombo vya habari vya kimataifa kuchukua na kurusha habari zozote za uchaguzi huo.

Ufaransa na Umoja wa Mataifa umekataa kutambua matokeo ya pili ambayo yalimwengua Ouattara kwenye nafasi ya ushindi.

Ndugu yangu, utajiju na maswali yatakayokujaa kichwani mwako!!

Friday 3 December 2010

Kenyan Football: Sad Story

Kenya National football team (Harambee Stars) for this year is almost out of competition for CECAFA Challenge cup in Dar es Salaam, Tanzania.  

  
They lost all their games so far after being beaten by Malawi by 3-2, and then by Ethiopia by 2-1. Now they will have to face tough opponents, the defending champions, The Uganda Cranes who have gained 4 points out of 2 games they have played.

It is so sad to see our neighbour Kenya is going out of competition so easily while last year they were runner-up after being beaten in the final by Ugandan team.

Kenya has been tough opponents in these competitions which are the oldest regional tournaments in Africa.

The problems probably are not related to the coach Jacob “Ghost” Mulee or players, but rather poor preparations. I am sure lack of appropriate football governing body in Kenya is the major factor for poor preparations.  
 
Probably FIFA which has now turn to have many corruptions scandals has a major role in distorting football programmes in Kenya, by deliberating ignore the elected football association and supporting the company to run the national league and international competitions. This has created big chaos, since the governing body recognised by Kenyan government is the one FIFA doesn’t want to hear. 
  
We all know Government has a role in improving National football team by supporting in various ways including some advice. But with the current situation in Kenya, it is practically impossible to run the intended programs.  
  
FIFA is not that clean to dictate what Kenyans they should do. This remind me what FIFA they did to our Tanzania when they stand firm to support corrupt leaders who were accused by our Government for financial misuse of the same FIFA money. They only gave up when the secretary general of football association of Tanzania was jailed for the same fraud charges and the chair was asked to return what he took illegally from the office. It was then, the proper elections were done and all corrupt leaders were axed out. Since then Tanzania has a steady football development, also football had grand support from the Government and of course the corrupt FIFA. 
  
I think FIFA should repent its decision on Kenya, and leave Kenya to manage her internal football activities which will help the region to have stiff competitions and see Eastern Africa roars into world cup!  
   
Huu ni mtazamo wangu tu!!

Thursday 2 December 2010

Tanesco Yaanzisha Blogu


Kwa wale wanaotaka kujua ratiba za mgao wa umeme, kutoa maoni kuhusu namna ya kuijenga na kuimarisha Tanesco na kadhalika, basi habari nzuri ni kuwa Tanesco wameanzisha baraza la mawasiliano wakitegemea msaada mkubwa kutoka kwenu wananchi mnaoishi Tanzania ili muwasaidie waendelee kuwaangazia maisha

Wanatoa rai ya kuwasaidia na sio kuwatukana kwani matusi si ustaarabu.

Nimeiona kwa Subi na pia link yao ni hii hapa

Wednesday 1 December 2010

Nimebanwa Mbavu

It appears as if I have abndoned my blog!!!!  
  
La hasha, I am occupied with activities for the end of the year.
I expect to take a vacation, therefore, lazima kila kitu kieleweke kabla sijaondoka.  
  
Just keep on visiting my blog, I appreciate and enjoy even on your silent tracking over.
You are all great, thank you!

See you soon