Member of EVRS

Saturday 18 February 2012

Adimiko la Muda

Kijiwe hiki kimeamua ya kuwa kitakuwa kimya hapa na pale wakati wadau watakapokuwa wanahama hama ili kubadili mazingira na kuweka mambo vichwani sawa. 
  
Kitakuwa kinajitokeza pale muda utakaporuhusu.  
   
Kama kawaida tupo wote!

Friday 17 February 2012

Waume wa Maswa Watakiwa Kupewa Elimu ya Uzazi

BAADHI ya wanawake wilayani Maswa, Shinyanga, wameomba waume zao washirikishwe katika elimu ya afya ya uzazi ili waweze kufahamu matatizo yanayowakumba pindi wanapokuwa wajawazito.
Ombi hilo lilitolewa juzi katika kijiji cha Gulungwashi kata ya Malampaka mbele ya Ofisa Utafiti wa shirika la Utu Mwanamke, Catherine Kamugumiya, wakati wakibainisha matatizo yanayowakabili kipindi cha ujauzito na kujifungua huku waume zao wakiwa mbali na matatizo hayo.
“Matatizo mengi ya uzazi yanayotukumba sisi wanawake wengi yanatokana na waume zetu kukosa elimu ya afya ya uzazi ukizingatia hawa ndiyo wasaidizi wetu wa karibu pindi tunapopata matatizo haya,” alisema Leah Nghumbi.

Pata habari kamili kupitia Tanzania daima hapa

Wednesday 15 February 2012

Matangazo katika Nyumba Za Kufikia Wageni




Hii ni mikakati ya kupambana na tabia zisizofaa kwa Jamii za Kitanzania. Hasa kipengele namba 8 na 12!

Tuesday 14 February 2012

Valentine's Day 2012!


People busy buying valentine's day gifts at shopping points as seen yesterday at Kigali, Rwanda


Just be happy and Love all !!!

Monday 13 February 2012

Zambia: New African Champions for 2012

Zambia Have won the 2012 African cup of Nations by beating Ivory Coast by penalties 8- 7. This is the first time for Zambia to clinch the cup. 

 
Both teams missed the 8th penalties. For Ivory Coast, Kolo Toure missed the 8th penalty and Gervinho missed the 9th penalty. 
 
The match was balanced, but Zambia predominate the game especially in the first half. Didier Drogba will not forget this match, as he missed a penalty on 70th Minutes by shooting far above the cross bar, probably they could have won the match on regular time,  but he missed the spot kick. 
  
Zambians, who were considered underdogs, emerged out different and eventually won the title. 
 
To reach the final, in the semi-final, Zambia won against Ghana by 1 – 0. Ghana and Ivory Coast were considered as the favourite teams to clinch the winners’ cup. 

Monday 6 February 2012

Flashback of Day dated 11.11.11

Watoto 11 waliozaliwa kwa siku moja katika hopitali moja huko India. 
   
Kitu cha muhimu katika picha hii, ni kuwa wote walizaliwa tarehe 11 mwezi wa 11, mwaka elfu mbili na 11.
Kila mtoto alikuwa na mzazi wake, kwa hiyo kuna wakina mama 11 waliojifungua kwenye hospitali hiyo na kwa siku hiyo.

Saturday 4 February 2012

Zambia Cruise to Semi-final in African Cup of Nations 2012

For the first time since 1996, Zambia's Chipolopolo manage to reach the semi-final for African Football tournament when they beat 10-Man Sudanese team by 3-0 at Bata. 
 
Goals were scored by Sunzu Stoppila, Christopher Katongo and James Chamanga. 
  
Another quarter-final game is on the way between favourite Ivory Coast and co-host Equatorial Guinea in Malabo. 

Thursday 2 February 2012

Breaking News: Ajali Mbaya ndani ya Shule ya Sekondari ya wasichana ya Korogwe

Gari dogo aina ya Toyota limewagonga wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Wasichana Korogwe wakati wakiwa katika mahafali ya wanafunzi wenzao wa kidato cha sita. Ajali hiyo imetokea chini ya nusu saa kutoka ninapoandika habari hii.  
  
Zaidi ya wanafunzi 10 wamejeruhiwa vibaya, na wanne kati ya hao wameumizwa na hawana fahamu wala kuonyesha dalili yoyote ya uhai. Bado hawajathibitishwa kama wako hai au wamekwisha fariki. 
  
Hilo gari lililowagonga, linasemekana lilikuwa limewaleta baadhi ya wazazi wa wanafunzi. Pia inasemekana lilikuwa katika mwendo kasi mkubwa wakati lilipoingia ndani ya eneo la shule.
Habari zaidi zitawasilishwa baadaye

Egypt (Misri): Vurugu Mpirani zaua watu zaidi ya 73

Habari hii si nzuri kwa wapenzi wa soka, kwani kumetokea vurugu kubwa iliosababibisha vifo vya wapenzi wa soka 73 na wengine zaidi ya 1,000 kujeruhiwa, wengine wakiwa wamejeruhiwa vibaya. Hali hii ilitokea  katika Jiji la Port Said mara baada ya kumalizika kwa mechi ya mpira wa miguu kati ya timu zenye upinzani mkali za Al Masyr ya Port Said na Al Ahly ya Cairo siku ya tarehe 1 Februari 2012.

Mechi hii ilimalizika kwa wenyeji Al Masry kuifunga Al Ahly kwa jumla ya magoli 3-1. Tafrani ilianzishwa na mchezaji wa Al Ahly ambaye inasemekana alifanya kitendo au ishara iliyotafsiriwa kama ni ishara ya vita, hivyo kusababisha mashabiki wa timu ya Al Masyr kuingia kwenye sehemu ya kuchezea mpira (football pitch) na kuanza kuwashambulia wachezaji wa Al Ahly, ambao iliwalazimu kukimbilia kwenye vyumba vya uwanja huo. Na kwenye majukwaa ya washabiki, wale wa Al-Ahly walishambuliwa na wakalazimika kukimbilia sehemu za kutokea, hali hii ilisababisha watu kukanyagana na kuongeza idadi ya vifo na majeruhi.
  
Hakuna juhudi yoyote iliyoonyeshwa na vikosi vya usalama kwa hatua ya dharura, kiasi kwamba watu walikuwa wanashambuliana kwa kila kilichowezekana au kupatikana ikiwa ni pamoja na chupa, mawe, fimbo nk  huku wana-usalama hao wakiangalia tu.   
 
Kutokana na vurugu zilizotokea Port Said, chama cha soka cha mpira cha Misri kililazimika kufuta mechi zote ikiwa ni pamoja na mechi kati ya Zamalek na Ismailia iliyokuwa inachezwa jijini Cairo. Wakati inafutwa, ilikuwa ni wakati wa mapumziko. Kutokana na kufutwa kwa mechi hiyo, kuna wakorofi waliamua kuwasha moto kujaribu kuuchoma uwanja wa mpira huo jijini Cairo, hivyo kusababisha mkanganyiko uwanjani.  
  
Katika picha zilizokuwa zinaonyeswa na kituo cha Tv cha Misri, kilionyesha watu wakishambuliana, na wengine kujihami vichwa kwa kutumia viti ili wasipigwa na mawe kichwani! 
  
Uongozi wa Misri utakutana kwa dharura alhamisi tarehe 2 Feb  2012 kujadili kwa dharura hatua zaidi za kuchukua.  
   
Kitendo hiki ni cha aibu kwa Taifa la Misri na kinaogofya kwenye ulingo wa soka duniani.