Member of EVRS

Saturday 31 December 2011

Kigamboni Wacharuka Kupinga Ongezeko la Nauli za Kivuko: Uozo Waanikwa

BUNGE LA TANZANIA

OFISI YA MBUNGE WA JIMBO LA KIGAMBONI

Kumb na: KIG/KVK/VOL.1/4                                                                    29 Disemba 2011
 
Mhe. Dkt John P. Magufuli (MB)
Waziri
Wizara ya Ujenzi
Dar es Salaam
 

YAH: KUSUDIO LA ONGEZEKO LA VIWANGO VYA NAULI KATIKA KIVUKO CHA KIVUKONI-KIGAMBONI
Kichwa cha habari hapo juu chahusika.

Wananchi wa Jimbo la Kigamboni wamepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa ya kusudio la kuongeza nauli za abiria, magari na vyombo vingine vinavyotumia huduma ya kivuko kati ya Kigamboni na Kivukoni kuanzia tarehe 1 Januari 2012.  
 
Kivuko hiki ni kiungo muhimu kwa wananchi wanaoishi upande wa Kigamboni ambao wengi wao ni watu wa kipato duni na hawana ajira za kudumu. Ongezeko la nauli kwa asilimia 100 ni kubwa sana na litawaathiri kiuchumi. Nimepigiwa simu nyingi na kuletewa malalamiko mengi katika siku ya leo kuhusiana na mpango huu wa kuongeza nauli. Wananchi wanataka kujua ni vigezo gani vilivyotumika kufikia nauli hizi mpya; vyombo gani vilivyopendekeza, kupitisha na kuidhinisha nauli hizi na wanataka kujua kwa nini hawakushirikishwa katika mjadala wa nauli mpya. 
 
Pamoja na ongezeko kubwa la wakazi na magari yanayotumia huduma ya kivuko, cha kushangaza ni kwamba mapato kwa siku yamekuwa ni takribani Tsh 8 milioni kwa siku kwa muda mrefu sasa. 
  
Ni dhahiri kumekuwa na upotevu mkubwa mikononi kwa watumishi wasio waaminifu wa kivuko. Mapato mengi yanapotea kwa njia zifuatazo: 
 
1.Baadhi ya watumishi wa kivuko kukatisha risiti hususan za magari kwa kutumia vitabu bandia.
  
2.Baadhi ya watumishi kuziuza tena tiketi zilizotumika badala ya kuzichana.
  
3.Baadhi ya watumishi na askari wanapitisha magari na abiria baada ya kupokea malipo ya pembeni.
  
Vilevile mafuta ya vivuko huuzwa kwa wavuvi wadogo wadogo katika maeneo ya Feri.
  
Mambo haya yote yanafanyika pasipo kificho, binafsi nimeshawahi kushuhudia yote niliyosema hapo juu yakifanyika na kuyatolea ripoti kwa uongozi wa kivuko. 
 
Ninaamini kuwa hatua zifuatazo zikichukuliwa mapato ya kivuko hiki yanaweza kufika zaidi ya Tsh 13 milioni kwa siku:

1.Kudhibiti uuzaji wa tiketi za abiria na magari. 
 
2.Kudhibiti ununuzi, utunzaji na matumizi ya mafuta yanayotumika kwenye vivuko. 
  
3.Kudhibiti idadi ya watu na magari yanayovuka bila kulipia huduma hii. 
  
4.Kupunguza gharama za uendeshaji ikiwa ni pamoja na kupunguza idadi ya vibarua. 
 
Kutokana na unyeti wa suala hili, nashauri zoezi hili lisitishwe ili kutoa fursa ya kujadiliana kuhusu upandishaji wa nauli na maboresho ya huduma hii kwa kushirikiana na wadau na wawakilishi wa wananchi katika Jimbo la Kigamboni. 
 
Natumaini mapendekezo haya yatafanyiwa kazi ili kuepuka kuwabebesha mzigo wa gharama za uendeshaji wakazi wa Kigamboni wanaotumia huduma ya kivuko pale Feri. 
 
Naambatanisha nakala ya barua yangu ya tarehe 19 Januari 2011 yenye kumbukumbu namba KIG/KVK/VOL.1/1 kwenda kwa Mkurugenzi Mkuu wa TEMESA ambayo ilitoa mapendekezo ya njia ya kuboresha huduma na vile vile kutaka ushirikishwaji wa wadau katika suala la ongezeko la nauli. Barua hii haijajibiwa hadi hivi sasa. 
 
Natanguliza shukrani zangu za dhati. 
 
Wako katika ujenzi wa Taifa

Mhe. Dkt Faustine Ndugulile (MB)

MBUNGE

Nakala: 
 
1.Mhe. Mizengo Pinda (MB)-Waziri Mkuu
 
2.Mhe. Mecky Sadick-Mkuu wa Mkoa Dar Es Salaam
 
3.Waheshimiwa Madiwani wote-Jimbo la Kigamboni
 
4.Wenyeviti wa Serikali za Mitaa-Jimbo la Kigamboni
  
5.Mkurugenzi Mkuu-TEMESA
   
Habari hii nimeipakua kutoka kwenye wavuti ya Dkt Faustine Ndugulile

Thursday 29 December 2011

Kiwango cha Elimu Jijini London, Uingereza Kinatia Aibu!

Nchi ya Uingereza ambayo inajivunia kuwa nchi mojawapo yenye ushawishi mkubwa katika masuala ya siasa na uchumi. Na pia kuwa taifa mojawapo duniani ambalo watu wengi hupenda kukimbilia huko wakitarajia kupata mavuno makubwa ya fedha kwenye mifuko yao. Na pia watu wengine kukimbilia kusoma huko wakiwa na imani ya kuwa vyeti watakavyovipata huko vitawasaidia kupata kazi kwa urahisi kwenye nchi zilizoendelea za Ulaya na Amerika. 
  
Hali hii inaweza kutoweka hivi karibuni ikiwa juhudi za ziada hazitafanyika kufanya marekebisho makubwa katika mfumo wa utoaji elimu nchini humo. 
  
Takwimu zilizotolewa mwezi wa Juni 2011, zinaonyesha ya kuwa asilimia 25 ya watoto wanaomaliza elimu ya msingi katika jiji la London hawajui kusoma wala kuandika, na wale wanaoenda sekondari, asilimia 20 ya hao wakimaliza elimu hiyo, pia hawawezi kusoma wala kuandika vizuri, na hata ukiwapa kitabu kusoma hadharani, hawajiamini kabisa. 
Habari hii haishii kwa watoto wa shule tu, bali hata watu wazima wanaofanya kazi jijini London, zaidi ya asilimia 15 yao, nao pia suala la kusoma na kuandika linawapa taabu sana! 
 
Habari hizi zilifichuka pale waziri mkuu wa sasa alipokuwa anasisitiza kazi zitolewe kwa vijana wa kiingereza badala ya wahamiaji. Wakati makampuni yatakayoendesha mashindano ya Olimpiki hapo mwakani yalipotoa nafasi za kazi na kuwataka vijana wa kiingereza kujitokeza na kujaza fomu za maelezo, vijana wengi wenyeji walikimbia na kugomea kujaza fomu hizo, ambapo waandaaji wa michuano hiyo walishangazwa na tukio hili. 
    
Katika mahojiano ili kufahamu kwa nini vijana wa kiingereza hawajitokezi, ndipo ilipobainika ya kuwa elimu ndio ilikuwa mgogoro, kwani vijana walikiri ya kuwa hawawezi kujaza fomu hizo kwa sababu hawajui kusoma wala kuandika!  
  
Hata hivyo, kuna mashirika mengine yamekuwa hayaajiri baadhi ya waingereza kwa sababu ama barua zao za maombi ya kazi zinakuwa na makosa mengi sana ya maneno (Poor spelling) ambapo ni karibu ya asilimia 40 za barua hizo hutupwa bila kuwaita kwenye usaili, au wanaoitwa, hudhihirisha wazi kuwa uwezo wao wa kusoma ni mdogo sana. Hii ilianishwa na habari hii hapa 
  
Kwa sasa mke wa Prince Charles,Camilla Windsor, anajihusisha na juhudi za kuongeza kutoa elimu bora kwa watoto wa uingereza ili baadaye waje kuendesha uchumi wa nchi yao ambao kwa sasa unaenda mrama kwani viwanda vingi vinakufa kwa uongozi mbovu, na kwa sasa uingereza uchumi wake unaendeshwa kwa kutegemea kukusanya kodi kwa wafanyakazi na wafanyabiashara ambao wengi wao ni raia kutoka nje ya Uingereza. 
  
Soma makala hii kwa kiingereza inayozungumzia elimu ya Uingereza kwa sasa

Wednesday 28 December 2011

Read Careful and Be Sensible!

Hey, Just be sensible. It is closer to the end of this year!

Photo from Uberhumor

Sunday 25 December 2011

Oh! It's Christmas!

Children enjoying the ride on Christmas day in Dar - Tanzania
Christmas is one of the most celebrated day in the world. 
At this season, everybody express love, peace and harmony.
  
Children usually they enjoy most, of course the parents becomes happy to see sweet smiles from their children, they even forget that the expenditures had just surged for the preparations of the event. To be noticed when they are about to pay the school fees etc :-)
  
Oh my kids, I love you dearly, enjoy the Christmas, as we are celebrating the birth of the holy child. 

Friday 23 December 2011

Picha za Mafuriko Dar es Salaam


Watu wakiokolewa na mitumbwi ya dharura

Bonde la Jangwani

Gari la Serikali likiwa limetumbukia katika Daraja lililobomoka

Rais wa Tanzania akikagua athari za mafuriko Dar

Picha nyingi kutoka kwa Haki Ngowi

Monday 19 December 2011

Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-Il Amefariki Dunia


Kim Jong Il


Rais Wa Jamhuri ya Korea (Korea ya Kaskazini) ama kiongozi mpendwa Kim Jong-il pichani hapo juu leo ametangazwa rasmi ya kuwa alikwishafariki dunia. 
Msemaji wa Serikali ya Korea Kaskazini, amedai rais wao mpendwa alifariki siku mbili zilizopita, yaani siku ya jumamosi tarehe 17 Disemba 2011. Inadaiwa ya kuwa alifariki kwa kupata mshtuko mkubwa wa moyo akiwa kwenye treni katika ziara ya ukaguzi, japo haujafafanuliwa ulikuwa ni ukaguzi wa nini. 
  
Vyanzo zaidi vya habari vinadai kuwa kilichochangia kifo chake ni uchovu mkubwa wa mwili na akili alivyokuwa navyo kiongozi huyu maarufu ambaye anakadiriwa alikuwa na miaka 69, japo mwaka aliozaliwa bado hauna uhakika sana kama ni kati ya mwaka 1941 au 1942. Ingawa anajulikana alizaliwa tarehe 16 February nchini Urusi, na alipewa jina la Yuri Irsenovic Kim kabla halijabadilishwa baadaye aliporejea Korea akiwa na miaka takribani 3.

Kim Jong-Un

Mtoto wake wa kiume ambaye ndio mdogo kuliko wote, Kim Jong -Un, mwenye umri wa miaka 27 ndio anatarajiwa kushika madaraka ya baba yake, japo umri wake bado ni kitendawili kwa madaraka anayotarajia kushikishwa. Kwa sasa mtoto huyu ndiye aliyechaguliwa kuwa kiongozi wa shughuli za mazishi ya Baba yake akiongoza jopo la watu 232 wanaoratibu mazishi hayo yatakayofanyika tarehe 28 Disemba 2011 jijini Pyongyang. 
   
Tangu Korea ya Kaskazini ikombolewe tarehe 15 Agosti 1945 imewahi kutawaliwa na viongozi wawili tu ambao no Kim Il-Sung na mwanaye ambaye amefariki sasa Kim Jong-Il ambaye aliingia madarakani kuanzia tarehe 8 Julai 1994 hadi kufariki kwake hapo tarehe 17 Mwezi huu. 
   
Kim Jong-Il alikuwa anatuhumiwa kuwa alikuwa ni dikteta kwa wananchi wake, na inadaiwa alikuwa hataki propaganda ya aina yoyote, hasa kutoka mataifa ya magharibi kuingia nchini kwake. Na inadaiwa vyombo vya habari nchini Korea ya Kaskazini vilikuwa haviruhusiwi kutangaza habari zozote za nje ya nchi yao!  Kimsingi vyote karibu vyote vya habari nchini Korea ya Kaskazini viinamilikiwa na serikali.
  
Pia kiongozi huyu alikuwa ni tishio kwa nchi majirani hasa kutokana kuwa na mpango wa kutengeneza silaha za kinyuklia kwa nia ya kuwatishia maadui zake ambao walikuwa ni Korea ya Kusini, Japan na Marekani. Hii inaweza kuwa ni moja ya sababu zilizofanya Korea ya Kusini kutangaza hali ya tahadhari mara tu ilipopata taarifa za kifo cha Kim Jong-Il.  

Friday 16 December 2011

European Champions League Draw: Last 16 Fixtures

Lyon (France)                          vs           APOEL (Cyprus) 
  
Napoli (Italy)                           vs           Chelsea (England) 
 
AC Milan (Italy)                      vs           Arsenal (England) 
 
Basel (Switzerland)                  vs          Bayern Munich (Germany) 
 
Bayer Leverkusen (Germany)  vs           Barcelona (Spain) 

CSKA Moscow (Russia)         vs         Real Madrid (Spain) 

Zenit St Petersburg (Russia)     vs         Benfica (Portugal) 

Marseille (France)                  vs          Inter Milan (Italy) 

The first legs will take place on 14/15 or 21/22 February 2012, while the return fixtures are scheduled for 6/7 or 13/14 March 2012.

Thursday 15 December 2011

Wanafunzi Wasiojiweza Rwanda Kuendelea Kusaidiwa Ada ya Elimu

Mkurugenzi wa MTN Rwanda Khaled Mikkawi akikabidhi hundi ya msaada wa MTN-Rwanda kwa mlezi wa Imbuto Foundation Mama Jeannette Kagame
Mfuko wa Maendeleo kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu wa Rwanda (Imbuto Foundation) ambao mlezi wake ni mke wa Rais Kagame, Mama Jeannette Kagame, umepokea kiasi cha faranga za Rwanda Milioni 90 kutoka kwa kampuni ya mtandao wa simu ya MTN-Rwanda kwa ajili ya kuwasaidia vijana waliopo shule za upili kiwango cha kidato cha kwanza hadi cha sita kwenye masuala ya ada na gharama nyingine za shule. 
 
Mfuko huu ni mahsusi kuwasaidia watoto walio katika matatizo ya kimaisha ambao wazazi wao hawajiwezi au hawapo tena duniani. 
  
Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2002, umeshasaidia zaidi ya vijana 5,000

Habari kutoka newtimes

Monday 12 December 2011

Ndio Matokeo ya Kuhukumiwa Kabla Hujatenda Kosa ...


Ikionekana huna kosa.... naye alikuwa ana imani ya kuwa lazima utakuwa na kosa.... Basi chunga sana kufuga Osama!

Thursday 8 December 2011

Talk of the Day as Manchester Clubs crash-out of Champions' League

In England, it is the time for Londoners and not Manchesters





CNN quotes : Manchester United and their city rivals Manchester City both made embarrassing exits from the Champions League on Wednesday.

Roy Keane on BBC : Man U ...."I think their best player tonight was Ryan Giggs. That sums it up - he's 37 or 38, you can't be depending on him. United got what they deserved tonight.


Fergie on Al-Jazeera "We're disappointed, there's no other way you can feel,'' .....
"It's a loss because it's the best tournament in the world."


Supersport says....Manchester United and Manchester City will begin 2012 scrapping with the also-rans of European football after ignominious Champions League exits .......... So used to dining with the continents's aristocrats in the second half of the season, the English champions now face the prospect of the less salubrious and much maligned Europa League.


Skysport narrates ...Manchester's nightmare scenario became a grim reality as both United and City were sent crashing out of the UEFA Champions League before the knockout stage.
Failing to progress from a group containing Otelul Galati, Benfica and Basel must surely rank as one of the lowest points in the managerial career of Sir Alex Ferguson, who could only look on stony-faced as his side were beaten 2-1 away by the Swiss side to slip below their opponents and into the Europa League.



Anyway.....I was looking for positive comments about Manchester Clubs, but I just end up into those.... eventually I abandon  further searching!!

Goodluck Manchesters in Europa League

Monday 5 December 2011

Mwaliko: Sherehe za Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara Jijini Kigali, Rwanda

Umoja wa Watanzania wanaoishi Rwanda unapenda kuwaalika watu wote katika hafla ya chakula na dansi katika kusheherekea miaka 50 ya uhuru wa Tanzania Bara (Tanganyika). 
  
Sherehe hizi zitafanyika tarehe 9.12.2011 jijini Kigali. Siku kama hiyo miaka 50 iliyopita ndipo Tanganyika ilipopata uhuru kutoka kwa wakoloni wa Kiingereza. 
  
Mbali ya chakula (Chenye asili ya Kitanzania) na dansi, kutakuwa na maelezo mafupi ya historia ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambao ndio uliozaa jamhuri ya Muungano ya Tanzania.



Watu wote mnakaribishwa kwa kiingilio kidogo cha faranga za Rwanda 8,000 tu. 
  
Mawasiliano kwa waratibu yameandikwa kwenye kadi za mwaliko. 
 
KARIBUNI SANA!

Friday 2 December 2011

Kenya Taxpayers Money Thrashed: Milimani courts ‘falling apart’

When you look at this photo.... It sounds like a very beatiful building.....

It cost Kenya Taxpayers' money amounting to 1 Billion Kenyan shillings for its renovations which lasted for 8 years since it was commenced!

Kenyan Chief Justice, Willy Mutunga after he toured the premises and witnessed the shoddy job on the building, which cost Sh1 billion. He said .... "To refer to this building as ultra modern is to insult both the English language and the intelligence of Kenyans,"

 
Mutunga sums all this as “administrative corruption and incompetence” and he had no kind words for professionals involved in the work.

  
Barely 10 months after it was commissioned, Chief Justice Willy Mutunga has sounded alarm over the safety of judicial staff and Kenyans using the building whose ceiling has caved-in, with water leaking all over. 

  
Door handles in almost all floors have broken down, lifts including the VIP ones stopped working and the water leakages keep on triggering electric faults. 
 
Get the touch of it here and here

Wednesday 30 November 2011

Mchungaji Arusha Atembezwa Uchi Kwa Kugomea Shughuli za Kimila

Mchungaji mmoja wa kanisa la pentekoste Jijini Arusha na ambaye ni mkazi wa kijiji cha Siwandeti, wilayani Arumeru alikamatwa na kutembezwa uchi baada ya kukataa kuhudhuria kikao cha kimila la kabila la wamasaai kilichohusu mambo ya tohara kwa kuwa aliona hakiendani na imani yake ya kidini.

 
Hatua ya kumtembeza uchi kwa takribani Saa 22 katika vijiji zaidi ya vinne na kuogeshwa kwenye maji ya baridi Saa 11:00 alfajiri kulitokana na yeye kugoma kutekeleza hukumu ya kutoa ng’ombe dume kama adhabu ya kutohudhuria kikao cha mila.
  
Miongoni mwa vijiji alivyotembezwa uchi mchungaji Lukumay ni pamoja na Ngaramtoni, Mringaringa, Kenyaki, Olevelosi, Kiranyi na Elerai. 
  
Habari zaidi kutoka kwenye Mwananchi

Monday 28 November 2011

Ni siku ya Uchaguzi DR Congo na Egypt

Wapinzani wakidhibitiwa na askari wa Congo katika viunga vya jiji la Kinshasa

Leo ni siku ya uchaguzi wa rais na wabunge katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC)
Katika kampeni za kujinadi kwa wagombea, kulikuwa na matukio mengi ya uvunjifu wa amani ambapo polisi walilazimika kutumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya wafuasi wa vyama mbalimbali waliokuwa wanapingana. 
Katika kampeni, lugha mbalimbali zilitumika kama njia ya mawasiliano kutegemea na mahali kampeni za kisiasa zilipokuwa zikifanyaika. Lugha kuu zilizotumika zaidi katika kampeni hizo ni Kilingala, Kifaransa na Kiswahili.  
   
Huu utakuwa ni uchaguzi wa kwanza wa kipekee kwa muda mrefu, kwani gharama za uchaguzi huu zimegharimiwa na nchi ya Kongo yenyewe.


Askari wa Misri karibu na Tahrir square

Wakati huo huo, nchi ya Misri nayo leo inafanya uchaguzi wake wa kuwachagua wabunge wa mabunge mawili ya nchi hiyo.  
Itakumbukwa kwa wiki kadhaa sasa kulikuwa na maandamano ya kuipinga serikali ya Kijeshi inayotawala nchi ya Misri baada ya kiongozi wake wa siku nyingi, Hosni Mubarak kuachia madaraka kufuatia shinikizo la wananchi kumtaka kuondoka madarakani, ambapo alitii baada ya vurugu kubwa kuzidi nje ya uwezo wa utawala wake.  
  
Pia kwa Misri, uchaguzi huu unahesabika kuwa wa uhuru zaidi kwa miaka zaidi 30 iliyopita.
Kulikuwa na matukio ya ucheleweshaji wa makaratasi ya kupigia kura kwenye vituo kadhaa vya Cairo na Alexandria.  
  
Tunawaombea wamalize uchaguzi kwa amani ili waweze kizijenga nchi zao.

DRC Photo from The Telegraph
Egypt photo from Guardian

Wednesday 23 November 2011

Uhamasishaji wa Kujikinga na Ukimwi


Mipira 80,000 ya kinga ya kiume ikiwa imening'nizwa Paris ikiwa ni kuhamasisha kujikinga na janga la UKIMWI.

Picha kutoka TravelNews

Tuesday 22 November 2011

Road slides Towards Sea After Heavy Rainfall


Landslide occured near Los Angeles, CA after heavy downpours over last sunday 20th Nov 2011.
Na casualties were reported to this natural disaster which occured along the coastal road.

Read more here

Monday 21 November 2011

Ugonjwa wa Katiba Mpya Tanzania:Unatibiwa kwa Kidonge cha Rangi Mbili

Siku chache zimepita baada ya Bunge la Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kuridhia muswada wa sheria utakaongoza na kuratibu jinsi ya kukusanya maoni ya katiba mpya. Japo wabunge wa Upinzani kwa idadi kubwa waliususia kabisa kwa kile kinachodaiwa kuletwa na kusomwa huku vipengele kadhaa vya sheria vikiwa vimevunjwa.  
  
Muswada ndio umeshapita, na rais Kikwete alithibitisha pale alipokuwa akiongea na "wazee wa Darisalama" japo kuna wengine hata mimi nilikuwa nawazidi umri japo sina sifa kamili ya kuitwa Mzee, nao walikuwa humo ati kama wazee! Mhesh. Rais aliahidi kuuwekea sahihi muswada uliopitishwa na wabunge (ambao kwa karibu asilimia 80 ya michango yao walikuwa nje kabisa ya muswada wenyewe), ili uwe sheria rasmi na kuanza kutumika mara moja. 
Pia aliwaagiza wabunge wa CCM mara alipokutana nao baada ya kikao cha bunge kilichoupitisha muswada huo kuwahi majimboni kwenda kueleza ujio wa neema na kiu ya katiba mpya kwa wananchi wanaowawakilisha.  
  
Hali hii ilichafuliwa na taarifa ya kamati teule ya bunge iliyoundwa kumchunguza David Jairo (ama vijana wanavyomuita DJ) kuwasilisha taarifa yao ambayo ilikuwa inachafua maana ya maadili ya kiuongozi. Kuna mapendekezo mengi tu yalitolewa ikiwa ni pamoja na kuchukuliwa hatua za kinidhamu ikijumuisha wote waliotajwa kwa makosa ikiwa ni pamoja na waziri Ngeleja akidaiwa alipewa takrima ya sh. 4M ambazo ni kinyume na matumizi ya fedha za uma. 
 
Nahisi wabunge wengi wa CCM watakuwa na wakati mgumu kwenda kuiuza rasimu ya katiba itakayokuja, na mijadala itahamia kwenye pengo la uadilifu lililo onyeshwa na baadhi ya watendaji wa serikali tawala na kuwa kigezo cha kukataa vifungu vitakavyoletwa.
Kuna viashiria ambata kwa sasa kuwa mwaka 2015 utakuwa mgumu sana kwa serikali iliyopo madarakani kukubalika, labda kama kutakuwa na kipengele cha kuchomeka serikali ya umoja wa kitaifa au yaje mabadiliko makubwa sana yatakayofanyika sasa kubadili fikra za watu wanaotaka mabadiliko ya kisiasa kwa mazuri au la, yaani, people they just want a change...   
  
Kuna taarifa zisizo rasmi kwamba katibu mkuu kiongozi anatarajiwa kustaafu mwishoni mwa mwezi ujao mwaka huu, labda itakuwa ni fursa ya kuachia ngazi bila kupoteza haki zake za muda aliolitumikia Taifa, kwa wale mtakaotaka kusema muda Taifa lililomtumikia ni nyie, na wala sio mimi. 
  
Watendaji wengine wa wizara ya nishati na madini inasemekana wameanza kujiandaa kukaa benchi, na pia mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali naye inawezekana hajui nini kitafuata hasa baada ya kumsafisha DJ na baadaye kuonekana kama taarifa yake aliiandikia kwenye kituo cha daladala bila kupitia hesabu kamili ili kubaini kasoro. Pia kuna wingu la shaka kwa sasa liko juu yake kuhusu utendaji wake wa kazi, japo anasifika kwa umakini wa kwenye hesabu za halmashauri za miji na wilaya. 
  
Tunachosubiri ni Kitendawili au bomu?!!

Don' Need a Bridge!

Cheers ha ha haa

Thursday 17 November 2011

Mchakato wa Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba Mpya ya Tanzania

Nimenukuu:
Maoni ya Dk. Faustine Ndugulile (Mbunge wa Kigamboni) kuhusu mchakato na muswada wa sheria ya mabadiliko ya Katiba mpya

Nchi yetu inatimiza miaka tarehe 9.12.2011. Kwa hiyo mjadala wa kufanya mapitio ya katiba yetu umekuja muda muafaka kwa taifa hili. Ni muda mrefu umepita na hivyo ni jambo jema kutafakari tulipotoka kama Taifa, tulipo na tuendako.

Tumekuwa na katiba ya mwaka 1977 ambayo imekuwa ikutuongoza hadi hivi sasa, lakini kama taifa tumeamua kuanza mchakato utakaopelekea kuwepo na katiba mpya itakayodumu vizazi na vizazi vijavyo.

Nashukuru kuwa sehemu ya mchakato wa kupitia muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba ambayo itaongoza mchakato mzima wa kupata katiba mpya.

Kwa babati mbaya sana muswada huu umezua mjadala mkubwa ndani na nje ya Bunge. Baadhi ya wananchi, wanaharakati na wanasiasa wanataka muswada huu usijadiliwe kutokana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kupinga uwasilishwaji kwa mara ya pili, wananchi kutopata fursa ya kuchangia na mamlaka ya Rais kwenye mchakato huu.

Ninaungana na watanzania wote wanaotaka katiba mpya. Ninaungana na watanzania wote wanaotaka katiba nzuri na yenye kuweka maslahi yaTaifa mbele na yenye kulinda haki za msingi za Raia wa nchi.

Sasa hizi tofauti zinatoka wapi? Kwanini kumekuwa na mtazamo tofauti katika suala hili?

Jioni ya leo nimejaribu kuwasiliana na watu mbali mbali kupata mawazo na maoni yao kuhusu muswada huu unaoendelea kwa sasa. Nimegundua yafuatayo:
  1. Baadhi ya watu hawana ufahamu mzuri wa kitu gani kinachoendelea kwa sasa. Baadhi ya watu wanafikiri kuwa ndio tumeshaanza kuandika hiyo katiba mpya pasipo kuwashirikisha wananchi.
  2. Uelewa wa nini kilicho ndani ya muswada bado ni mdogo hata kwa wale wasomi.
Vilevile kuna matatizo mengine. Kuna watu ambao kipato chao cha kuendesha maisha kinatokana na mchakato huu wa Katiba Mpya. Watu hawa wanapata fedha nyingi za wafadhili na baadhi yao wanaleta mkanganyiko wa makusudi ili waendelee kushibisha matumbo yao. Wapo wengine wanaouangalia mchakato huu kwa mtazamo wa kiitikadi, kidini, Uzanzibari na Utanzania Bara. Ukichanganya yote hapo juu na upotoshaji unaendelea kwenye mitandao na vyombo vya habari, unakuta suala hili linazidi kuwachanganya wananchi.

Kimsingi kinachofanyika sasa hivi ni kutengeneza sheria itakayoweka utaratibu wa kuandaa katiba mpya. Binafsi nimeisoma mara kadhaa na ninaona inakidhi mahitaji iliyokusidiwa. Nasema hivyo kwa sababu zifuatazo:
  1. Maboresho yanayozingatia hoja zilizotolewa na wadau wengi zimeongezwa kwenye muswada huu. 
  2. Nchi ya Zanzibar ambayo ni wadau wa Muungano wamepata uwakilishi wa kutosha. Raisi wa Tanzania Bara na Raisi wa Zanzibar watashirikiana katika kila hatua ya mchakato wa katiba hii. Hakuna atakayefanya maamuzi ya peke yake.
  3. Madaraka ya Rais yanayolalamikiwa yamepunguzwa sana kwenye muswada huu. Kwanza, Maraisi wote watashirikiana kutoa maamuzi. Pili, hadidu za rejea zimeshainishwa badala ya Raisi kuja na za kwake. Tatu, sifa na vigezo vya wajumbe wa tume zimeshainishwa.Kwa hiyo majukumu ya Raisi ni machache sana na maamuzi mengi yatafanywa na wananchi.
  4. Ushirikishwaji wa wananchi utakuwa ni mkubwa. Nchi nyingine zimeweza kutengeneza katiba kwa kupitia Bunge la Katiba au chakato wa kura za maoni (Referendum). Sisi Tanzania tumeamua kutumia njia zote mbili. Wananchi watashirikishwa kwa kutoa maoni yao kwenye mikutano ya tume inayosimamia mchakato wa katiba mpya, wananchi watashirikishwa kwenye mabaraza ya mapitio ya katiba, wananchi watashirikishwa kwenye Bunge la Katiba, wananchi watashirikishwa kwenye kura za maoni (Referendum).
Kwa mtazamo wangu ni vyema tukakamilisha muswada huu ili kazi kubwa na ya msingi iliyo mbele yetu iweze kuanza. Kuna mambo ya msingi ambayo kama Taifa tungependa kujadili ikiwa ni pamoja na mambo yafuatayo:
  1. Muundo wa Serikali-Tungependa Serikali iwe kubwa kiasi na ya aina gani, masuala ya Serikali ya Mseto (ikiwa chama kinaongoza uchaguzi kikashindwa kupata zaidi ya nusu ya kura zote), mamlaka na madaraka ya Raisi, uthibitishaji wa Bunge kwa viongozi n.k.
  2. Usimamizi na uthibiti wa Rasilmali zetu kama vile ardhi, madini, gesi na kama tutabahatika kupata mafuta. 
  3. Mfumo wa Bunge tunalotaka
  4. Uwakilishi wa wananchi wasio na vyama (Zaidi ya watanzania millioni 30 si wanachama wa vyama vya siasa) na suala la wagombea binafsi 
  5. Masuala ya uwakilishi wa jinsia na makundi maalumu kwenye sehemu za maamuzi
Tutumie muda mwingi katika hatua zinazofuata ili kujadili mambo ya msingi kama nilivyoainisha baadhi yake hapo juu.

Mchakato wa katiba ni mrefu. Niwasihi watanzania wenzangu tujadili kuhusu katiba tunayotaka pasipo kuweka masuala ya udini, maslahi binafsi, itikadi na sehemu ya Jamhuri tunapotoka. Tufanye hivi pasipo kuweka jazba na fujo. Tukifanya hivi tutafika salama. Wanaharakati watumie fursa hii kuwaelimisha wananchi haki zao na pia kuwapa elimu ya kutosha ili waweze kuchangia kwenye mjadala huu. Wanaharakati wasitumie fursa hii kufanya fujo, kuleta vurugu na kupotosha umma.

Mimi binafsi ningependa kuona tunapata katiba yenye maslahi kwa Taifa letu na vizazi vitakavyokuja baadaye. Tuna deni hilo kwao. Hatma ya Taifa hili iko mikononi mwetu. Hekima na busara zinahitajika sana wakati huu. Tutangulize Utaifa kwanza na maslahi ya nchi hii mbele.

Mungu Ibariki Tanzania

Dk. Faustine Ndugulile-Mbunge Kigamboni

15/11/2011

Dr Faustine angependa kupata maoni yako katika suala hili ili kuweza kumjenga kihoja katika kutambua watanzania wanapenda nini katika suala hilo. Kwa mtizamo chanya au hasi.

Saturday 12 November 2011

Short-cut to Heaven!

 Enjoying the siesta!

 Yesterday... was watching the game till dawn!!!
It doesn't cost a thin' here!!

Ha ha haaa

Friday 11 November 2011

Dr. Hemed Abbas Kilima: Ninavyokukumbuka

Sekta ya Afya ya Tanzania imempoteza Mtaalamu aliyebobea katika fani ya macho, Dr Hemed Abbas Kilima (Pichani juu) aliyefariki jana tarehe 10 Nov 2011 kutokana na ajali mbaya ya gari.

Hayati Dr Kilima alikuwa anasafiri kutoka Mbeya kuelekea Dar es Salaam alipopata ajali hiyo pale gari aliyokuwamo ilipogongwa na basi eneo la Al-Jazeera.  
 
Ni habari ya masikitiko kwa wana-taaluma wa afya hususan upande wa macho.  
  
Dr Kilima, mpaka anapoteza uhai wake akiwa bado ni kijana wa miaka 42 tu, alishapata shahada tatu katika fani ya afya zikiwa ni pamoja na:-
  • Shahada ya udaktari wa binadamu kutoka chuo kikuu cha tiba za Afya na sayansi ya Jamii - Muhimbili
  • Shahada ya uzamili katika fani ya macho kutoka chuo kikuu cha Tumaini
  • Shahada ya afya ya jamii kwa macho kutoka London School of hygiene and tropical medicine

Mbali ya hayo, alikuwa ni
  • Daktari bingwa wa magonjwa ya macho kwa watoto (Fellow- Paediatric Ophthalmology) aliyojifunza CCBRT - Dar es Salaam.
  • Fellow wa Eastern Africa college of Ophthalmology
  • Mwenyekiti msaidizi wa chama cha madaktari na wanataaluma wa Macho Tanzania.  
  
Ninamkumbuka Dr Kilima, kwani kwenye kozi ya shahada ya uzamili kwenye fani ya macho (Master of Medicine - Ophthalmology), tulikuwa darasa moja na tulikuwa wawili tu, mimi na yeye, kwa hiyo tulipitia hatua nyingi kimasomo ikiwa ni pamoja na kusoma, kufanya kazi, kufanya tafiti na kujiandaa kwa mitihani. Mbali na hayo tulikuwa tunasafiri sehemu mbalimbali pamoja ndani na nje ya nchi katika kutekeleza majukumu ya fani yetu. 
  
Tulipeana ushauri wa mambo mengi katika masomo na kujiendeleza kitaaluma, na kama tulikuwa tunafuatana katika kisomo na kujiendeleza kama vile mmoja akibandua mguu mwenzie anafuata, na hata nilipomaliza fellowship yangu naye baadaye alijiunga na kozi kama hiyo kwa fani tofauti kidogo tu, na alihitimu vyema mwaka uliopita.  
  
Na pia ndie niliyemuachia mikoba ya Mwenyekiti msaidizi wa Chama cha madaktari na wanataaluma wa afya macho Tanzania kabla sijapata nafasi zaidi katika shirikisho la taaluma hii kwa Ukanda wa Afrika mashariki (Ophthalmological Society of Eastern Africa).  
 
Mpaka anatutoka, alikuwa ni Daktari anayefanya kazi katika hospitali ya rufaa ya Mbeya, na mratibu wa macho kwa kanda ya kusini na nyanda za juu. Hivyo, Taifa limempoteza mtu muhimu ambaye bado alikuwa na muda mrefu wa kuendeleza huduma ya afya na kuwainua wengine. 
 
Binafsi nimempoteza mwenza na mshirika mkubwa kikazi, na pia nimempoteza rafiki wa karibu ambaye nilitarajia kushirikiana naye sana kuweza kuinua fani ya afya ya macho kwa Tanzania. 
  
Bwana alitoa, bwana ametwaa. 
 
Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi, Amen.

Tuesday 8 November 2011

Vote for Mount Kilimanjaro as one of The New 7 Wonders of the World



Mount Kilimanjaro is located in Northern Tanzania, it lies few degree below the equator line.
It is the highest mountain in African continent, the highest point is at Kibo peak which is 5,895 metres above sea level.
It is an amazing mountain because of its location along the tropic, and its peak is covered by snow through out the year. Everything is natural.  
 
Apart from that, the whole of its basement is occupied by wild animals living freely without causing harm to neighbouring villages. 
  
Visiting and climbing this mountain, you will not only reach the highest point in Africa, but also you will enjoy seing ecological diversity and fresh atmosphere which is almost the same all year round. 
  
Few kilometres from Mount Kilimanjaro, you will be able to see the second highest mountain in Tanzania, mount Meru located in Arusha, and if you move further to north west you may get an opportunity to visit Ngorongoro crater, which is one of great wonders of the world filled again with all diversity you may think in the tropics.  
 
Natural beauties of mount Kilimanjaro has attracted me to vote for this mountain to be among the new seven wonders of the world. What about you? Just follow this link and follow instruction to cast your vote for Mount Kilimanjaro by using telephone or online. 
In Tanzania, you can vote through SMS by sending a message to number 15771 from any telephone network.
Sala pekee hazitoshi, piga kura yako tafadhali!
  
The deadline for voting is on 11th Nov 2011 (11.11.11)

Friday 4 November 2011

Man's Facial Image Seen in Ultrasound


A mystical image or sheer coincidence? Either way, that’s one sad ‘nad.
Doctors in Canada were scanning through ultrasound images of a 45-year-old man with a painful mass in his testicles when they did a doubletake. There was a man's face staring up at them, the mouth grimacing as if he were in agony.
"It looked like a man screaming in pain, which I thought was hilarious considering the clinical picture of the poor guy," Dr. G. Gregory Roberts, School of Medicine at Queen's University, Kingston, Ontario, told msnbc.com

Roberts and urologist Dr. Naji J. Touma reported their amazing discovery -- which ranks right up with the grilled cheese Madonna or pancake Jesus -- in a recent issue of the medical journal Urology.
In the article, "The Face of Testicular Pain: A Surprising Ultrasound Finding," the doctors revealed that, upon spotting the distinctive tumor, a "brief debate ensued on whether the image could have been a sign from a deity (perhaps "Min" the Egyptian god of male virility; however, the consensus deemed it a mere coincidental occurrence rather than a divine proclamation."

Click here for full article

Thursday 3 November 2011

Tuesday 1 November 2011

Joseph Machele: Mtanzania Aliyepata Nishani ya Heshima ya Franklin Nchini Mexico

Joseph with assistant of the Ambassador to the US Embassy in Mexico city  Mr.  John Feeley Deputy Chief of Mission.caption

Joseph na Mkewe Mariana

Rafiki na wafanyakazi wenzake Joseph - Ubalozi wa Marekani Mexico
Joseph Machele, Mtanzania ambaye anaishi Mexico city nchini Mexico, amepata tuzo ya heshima ya Franklin (Franklin Award) ambayo hutolewa kila mwaka kwa wananchi wa Marekani au wanaofanya kazi katika idara za serikali ya Marekani ambao mchango wao kwa Taifa la Marekani katika fani mbalimbali za kazi zao umepita kipimo na kuweza kusababisha ufanisi mkubwa wa kazi au kuleta faida kwa uchumi au hali ya usalama kwa Marekani. 

   
Joseph Machele ambaye ni Mtanzania anayefanya kazi katika ubalozi wa Marekani nchini Mexico, ameweza kupata tuzo hiyo kwa utumishi bora na kuwa mbunifu. Allipata siku ya tarehe 12 Oktoba 2011, baada ya kupewa na naibu balozi wa Marekani nchini Mexico Bw. John Feeley.
Kupitia kujituma kwake na maarifa yake binafsi, aliweza kuokoa zaidi ya dola za kimarekani 115,000 kwa mwaka mmoja ambazo zingetumika kulipia gharama za kusafirisha samani na vifaa vya kukodisha na vitu vingine vidogo vidogo kwa ajili ya makazi ya watumishi wageni wanaoenda kufanya kazi kwenye ubalozi wa Marekani nchini Mexico.  
 
Mbali ya Joseph Machele kupata tuzo ya heshima, pia alijipatia kitita cha dola kama zawadi yake katika juhudi zake binafsi akiwa kazini. Alifanikiwa kuokoa kiasi hicho cha fedha kwa kuwashawishi wanaokodisha vifaa hivyo kutoa usafiri wa bure kusafirisha vifaa hivyo, jambo ambalo maafisa wa ubalozi wa Marekani walikuwa wanadhani ni kitu kisichowezekana kabisa. 
  
Hongera sana mdogo wangu Joseph kwa juhudi zako binafsi. Nakufahamu sana tangu kwenye ujana wako, ni mtu ambaye upo makini sana katika kazi zako. Usiishie hapo tu, bali ongeza bidii zaidi kwani mafanikio yako ni sifa kubwa kwetu sote tunaoishi Bara pevu na lenye utajiri mkubwa.

Monday 31 October 2011

World's Population Hits 7 Billion!!


The world's population is said to hit 7 billion today! 
  
There is an increase of world populaton by 100% for the past 50 years. 
  
I am trying to imagine what will happen in the next 50 years. Population increases, food and water reduced, there will be a big imbalance between population's growth and source of human survival on this planet.
Coming to global warming effects......now where are we heading?  
  
Okay, welcome the 7th billion neonate!  

Photo from http://www.ourbreathingplanet.com/

Thursday 27 October 2011

Age Ain't Anythin' ... But Just a Number - Marriage at 120 Years Old

The newly wed couple

 
With family members

At the grand old age of 120, Hazi Abdul Noor has married for a second time and become the world’s oldest bridegroom. 


Six years after his first wife died, he has tied the knot again with Samoi Bibi, 60, in the village of Satghori in North-East India. 
 
Despite looking relatively fresh-faced for someone who has been a centenarian for 20 years, he presides over a family of 122 - including two sons, four daughters and a lot of grandchildren. 
 
This marrieage band was tied on 23 October 2011, and Hazi becomes the oldest man known to be married at the age of 120 years. 
 
The marriage ceremony was attended by more than 500 people. 
 
Source: Mail online

Wednesday 26 October 2011

Monday 24 October 2011

President Paul Kagame Admires The Late Julius Nyerere

Maria Nyerere on behalf of her late husband, receive a National prestigious Medal awarded to the Late Nyerere for his contribution on human rights fights by President Kagame in Kigali, Rwanda

I have been wondering all this time since I came to Rwanda about His excellency President Kagame the way he leads Rwanda....

Being born and grew up in Tanzania during Nyerere's Presidential time, I had no doubts that Rwandan President was taking good ideology of Mwalimu Julius Nyerere (The Father Of Nation), not in all aspects, but at least things which are applicable in Rwanda.

I have been observing Kagame's leadership and legacy, terms of services, communal develeopment, health status and services, country economy ownership, fights against public fund misuse, control of environment, nature and wild life, military training and discipline, living in harmony and peace, guided daily living life, control of chaotic news and National food and social security in general.

Eventually, I discover this truth....
In the interactive session President Kagame spoke of his admiration for the late Julius Nyerere



“I had a chance during my adult life to meet with the former President of Tanzania, the late Mwalimu Julius Nyerere. I was impressed by the way he was full of character and presence – he was the kind of person who never shied away from saying and doing what he believed was good for his people”.





On what he looked for in leaders, President Kagame said that a good leader should be able to integrate different ideas and know how to mobilise suitable players capable of delivering and contributing to the success of the system

Extracted form Kagame's website



Friday 21 October 2011

Gadhafi: Received Brutal Death from Mob Justice

End of former Libyan leader, Mouammar Gadhafi was typically horrible! 
  
The mob justice, that was the ultimate judgement for him which led to his death.
He was murdered brutally, beaten with anything available and anywhere where the kick manage to reach him. He was dragged and soaked on his own blood. 
  
He was shot too, in the head and had some bone shattered. He suffered multiple visceral ruptures from the kicks around his abdomen.  
  
He was undressed without being unbuttoned, his clothes which were already soaked with his blood were simply ripped of into pieces. He was stripped off too and people made fun of his corpse by taking videos and make photo with the laid down Gadhafi's corpse.  
  
He died in severe pain and agony as the mob hit him hard helplessly. He actually witness every stage of his death while suffering from severe pain from kicks, fists, iron bars, dragging on the rough ground and so on. 
  
It was really a brutal and shocking death 

Thursday 20 October 2011

Habari Tata: Gadhafi Kakamatwa / Kauawa?

Kuna taarifa zisizo rasmi zinazodai ya kuwa aliyekuwa Kiongozi wa Libya kwa muda mrefu, Mwanamapinduzi Kanali mstaafu Moammar Gadhafi ameuawa baada ya kujeruhiwa miguu yote miwili katika shambulio la anga la NATO lililolenga msafara wa Gadhafi alipokuwa anatoroka mji wa Sirte.
Inadaiwa ya kuwa chanzo cha kifo cha Gadhafi ni majeraha aliyoyapata kwenye miguu yake. 
 
Kuna madai mengine yanayosema ya kuwa aliyekuwa kiongozi wa mashambulizi ya Majeshi tiifu kwa Gadhafi, Abu Bakr Younus Jabr naye ameuawa katika shambulio hilo.  
  
Wakati huo huo, wasemaji wa jeshi la waasi wa Libya, wanadai ya kuwa wamemkamata Gadhafi akiwa hai katika mji wa Sirte, na kuwa alikuwa amejificha katika shimo na aliomba asipigwe risasi! Kuna muasi mmoja anadai alishuhudia kukamatwa kwa Gadhafi.  
  
Hata hivyo, habari hizi bado alijathibitishwa na kujua ukweli upo wapi.

Wednesday 19 October 2011

CCM: Chama Rasmi cha Upinzani Wa ....

Mambo ya siasa :-((  

Kusema ukweli huwa ni porojo na kuteka saikolojia ya hadhira ambayo mtu anaamua kujinadi mbele yao ili iweze kumpa rungu la kuwachunga au kuwaongoza. 
  
Najaribu kukumbuka pale ambapo "Chama Chetu Maarufu" kilipoweka hadharani nia kubwa ya kujisafisha kwa kuondoa vishubaka vya kufichia waovu ili kionekane safi tena kama kilivyokuwa enzi za Baba wa Taifa.
Kikajipa miezi mitatu kuamua hatma ya wale wevi na wenye tuhuma nzito kujitoa taratibu kwa heshima na staha, vinginevyo cha moto wangekiona. 
  
Sina hakika hicho "Chama Chetu Maarufu" kinahesabuje siku kwenye mwezi mmoja, maana kwa kalenda yetu ... tunafikiri tumeshapiga kona mbili au zaidi za hiyo miezi mitatu. 
  
Kila mara tunasikia wimbo wa hiki "Chama Chetu Maarufu" ya kuwa hakiwezi kuendelea kukaa na watuhumiwa, ni lazima kiwakoroge na kuwamwaga, hata jana kwenye jukwaa la kisiasa, kupitia msemaji wake kilisema hadithi ile ile, ya kuwa ni lazima kitawaondoa, na ati hao ma-bazazi, wanatumia fedha nyingi sana kuhakikisha wanakikandamiza Chama Chao na kuhakikisha kinaingia kwenye kambi rasmi ya upinzani! 
  
Nahisi huu wimbo wa kukisafisha Chama hiki, karibu utatoa vimelea sugu vya kutokusikilizwa tena, kwani hata dawa ukiitumia tu bila mpangilio kwa muda mrefu na mara kwa mara, basi vimelea huizoea na kugeuka sugu na kuendelea kuishi na kuzaana tena kwa kasi kubwa.   
    
Tunangoja siku moja hapo hali ya kushangilia itakapobadilika na kuwa ya kuzomea, halafu sijui wasemaji nao watakuwa wameshaota usugu, na kutafsitri kuzomea huko ni kama vile kushangilia.  
  
Basi na tuiangalie hii bendera hapo juu inavyopepea, kama ipo sawa au ni kinyume. Tuache kuangalia kama ina vitu vyote vinavyotakiwa, bali tuangalie kama kweli inasonga mbele, na imekaa sawa. Kutokea hapo, tunaweza kuamua kama tumeridhika na tunataka kuendeshwa kama bendera ilivyo au tutataka kuiweka sawa na kuendelea na kitu kilicho sahihi. Bila kusahau, tunaweza kuangalia hata na jirani yetu, ... je, naye bendera yake ipo sawa, na tunakubaliana na alivyoiweka, na je tunaweza kumuunga mkono akatuelekeza kule tunapotaka kwenda?  
  
Tumefika wakati wa kuchagua chombo kitakachotupeleka kule tunapotaka kufika (na sio kwenda) tukiwa na imani kweli kitatufikisha, na tuachane na dhana ya kumchagua nani wa kutufikisha bila kuangalia hata uwezo wake, mabadiliko yake yenye tija, uzoefu na historia yake katika safari yetu hii ya maendeleo. 

  
Nimeibuka tu toka usingizini nikajikuta naadika yote haya, ngoja nikapate kikombe cha kahawa nitafakari zaidi....

Monday 17 October 2011

Wednesday 12 October 2011

Saturday 24 September 2011

Chombo cha Utafiti wa Anga cha NASA Hakijulikani Kimeangukia Wapi

mchoro wa kuigiza wa chombo kinapolipuka moto mara kiingiapo katika anga ya Duni
Chombo cha angani (Satellite) kinachomilikiwa na NASA, ambacho kilikuwa anagani kwa zaidi ya miaka 20 kikifanya utafiti wa hali ya hewa, kwa sasa kinasemekana kimekwisha rejea duniani, inasemekana wamiliki wa chombo hicho (NASA) wanahisi kwa kiasi kikubwa kimekwisha anguka duniani, japo hawajui ni sehemu gani kimeangukia.  
   
Awali walitegemea kingeanguka katika bahari ya Pacific, lakini katika hali isiyokuwa ya kutarajiwa, kilipoingia kwenye anga ya dunia (Earth atmosphere) kilionekana kama kimepunguza kasi ya kuanguka, hivyo badala ya kutarajiwa kuanguka siku ya ijumaa, NASA ilikadiria kitaanguka jumamosi usiku au jumapili alfajiri. 
  
Chombo hicho chenye ukubwa kama wa basi kubwa, na kinachokadiriwa kuwa na uzito wa tani 6, mpaka sasa hakijulikani kilipo, na wala hakuna mtu aliyekwisha kutoa taarifa kama wameona mabaki yake. Na kwa kuwa mpaka sasa hivi NASA haijapokea taarifa yoyote ya majeruhi au madhara ya aina yoyote, wanaamini chombo hiki kimeanguka baharini, lakini hawajui ni sehemu gani.  

Bado wantafuta habari ya wapi mabaki ya chombo hiki yataonekana ili wawe na uhakika ya kuwa ni kweli kimekwisha anguka kwenye uso wa dunia. 
  
Pata habari zaidi hapa

Friday 23 September 2011

Chama cha Upinzani Chashinda Uchaguzi Mkuu wa Zambia

Chama cha Upinzani  nchini Zambia, Patritic Front kimefanikiwa kupata ushindi wa urais pale bwana Michael Chilufya Sata (Miaka 73) alipotangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi wa Rais wa nchi hiyo.
Ukiwa ni msimu wake wa nne kwa bwana Sata kugombea nafasi hiyo, safari hii amefanikiwa kumshinda bwana Rupiah Banda, ambaye ndiye alikuwa anashikilia wadhifa huo.  
  
Uchaguzi huu kwa mara ya kwanza ulileta tafrani ambayo ilisababisha Tanzania, ambao ni nchi jirani na Zambia kwa upande wa kaskazini, kufunga mpaka wake na Zambia kuepusha wimbi la wakimbizi na waleta fujo kuingia Tanzania bila mpangilio. 
 
Sata amepata jumla ya 43% ya kura zote halali zilizopigwa, akifuatiwa na Bwana Banda aliyepata 36% ya kura zote halali zilizopigwa. 
  
Ninahisi ya kuwa uchaguzi huu wa Zambia utakuwa umetoa funzo fulani kwa siasa za kiafrika na hasa nyumbani kwetu Tz na nchi nyingine kama Zimbabwe na Uganda.  

Wednesday 21 September 2011

Life is Full of Challenges! Python Hunting

How can you get hold of python without causing harm to it and yourself!

Follow very few and courageous steps like these gentlemen!

 Ensure security for your hand skin, because this will be hand python will try to attack or swallow. Animal skin is the best fooling instrument for the python, It smell like its favourable food eeeh!
Aye, also you avoid to go to hospital for unnecessary anti-tetanus vaccinations.

 Somebody waiting should have very good ears and strong to pull you when the time is due to do so...


 You see good source of natural light which is somehow fearful for the python
But, of course will make you see better...

 Be alerted, very sharp and each hand ready for action...

 Hurrraaaaah!..... Then shout to be pulled out


 Proud python catcher

They consider very well animal rights!! Where are they heading to? May be to a zoo, or return it to the thick forest to protect their domestic animals which are favourite meal for the "stranger" or to sell it to mafisadi!!

I wish I could have known the source of this....., but thanks Mdau for reviving photos.