Member of EVRS

Showing posts with label Egypt. Show all posts
Showing posts with label Egypt. Show all posts

Thursday, 2 February 2012

Egypt (Misri): Vurugu Mpirani zaua watu zaidi ya 73

Habari hii si nzuri kwa wapenzi wa soka, kwani kumetokea vurugu kubwa iliosababibisha vifo vya wapenzi wa soka 73 na wengine zaidi ya 1,000 kujeruhiwa, wengine wakiwa wamejeruhiwa vibaya. Hali hii ilitokea  katika Jiji la Port Said mara baada ya kumalizika kwa mechi ya mpira wa miguu kati ya timu zenye upinzani mkali za Al Masyr ya Port Said na Al Ahly ya Cairo siku ya tarehe 1 Februari 2012.

Mechi hii ilimalizika kwa wenyeji Al Masry kuifunga Al Ahly kwa jumla ya magoli 3-1. Tafrani ilianzishwa na mchezaji wa Al Ahly ambaye inasemekana alifanya kitendo au ishara iliyotafsiriwa kama ni ishara ya vita, hivyo kusababisha mashabiki wa timu ya Al Masyr kuingia kwenye sehemu ya kuchezea mpira (football pitch) na kuanza kuwashambulia wachezaji wa Al Ahly, ambao iliwalazimu kukimbilia kwenye vyumba vya uwanja huo. Na kwenye majukwaa ya washabiki, wale wa Al-Ahly walishambuliwa na wakalazimika kukimbilia sehemu za kutokea, hali hii ilisababisha watu kukanyagana na kuongeza idadi ya vifo na majeruhi.
  
Hakuna juhudi yoyote iliyoonyeshwa na vikosi vya usalama kwa hatua ya dharura, kiasi kwamba watu walikuwa wanashambuliana kwa kila kilichowezekana au kupatikana ikiwa ni pamoja na chupa, mawe, fimbo nk  huku wana-usalama hao wakiangalia tu.   
 
Kutokana na vurugu zilizotokea Port Said, chama cha soka cha mpira cha Misri kililazimika kufuta mechi zote ikiwa ni pamoja na mechi kati ya Zamalek na Ismailia iliyokuwa inachezwa jijini Cairo. Wakati inafutwa, ilikuwa ni wakati wa mapumziko. Kutokana na kufutwa kwa mechi hiyo, kuna wakorofi waliamua kuwasha moto kujaribu kuuchoma uwanja wa mpira huo jijini Cairo, hivyo kusababisha mkanganyiko uwanjani.  
  
Katika picha zilizokuwa zinaonyeswa na kituo cha Tv cha Misri, kilionyesha watu wakishambuliana, na wengine kujihami vichwa kwa kutumia viti ili wasipigwa na mawe kichwani! 
  
Uongozi wa Misri utakutana kwa dharura alhamisi tarehe 2 Feb  2012 kujadili kwa dharura hatua zaidi za kuchukua.  
   
Kitendo hiki ni cha aibu kwa Taifa la Misri na kinaogofya kwenye ulingo wa soka duniani.

Monday, 28 November 2011

Ni siku ya Uchaguzi DR Congo na Egypt

Wapinzani wakidhibitiwa na askari wa Congo katika viunga vya jiji la Kinshasa

Leo ni siku ya uchaguzi wa rais na wabunge katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC)
Katika kampeni za kujinadi kwa wagombea, kulikuwa na matukio mengi ya uvunjifu wa amani ambapo polisi walilazimika kutumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya wafuasi wa vyama mbalimbali waliokuwa wanapingana. 
Katika kampeni, lugha mbalimbali zilitumika kama njia ya mawasiliano kutegemea na mahali kampeni za kisiasa zilipokuwa zikifanyaika. Lugha kuu zilizotumika zaidi katika kampeni hizo ni Kilingala, Kifaransa na Kiswahili.  
   
Huu utakuwa ni uchaguzi wa kwanza wa kipekee kwa muda mrefu, kwani gharama za uchaguzi huu zimegharimiwa na nchi ya Kongo yenyewe.


Askari wa Misri karibu na Tahrir square

Wakati huo huo, nchi ya Misri nayo leo inafanya uchaguzi wake wa kuwachagua wabunge wa mabunge mawili ya nchi hiyo.  
Itakumbukwa kwa wiki kadhaa sasa kulikuwa na maandamano ya kuipinga serikali ya Kijeshi inayotawala nchi ya Misri baada ya kiongozi wake wa siku nyingi, Hosni Mubarak kuachia madaraka kufuatia shinikizo la wananchi kumtaka kuondoka madarakani, ambapo alitii baada ya vurugu kubwa kuzidi nje ya uwezo wa utawala wake.  
  
Pia kwa Misri, uchaguzi huu unahesabika kuwa wa uhuru zaidi kwa miaka zaidi 30 iliyopita.
Kulikuwa na matukio ya ucheleweshaji wa makaratasi ya kupigia kura kwenye vituo kadhaa vya Cairo na Alexandria.  
  
Tunawaombea wamalize uchaguzi kwa amani ili waweze kizijenga nchi zao.

DRC Photo from The Telegraph
Egypt photo from Guardian