Member of EVRS

Thursday 30 September 2010

Tuesday 28 September 2010

Monday 27 September 2010

Kenya Airways: Nao Wamo Kwa Ndege za Mitumba


 Nilikuwa kimya kwa siku kadhaa, kwani nilikuwa mimekabiliwa na majukumu yanayohusu mipango ya maendeleo na utoaji huduma za macho, mpango huu unahusisha juhudi binafsi za wananchi wazalendo na wazawa katika ukanda wa Afrika Mashariki, na kwa kuanzia, Kenya ndio imekuwa ya kwanza kuratibu mpango huu kwa nchi shirikishi za umoja huu wa kanda ya Afrika Mashariki.
Kwa kuwa nilikabiliwa na zaidi ya masaa 40 bila ya kulala kutokana na usafiri kuanza saa 6 usiku na kuondoka usiku wa manane ilhali mkutano ulikuwa unaanza saa 2 asubuhi hadi saa 2 usiku, na baada ya hapo kuandika muhtasari.. hakika siwezi kusema zaidi........



kusafiri, ni kuona mengi na pia kujifunza mengi. Hapo jana wakati narejea Kigali, nilipokuwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta, Nairobi, niliona ndege kwa mbali, nikadhani ni ya KLM, lakini kwa kuwa nimezoea kuona madege ya KLM ambayo huja huku, nikashangaa kwa nini safari hii wameleta ndege ndogo, tena jioni.. ..... wakati huwa zinatua huku usiku na kuondoka usiku huo huo..... nikawa na maswali...


Kusoma jina la ndege likawa halifanani na rangi ya ndege niliyoizoea!, nilihisi bado nina usingizi, na hivyo rangi zikawa zinanichanganya. Nilipata moyo baada ya kuona kuna baadhi ya wasafiri wenzangu nao walikuwa wakishangaa kama mimi. Wengine walikuwa wakikenua meno na kucheka, kwani nao naona walikuwa wanshangaa hizo rangi za ndege kuwa ni za KLM wakati shirika linaloimiliki ni Kenya Airways

Tukutane tena wakati mwingine, kwani safari hii ilinifurahisha kwa mengi ambayo iliniwezesha kukaa miji mitatu, kwenye nchi tatu tofauti kwa siku moja!!

Friday 24 September 2010

Google translator Ruins Swahili-English Meaning

Many people have been laughing when reviewing or translating swahili words into English by using google translator...
I did not pay critical attention regarding these translations until recently when I tried to translate what I had written using google translator.

What came out of it... ugh!....senseless meaning, in fact, if you know well swahili language, you may think something is wrong with your computer or your eyes :-)

It is my hope that google company will review swahili vocabularly and put more appropriate words to enable appropriate translation.

Wednesday 22 September 2010

Vituko Bongo: Mwanaume Mmbeya "Aolewa"

Bongo... kila kukicha hakuishi vituko

Kuna habari hii iliyoandikwa kwenye Global publishers ambapo mwanaume mmoja tena ambaye ana mke, amekuwa na tabia ya kuwapigia simu wake wa wanaume ambao anawajua pindi tu anapowakuta wamesimama mahali popote na mwanamke mwingine

Tukio hilo la aina yake lilitokea Septemba 17, 2010 Sinza ya Kumekucha jijini Dar es Salaam jirani kabisa na hoteli ya Lion ambako mwanaume aliyedaiwa kufanyiwa kitendo hicho anaishi.

Msafara wa magari ya kifahari yapatayo kumi na tano yaliwasili nyumbani kwa mwanaume huyo ndani yake kukiwa na waalikwa walioonekana kuwa na furaha za shamrashamra hizo.


Msafara huo ulipofika nje ya nyumba ya mwanaume huyo mwenye mke ulisimama huku matarumbeta yakipulizwa na watu wakiserebuka kwa ngoma ya Baikoko iliyokodishwa toka jijini Tanga.

Hata hivyo, ilidaiwa kwamba mwanaume huyo ambaye bado kijana alipochungulia nje na kuona wageni akiwemo ‘bwanaharusi’ aliingia mitini kwa kutumia mlango wa nyuma kwani toka jana yake alishanyetishiwa kuwepo kwa ‘ndoa’ hiyo ya aina yake.

Akiongea na waandishi wetu eneo la tukio, mmoja wa wageni waalikwa (hakupenda kutaja jina lake) alisema kuwa, wamealikwa katika sherehe ya ‘ndoa’ ya kijana huyo kwa lengo la kumshikisha adabu na kuachana na tabia yake ya ambea mtaani anakoishi.

Leo Katika Kona ya Siasa: Dr Faustine Ndugulile

Dr Faustine Ndugulile, wakati akitambulishwa na JK kwa wakazi wa Kigamboni siku ya uzinduzi rasmi wa Kampeni jimbo la Kigamboni


Dr Faustine akimwaga sera katika harakati za kuomba kura


Safari ya kugombea ubunge si kazi ndogo.  
Inahitaji maandalizi ya kutosha, uelewa wa hali ya juu kuhusu matatizo ya wananchi unaotaka kuwawakilisha, nia ya dhati katika kuyatatua matatizo bila kutanguliza maslahi yako binafsi na ahadi zinazotekelezeka. 
  
Kwani kipimo cha imani ya wananchi unaotaka kuwawakilisha, kitaoanisha ahadi zako na utekelezaji wake.
  
Safari hii ya kupata ridhaa ya wananchi pia inazua maadui kwa sababu mbalimbali zikiwamo tofauti za kisera na pia maslahi binafsi.   
  
Inahitaji moyo wa dhati, dhamira ya kweli na utashi wa kimawazo kutimiza matumaini ya watu. Na pia inahitaji uimara na msimamo thabiti katika ukweli unaouamini.  
  
Chagua mtu atakaye kufaa na kukuwakilisha vyema.  
   
Habari hii Imenukuliwa kutoka kwa mwanasiasa

Tuesday 21 September 2010

Posting Comments

Dear my readers. 
 
I will do very little modification on posting  comments to this blog.  
  
This is because of overwhelming spams especially on my older posts.  
  
If this will not solve the problem, later on, I will be forced to put comments moderation which I understand will delay your comments to be posted especially at the time where I will not be able to access my mails.  
 
Tupo pamoja

Sunday 19 September 2010

Watoto walemavu wa Tanzania Watumika Kama Kitega Uchumi Kenya

Juzi jioni mtanzania mmoja ambaye anaishi jijini Nairobi kwa muda mrefu sasa aliyejulikana kwa jina la Yohana Kulwa pamoja na mkewe raia wa Kenya walikamatwa na makachero wa Kenya baada ya kugundulika kuwa alikuwa anawatumia watoto walemavu kutoka Tanzania kama mradi wa kujipatia kipato.

Watoto hao wadogo chini ya miaka 10, wamekuwa wakichukuliwa na gari kutoka nyumbani kwa Yohana saa 10 alfajiri mpaka katikati ya Jiji la Nairobi, na kisha wanapakiwa kwenye mkokoteni ambao huanza kuwasambaza sehemu mbalimbali za Jiji la Nairobi ambazo zinapitwa na watu wengi.

Watoto hao hukaa wakiomba kuanzia asubuhi mpaka jioni bila hata chakula, ikifika muda wa saa 9 alasiri, wengi huwa wamechoka sana na njaa, na hivyo kupitiwa na usingizi, ukizingatia huamshwa mapema karibu ya saa 9 usiku.

Ifikapo jioni, watoto hao hujisogeza taratibu kwa kujivuta barabarani hadi kwenye sehemu ambapo gari hilo huja kuwachukua.

Watu walio kwenye mtandao huo, huwa wajanja, kwani jioni uhakikisha ya kuwa mwendesha mkokoteni yupo karibu, ambapo hutumika kukinga watu wasione hao watoto wanapopakiwa kwenye gari na kurudishwa kwa tapeli huyo wa Kitanzania na mkewe.

Siku polisi walipowafuatilia walimkuta mtanzania huyo na mkewe wakiwa wanagalia runinga kwa starehe zao, huku walemavu wao wakiingizwa ndani mmoja mmoja.

Polisi walipohesabu pesa walizoingia nazo hao siku hiyo, walipata jumla ya KSh zaidi ya 13,000 (Karibu ya dola za marekani 150), na inasemekana kila siku watoto hao huja na kiasi kama hicho.

Uchunguzi wa polisi bado unaendelea, na inatarajiwa wezi hawa watafikishwa mahalamani wiki ijayo.

Wakati huo huo, polisi wa Kenya, jana wamekamata watu wengine tena ambao hutumia chokoraa pia kwa mtindo huo huo kwa kuwatumia kama nguvu kazi, tofauti ni kuwa watoto hawa sio walemavu, na walikutwa na jumla ya zaidi ya ksh 2,000 kama makusanyo ya siku hiyo ya jana.

Kwa mtazamo wangu:
Huyo mtanzania anatakiwa kupata adhabu kali, si ajabu aliwachukua watoto hao toka kwa wazazi wao kwa kuwadanganya ya kuwa anawapeleka kusoma au ....., kumbe ni tapeli mkubwa

NB. Watoto hao walionyeshwa kwenye runinga ya Citizen tangu wanachukuliwa na gari dogo asubuhi, kubebwa kwenye mkokoteni, wakiwa kazini, jioni walipokuja kuchukuliwa na mwisho wakati Mtanzania huyo alipokamatwa na mkewe. Na matapeli hao walikiri kufanya mchezo mchafu huo.

Friday 17 September 2010

Toddler survived while playing at a Busy Highway

This toddler was filmed crawling on the busy road in Antalya, Turkey while his mother was fast asleep near the busy highway.

She could not realised that the baby was awake .... and wanted to play with "big toys" passing on the road.

Thanks to the truck driver who saw him and signaled cars to slow down and eventually the baby was rescued.

When the baby was presented to his mother, ... the mother was shocked.

Thursday 16 September 2010

Chunga sana wezi wanaotumia Mtandao wa Mawasiliano

Maendeleo huja na raha Zake. Sula zima la mawasiliano limefikia hatua kubwa sana ya maendeleo, mawasiliano yanakwenda kwa haraka sana, na dunia imekuwa ni ndogo.

Mifano mzuri ni kama vile mitandao ya facebook, blogu, flikr, tweeter nk.
Unaweza kuwasiliana na mtu usiyemfahamu na mkawa marafiki bila hata kuonana au kujuana....lakini kila zuri huja na matatizo yake, suala la mawasiliano nalo halijaachwa nyuma

Kwa sasa mtandao wa mawasiliano umevamiwa na wezi (cyber crimes), ambao wamekuwa wakiwaaibia watu kwa mbinu mbalimbali.

Huko Kenya kuna dada mmoja ameibiwa jumla ya Ksh 100,000 (zaidi ya dola za kimarekani 1,000) kutoka kwa mtu aliyekuwa anajifanya anampenda sana baada ya kuwasiliana kupitia mawasiliano ya mtandaoni kwa wale wanaotafuta wapenzi wa kudumu (soul mates).

Dada huyo alikuwa akiibiwa kidogokidogo kwa kuwa kijana huyo alikuwa anamtumia ujumbe kuwa mara kakamatwa na polisi zinahitajika ksh 20,000, siku nyingine ati malipo ya hospitali, huku akijidai kuwa kwa wakati huo akiwa hana pesa, mpaka atoke hospitali nk. Na dada huyo alikuwa akimtumia pesa kupitia huduma ya M-Pesa akiamini anamtumia mpenzi wake kumuokoa na matatizo ya ghafla yaliyompata.

Kijana huyo mwizi, inasemekana ya kuwa alikuwa akikataa kumpeleka rafiki yake huyo wa kike mahali alipokuwa anakaa, na kwa sasa amepotea kabisa na wala hapatikani kwa simu. Kufika leo, ndio huyo dada akagundua ya kuwa ametapeliwa, na kimsingi ameishiwa na akiba yake yote aliyokuwa amejiwekea.

Nafikiri hili ni onyo kwa watu ambao wanakubali kudanganyika na wezi wa mitandaoni.
Chunga sana kuhusiana na watu ambao wanakuja na mahitaji ya pesa mtandaoni...

Wednesday 15 September 2010

Kampeni za Uchaguzi 2010 Tanzania

Habari hii nimeitoa kwa mwanablogu kijana, Upepo Mwanana ambaye anatarajia kupiga kura yake kwa mara ya kwanza mwaka huu. Na huu ndio mtazamo wake:

Nimekuwa nikfuatilia kampeni za siasa, kwani sitaki kufanya makosa wakati utakapowadia wa kumchagua kiongozi wangu wa baadaye, ukizingatia ya kuwa hii itakuwa ni mara yangu ya kwanza kushiriki katika zoezi zima la kupiga kura za kuchagua viongozi wa nci yetu,

Nimekuwa nikisikiliza kwa makini sera za wagombea mbalimbali na kuzipima kama zina ukweli, ushawishi, na pia kuangalia kama kweli zinatekelezeka au ni changa la macho.

Nahisi naanza kukata tamaa, kwani wanasiasa au wagombea nafasi za kisiasa badala ya kuhubiri sera za vyama vyao, wamekuwa mstari wa mbele kusikiliza mwenzie alisema nini, na wao kusema ya kwao kutokana na wengine walichosema hapo awali, na mwisho hakuna kampeni tena bali ni kupeana vidonge na kujibu mapigo!!!!!

Sie tunaotaka kupima sera tumejikuta tukipima nani ni bingwa wa kujibu mashambulizi, na mara ,,, hatimaye zoezi la kupiga kura litafika.. sasa hapo tutampigia kura nani?, nahisi hatutakuwa tumempata kiongozi atakayekidhi tulichotaka kusikia kabla ya kuamua.

Mpaka sasa mimi naona wengi ni wahuni na matapeli tu. Wanabembeleza wachaguliwe kwa matakwa yao binafsi. Na kwa maono yangu, naona vyama vimeelekeza nguvu na pesa nyingi kwa wagombea urais, kwani kutumia helikopta nyingi na magari utitiri kwa mgombea mmoja, wakati wagombea ubunge na udiwani wakiswaga lami ni kuonyesha ishara ya uchoyo na unafiki tu

HATUDANGANYIKIIIIIII

Tuesday 14 September 2010

Furahia Mzaha: Mchagga Hapotezi Kitu


Mchagga alinunua mbuzi kwenye sikukuu ya idd...

Alipomfikisha nyumbani, akampa maelekezo mpishi wake
Nusu ya nyama ipike kwa ajili ya pilau, na itakayobaki itie kwenye friza!

Kichwa .. tengeneza supu na miguu fanya mchuzi chukuchuku!

Ngozi usitupe eeh, utaikausha na kuifanya mswala.

Utumbo, pikia na ndizi

Mifupa tutawauzia wenye mbwa, tena Massawe anao wawili na wamekonda kwa kukosa chakula.

Mafi yote kusanya na kupeleka shambani, hiyo mbolea.

Mpishi kwa kuona kakosa cha kwake, hata kwato...akamuambia bosi wake

Hutaki na sauti ya mbuzi tufanyie ring tone ya simu yako, mie naweza kutengeneza kwa alfu tu

Nashukuru mdau kwa kunitumia kisogeza siku!

picha pekee kutoka hapa

Monday 13 September 2010

Museveni: Uganda's Life President?

President Yoweri Kaguta Museveni (66 years old), yesterday, was re-elected as chairperson of Uganda's ruling party, National Resistance Movement and presidential candidate for 2011 General elections.

This will be his 4th term if he wins the next year elections, and he will face his old friend and personal physician during guerilla war, Kizza Besigye, who was also elected by coalition of some opposition parties as their presidential candidate.

He cross through un opposed in a meeting attended by more than 15,000 party members. It is said there was another presidential aspirant whose name was eliminated by Uganda's National Electoral Commision.

According to serious observers, they say Museveni popularity is fading year after year, as in 1996 he swooped 75% of all votes, but in 2001 he dropped to 69%, and last elections in 2006, he further dropped to 59%.
For those who believes in African pre-election polls, Museven stands at 45% support, and Kizza stands at 35%.

Museveni, still has strong hold to rural communities which helps him to gain advantages over opposition parties.

This year elections was dominated by some frauds among candidates which provoked some chaos here and there during the election processes especially in the primaries.

Hon. Museveni can image himself among people who are looking for his informations using google search engine. He will be astonished to see what people they want to know about him through internet like this below....
I wish the peaceful elections for Uganda next year.

Sunday 12 September 2010

Miss Tanzania 2010: Genevieve Emmanuel Mpangala

Muda mfupi uliopita, Genevieve Emmanuel Mpangala (pichani juu) ameshinda Taji la Vodacom miss Tanzania 2010 kwenye mchuano mkali uliofanyika katika ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.

Itakumbukwa ya kuwa Genevieve ndiye aliyeshinda taji la miss Temeke 2010.



Pichani juu, Genevieve akitoa chozi mara tu baada ya kutangazwa mshindi na kuvishwa taji la miss Tanzania.


Binafsi namtakia kila la heri na kuwa balozi wetu mzuri kwenye mashindano ya miss world 2010 yatakayofanyika nchini China baadaye mwaka huu.

Saturday 11 September 2010

First Victims of Pastor Terry Jones

Even before Pastor Terry Jones' day for Koran burning arrived. It has been reported that three people were killed in Afghanistan on friday 10th October 2010.

The victims were shot dead at NATO base run by German troops in Afghanistan.

The shooting was provoked by the protestors' acts of stonning the NATO base in response to Pastor Jones announcement that he was planning to continue on the process of burning copies of the Holy Koran.

Pastor Jones, the founder of small church - Dove World Outreach Centre, in Gainesville, Florida, which has about 50 worshippers. He is insisting that the islamic cultural center and mosque scheduled to be built at ground zero at the former WTC should be re-located away from Ground zero, otherwise his plan to burn koran will continue.

Read here for more information.

Friday 10 September 2010

Sikukuu ya Idi na Kazi

Picha: Mmachinga wa huku akiwa kazini akiuza vifaa vya wapenzi wa Urastafari kama alivyo onekana mtaani leo.


Leo ni sikukuu ya Idi.
Hapa Kigali ilikuwa ni siku ya mapumziko, nasikia kwa hapa inasheherekewa kwa siku moja tu.
Tofauti niliyoiona ni kuwa ofisi za serikali, mabenki na maduka machache ndio yaiyokuwa yamefungwa.
Sehemu kubwa ya wafanya biashara walikuwa kazini kama kawaida.
Waislamu kwa hapa Rwanda ni wachache sana.
Eid Mubarak!

Wednesday 8 September 2010

Maonyesho ya Kimataifa ya Biashara Kigali, Rwanda - 2010

Leo ilikuwa ni siku ya mwisho ya maonyesho ya kimataifa ya biashara hapa Rwanda maarufu kama EXPO 2010 yaliyokuwa yakifanyika katika viwanja vya Gikondo.
Nchi mbalimbali zilishiriki zikijumuisha nchi zote za Afrika mashariki na nyingine kutoka nje.
Kwa wengine tumeweza kufaidi kupata bidhaa za nyumbani Tanzania kwa bei ya nyumbani, kwani mara nyingi bidhaa za Tanzania kwenye soko la huku ni ghali, kwani zinaheshimika ya kuwa na ubora wa hali ya juu. Wananchi wakigaguliwa na askari kabla ya kuingia viwanjani, ni upekuzi wa kupapasa mwili wote usije ukawa umebeba silaha na kuleta vurugu
Kuelekea lango kuu la kuingia kwenye maonyesho kwa ndani

Baadhi ya bendera za nchi washiriki

Kibanda cha jadi kilichokuwa na mvuto. Sharti la kuingia ndani ya banda ilikuwa ni lazima kuvua viatu na kuviacha nje kwenye lango la kuingilia humo. Nafikiri wale wapenzi wa kutembea na soksi zilizotoboka, na miguu isiyo oshwa walikuwa wanakiona kibanda hiki ni sumu kwao.



Tuesday 7 September 2010

American Pastor to create Havoc in Islamic World?

Pastor Terry Jones of a small church called Dove World Outreach Center in Gainesville, Florida has a strong impulse to burn the moslem holy book - Koran to mark the rememberance of September 11 attack at WTC twin towers.

He has been warned by the commander of armed forces in Afghanistan General David Petraeus not to do so, because of the after effect reaction in the moslem world as a result of what he is intending to do. But it seems he is not convinced to stop his plans.

Read here

Monday 6 September 2010

Kagame aapishwa kuwa Rais wa Rwanda

Rais Kagame wa Rwanda ameapishwa leo kuwa Rais kwa muhula wa pili.
Sherehe hii ilihudhuriwa na viongozi wa nchi mbalimbali kutoka nchi kadhaa za kiafrika.
Baadhi ya viongozi hao ni kutoka Burkina Faso, Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, Afrika ya Kati, Kenya, Malawi, Ethiopia, Liberia n.k.


Kagame akila kiapo leo.
Rais Kagame akisaini hati ya kiapo huku aiangaliwa na jaji mkuu wa Rwanda Aloysie Cyanzaire


Gwaride lililokuwa limeandaliwa mahsusi kwa shughuli ya leo kwenye uwanaja wa Amahoro.


Katika hotuba yake, Rais Kagame aliwashukuru viongozi wa kiafrika kwa kukubali mwaliko na kuonyesha mshikamano wao. Pia aliwashukuru wanyarwanda kwa kuchagua serikali ambayo wanaona itakidhi matakwa ya maendeleo ya wanyarwanda.
Lakini alikemea vikali tabia za baadhi ya mashirika ya kimataifa na haki za binadamu kwa kuamua kwa makusudi kupotosha ukweli wa amani iliyopo Rwanda, na kuamua kutangaza propaganda za uongo kuhusu hali iliyopo Rwanda kwa sasa.

Alionyesha kushangazwa kwa mashirika hayo kutozingatia hali halisi ya kisiasa ya Rwanda katika kipindi hiki cha mpito baada ya mauaji ya kimbari ya mwaka 1994.

Mwisho alisisitiza ya kuwa hakuna maendeleo yanayokuja bila kuwa na demokrasia (Hiki ni kijembe kwa wale wanaoisifia Rwanda kuwa na maendeleo makubwa sana na huku wakisema hakuna demokrasia kabisa). Na aliyakemea mashirika hayo kuwa yanataka kuchochea gurudumu la umaskini na maendeleo duni kwa nchi zinazoendelea kama Rwanda ( Perpetuates cycle of poverty and underdevelopment).

Alionya ya kuwa Rwanda kamwe haitakubali kuamriwa cha kufanya kama Taifa, akiwa na maana utaifa na mahitaji ya Rwanda ndio yanayopewa kipaumbele.


Quot from Kagame: A successful society, achieves National cohesiveness and common interests.

Hotuba hii ilinigusa sana, hasa ukizingatia juzi nimepokea taarifa ya kuwa kuna mashirika tajiri, eti kwa kuona kuna uhaba mkubwa wa madaktari wa fani fulani za magonjwa katika nchi za kiafrika, basi wanataka kuelekeza misaada yao ambayo walikuwa wakiitoa kwa kutoa mafunzo kamili ya udaktari kwenda kuwafundisha watu watakaowaokota mitaani na kuwapa mafunzo mafupi ya kutibu watu ikiwa ni pamoja na upasuaji ili waongeze idadi ya "madaktari" wa fani hizo katika nchi za kiafrika. (J*^ga kabsaaa)
Nikiwa mmoja wa wadau katika fani hizo zenye upungufu, tuliombwa kutoa mapendekezo kama kipima joto, ingawa wao ati walishakubaliana. Nahisi joto wamekwishalipata.

Picha kutoka Kagame fan club

Sunday 5 September 2010

Rwanda: Paul Kagame Kuapishwa Kesho Muhula wa Mwisho

Kesho, kutakuwa na sherehe ya kuapishwa kwa Paul Kagame kuwa rais kwa kipindi chake cha mwisho cha urais cha miaka 7. Hii ni kwa mujibu wa katiba ya sasa ya Rwanda.
Kwa ujumla Kagame bado anakubalika sana na wanyarwanda. Pichani juu: Katikati ya Jiji la Kigali kama linavyo onekana wakati wa jioni kutoka nyumbani kwangu.

Tangu mwezi wa nne, kumekuwa na marekebisho makubwa ya bararbara ikiwa ni pamoja na upanuzi kwa kuongeza njia mbili kwenye baadhi ya barabara ambazo zilikuwa na msongamano wa magari, na pia barabara zilizokuwa zimeanza kuonyesha dalili ya kuanza kuchakaa, hasa zile barabara maalumu zinazopita kwenye ofisi za balozi na wizara za serikali


Wajenzi ni wachina, lakini hawa sio wale feki, kwani wanafanya kazi kwa makini na kwa haraka, sio kama wale waliotengeneza barabara ya Sam Nujoma kule Dar es Salaam.

Wachina hawa, wana imani kubwa na sementi ya Tanzania, kwani katika ujenzi wa sehemu za wapita miguu, mitaro na kusimika nguzo za taa za barabarani wanatumia sementi pekee ya Twiga kutoka Dar es Salaam, Tanzania.



Shughuli ya kuweka lami mpya ilikuwa inaenda sambamba na kuweka taa mpya na kuondoa za zamani, ambazo baadhi yake zilikuwa haziwaki, lakini wamebadili zote kabisa hasa barabara muhimu.
Kwa sasa barabara zimekamilika na wamemaliza kupaka rangi kingo za barabara ili zionekane kwa madereva kwa urahisi na pia kupanda miti na maua.
Kesho ni siku ya mapumziko, lakini nahisi jumanne nayo inaweza kuwa mapumziko iwapo watu watasheherekea sana kuapishwa huko kwa rais Kagame, kwani watu hupenda kukesha usiku kucha kwenye uwanja wa Taifa wa Amahoro, hivyo kushindwa kufanya kazi siku inayofuata.


Saturday 4 September 2010

Algeria 1 - 1 Tanzania for AFCON 2012 Qualifying Race

Tanzania managed to hold the host Algeria 1 - 1 at an encounter which was dominated by the Desert Foxes - Algeria.

Algeria which is superior to Tanzania in FIFA ranking, fails to score many goals on several opportunities they got. Thanks to Tanzanian goalkeeper who saved numerous number of what was looking to go inside the net.

All goals werescored in the first half, Tanzania got the goal in 34th minute, and Algeria equalised at 45th minute.

Algeria still is facing hard time for the 5th game in a row without any win, and have scored not more than 1 goal among the 8 games they have played so far including today's match.

Tanzania similaly, hasn't won in their last 6 games, but at times had managed to score more than one goal in a match.

Prior to this match, Tanzania coach declare that his team will fight to the last nail knowing they are going to face tough opponents, and he was determined to come out with one point, or even three!

His dream came out true!

Friday 3 September 2010

Vurugu za Mikate Msumbiji!


Juzi usiku nilikuwa naangalia TV Mozambique kupitia satellite dish.

Kwa kuwa sielewi kireno, nilibaki nikishangaa kuona watu wanaume kwa wanawake tena wa rika zote wakivamia maduka na kuiba kila kitu kilichokuwepo, na huku barabarani vijana wa kiume wakichoma matairi ya magari.

Nilimshuhudia dada mmoja labda akiwa kwenye miaka kama 20 hivi akitoka na mabeseni kama 10 hivi kwenye duka lililovamiwa huku akikimbia akiwa na tabasamu usoni. Hakufika mbali kwani alivamiwa na kundi la vijana wa kiume wakiwamo na watoto kama wa miaka 12 – 13 wakampokonya mabeseni yote huku wakimwachia majeraha makubwa kichwani na usoni na huku akiwa tayari kagalagazwa chini.
Yote hii ilikuwa ni purukushani ya kumnyang’anya mabeseni ili na wao wajipatie. Kilichofuatia ni kilio na kicheko kikafutika kabisa usoni pake.

Pia niliwaona akina mama wa makamo na akina baba pia wakiiba unga kwenye duka la vyakula na kukimbia!

Jana ndio nikapata jibu kuwa waliamua kufanya fujo baada ya serikali ya Msumbiji kupandisha bei za vyakula. Lakini kilichowakera zaidi ni kupandisha sana bei ya MIKATE!!!

Polisi waliingilia kati na kufyatua risasi za moto. Vurugu hizi zimesababisha vifo vya watu 7 na wengine kadhaa kujeruhiwa.

Pamoja na kuwa hali leo asubuhi imeanza kutengemaa kidogo, ingawa bado usafiri wa wananchi haujarudi sawasawa, serikali ya Msumbiji imetamka ya kuwa haitapunguza ongezeko la bei kama ilivyokuwa imeahidi jana kwamba itapitia upya.

Swali kubwa…. Tunaelekea wapi sisi nchi za Kiafrika? Je, sera za serikali zetu zina angalia hali ya wananchi kabla ya kufanya maamuzi au…?

Kwangu siamini kuwa suala la kupandisha bei ya mikate tu ndio inaweza kuleta vurugu kama hizi.

Habari za kina click here

Photo: By Reuters

Thursday 2 September 2010

Dr. Faustine Ndugulile Anaomba Kura Yako

Dr Faustine, mwanablogu mwenzetu, ameingia kwenye kinyang'anyiro cha ubunge jimbo la Kigamboni Dar es Salaam.

Ana ujumbe mfupi tu kwa wana-Kigamboni.

Anawaomba kura zao ili waweze kushirikiana pamoja kutatua kero zinazowakabili ili kuleta maendeleo ya kweli kwa Kigamboni.