Member of EVRS

Friday 31 August 2012

UEFA Champions League 2012 /13 Groups


Group A

FC Porto (Portugal)
Dynamo Kiev (Ukraine)
Paris Saint-Germain (France)
Dinamo Zagreb (Croatia)  
 
Group B
Arsenal (England)
Schalke 04 (Germany)
Olympiacos (Greece)
Montpellier (France) 
  
Group C
AC Milan (Italy)
Zenit Saint Petersburg (Russia)
Anderlecht (Belgium)
Malaga (Spain)  
  
Group D
Real Madrid (Spain)
Manchester City (England)
Ajax Amsterdam (Netherlands)
Borussia Dortmund (Germany)  
  
Group E
Chelsea (England)
Shakhtar Donetsk (Ukraine)
Juventus (Italy)
Nordsjaelland (Denmark) 
  
Group F
Bayern Munich (Germany)
Valencia (Spain)
Lille (France)
BATE Borisov (Belarus) 
  
Group G
Barcelona (Spain)
Benfica (Portugal)
Spartak Moscow (Russia)
Celtic (Scotland)  
  
Group H
Manchester United (England)
SC Braga (Portugal)
Galatasaray (Turkey)
CFR-Cluj (Romania)



Group E

Thursday 30 August 2012

Rwanda: Makahaba wauawa na Watu Wasiojulikana

Kumezuka wimbi la mauaji ya wasichana Nchini Rwanda. Mpaka sasa wanaohusika na mauaji hayo hawajajulikana.  
Mauaji hayo yanawalenga wasichana makahaba. Kwa mwezi huu wa Agosti pekee, wasichana 15 wamekwishauawa kwa njia mbali mbali ikiwa ni pamoja na kukatwa katwa kwa vitu vya ncha kali au kunyongwa.  
Jana mchana kuna habari ya kuwa wasichana watatu waliuawa kwa kunyongwa kwenye nyumba moja ambayo ipo sehemu ya makazi ya watu wengi. Mauaji hayo yanahisiwa kufanywa nyakati za mchana.  
Hata majirani walistaajabu kupata habari za vifo hivyo, bila wao kusikia au kuhisi chochote.
Kwa sasa, katika nchi ya Rwanda, masuala ya kuendesha shughuli za ukahaba ni kosa la jinai.  
  
Hakuna shaka mauaji haya hayahusiani na vyombo vya dola, bali kuna uwezekano yanaendeshwa na watu wanaochukia shughuli za ukahaba. 

Tuesday 28 August 2012

Bila Onyo... Mambo hayaendi!


Wakati niliokuwa natembea mitaa ya katikati ya jijini Kampala, Uganda kwenye siku za mwisho wa wiki nilikutana na bango hili. 
Nafikiri nia ni nzuri kuwatishia nyau madereva wasiojali sehemu wanapoegesha magari yao.
  
Lakini naona hilo tozo la adhabu ni dogo, kwani ni sawa na dola 2 tu za kimarekani!  
 
Kilichonkiuna zaidi.... miaka 4 iliyopita, nilipita eneo hili, lilikuwa na uzio kama huu, sasa sijui huko ndani wanajenga nini ambacho kwa miaka 4 hakijaweza kuonekana! 
  
Naendelea kuchanja mbuga!

Saturday 25 August 2012

Rais Kagame Aahidi Kuendelea Kudhamini Kombe la Kagame, Yanga nayo Yapata ushindi Kigali

Rais Paul Kagame akipokea Kombe la Kagame kutoka kwa nahodha Haroub (Kushoto) na Kocha mkuu Saintfiet (Kulia) wa Yanga ambao walifanikiwa kushinda michuano ya Kagame ya Afrika mashariki na kati kwa mwaka 2012
Siku ya Juzi, Rais Kagame wa Rwanda alilipokea kombe ambalo limepewa jina lake kutoka kwa nahodha na kocha wa timu ya mpira wa miguu ya Yanga ya Tanzania.
Mbali ya kulipoke kombe hilo, aliahidi na kupendelea udhamini wake wa kombe hili uendelee hata pale atakapo staafu na mambo ya siasa. 
   
Rais Kagame amekuwa akitoa jumla ya dola za Kimarekani 75,000 kila mwaka kwa Shirikisho la soka la Afrika Mashariki na Kati (CECAFA). Kati ya hizo, dola 60,000 zinaenda kwa washindi wa kwanza hadi wa tatu, na dola 15,000 kuendesha shughuli za michezo hiyo. 

  
Mazoezi ya timu ya Yanga, Kigali

Timu ya Yanga ilienda Kigali, Rwanda kwa mwaliko wa rais Kagame mwenyewe, na imepangiwa kucheza michezo mitatu ya kirafiki, wa kwanza ulikuwa siku ya ijumaa tarehe 24 Agosti 2012 dhidi ya Mabingwa wa soka nchini Rwanda, Rayon sports, ambao wenyeji, yaani Rayon sports, wamefungwa magoli 2 - 0. 
   
Mbali na mwaliko huu walioupata Yanga kutoka kwa Rais wa Rwanda, pia wamepata mwaliko mwingine kutoka kwa Rais wa Tanzania.  
   
Picha na sehemu kubwa ya habari kwa kimombo nimeitoa hapa, na picha na maelezo kiasi ya Rwanda yanapatikana hapa japo yapo kwa lugha ya kinyarwanda!

Sunday 19 August 2012

IDDI NJEMA KWA WOTE!

Blogu ya Hadubini inapenda kuwatakia heri na baraka zote kwa Waislamu popote Duniani katika kusheherekea sikukuu hii ya Iddi. 
  
Wadau wa blogu hii wanaamini katika mfungo wote wa Ramadhan waislamu wote wamekuwa wanaombea amani na utulivu duniani pote. 
 
Tunamuomba Mwenyezi Mungu aziskilize sala zote zilizoombwa wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani na kuzipa baraka zake. 
  
Eid Mubarak!

Rada ya Utata Uwanja wa Ndege Dar es Salaam Imeharibika

Uwanja wa kimataifa wa ndege uliopo jijini Dar es Salaam kwa muda sasa umeshindwa kutoa mawasialiano ya kuongozea ndege kwa kutoa taarifa muhimu za mabadiliko ya hali ya hewa.
Habari hii niliishtukia wakati nilipokuwa naangalia matarajio ya mabadiliko ya hali ya hewa kwa muda wa wiki nzima tunayoianza kupitia mtandao huu, Mtandao huu ulionyesha ya kuwa rada iliyopa kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Dar es Salaam haitoi taarifa yoyote. 
  
Rada hii hutoa vielelezo vyote muhimu vinavyohusiana na hali ya hewa ikiwa ni pamoja na kiasi cha joto, hali ya unyevu, kasi na mwelekeo wa upepo, hali ya mawingu, mvua na radi. Na pia kama kutatokea mabadiliko ya ghafla, basi rada hii hutoa taarifa ili marubani wa ndege waweze kujiandaa au kutoa maamuzi ya mahali pa kutua iwapo hali ya hewa ni mbaya sana. Mbali ya yote hayo, pia rada hii hutoa taarifa ya vyombo vya anga mahali vilipo na upande vinapoelekea ili kuweza kuziongoza ndege na kufika salama sehemu zinapotarajia kutua.

Katika pitapita yangu nikakuta taarifa hii ambayo ikanihakikishia ya kuwa ni kweli rada hiyo imeharibika tangu tarehe 3 August 2012, taarifa hii ilithibitishwa na mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya hali ya hewa, ambaye alidai kuna kifaa kimeharibika ambacho kimesababisha rada hiyo kushindwa kufanya kazi. Kifaa kilichoharibika kitaweza kupatikana sehemu moja tu, kwa wale walioiuzia Tanzania rada hiyo kwa bei ya kuruka, yaani kampuni ya Uingereza (BAE Systems), ambayo ililazimika kurudisha chenji iliyojipatia kiwizi. Lakini kwa sasa, ile chenji ambayo kampuni hii ilirudisha Tanzania, itabidi itumike kwa kurudi tena kwao hao hao waliokuwa wameiibia serikali ya Tanzania ili waweze kutengeneza na kuleta kifaa kilichoharibika! 
  
Kwa sasa marubani wanategemea mawasiliano ya kizamani na kutumia akili yao binafsi hasa kwenye kutua na kuruka, kwani kasi ya upepo na ndege zilizo karibu haziwezi kuonwa na rada hii. 
  
Uwanja wa kimataifa wa ndege wa Dar es Salaam, ni mmoja wa viwanja ambavyo vina ndege nyingi zinazotua na kuruka katika ukanda huu wa Afrika mashariki, kwa hiyo kukaa bila rada kunahatarisha hali ya usalama kwa vyombo vinavyoruka katika anga la Tanzania. Wasiwasi huu umeonyeswa na matangazo ya BBC kupitia idhaa yake ya kiingereza usiku wa jumamosi 18 Agosti 2012.

Sunday 12 August 2012

Dk. Steven Ulimboka Arejea Tanzania

Leo mchana, Dr Steven Ulimboka amerejea nchini akiwa buheri wa afya na nguvu kamili. 
 
Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ghafla ulifurika watu ambao wengi wao hawakutegemea kurudi kwa Dk Ulimboka.
Katika makundi yaliyoenda kumpokea ni pamoja na jopo la madaktari wenzake na wana harakati wa haki za binadamu.

Kwa maneno machache kabisa, Dk Ulimboka amesema ya kuwa ni yeye kwa sasa ni mzima kabisa, na yupo tayari kuwajibika kwa shughuli yoyote ndani ya uwezo wake.  
   
Nao madaktari wenzake, mbali ya kufurahia ujio wake akiwa mzima, wameendelea kusisitiza ya kuwa ni muhimu kwa serikali kuweka vifaa na madawa ya kutosha kuwahudumia wananchi hapa nchini, kwani sio wananchi wote wanaweza kupelekwa nje kwa matibabu ambayo hayapatikani nchini.
 
Neno langu....... sitegemei tena kuwepo na jaribio lingine la kumteka na kumjeruhi mtu huyu. Ni muhimu sana waliolitenda tukio hili wapewe stahiki yao ili kuondoa wingu la uoga na kutokuaminiana. Nina imani jamii ya madaktari na ile ya wanatuhumiwa waliotenda tukio hili wanahitaji kufanya kazi kwa ushirikiano zaidi kuliko hali ya kutokuaminiana iliyopo sasa.

Kila la heri Dk Steven Ulimboka

Uganda wins First 2012 Olympic Medal via Men's Marathon

I do not understand why people they say Ugandan Stephen Kiprotich gold medal win for 2012 London Marathon came unexpectedly! 
  
I am sure this man was determined and he met the qualification standard for participating in the event. Therefore he had an equal chance to clinch the medal like the usual common teams from Kenya and Ethiopia.

Anyway, he fought to the end to clinch the first olympic medal for his country clocking 02:08:11, he was followed by Kenyans Abel Kirui 2:08:27 and Wilson Kipsang 02:09:37 in second and third position respectively. It appears the name beginning with "K" had a lucky chance to clinch a medal!!

Other East African countries marathon athletes could not beat the clock on time as Tanzanian Faustine Mussa finished on 33rd position and Samson Athumani went to the finishing line at 66th position.

The Rwandan fellow Mvuyekure was exhausted, at times he had to walk rather than running, he finished 79th.
The last person to finish olympic for this year was Tsepo Ramonene of Lesotho clocking at 02:55:54 on 85th position.

For full list of men Marathon results click here

Distinguished Medals for "Olympic Veterans"


Just thinking aloud ....... International Olympic Committee should think about giving distinguished medals to countries which are "veteran participants" (Participating for a longer time without winning any medal!)
Probably this will be the stimulant for those countries to wake up....
 

Friday 10 August 2012

Mpaka wa Tanzania na Malawi: Hali ya Wasiwasi Yatanda Malawi

Mara baada ya waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Tanzania, Bernard Membe kutangaza katizo la makampuni yanayofanya utafiti wa mafuta na gesi katika ziwa Nyasa upande wa Tanzania kupitia nchi ya Malawi kuacha kazi hiyo mara moja. Kwa mujibu wa kituo cha runinga cha Taifa cha Msumbiji, kimesema wananchi wa Malawi wanaoishi karibu na Tanzania ikiwa ni pamoja na mji mkuu wa Malawi wa Lilongwe, wameingiwa na hofu ya kutokea vita baina ya nchi yao na Tanzania. 
  
Kwa mujibu wa Kituo cha matangazo ya runinga ya Msumbiji, kauli za Membe na mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya masuala ya usalama na mambo ya nje, Edward Lowasa, zimesababisha baadhi ya wakazi wa maeneo hayo kujiandaa kuhama maeneo yao iwapo mapigano yataanza.  
   
Waziri wa mambo ya nje wa Malawi, Ephraim Chiume, aliwatoa wasiwasi wananchi wa Malawi kwa kusema mazungumzo ya kidiplomasia na Tanzania yamekwisha anza, japo alisisitiza ya kuwa upande wa mashariki wa ziwa nyasa linalopakana na Tanzania ni mali ya Malawi kwa mujibu wa makubaliano ya wakoloni wa kiingereza na Wajerumani unaoitwa Heligoland wa mwaka 1890 ambao Malawi wanadai unatambuliwa na Umoja wa Afrika. 
  
Kwa upande wa Tanzania, hawautambui mkataba huu, ila wao wanafuata ule wa awali kabla ya makubaliano ya wakoloni hawa.