Member of EVRS

Tuesday 31 May 2011

While FIFA is Melting....

My sports attire.
I am just busy, I don't mind about FIFA bluffs!

Sunday 29 May 2011

Football Affairs


The only and the only best team in the world in this season.. Barcelona had won the Europen clubs highest title.
 
As a football fan, I congratulate Barcelona, and I am very sorry for Fergie and Man U fans!
 
When one door is closed, it is time to seach for another one, rather than standing idol and asking your self why this .... closed

Friday 27 May 2011

Artist Weekend!

The world is full of arts and artists, arts and Architectures and so on
I am sure you are one them, just give a thought and work on it, then you are an artist.

I love this at Millenium Park, Chicago, IL

I wish you a nice weekend!

Tuesday 24 May 2011

Waasisi wa CCJ: Je, Tuwape Hongera?

Nilikuwa nafuatilia malumbano au sijui niiteje yanayohusu kuanzishwa kwa Chama Cha Jamii (CCJ) Ambayo kwa mtazamo wangu, ninaona kama yalikuwa yanalenga kuumbuana kwa baadhi ya wanansiasa.

Pia niliweza kumsikiliza kada mmoja wa CCM mwenye asili ya Arusha kupitia kwenye runinga akithibitisha kufanya mazungumzo na viongozi waandamizi walipo serikalini na kwenye Chama Tawala, ya kuwa ni kweli aliombwa na viongozi hao agombee ubunge kupitia CCJ mara usajili wake utakapo kamilika.

Wanao onekana kurusha "bomu" hili, wanaeleza madhumuni ya mpango wa kuanzishwa CCJ yalikuwa ni kupambana na ufisadi ambao ulionekana kukielemea chama tawala, na kama vile chama hicho kilikuwa kimefumba macho na kuziba masikio kukwepa sauti ya chura aliyekuwa anapiga kelele za kuwazomea mafisadi.  
Vyama vingine kama CHADEMA, NCCR-Mageuzi, CUF nk, navyo vipo katika mapambano makali dhidi ya mafisadi.  
 
Kwa mtazamo wangu.... mimi ninaona madhumuni ya CCJ yalikuwa mazuri katika kupambana na rushwa, wizi wa mali za uma, utapeli na kujilimbikizia mali kwa baadhi ya watanzania wachache ambao ni walafi na wasio na utu hata chembe kwa watanzania wenzao.  
Kwa maana hiyo, viongozi au mtu yeyote aliyekuwa mstari wa mbele kuanzisha CCJ ni mtu safi na anayekubalika, kwa mantiki hiyo, wanaotjwa kuwa ndio ufunguo wa CCJ wanapaswa kupongezwa. 
   
Nafikiri watu wengi watakubalinana nami, kwamba hii si kashfa, hawa watu walikuwa wanaona mbali, na inaweza kuwa ndio iliyokuwa changamoto, kwa chama tawala kuja na sera ya kujivua gamba, na chagizo kubwa likiwa limetokana matokea ambayo hayakuwa yametarajiwa na chama fulani, huku wale waliokuwa wanaona kwa macho, walishajuwa nini kitatokea.  
  
Tunaomba wenye "mabomu" ya aina hii, waendelee kuyaleta ili tuchambue mchele na pumba vizuri.

Friday 20 May 2011

Enjoy the coming Weekend at....

I have no obligation, no options, nothing to think about...., no cracking ma head, no shouting, nothing to hear on news media...    no football watching, gotta nothin to loose!
  
I had a long week, full of muscle and brain bumping, and I need my weekend, thoughtless, and ... just relaxing, then thinking about the gym next week, yeah, that is it. 
  
I am not sure about blogging... but some times I encounter something sooo funny than you make think... But I have already made a decision..... 
  
Just join me at the relaxation therapy over this weekend. Cheers!!

Wednesday 18 May 2011

Simple Management of Overweight

Just as I was perusing other blogs to know what other people have in their mind, I came across this important messages for those people who are trying to reduce weight.
 
Strictly I mean, to reduce overweight and not not to gain underweight.. please. 
 
Read full article from Home remedies to understand the causes, symptoms, tips to follow on weight loss process and finally some home remedies which can facilitate excessive weight loss.
There are several other home and herbal remedies for different conditions from this website. In addition, there are healthy and beauty tips all compiled in this website. 
 
Just remember that honey can do a lot of wonders to your health.

Photo from english.peopledaily

Tuesday 17 May 2011

Babu wa Loliondo Keshavuna karibu Shilingi Bilioni 2

Kutokana na hesabu zinazowekwa na watumishi wa Babu wa Loliondo, watu au wagonjwa zaidi ya milioni tatu wamekwishapata kikombe cha dawa tangu alipoanza shughuli hiyo mwezi wa august mwaka jana. 
  
Gharama kwa kila mtu ni ndogo, yaani shilingi mia tano tu, ambazo kwa utaratibu wa kawaida wa TRA haziwezi kuandikiwa risiti, kwani ni chini ya kiwango cha shilingi za kitanzania 1,000 ambazo kisheria lazima uandike risiti. 
 
Kwa hesabu za haraka, Babu Ambilikile amekwisha ingiza zaidi ya shilingi za kitanzania bilioni 1.5, na inakadiliwa akimaliza mwaka atakuwa amezidisha shilingi bilioni 2. 
 
Na kwa kipindi hiki, wataalamu wa hesabu, wanakadiria zaidi ya shilingi trilioni moja, zimekwishatumiwa na watu mbalimbali kwa ajili ya kusafiri kutoka sehemu mbalimbali duniani kuelekea Samunge pekee, ambapo Mchungaji Ambilikile yupo. Hii haijumuishi chakula, malazi, matengenezo ya magari na gharama nyingine zikiwapo za kupata vibali na mawasiliano. 
  
Hizi pesa alizojipatia mchungaji mstaafu hazina ufisadi, kwani kila mtu anajipeleka mwenyewe, japo mchungaji amesisitiza lazima akugawie yeye mwenyewe, sina hakika kama ni udhibiti wa mapato au kuepusha matapeli wasije ichakachua dawa yake. 
 
Lakini wezi wanaonywa, ya kuwa pesa hazikai Loliondo, na ukiziiba, basi vikombe vyote walivyokunywa watu vinajaa tumboni mwa mwizi.... 
 
Habari ndiyo hiyo.....

Sunday 15 May 2011

Fahari au Utumwa wa Kublogu

Kazi ya ku-blogu si ndogo kama wapenzi wa kusoma blogu wanavyofikiria. 
  
Kila siku lazima utafute jambo ambalo litawapa habari mpya wasomaji wako au kuwaburudisha.
Na kama unataka kuwasiliana na watu au kujua nini kinachoendelea kwenye mitandao ya kijamii, basi ni lazima uwe na laptop, kamera ya kunasa matukio, simu yenye uwezo wa kupokea taarifa mbalimbali na nyenzo za kuhamisha taarifa hizo kutoka kwenye kinasio cha kwanza na kwenda cha pili. 
  
Mbali ya yote hayo, kuna gharama za kutumia simu au internet, na pia muda wa mtu binafsi, wakati mwingine unalazimika kula huku ukiwasiliana na kupata habari za watu wengine. 
 
Kaka Fadhy... upoooooo!

Friday 13 May 2011

Ujumbe Katika Nguo

Bado natafakari ujumbe kwenye T-shirt ya huyu ndugu niliyemkuta kwenye kivuko akielekea Kigamboni hivi karibuni.

Nawatakia mapumziko mema ya mwisho wa wiki.... Na kwa wale wapenzi wa mpira wa miguu, najua wengine mtatoka mmenuna kwa siku hizi mbili zijazo :-)

Thursday 12 May 2011

Mla Nyama za watu Aumbuka!

Katika mambo ambayo si ya kistaarabu, kuna mtu mmoja huko nchini Slovakia, aliingia kwenye mtandao wa internet na kuweka tangazo la kutafuta mtu aliyekuwa tayari kujiua na kukubali mwili wake uliwe na huyu jamaa chizi au asiye na ustaarabu.

Cha kushangaza, raia mmoja wa Uswisi alijitokeza na kuwa tayari kuliwa nyama pindi atakapomaliza kujiua. Lakini inaonekana Malaika Israeli alikuwa bado ana shughuli nyingi kiasi cha kushindwa kuja kuitoa roho ya Mswisi huyu.... kwani Mswisi huyo alibadili uamuzi wa kujiua, na hivyo kulifikisha suala lake kwenye vyombo vya usalama.

Baada ya hapo, polisi waliandaa mtego wa kumshika "mla nyama za watu", huku wakimtumia mtu aliyetarajiwa kuliwa kama chambo cha kumnasa huyo "mla watu".

Katika harakati za kumkamata huyo "mla watu", polisi mmoja alijeruhiwa baada ya kufyatuliwa risasi na mtuhumiwa, ingawa polisi nao walifanikiwa kumjeruhi vibaya "mla watu" huyo a.k.a mamba.

Angalia video na habari ya huyu chizi hapa

Tuesday 10 May 2011

Kumbe! Kuna Tofauti ya Kiingereza cha Kuzungumza na Kuandika!

Kimya kikuu ..... 
  
Nilikuwa nyumbani kwa mapumziko mafupi, cha zaidi niliususia mtandao wa aina yoyote, ila , sikuachana na kupiga mitaa, hata nilipofika katikati ya Jiji la Darisalama, kwenye mtaa wa Mosque, nikakumbana na tangazo la kuwahabarisha wateja wa duka fulani ya kuwa kuna bidhaa mpya zilizoingia, tena bango lenyewe lilikuwa kubwaaa! 
  
Basi nilipata burudani tosha baada ya kuungua na joto na foleni zisizo na mwenyewe! 
 
Napenda kuwasalimu tena, baada ya kubisha hodi..