Member of EVRS

Saturday 31 December 2011

Kigamboni Wacharuka Kupinga Ongezeko la Nauli za Kivuko: Uozo Waanikwa

BUNGE LA TANZANIA

OFISI YA MBUNGE WA JIMBO LA KIGAMBONI

Kumb na: KIG/KVK/VOL.1/4                                                                    29 Disemba 2011
 
Mhe. Dkt John P. Magufuli (MB)
Waziri
Wizara ya Ujenzi
Dar es Salaam
 

YAH: KUSUDIO LA ONGEZEKO LA VIWANGO VYA NAULI KATIKA KIVUKO CHA KIVUKONI-KIGAMBONI
Kichwa cha habari hapo juu chahusika.

Wananchi wa Jimbo la Kigamboni wamepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa ya kusudio la kuongeza nauli za abiria, magari na vyombo vingine vinavyotumia huduma ya kivuko kati ya Kigamboni na Kivukoni kuanzia tarehe 1 Januari 2012.  
 
Kivuko hiki ni kiungo muhimu kwa wananchi wanaoishi upande wa Kigamboni ambao wengi wao ni watu wa kipato duni na hawana ajira za kudumu. Ongezeko la nauli kwa asilimia 100 ni kubwa sana na litawaathiri kiuchumi. Nimepigiwa simu nyingi na kuletewa malalamiko mengi katika siku ya leo kuhusiana na mpango huu wa kuongeza nauli. Wananchi wanataka kujua ni vigezo gani vilivyotumika kufikia nauli hizi mpya; vyombo gani vilivyopendekeza, kupitisha na kuidhinisha nauli hizi na wanataka kujua kwa nini hawakushirikishwa katika mjadala wa nauli mpya. 
 
Pamoja na ongezeko kubwa la wakazi na magari yanayotumia huduma ya kivuko, cha kushangaza ni kwamba mapato kwa siku yamekuwa ni takribani Tsh 8 milioni kwa siku kwa muda mrefu sasa. 
  
Ni dhahiri kumekuwa na upotevu mkubwa mikononi kwa watumishi wasio waaminifu wa kivuko. Mapato mengi yanapotea kwa njia zifuatazo: 
 
1.Baadhi ya watumishi wa kivuko kukatisha risiti hususan za magari kwa kutumia vitabu bandia.
  
2.Baadhi ya watumishi kuziuza tena tiketi zilizotumika badala ya kuzichana.
  
3.Baadhi ya watumishi na askari wanapitisha magari na abiria baada ya kupokea malipo ya pembeni.
  
Vilevile mafuta ya vivuko huuzwa kwa wavuvi wadogo wadogo katika maeneo ya Feri.
  
Mambo haya yote yanafanyika pasipo kificho, binafsi nimeshawahi kushuhudia yote niliyosema hapo juu yakifanyika na kuyatolea ripoti kwa uongozi wa kivuko. 
 
Ninaamini kuwa hatua zifuatazo zikichukuliwa mapato ya kivuko hiki yanaweza kufika zaidi ya Tsh 13 milioni kwa siku:

1.Kudhibiti uuzaji wa tiketi za abiria na magari. 
 
2.Kudhibiti ununuzi, utunzaji na matumizi ya mafuta yanayotumika kwenye vivuko. 
  
3.Kudhibiti idadi ya watu na magari yanayovuka bila kulipia huduma hii. 
  
4.Kupunguza gharama za uendeshaji ikiwa ni pamoja na kupunguza idadi ya vibarua. 
 
Kutokana na unyeti wa suala hili, nashauri zoezi hili lisitishwe ili kutoa fursa ya kujadiliana kuhusu upandishaji wa nauli na maboresho ya huduma hii kwa kushirikiana na wadau na wawakilishi wa wananchi katika Jimbo la Kigamboni. 
 
Natumaini mapendekezo haya yatafanyiwa kazi ili kuepuka kuwabebesha mzigo wa gharama za uendeshaji wakazi wa Kigamboni wanaotumia huduma ya kivuko pale Feri. 
 
Naambatanisha nakala ya barua yangu ya tarehe 19 Januari 2011 yenye kumbukumbu namba KIG/KVK/VOL.1/1 kwenda kwa Mkurugenzi Mkuu wa TEMESA ambayo ilitoa mapendekezo ya njia ya kuboresha huduma na vile vile kutaka ushirikishwaji wa wadau katika suala la ongezeko la nauli. Barua hii haijajibiwa hadi hivi sasa. 
 
Natanguliza shukrani zangu za dhati. 
 
Wako katika ujenzi wa Taifa

Mhe. Dkt Faustine Ndugulile (MB)

MBUNGE

Nakala: 
 
1.Mhe. Mizengo Pinda (MB)-Waziri Mkuu
 
2.Mhe. Mecky Sadick-Mkuu wa Mkoa Dar Es Salaam
 
3.Waheshimiwa Madiwani wote-Jimbo la Kigamboni
 
4.Wenyeviti wa Serikali za Mitaa-Jimbo la Kigamboni
  
5.Mkurugenzi Mkuu-TEMESA
   
Habari hii nimeipakua kutoka kwenye wavuti ya Dkt Faustine Ndugulile

Thursday 29 December 2011

Kiwango cha Elimu Jijini London, Uingereza Kinatia Aibu!

Nchi ya Uingereza ambayo inajivunia kuwa nchi mojawapo yenye ushawishi mkubwa katika masuala ya siasa na uchumi. Na pia kuwa taifa mojawapo duniani ambalo watu wengi hupenda kukimbilia huko wakitarajia kupata mavuno makubwa ya fedha kwenye mifuko yao. Na pia watu wengine kukimbilia kusoma huko wakiwa na imani ya kuwa vyeti watakavyovipata huko vitawasaidia kupata kazi kwa urahisi kwenye nchi zilizoendelea za Ulaya na Amerika. 
  
Hali hii inaweza kutoweka hivi karibuni ikiwa juhudi za ziada hazitafanyika kufanya marekebisho makubwa katika mfumo wa utoaji elimu nchini humo. 
  
Takwimu zilizotolewa mwezi wa Juni 2011, zinaonyesha ya kuwa asilimia 25 ya watoto wanaomaliza elimu ya msingi katika jiji la London hawajui kusoma wala kuandika, na wale wanaoenda sekondari, asilimia 20 ya hao wakimaliza elimu hiyo, pia hawawezi kusoma wala kuandika vizuri, na hata ukiwapa kitabu kusoma hadharani, hawajiamini kabisa. 
Habari hii haishii kwa watoto wa shule tu, bali hata watu wazima wanaofanya kazi jijini London, zaidi ya asilimia 15 yao, nao pia suala la kusoma na kuandika linawapa taabu sana! 
 
Habari hizi zilifichuka pale waziri mkuu wa sasa alipokuwa anasisitiza kazi zitolewe kwa vijana wa kiingereza badala ya wahamiaji. Wakati makampuni yatakayoendesha mashindano ya Olimpiki hapo mwakani yalipotoa nafasi za kazi na kuwataka vijana wa kiingereza kujitokeza na kujaza fomu za maelezo, vijana wengi wenyeji walikimbia na kugomea kujaza fomu hizo, ambapo waandaaji wa michuano hiyo walishangazwa na tukio hili. 
    
Katika mahojiano ili kufahamu kwa nini vijana wa kiingereza hawajitokezi, ndipo ilipobainika ya kuwa elimu ndio ilikuwa mgogoro, kwani vijana walikiri ya kuwa hawawezi kujaza fomu hizo kwa sababu hawajui kusoma wala kuandika!  
  
Hata hivyo, kuna mashirika mengine yamekuwa hayaajiri baadhi ya waingereza kwa sababu ama barua zao za maombi ya kazi zinakuwa na makosa mengi sana ya maneno (Poor spelling) ambapo ni karibu ya asilimia 40 za barua hizo hutupwa bila kuwaita kwenye usaili, au wanaoitwa, hudhihirisha wazi kuwa uwezo wao wa kusoma ni mdogo sana. Hii ilianishwa na habari hii hapa 
  
Kwa sasa mke wa Prince Charles,Camilla Windsor, anajihusisha na juhudi za kuongeza kutoa elimu bora kwa watoto wa uingereza ili baadaye waje kuendesha uchumi wa nchi yao ambao kwa sasa unaenda mrama kwani viwanda vingi vinakufa kwa uongozi mbovu, na kwa sasa uingereza uchumi wake unaendeshwa kwa kutegemea kukusanya kodi kwa wafanyakazi na wafanyabiashara ambao wengi wao ni raia kutoka nje ya Uingereza. 
  
Soma makala hii kwa kiingereza inayozungumzia elimu ya Uingereza kwa sasa

Wednesday 28 December 2011

Read Careful and Be Sensible!

Hey, Just be sensible. It is closer to the end of this year!

Photo from Uberhumor

Sunday 25 December 2011

Oh! It's Christmas!

Children enjoying the ride on Christmas day in Dar - Tanzania
Christmas is one of the most celebrated day in the world. 
At this season, everybody express love, peace and harmony.
  
Children usually they enjoy most, of course the parents becomes happy to see sweet smiles from their children, they even forget that the expenditures had just surged for the preparations of the event. To be noticed when they are about to pay the school fees etc :-)
  
Oh my kids, I love you dearly, enjoy the Christmas, as we are celebrating the birth of the holy child. 

Friday 23 December 2011

Picha za Mafuriko Dar es Salaam


Watu wakiokolewa na mitumbwi ya dharura

Bonde la Jangwani

Gari la Serikali likiwa limetumbukia katika Daraja lililobomoka

Rais wa Tanzania akikagua athari za mafuriko Dar

Picha nyingi kutoka kwa Haki Ngowi

Monday 19 December 2011

Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-Il Amefariki Dunia


Kim Jong Il


Rais Wa Jamhuri ya Korea (Korea ya Kaskazini) ama kiongozi mpendwa Kim Jong-il pichani hapo juu leo ametangazwa rasmi ya kuwa alikwishafariki dunia. 
Msemaji wa Serikali ya Korea Kaskazini, amedai rais wao mpendwa alifariki siku mbili zilizopita, yaani siku ya jumamosi tarehe 17 Disemba 2011. Inadaiwa ya kuwa alifariki kwa kupata mshtuko mkubwa wa moyo akiwa kwenye treni katika ziara ya ukaguzi, japo haujafafanuliwa ulikuwa ni ukaguzi wa nini. 
  
Vyanzo zaidi vya habari vinadai kuwa kilichochangia kifo chake ni uchovu mkubwa wa mwili na akili alivyokuwa navyo kiongozi huyu maarufu ambaye anakadiriwa alikuwa na miaka 69, japo mwaka aliozaliwa bado hauna uhakika sana kama ni kati ya mwaka 1941 au 1942. Ingawa anajulikana alizaliwa tarehe 16 February nchini Urusi, na alipewa jina la Yuri Irsenovic Kim kabla halijabadilishwa baadaye aliporejea Korea akiwa na miaka takribani 3.

Kim Jong-Un

Mtoto wake wa kiume ambaye ndio mdogo kuliko wote, Kim Jong -Un, mwenye umri wa miaka 27 ndio anatarajiwa kushika madaraka ya baba yake, japo umri wake bado ni kitendawili kwa madaraka anayotarajia kushikishwa. Kwa sasa mtoto huyu ndiye aliyechaguliwa kuwa kiongozi wa shughuli za mazishi ya Baba yake akiongoza jopo la watu 232 wanaoratibu mazishi hayo yatakayofanyika tarehe 28 Disemba 2011 jijini Pyongyang. 
   
Tangu Korea ya Kaskazini ikombolewe tarehe 15 Agosti 1945 imewahi kutawaliwa na viongozi wawili tu ambao no Kim Il-Sung na mwanaye ambaye amefariki sasa Kim Jong-Il ambaye aliingia madarakani kuanzia tarehe 8 Julai 1994 hadi kufariki kwake hapo tarehe 17 Mwezi huu. 
   
Kim Jong-Il alikuwa anatuhumiwa kuwa alikuwa ni dikteta kwa wananchi wake, na inadaiwa alikuwa hataki propaganda ya aina yoyote, hasa kutoka mataifa ya magharibi kuingia nchini kwake. Na inadaiwa vyombo vya habari nchini Korea ya Kaskazini vilikuwa haviruhusiwi kutangaza habari zozote za nje ya nchi yao!  Kimsingi vyote karibu vyote vya habari nchini Korea ya Kaskazini viinamilikiwa na serikali.
  
Pia kiongozi huyu alikuwa ni tishio kwa nchi majirani hasa kutokana kuwa na mpango wa kutengeneza silaha za kinyuklia kwa nia ya kuwatishia maadui zake ambao walikuwa ni Korea ya Kusini, Japan na Marekani. Hii inaweza kuwa ni moja ya sababu zilizofanya Korea ya Kusini kutangaza hali ya tahadhari mara tu ilipopata taarifa za kifo cha Kim Jong-Il.  

Friday 16 December 2011

European Champions League Draw: Last 16 Fixtures

Lyon (France)                          vs           APOEL (Cyprus) 
  
Napoli (Italy)                           vs           Chelsea (England) 
 
AC Milan (Italy)                      vs           Arsenal (England) 
 
Basel (Switzerland)                  vs          Bayern Munich (Germany) 
 
Bayer Leverkusen (Germany)  vs           Barcelona (Spain) 

CSKA Moscow (Russia)         vs         Real Madrid (Spain) 

Zenit St Petersburg (Russia)     vs         Benfica (Portugal) 

Marseille (France)                  vs          Inter Milan (Italy) 

The first legs will take place on 14/15 or 21/22 February 2012, while the return fixtures are scheduled for 6/7 or 13/14 March 2012.

Thursday 15 December 2011

Wanafunzi Wasiojiweza Rwanda Kuendelea Kusaidiwa Ada ya Elimu

Mkurugenzi wa MTN Rwanda Khaled Mikkawi akikabidhi hundi ya msaada wa MTN-Rwanda kwa mlezi wa Imbuto Foundation Mama Jeannette Kagame
Mfuko wa Maendeleo kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu wa Rwanda (Imbuto Foundation) ambao mlezi wake ni mke wa Rais Kagame, Mama Jeannette Kagame, umepokea kiasi cha faranga za Rwanda Milioni 90 kutoka kwa kampuni ya mtandao wa simu ya MTN-Rwanda kwa ajili ya kuwasaidia vijana waliopo shule za upili kiwango cha kidato cha kwanza hadi cha sita kwenye masuala ya ada na gharama nyingine za shule. 
 
Mfuko huu ni mahsusi kuwasaidia watoto walio katika matatizo ya kimaisha ambao wazazi wao hawajiwezi au hawapo tena duniani. 
  
Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2002, umeshasaidia zaidi ya vijana 5,000

Habari kutoka newtimes

Monday 12 December 2011

Ndio Matokeo ya Kuhukumiwa Kabla Hujatenda Kosa ...


Ikionekana huna kosa.... naye alikuwa ana imani ya kuwa lazima utakuwa na kosa.... Basi chunga sana kufuga Osama!

Thursday 8 December 2011

Talk of the Day as Manchester Clubs crash-out of Champions' League

In England, it is the time for Londoners and not Manchesters





CNN quotes : Manchester United and their city rivals Manchester City both made embarrassing exits from the Champions League on Wednesday.

Roy Keane on BBC : Man U ...."I think their best player tonight was Ryan Giggs. That sums it up - he's 37 or 38, you can't be depending on him. United got what they deserved tonight.


Fergie on Al-Jazeera "We're disappointed, there's no other way you can feel,'' .....
"It's a loss because it's the best tournament in the world."


Supersport says....Manchester United and Manchester City will begin 2012 scrapping with the also-rans of European football after ignominious Champions League exits .......... So used to dining with the continents's aristocrats in the second half of the season, the English champions now face the prospect of the less salubrious and much maligned Europa League.


Skysport narrates ...Manchester's nightmare scenario became a grim reality as both United and City were sent crashing out of the UEFA Champions League before the knockout stage.
Failing to progress from a group containing Otelul Galati, Benfica and Basel must surely rank as one of the lowest points in the managerial career of Sir Alex Ferguson, who could only look on stony-faced as his side were beaten 2-1 away by the Swiss side to slip below their opponents and into the Europa League.



Anyway.....I was looking for positive comments about Manchester Clubs, but I just end up into those.... eventually I abandon  further searching!!

Goodluck Manchesters in Europa League

Monday 5 December 2011

Mwaliko: Sherehe za Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara Jijini Kigali, Rwanda

Umoja wa Watanzania wanaoishi Rwanda unapenda kuwaalika watu wote katika hafla ya chakula na dansi katika kusheherekea miaka 50 ya uhuru wa Tanzania Bara (Tanganyika). 
  
Sherehe hizi zitafanyika tarehe 9.12.2011 jijini Kigali. Siku kama hiyo miaka 50 iliyopita ndipo Tanganyika ilipopata uhuru kutoka kwa wakoloni wa Kiingereza. 
  
Mbali ya chakula (Chenye asili ya Kitanzania) na dansi, kutakuwa na maelezo mafupi ya historia ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambao ndio uliozaa jamhuri ya Muungano ya Tanzania.



Watu wote mnakaribishwa kwa kiingilio kidogo cha faranga za Rwanda 8,000 tu. 
  
Mawasiliano kwa waratibu yameandikwa kwenye kadi za mwaliko. 
 
KARIBUNI SANA!

Friday 2 December 2011

Kenya Taxpayers Money Thrashed: Milimani courts ‘falling apart’

When you look at this photo.... It sounds like a very beatiful building.....

It cost Kenya Taxpayers' money amounting to 1 Billion Kenyan shillings for its renovations which lasted for 8 years since it was commenced!

Kenyan Chief Justice, Willy Mutunga after he toured the premises and witnessed the shoddy job on the building, which cost Sh1 billion. He said .... "To refer to this building as ultra modern is to insult both the English language and the intelligence of Kenyans,"

 
Mutunga sums all this as “administrative corruption and incompetence” and he had no kind words for professionals involved in the work.

  
Barely 10 months after it was commissioned, Chief Justice Willy Mutunga has sounded alarm over the safety of judicial staff and Kenyans using the building whose ceiling has caved-in, with water leaking all over. 

  
Door handles in almost all floors have broken down, lifts including the VIP ones stopped working and the water leakages keep on triggering electric faults. 
 
Get the touch of it here and here