Member of EVRS

Wednesday 30 November 2011

Mchungaji Arusha Atembezwa Uchi Kwa Kugomea Shughuli za Kimila

Mchungaji mmoja wa kanisa la pentekoste Jijini Arusha na ambaye ni mkazi wa kijiji cha Siwandeti, wilayani Arumeru alikamatwa na kutembezwa uchi baada ya kukataa kuhudhuria kikao cha kimila la kabila la wamasaai kilichohusu mambo ya tohara kwa kuwa aliona hakiendani na imani yake ya kidini.

 
Hatua ya kumtembeza uchi kwa takribani Saa 22 katika vijiji zaidi ya vinne na kuogeshwa kwenye maji ya baridi Saa 11:00 alfajiri kulitokana na yeye kugoma kutekeleza hukumu ya kutoa ng’ombe dume kama adhabu ya kutohudhuria kikao cha mila.
  
Miongoni mwa vijiji alivyotembezwa uchi mchungaji Lukumay ni pamoja na Ngaramtoni, Mringaringa, Kenyaki, Olevelosi, Kiranyi na Elerai. 
  
Habari zaidi kutoka kwenye Mwananchi

No comments: