Member of EVRS

Friday 17 February 2012

Waume wa Maswa Watakiwa Kupewa Elimu ya Uzazi

BAADHI ya wanawake wilayani Maswa, Shinyanga, wameomba waume zao washirikishwe katika elimu ya afya ya uzazi ili waweze kufahamu matatizo yanayowakumba pindi wanapokuwa wajawazito.
Ombi hilo lilitolewa juzi katika kijiji cha Gulungwashi kata ya Malampaka mbele ya Ofisa Utafiti wa shirika la Utu Mwanamke, Catherine Kamugumiya, wakati wakibainisha matatizo yanayowakabili kipindi cha ujauzito na kujifungua huku waume zao wakiwa mbali na matatizo hayo.
“Matatizo mengi ya uzazi yanayotukumba sisi wanawake wengi yanatokana na waume zetu kukosa elimu ya afya ya uzazi ukizingatia hawa ndiyo wasaidizi wetu wa karibu pindi tunapopata matatizo haya,” alisema Leah Nghumbi.

Pata habari kamili kupitia Tanzania daima hapa

No comments: