Member of EVRS

Monday 30 July 2012

Watazamaji Wabadili Matokeo ya Waamuzi Kwenye Olimpiki

Kushoto Cho akishangilia alipotangazwa mshindi na picha ya Kulia akiwa na butwaa mara matokeo yalipobatilishwa
 Katika hali isiyo ya kawaida, waamuzi na majaji wa shindano la judo kati ya Cho Jun-Ho wa Korea Kusini na Ebinuma Masashi wa Japan, ilibidi wabadili maamuzi ya kutangaza mshindi pale hapo awali walipomtangaza Cho kuwa mshindi kwa kunyanyua bendera za rangi ya bluu ambayo ndio iliyokuwa inawakilisha mwenye mavazi ya bluu.
Lakini, mashabiki walizomea uamuzi huo, ikabidi majaji na waamuzi wakae tena na kujadili kabla hawajabatilisha matokeo na kumtangaza  Masashi wa Japan kuwa mshindi
Maamuzi yalipobadilishwa

Hali hii inatia wasiwasi ya kuwa majaji hawako makini, au kwa makusudi wanawatoa baadhi ya washindani. Katika angalia yangu, kuna maamuzi waliyotoa kwenye mchezo wa masumbwi hata na mimi yalinipa mashaka.

Habari huu kutoka Euro sport

1 comment:

emuthree said...

Sasa wakikutana na wale wenye hasira, inaweza ikamgeukia mwamuzi akageuzwa hasusa