Member of EVRS

Sunday 29 July 2012

Yanga Bingwa Kombe la Kagame 2012


Timu ya Yanga ya Dar es Salaam, Tanzania imefanikiwa kutetea kombe lake la Klabu Bingwa Afrika Mashariki ambalo kwa sasa limepewa jina la Kombe la Kagame baada ya kuifunga timu ya Azam ya Dar es Salaam pia kwa jumla ya magoli 2 - 0. 
  
Magoli ya Yanga yalifungwa na Hamis Kiiza katika dakika ya 45 na Said Bahanuzi katika dakika ya 90.
  
Kwa sasa, Yanga imefanikiwa kulichukua kombe hili kwa mara ya tano. 
  
Hapo awali, Timu ya Vita Club, kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ilifanikiwa kuifunga timu ya APR ya Rwanda kwa magoli 2 - 1 na kujiwezesha kushika nafasi ya tatu.  
   
Binafsi, nazipongeza timu zote za Tanzania kufanikiwa kufika katika hatua za mbele na hatimaye fainali kuzikutanisha timu za Tanzania pekee

No comments: