Member of EVRS

Wednesday 30 March 2011

Sherehe za Kumuaga Josephine Ulimwengu - Rwanda

Mwishoni mwa wiki iliyopita, Umoja wa Watanzania wanaoishi Rwanda - UTARWA - Ulifanya sherehe fupi ya kumuaga aliyekuwa mwenyekiti wa umoja huo Mama Josephine Marealle- Ulimwengu ambaye amepata kazi mpya ambayo inashughulikia masuala ya watoto kwa nchi sita zilizo katika ukanda wa Afrika ya Kati.
Ofisi yake itakuwa Addis Ababa, Ethiopia.
Kabla ya kupata kazi hiyo mpya, Josephine alikuwa mwakilishi mkazi wa shirika la CARE International kwa hapa Rwanda.

Katika mambo aliyowaasa watanzania wanaoishi Rwanda, aliwasihi kujituma, kufanya kazi kwa malengo ya kujiendeleza kitaaluma na kiutendaji na pia kusisitiza kukumbuka na kufanya shughuli za maendeleo nyumbani Tanzania.
Na mwisho alisisitiza, ya kuwa wasiwe waoga kufanya maamuzi ambayo wanahisi yatawaletea maendeleo kimaisha na kiutendaji.

Mwisho wa kauli mbali mbali za viongozi wa UTARWA akiwepo pia balozi wetu nchini Rwanda, Watanzania waliburudika kwa vyakula, vinywaji na muziki mwororo wa nyumbani ukichagizwa na utani wa makabila mbalimbali ya Tanzania.

Pata habari picha hapo chini!



Mwenyekiti Mpya wa UTARWA Bw,. Thambikeni akisoma risala kwa niaba ya wana-UTARWA

Mlezi wa UTARWA Mhesh. Balozi wa Tanzania nchini Rwanda akitoa wosia

Mwenyekiti aliyemaliza muda wake Mama Josephine Ulimwengu akipokea zawadi ya UTARWA kutoka kwa Balozi Dk Matiko

Josephine akiifurahia kwa moyo wote zawadi aliyopewa

Kauli ya kuwaasa wana UTARWA


Wana UTARWA wanabadilishana hili na lile huku wakisubiri "Ndafu"

Tuesday 29 March 2011

Sababu ya Watu Wengi Kuwahi Kwa Babu wa Loliondo

Kama inavyojulikana... watu wengi wanaenda kijiji cha Samunge kwa "Babu" pichani hapo juu, kupata tiba mbadala ya magonjwa sugu na yasiyotibika katika hospitali za kawaida.  
  
Mbali ya sababu hiyo kuu, kuna baadhi ya watu, labda wengi wanataka kuwahi hasa kwa kuzingatia umri wa Mchungaji mstaafu Ambilikile au maarufu kama "Babu". Kwani watu wengine wamekuwa na wasiwasi ya kuwa ni mzee sana, na kazi anayofanya sasa kuanzia asubuhi hadi usiku inamchosha sana. Hivyo, wamekuwa na wasiwasi labda siku zake za kuishi duniani zipo ukingoni, na hivyo wanataka kumuwahi kabla hajaitwa kwenye hukumu ya haki na ya mwisho!!!!! 
 
Nimekwisha pata habari kwa watu watatu walionithibitishia nia yao ya kuwahi huko Loliondo kuwa sababu nyingine ya muhimu kwa wao kwenda mapema ni huo umri wa Babu!!.
  
Hapa Rwanda, kuna watu wanajiandaa kukodi gari hadi kwa Babu huko Loliondo. 
 
Picha kutoka Bongocelebrity

Friday 25 March 2011

Will be Returned Unopened?

Britain’s oldest virgin says her longevity is thanks to her never having sex.


Clara Meadmore recently celebrated her 107th birthday and says she never bothered bumping nasties with anyone because it seemed like too much hassle.

Clara says she knew she would stay single from the age of 12 and focused on her career.

“People have asked whether I am a homosexual and the answer is no. I have just never been interested in or fancied sex,” says Clara.

“I imagine there is a lot of hassle involved. I have always been busy doing other things.

“I’ve never been bothered about relationships.

“When I was a girl you only had sex with your husband and I never married.” - Daily Voice

Source:

Thursday 24 March 2011

9 Years old Turned to be a Hero


Anaiah on the wheel chair above, some few weeks ago she turned to be a hero by saving life her younger sister Camry by pushing her away out of impending car crash unto them, and let herself being hit!
She knew that her sister will not run fast away from the rushing truck, in her quick mind she saw the best way was to gear the speed of her sister by a pushing her away from the accident stream!

Well.... it is unfortunate, that she lost one of her leg and a kidney, also injured spleen and long way for rehabilitation. But she is still alive!

Read more to see this "shujaa"

Wednesday 23 March 2011

Rais wa Guatemala kumtaliki mkewe Sababu ya Mkewe Kutaka Urais!

Siasa.... kweli ni mchezo usio na maadili wala staha.  
  
Rais wa sasa wa Guatemala anayemaliza muda wake, Alvaro Colom, anatarajiwa kumpa talaka mkewe Sandra Torres de Colom kwa kile kinachodaiwa ya kuwa mkewe anataka kumrithi kiti cha urais.  
  
Mchakato wa kutengua ndoa hiyo umekwisha anza kwenye mahakama ya Guatemala na utachukua kama mwezi mmoja kukamilika.  
  
Katiba ya Guatemala, hairuhusu mtu yeyote aliye karibu kiundugu au ki-uwenza na rais aliyepo madarakani kugombea kiti cha urais baada ya muda wa rais aliyepo madarakani kumalizika kikatiba. 

Guatemala itafanya uchaguzi wake mwezi septemba mwaka huu.

Habari zaid kwa kiingereza, soma hapa

Monday 21 March 2011

Healing by Believing: Kupona kwa Imani

Makala hii aliyoitoa Subi kwenye WAVUTI imenivutia sana.

Hii inatokana na wananchi wa kawaida, viongozi wa kiserikali na kidini, matajiri na raia wa kigeni waliokulia kwenye dawa zilizohakikiwa, kusahau yote na kwenda Loliondo kwa Babu kupata kikombe cha dawa ya aina moja ambayo inatibu maradhi ya aina yoyote. 
  
Na pia dawa hii imeleta chuki kwa baadhi ya watu wanaojiita ni mitume wa Mungu au Manabii na kufikia hata kumlaani Babu wa Loliondo kwa kumuhusisha na wale wahubiri wa uongo walioandikwa katika Biblia takatifu, lakini baadaye ilikuja kugundulika ya kuwa hao manabii na wahubiri wa neno la uzima wameanza kupoteza waumini katika makanisa yao, na kuna uwezekano mkubwa ndio sababu ya wao kumpigia kelele Babu wa Loliondo!

Kutokana na wimbi kubwa la watu kukimbilia kwa Babu, serikali ya mkoa wa Arusha imelazimika kutoa vibali vya usafirishaji vya muda kwa baadhi ya magari, ili kuwezesha kupungua kwa nauli inayotozwa kwa sasa kwa wagonjwa kuelekea Loliondo.

Bofya hapa kwa Subi upate habari picha.

Sunday 20 March 2011

2011: Bitter Year for Our Earth!

New War zone has erupted in Libya.
Gaddhafi attacking his feloow country men identified as rebels
UN is attacking Gaddhafi arms.

Arabic world is facing revolutionary changes, some countries is chaotic situation.... people loosing life and power.....
 
Japan is facing hard time following natural disaster, the strongest quake in near future, followed by Tsunami. 
More than 17,000 people feared dead, and now the country sufferring from presumed deadly radiation disaster into the water, soil, plants, animals... 
Effects will be known over ten years to come....  probably, will reach the neighbouring countries...

Ivory Coast, innocent women, just gunned down, simply someone just seized the power, and doesn't know the word . NO...

Poverty, HIV crises,  .......

This is just the beginning of 2011, and not 2013!

Wish you a lovely sunday full of prayers!

Thursday 17 March 2011

Puzzle From an Eye Corner

A little girl was sent to ana eye doctor after sustaining injury on her left eye following a blunt trauma from a fellow friend. The girl was complaining that the injuried eye was not seeing clearly.

An eye Doctor decided to examine both eyes thoroughly and finally he checked her vision, and he could not detect any deficient. He decided to do the visual field test by what they call confrontation test, where the girl had to fix her uncovered eye to the uncovered eye of the Doctor.

The eye doctor was puzzled to note that the girl was able to lacate and count accurately the fingers in all fields including the one an eye Doctor could not see!

The eye Doctor decided to put his fingers behind the girl's head, but yet the girl counted accurately the fingers!
The Doctor turned his head at his back to look for any puzzling event, but he just saw his usual wall at his back with nothing which can explain the girl's response, he then  pulled his chair and sat down with a deep a thoughts.

He eventually told the girl that her eye is okay, will recover from pain and she will be able to see clear in few days, but he finally asks her, how did she managed to see fingers behind her back?

What she answered... The Doctor was embarassed and admitted that he had learnt a lesson.

My readers, it is time for you to give your thoughts!!

Why do you think the Doctor turned his head and look behind his back wall when the girl was able to count fingers behind her back correctly?
Can you explain how did the girl managed to see the finger behind her back?
Can you guess the answer the girl gave to the Doctor?

I promise, if you get 50% or above from these questions, you are absolutely genius!!!

Wednesday 16 March 2011

Fly With Air Tanzania: The Wings of Kilimanjaro

I need your support! 
 
Kindly remove those bugs who are draining my life through corruptions. 
 
Support me, please come on board, I promise to make you happy.
Without you... I am as good as dead!  
 
Pleeeeaaaaaaaaaaase!

Have you changed your mind!

Thank you for your support... Fly with Air Tanzania!

Tuesday 15 March 2011

Kona ya Siasa: CCM Waanza Kudonoana

Katika kile kinachoonekana fukuto la moto ndani ya chama tawala cha Tanzania (CCM), kumeanza kutokea shutuma za kulaumiana ndani ya chama hicho.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, mkutano wa UVCCM ambao ulifanyika  Kibaha, mkoa wa Pwani, ulihitimisha kikao chao kwa kutoa kauli kali kwa mawaziri wakuu waliopita, mmoja akiwa kamaliza muda wake wakati wa awamu ya tatu, na mwingine muda wake ulichakachuliwa mapema na kulazimika kujiuzulu. 
  
Shutuma zililengwa kwao ati kwa sababu waliishauri ama serikali au Chama Chao kuhusu masuala ya nchi na wanachi au kurekebisha mfumo wa utendaji na kujibu hoja za baadhi ya wapinzani kupitia kwenye vyombo vya habari badala ya kutoa ushauri kwenye vikao vya Chama hicho au kumshauri mwenyekiti wao kwa faragha!  
   
Vijana hao walidiriki kumshauri ati mwenyekiti wao awatose hao mawaziri wakuu wastaafu ambao ni wajumbe wa Halmashauri kuu ya chama hicho ili kukinusuru chama hicho, kwani wastaafu hao wana nia ya kuwania urais 2015 kwa staili ya kukichafua chama au mwenyekiti wao......
Si hapo tu, tumesikia pia kuna baadhi ya mawaziri wamezuiliwa kuendelea na utendaji wa kazi zao kwa kuzingatia sheria, ati kwa sababu kasi yao ni kubwa mno na inahatarisha amani! 
  
Mimi binafsi sioni tatizo lolote kwa mtu kusema ukweli kutokana na hali halisi, sipendi kuwasemea chochote hao wanaotishiwa kutoswa, kwani wanasema msema kweli ni mpenzi wa MUNGU! 
   
Pia ina ashiria ya kuwa kuna kikundi kinachotaka kuendesha Chama hicho, kwani suala la kumuambia mwenyekiti wao awatose, ni kukiuka demokrasia ndani ya chama hicho kwa kumfanya mtu mmoja kuwa na maamuzi ndani ya chama hicho, kwangu mimi naona huo ni ubabe zaidi kuliko busara. 
  
Mimi ningependa kusikia watu wanajadili namna ya kutatua matatizo yaliyopo Tanzania na sio kuanza kuwauma wale wanaosema ukweli au kuweka wazi matatizo yaliyopo nchini.  
 
Maendeleo ni kwa watanzania wote na sio ya mtu binafsi, tabaka la watu au chama fulani!
Nawashauri baadhi ya wanasiasa wetu waende Loliondo kwa Babu kupata tiba ya fikra na vitendo!!. :-(

Sunday 13 March 2011

Did I experience the Japan Quake Effects in Africa

Japan Quake disaster has triggered multiple problems
  • Huge devastation following sweeping of houses, property and lives
  • Poor weather condition at this time of season where the temperature especially at night is freezing. Forecast has shown that by wednesday the highest temperature will be 5'C and lowest being 0'C.
  • There is greater shortage of water and food, some people have reported that now feeds on only juice as the "full meal". Many shops and supermarkets are closed.
  • Nuclear plant is in danger of explosion, as the first nuclear reactor exploded yesterday releasing some few dangerous radioactive materials in the surrounding, by which nuclear specialist have concluded that they are not really harmful to the body, but advised people to be evacuated at least 20 km away within the radius of the nuclear plant!
  • Numerous people are missing. Rescue teams uncover many dead bodies than rescuing stranded victims.

Unpredictable events
  • An old man was rescued 18 km offshore after suffering two days alone in cold without food. He was found on top of his house's roof.
  • Cars were found in the corridors of houses
  • Boats and ferry were found clugged several kilometres within the mainland.
  • Miraculous stories as how people survived the Tsunami hit.

On my side:, on friday morning (at +2 GMT) while I was outside my house preparing to go to work, I had a feeling as if I am gonna fall, the feeling which I usually get when I am in the the train or bus, and then the train/bus starts moving while I am standing without any support. I had to hold my hand on wall, as I thought I had some kind of imbalance which I could not explain.
Later I heard that there was Tsunami in Japan, and while noting the time when the quake hit Japan, I realised that it was almost close to the time I had that feeling at +2 GMT location, right in the mid or heart of Africa. I am not sure whether this was just a coincidence from, or in fact, there was a kind of global movement which by chance I happen to get its feeling.

My condolences to all families who have lost their love ones from this disastrous Quake in Japan.

Friday 11 March 2011

Japan Yakumbwa na Tsunami

Tetemeko kubwa la ardhi limetokea km 150 kutoka ufukwe wa Japan karibu na mjo wa Tokyo kama saa 3 zilizopita na kusababisha maafa makubwa.


Tetemeko hilo lilikuwa na nguvu za 8.9 katika vipimo vya tetemeko.

Pwani ya Japan ilipigwa na mawimbi yenye urefu wa mpaka mita 4 hadi 10 na kusababisha mafuriko katika jiji la Tokyo na miji mingine.

Mitaa imejaa maji nab ado yanaongezeka, mito inafurika, barabara na madaraja yanabomoka, na watu walio kwenye magari wanashuhudia maji yanawafuata kwa kasi na kuwazoa bila kujisaidia.

Kibaya zaidi, kituo cha kusafisha mafuta kimojawapo kimelipuka moto mkali sana ambao unaonekana kuvielemea vikosi vya kuzima moto.

Tahadhari imetolewa kwa watu wanaoishi karibu na Japan ikiwa ni pamoja na Sehemu ya Urusi, Indonesia, Philippines, Taiwan, Visiwa vya Marshal, Fiji, Guam, Papua New Guinea, Kiribati, Hawaii. Sehemu nyingine ni Australia, New Zealand, Amerika ya Kusini hasa Chile na Ecuador, pia hadi Mexico ya kuwa wajiandae na kuchukua tahadhari kwani kuna uwezekano maeneo hayo kufikiwa na Tsunami hii. Imekadiriwa ya kuwa kwa sasa hivi, mawimbi ya bahari kutokana na Tsunami yanasafiri kwa kasi kubwa.

Mpaka sasa huko Japan, kuna vifo kadhaa vimekwisha tokea na watu wengi hawajulikani mahali walipo.

Serikali ya Japan imewaomba wananchi waliopo eneo la janga, waelekee sehemu zenye usalama ambazo zipo kwenye miinuko au majengo marefu yaliyo imara.

Wednesday 9 March 2011

Trip Advisor: Dirtiest Hotels in Europe


Some of the hotels were picked as dirtiest in Europe as reported by travellers to Trip advisor network

  1. Club Aqua Gumbet, Turkey - Here they reported that whenever there is a rain, sewarage water floods the pool
  2. Altin Orfe Hotel, Icmeler, Turkey - Complaints were related to air condition systeme to drip water over the bed!
  3. Cromwell Crown Hotel, London, UK - Carpets dusts the legs whenever you walk over them
  4. Corbigoe Hotel, London, UK - Filthy stained walls!
  5. Park Hotel, London, UK - Bed bugs crawling over the bed
  6. Hotel de Lantaerne, Amsterdam, Nerherlands - Unsuitable for human!!

Other hotels were regarded as dirty due to multiple spotted bed sheets, freely moving mice in every room, stinky rooms like wet animals etc

If you want to laugh, just pound here

Tuesday 8 March 2011

Happy Women's Day!

Leo ni siku ya Wanawake Duniani.
Kuna kila msemo unaohusu kuwaenzi akina mama, kwani umuhimu wao unajulikana duniani kote.

Sina jipya la kuongeza zaidi ya kuwapongeza wanawake wote Duniani!

Kila la heri na furaha kwenye siku ya wanawake Duniani!
    Happy Women's Day!
       Feliz Dia da Mulher!
              ¡Feliz DĂ­a de la Mujer!
                  Jour heureux de femmes!
                      Giorno felice delle donne! 
                             ХчастлОĐČыĐč ĐŽĐ”ĐœŃŒ Đ¶Đ”ĐœŃ‰ĐžĐœ!
                                    ćčžă›ăȘć„łæ€§æ—„!
De gelukkige Dag van Vrouwen!
GlĂŒcklicher Frauen-Tag!

Sunday 6 March 2011

Mkutano wa Mwaka wa Umoja wa Watanzania Waishio Rwanda - UTARWA

Jana Jumamosi Umoja wa watanzania waishio Rwanda walifanya mkutano wa mwaka katiaka hoteli ya Foeyes ambayo inamilikiwa na watnzania hapa mjini Kigali, Rwanda.
Mkutano huo ulikuwa ni wa kujadili mambo mbalimbali yaliyotukia katika umoja huu kwa mwaka mmoja uliopita ambao ulikuwa wa mafanikio sana.

Mbali ya hayo, pia ulipokea taarifa kutoka ofisi ya ubalozi wa Tanzania hapa Rwanda kuhusu matukio mbalimbali yaliyotokea nyumbani Tanzania tangu mkutano wa mwisho uliofanyika mwaka jana. Miongoni mwa taarifa zilizopokelewa ni pamoja na milipuko ya mabomu huko Gongo la Mboto na hali ya tatizo la umeme nyumbani na hatua zinazoendelea kuchukuliwa.

Mbali ya mkutano huu, kulikuwa na chakula maalumu cha kitanzania kiliandaliwa kikisindikizwa na muziki wa kitanzania pia. Vyote vilifanywa kama kuukaribishwa mwaka mpya wa 2011.

Pata habari picha hapa chini:

Wajumbe wakiingia kwenye chumba cha mkutano

Ukumbi wa Mikutano hapa Kigali, Rwanda ulifanyika katika mgahawa wa Kilimanjaro ndani ya Foeyes Premier Hotel

Maandalizi ya mwisho kutoka kwa viongozi wa UTARWA

Wajumbe wakipitia dondoo kabla ya mkutano kuanza


Mkutano ukiendelea chini ya Uongozi wa mwenyekiti Josphine M- Ulimwengu kabla hajang'atuka rasmi huku akiwa na mgeni mashuhuri mhesh Balozi wa Tanzania nchini Rwanda Dk Matiko aliyekaa katikati



Thursday 3 March 2011

Uongo wa Waziri Mkuu Pinda Bungeni!!

Kwa wale wanaokumbuka katika kikao cha Bunge la Tanzania kilichopita, Spika Makinda alimwagiza Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema kuwasilisha ushahidi kimaandishi kuthibitisha ya kuwa Mhesh Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Pinda alitoa taarifa ya uongo bungeni kuhusiana na mauaji yaliyotokea Arusha mara baada ya polisi kuzuia kufanyika kwa maandamano hayo.

Itakumbukwa ya kuwa Spika Makinda alikataa ushahidi huo kutolewa bungeni na kufafanua ya kuwa aliagiza uletwe kwa maandishi tu.

Godbless Lema aliwasilisha ushahidi wake akibainisha kwa ujumla uongo 10 ambao Pinda aliutoa katika bunge.

Soma hapa kwenye blog ya Mnyonge... upate ushahidi wote wa Mhesh Lema

Wednesday 2 March 2011

Creek Technology of Human Beings!


Thanks Mdau for this funny caption!