Mkutano huo ulikuwa ni wa kujadili mambo mbalimbali yaliyotukia katika umoja huu kwa mwaka mmoja uliopita ambao ulikuwa wa mafanikio sana.
Mbali ya hayo, pia ulipokea taarifa kutoka ofisi ya ubalozi wa Tanzania hapa Rwanda kuhusu matukio mbalimbali yaliyotokea nyumbani Tanzania tangu mkutano wa mwisho uliofanyika mwaka jana. Miongoni mwa taarifa zilizopokelewa ni pamoja na milipuko ya mabomu huko Gongo la Mboto na hali ya tatizo la umeme nyumbani na hatua zinazoendelea kuchukuliwa.
Mbali ya mkutano huu, kulikuwa na chakula maalumu cha kitanzania kiliandaliwa kikisindikizwa na muziki wa kitanzania pia. Vyote vilifanywa kama kuukaribishwa mwaka mpya wa 2011.
Pata habari picha hapa chini:
![]() |
| Wajumbe wakiingia kwenye chumba cha mkutano |
![]() |
| Ukumbi wa Mikutano hapa Kigali, Rwanda ulifanyika katika mgahawa wa Kilimanjaro ndani ya Foeyes Premier Hotel |
![]() |
| Maandalizi ya mwisho kutoka kwa viongozi wa UTARWA |
![]() |
| Wajumbe wakipitia dondoo kabla ya mkutano kuanza |
![]() |
| Mkutano ukiendelea chini ya Uongozi wa mwenyekiti Josphine M- Ulimwengu kabla hajang'atuka rasmi huku akiwa na mgeni mashuhuri mhesh Balozi wa Tanzania nchini Rwanda Dk Matiko aliyekaa katikati |








