Member of EVRS

Showing posts with label UTARWA. Show all posts
Showing posts with label UTARWA. Show all posts

Sunday, 6 March 2011

Mkutano wa Mwaka wa Umoja wa Watanzania Waishio Rwanda - UTARWA

Jana Jumamosi Umoja wa watanzania waishio Rwanda walifanya mkutano wa mwaka katiaka hoteli ya Foeyes ambayo inamilikiwa na watnzania hapa mjini Kigali, Rwanda.
Mkutano huo ulikuwa ni wa kujadili mambo mbalimbali yaliyotukia katika umoja huu kwa mwaka mmoja uliopita ambao ulikuwa wa mafanikio sana.

Mbali ya hayo, pia ulipokea taarifa kutoka ofisi ya ubalozi wa Tanzania hapa Rwanda kuhusu matukio mbalimbali yaliyotokea nyumbani Tanzania tangu mkutano wa mwisho uliofanyika mwaka jana. Miongoni mwa taarifa zilizopokelewa ni pamoja na milipuko ya mabomu huko Gongo la Mboto na hali ya tatizo la umeme nyumbani na hatua zinazoendelea kuchukuliwa.

Mbali ya mkutano huu, kulikuwa na chakula maalumu cha kitanzania kiliandaliwa kikisindikizwa na muziki wa kitanzania pia. Vyote vilifanywa kama kuukaribishwa mwaka mpya wa 2011.

Pata habari picha hapa chini:

Wajumbe wakiingia kwenye chumba cha mkutano

Ukumbi wa Mikutano hapa Kigali, Rwanda ulifanyika katika mgahawa wa Kilimanjaro ndani ya Foeyes Premier Hotel

Maandalizi ya mwisho kutoka kwa viongozi wa UTARWA

Wajumbe wakipitia dondoo kabla ya mkutano kuanza


Mkutano ukiendelea chini ya Uongozi wa mwenyekiti Josphine M- Ulimwengu kabla hajang'atuka rasmi huku akiwa na mgeni mashuhuri mhesh Balozi wa Tanzania nchini Rwanda Dk Matiko aliyekaa katikati



Sunday, 25 July 2010

Mkutano wa Watanzania waishio Rwanda

Jana tarehe 24 julai 2010, umoja wa Watanzania waishio Rwanda tulikutana kama kalenda yetu ilivyokuwa imepanga, ulikuwa ni mkutano wa kwanza baada ya kuanzisha rasmi umoja huu ambao kwa ufupi unaitwa UTARWA na ulifanyika katika eneo la ubalozi wa Tanzania, Rwanda.

Uongozi mpya wa umoja huu chini ya Mwenyekiti wetu Mama Josephine Marealle-Ulimwengu (Katikati katika picha hii chini) ulipanga mikakati mbalimbali ya kuuendeleza umoja huu katika mpangilio maalumu wenye viambatanisho na ufuatiliaji wa matukio mbalimbali ya umoja, ikiwa ni pamoja na malengo yanayokusudiwa kwa muda maalumu. Katika masuala muhimu yaliyojadiliwa ilikuwa ni pamoja na kuwa na ofisi ya kudumu ikiwa pamoja na samani, tovuti, na pia kuanzisha klabu kwa ajili ya kubadilishana mawazo na pia kuandaa matamasha ya michezo hasa ya kujenga afya.


Watanzania kwa umoja wao, waliweza kuchanga papo hapo pesa ambazo zilitosha kununulia mashine ya kudurufu karatasi.


Uongozi wa UTARWA, pia uliweka wazi kwa majadiliano mti wa mawasiliano waliouandaa, ambao utaweza kuunda mtandao wa Watanzania wote wanaoishi Rwanda. Njia hii itawezesha mawasiliano kuwa ya haraka.

Pichani juu, maelezo kuhusu mti wa mawasiliano yakitolewa kwa wajumbe wote ndani ya ofisi ya ubalozi wa Tanzania, Rwanda.
Shughuli nyingine ambayo uongozi umekuwa ukifanya, ni kuandaa tovuti ambayo itakuwa na taarifa za wanachama wote, ikiwa ni pamoja na familia zao kadri mwanachama atakavyojaza kwenye fomu maalumu ya kuingia uwanachama. Na hii data base itakuwa inaweza kuonwa na viongozi tu, iwapo mwanachama atataka taarifa zake, basi ataweza kuzipata.

Pichani juu, wakati wa utambulisho wa tovuti ya UTARWA, ambayo itakuwa na taarifa nyingi za nyumbani, hapa Rwanda, habari za magazeti na blogu mbalimbali.


Pichani juu, baadhi ya wajumbe wa UTARWA wakisikiliza kwa makini maelezo yanayohusiana na tovuti.
Katika shughuli zilizopangwa baadaye, ni kuchangisha pesa ili kutunisha mfuko wa jumuiya ya akina Mama wa Kitanzania waishio Rwanda, na vitaandaliwa vyakula maalumu vya kitanzania hapo tarehe 3 oktoba 2010.



Tuesday, 25 May 2010

Umoja Wa Watanzania Wanaoishi Rwanda: UTARWA wapata Viongozi

Takribani wiki 2 zilizopita, Watanzania waishio Rwanda tumeweza kufanikisha kuunda umoja wetu ambao unajulikana kwa kifupi kama UTARWA.
Jumuiya hii iko chini ya ulezi wa Balozi wa Tanzania nchini Rwanda. Jumuiya hii au umoja huu uko mbioni kusajiliwa na una madhumuni makuu ya kuwakutanisha Watanzania waishio Rwanda, na pia kupeana taarifa na kusaidiana pindi Mwanachama anapopata tatizo lolote.
Zoezi la kuandikisha wanachama likiendelea kabla ya kuanza mkutano


Wajumbe wakipitia rasimu ya katiba ya jumuiya kabla ya kuifanyia marekebisho ya mwisho na kuipitisha

Wajumbe wakisikiliza kwa makini hotuba ya Mhe Balozi wa Tanzania nchini Rwanda Dr Matiko Chacha Marwa ambayo aliitoa baada ya kupata viongozi wa Jumuiya.
Katika mambo aliyoyasisitiza ni kuwasihi Watanzania kuchangamkia fursa ya kufanya biashara Rwanda ambako kuna soko kubwa la bidhaa za Tanzania kwani zina viwango vya ubora wa hali ya juu kuliko bidhaa nyingi hapa.
Balozi Marwa Alitoa ushauri kwa watu wajihamasishe na kusambaza taarifa za kuja Rwanda kufanya biashara, na pia alisisitiza ya kuwa Serikali ya Rwanda imefungua milango kwa wanajumuiya ya Afrika Mashariki kuingia Rwanda na kufanya shughuli halali bila kulipia viza.
Viongozi wa UTARWA chini ya mwenyekiti Josephine Marealle-Ulimwengu (wa sita kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na mhesh Balozi Marwa (Wa tano kutoka kushoto)


Mambo yakiendelea baada ya mkutano, wajumbe wakiendelea kukifumua kiswahili kwa furaha, kama aonekanavyo mdau mkuu wa blogu hii (mwenye kofia maalumu ya Tanzania) akiteta jambo kwa furaha :-)