Member of EVRS

Friday 30 October 2009

Mtafaruku wa Kubandika


Wapitiao njia hii mtaniwia radhi mkiona mambo hayaendi vyema.

Nimekuja kugundua unapoitwa kuwa msimamizi wa mitihani (external examiner) na kupewa jukumu la kutamka kwamba mtahiniwa huyu ameridhisha baraza la watahini na hivyo anastahili kufaulu mtihani ili asubiri graduation.. Ni adhabu kubwa.

Kwani inabidi na wewe urudi tena kwenye vitabu na kubukua ili mtahiniwa asije akakugonga nyundo ya kisogoni.

Kwa wiki mbili zijazo nitakuwa na kibarua cha kutoa maamuzi hayo. Mkiona blog imevaa suruali pwete, basi mjue vijana wamenitolea macho kweli kweli. Taabu lugha... kifaransa na kiingereza, lazima uvume kotekote ili wasikupige chenga.

Wikiendi njema

8 comments:

Fadhy Mtanga said...

Kila la kheri kaka. Ni matumaini yangu mambo yatakwenda uzuri.

Yasinta Ngonyani said...

Nakutakia wikiend njema kaka Chib na kila kitu kitakuwa sawa

Masangu Matondo Nzuzullima (MMN) said...

Naijua sana hiyo kazi. Usipokuwa makini unaweza kujikuta wewe ndiyo unafanya hiyo PhD badala ya mwanafunzi mwenyewe. Kasheshe inakuja pale mwanafunzi anapokuwa ametumia nadharia ambayo bado ni ngeni kwako. Inabidi uchepuke kweli ili usiachwe nyuma. Ndiyo maarifa yanavyosonga mbele.

Nenda ukatimize wajibu huo muhimu sana kitaaluma. Matunda yake daima huja na ridhiko linaloletwa na kujua kwamba umesaidia katika kueneza maarifa "mapya" hapa duniani. Kazi njema mkuu!

Faith S Hilary said...

Lots of luck kaka! I hope you will be totally fine! God Bless! xx

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...

amen!

John Mwaipopo said...

kila la heri. kazi ngumu hiyo ati!

chib said...

Jamani nawashukuru sana, nilikuwa nimezama kwenye buku japo nisiende kuwaaibisha wa-Bongo huku mitaani. Nipo fiti sasa, na wala sio kwamba nimeegesha, kwamba ukinitikisa basi nimebaki kama kikaragosi. Nimeshiba kabisa

Simon Kitururu said...

Nahisi nimechelewa hapa!:-)
Ila nakuaminia Mkuu!