Member of EVRS

Friday 9 October 2009

Obama: Apata Nishani ya Amani ya Nobel 2009

Rais wa Marekani, Barack Obama, ameshinda tuzo ya amani na Nobel 2009 baada ya kushika madaraka ya urais kwa miezi 9 tu!

Kuchaguliwa kwake kumekuja kwa mshangao wa wengi na bla kutarajiwa, kwani watu wengi hawakuwa wamemfikiria, na katika majina yaliyokuwa yanatajwa hapo awali, yeye hakuwemo. Mpaka sasa haijajulikana ni nani aliyempendekeza.

Pia ni kiongozi wa kipekee ambaye amepewa tuzo hiyo kwa juhudi za amani, hata kabla matunda ya juhudi zake hayajaonekana hasa huko mashariki ya kati.

Wasemaji wanasema hili ni pigo jingine kwa utawala wa rais aliyemtangulia George Walker Bush ambaye utawala wake ulichukuliwa kuwa wa mabavu kwa nchi za mashariki ya kati.

Binafsi, nampongeza rais Obama kwa mafanikio na ushindi huo.

5 comments:

John Mwaipopo said...

hii inatosha kwa mimi kwa sasa kusema duh!

John Mwaipopo said...

nahisi hili jamaa lichawi!

Yasinta Ngonyani said...

Nami pia nampongoza sana Hongera Barack Obama.

chib said...

John...., yaani, umenifanya nifurahi weekend hii yote. Sijui niseme huyu jamaa ana kismet au vp!!

Baraka said...

Nyota yake ni angavu