Member of EVRS

Monday 28 February 2011

Maudhi ya TBC1 Usiku wa Manane!


Shirika la Utangazaji la Tanzania, kupitia kituo chake cha TBC 1 jana usiku lilizidiwa na maarifa ya teknolojia pale kiliposhindwa kuoanisha picha na sauti kwenye kipindi kilichokuwa kinarushwa muda wa saa 7 za usiku wa kuamkia leo kwa saa za nchi za Afrika mashariki. 

Nilikumbana na tatizo hilo wakati nilipokuwa nimetoka kazini usiku kwa saa za sehemu nilipo ilikuwa bado ni mapema kidogo kuliko Tanzania. Wakati TBC 1 ikiwa inarusha matangazo ya kituo cha televisheni cha Urusi (RT) ambacho kilikuwa na matangazo yanayohusiana na utafiti wa kisayansi kwa kutumia panya maalumu.  
  
Badala ya kusikika sauti za matangazo yaliyokuwa yanatangazwa, kulisikika milio ya muziki wa taarabu, tena huenda nyimbo hizo zikawa ni zile za kwenye harusi. Kwa ufupi, ilikuwa ni kero kwa sisi tuliokuwa tunataka kusikiliza maendeleo ya sayansi na teknolojia duniani. ilichukua kama nusu saa kukiwa na tatizo hili, na baadaye TBC 1 maji yaliwazidi kimo, wakaamua kuondoa sauti kabisa kwenye matangazo ya muda huo, na kubakiza picha pekee. Hapo ilitubidi tuendeleena kuangalia TV "bubu", hadi ilipofika saa 8.00 za usiku (EAT) nikaamua kulala kwa kuona ya kuwa nilikuwa napoteza muda tu.

Nilimkumbuka Tido Mhando ambaye aliacha au kuachishwa kazi TBC kwa madai ya kuwa mkataba wake ulikuwa umekwishamalizika huku kukiwa na fununu zilizokuwa zimezagaa ya kuwa aliwaudhi watu fulani wakati wa kampeni za uchaguzi wa oktoba 2010 na hivyo kuamua kutoongeza mkataba wake kwenye shirika la TBC.

Bado najipa moyo ya kuwa hilo lilikuwa ni tatizo la bahati mbaya, japo inashangaza kuona mafundi wa mitambo (IT) wa TBC walishindwa kurekebisha tatizo hili kwa zaidi ya saa moja, na kuachia taarabu ikiunguruma kwa zaidi ya nusu saa.

Mwendo mlima!

Sunday 27 February 2011

Makazi ya Rais Joseph Kabila Yashambuliwa

Watu ambao bado hawajajulikana au ambao imeamuliwa wasitajwe majina yao leo hii wameshambulia makazi ya rais wa jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo bwana Joseph Kabila katika eneo la Gombe jijini Kinshasa, ambako katika eneo hilo kuna ofisi nyingi za balozi za nchi mbalimbali.
Walinzi wa makazi hayo walikuwa makini na kufanikiwa kuwaua washambulizi hao kwa jumla ya 6 papo hapo na wengine kukamatwa.

Inasemekana kwa uchache, watu tisa wamekwishapoteza maisha. Habari ambazo bado zimetoka punde, zinadai waliokuwa wameshambulia makazi hayo ni makomandoo, na walikuwa na silaha kubwa za moto. Inadaiwa wakati wa shambulizi hilo, Rais Kabila alikuwepo kwenye makazi yake, ingawa kuna taarifa nyingine zinadai hakuwapo muda huo, ila alirejea baada ya kusikia kuna tukio katika makazi yake.

Mara baada ya milio ya risasi kusikika, watu waliokuwa karibu na makazi ya rais Kabila walitawanyika kwa mbio kali sana.

Kwa sasa barabara zote karibu na Makazi ya Kabila zimedhibitiwa kwa askari na vifaru vikiwa vimeziba njia zote za kuelekea makazi hayo ya Rais.

Rais Joseph Kabila anatarajiwa kumaliza muhula wake wa urais baadaye mwaka huu, na kutakuwa na uchaguzi mwingine hapo Novemba mwaka huu.

Friday 25 February 2011

Wish you a lovely weekend

This week has been very busy for me  
  
Just like busy people in Libya with different purposes!!  
  
I just want to wish you a lovely weekend. Hopefully Arsenal fans will enjoy the coming sunday!!!!!


I am just... thinking aloud!

Wednesday 23 February 2011

Gaddafi's speech excerpts



What is your comment regarding this speech!!

Monday 21 February 2011

TANZIA

Umoja wa watanzania wanaoishi Rwanda (UTARWA) Unatoa taarifa ya masikitiko kwa Watanzania wote ya  kuwa ndugu yetu Kitila Mkumbo amefiwa na Kaka yake mkubwa (wa kwanza katika familia) huko Dar-es-Salaam. Mwili wa marehemu utapelekwa Singida kwa Mazishi.
  
Mwanafamilia mwenzetu Kitila Mkumbo ameondoka leo mchana kuelekea Singida tayari kwa shughuli za maziko. 
  
Tafadhali tuwakumbuke familia ya Kitila katika wakati mgumu walionao.

  
Mwenyezi Mungu ailaze Roho ya marehemu pema peponi. Amen.

Sunday 20 February 2011

Uganda: We Cannot Help You

Yoweri Kaguta Museveni, has joined the club of longest serving African presidents after winning the 4th term presidency term by scooping over 68% of all the votes casted on last friday.

The first runner up. Kizza Besigye gained 26%, and less than 6% of the presidential votes were shared among other presidential aspirants. 
  
Besigye has repeatdly say that this elections was fraudulent and should be disregarded. He added that there were a lot of corruptions especially to buy local parties electoral observors, in particular, from opposition parties. He further claims that Museven will be evicted in Egypt's style if he forces himself into country leadership.  
 
Many international observers casted their voices that presence of armoured millitia men and police forces, had created fear among voters which necessitated some of them to abandon voting exercise. 
   
Other East African countries are still astonished to see thier co-member Uganda violating the democraticy by bending the limitations of presidencial terms and assuming the kingdomship. This has serious consequences on the move to establish East African Community with common market and currency.

This is similar to Libyan issue, when President Ghaddafi was urging to have one sovereign government for Africa, while himself had been in power for more than 4 decades.
Many African head of States appeared to have ignored his proposal simply because he was preaching contrary to what he was doing.

Friday 18 February 2011

Rwanda: Kuanza Kufundisha Masomo kwa Kinyarwanda Kwenye Shule za Msingi

Hivi karibuni Nchi ya Rwanda imeamua kuanza kufundisha masomo ya shule za Msingi kwa Kinyarwanda, na pindi watotot watakapoingia shule za sekondari ndio wataanza kujifunza masomo yote kwa kiingereza.

Hatua hii imekuja muda si mrefu sana tangu Serikali ya Rwanda kubadili ghafla mfumo wa masomo na lugha rasmi kitaifa kutoka kwenye lugha ya kifaransa na kuingia katika lugha ya kiingereza.  
 
Nia na madhumuni ya kuanza kufundisha kinyarwanda shule za msingi, ni pamoja na kukuza lugha asili na pia kuwapa nafasi watoto kujifunza kikamilifu sarufi na mambo mengine kadhaa ya kinyarwanda. 
  
Kwa sisi wageni, na baadhi ya wanyarwanda waliozaliwa na kukulia nje ya Rwanda, huwa tunapata changamoto kusoma maandishi ya lugha hii, kwani mengine yanavyo andikwa na kutamkwa ni tofauti kabisa. 
  
Nimeshashuhudia baadhi ya wanyarwanda wakisoma matangazo kwa kinyarwanda, na kufikia mahali wasijue neno fulani lina maana gani kutokana na tofauti kati ya maandishi na yanavyotamkwa.  
  
Natoa mfano rahisi kabisa, jina Kacyiru hutamkwa kama "kaachiru", na neno lingine kama Kimicanga hutamkwa kama "Chimichanga", na kali kidogo ni Kimironko ambalo hutamkwa kama "Chimirong'o", nyingine yenye ka-ugumu kiasi ni Kicukiro wao wanatamka "Chichuchiro".
Hii ni mifano tu, bado kuna nyingine ngumu zaidi. 
  
Kuna baadhi ya watu wameanza kulalamika na suala la kubadili kwa haraka lugha za mawasiliano na kufundisha, lakini kwangu mfumo huu wa shule naona hauna tofauti sana na ule tulio nao nyumbani Tanzania, kwani nasi shule za msingi tunatumia kiswahili, japo kuna wachache wameanza kuvuruga matunda ya vijana wetu wanaomaliza sekondari kwa kuwapika nusu nusu na kutoka wakiwa wabichi.  
  
Nawatakia mapumziko mema ya mwisho wa wiki!

Thursday 17 February 2011

Mlipuko wa Mabomu Tanzania: Tunajifunza nini?

Wahanga wa mabomu ya Gongo la Mboto wakigaa gaa na maumivu huku wakiendelea na kupata huduma sakafuni katika hospitali zetu

Usiku wa kuamkia leo, viunga vya Gongo la Mboto kulikuwa na balaa la aina yake mara baada ya mabomu kulipuka kutoka kwenye maghala ya Kikosi cha jeshi la Wananchi wa Tanzania huko huko Gongo la Mboto.

Maghala yote ya kuhifadhia mabomu yanasemekana yameangamia kabisa ikiwa ni pamoja na mabweni mawili ya askari, magari na nyumba kadhaa za wananchi walikuwa wanaishi jirani na eneo la kikosi hicho.

Wanajeshi waliokuwa kwenye mabweni, inasemekana wamesalimika baada ya kukimbia mara milipuko ilipoanza.
Chanzo hakijajulikana, na huenda kisijulikane kutokana na mazoea ya kutotangaza taarifa za ukweli. 
 
Wakazi wa maeneo ya tukio walipagawa kutokana na milipuko iliyoanza kwenye muda waasaa 2 usiku mpaka alfajiri, na milio hii ilisikika karibu maeneo yote ya Dar es Salaam.

Taarifa mbalimbali zinasema watu wengi wanahofiwa kufariki, na tayari idadi inayozidi 25 wamekwishatambuliwa kufariki. na mamia kadhaa kujeruhiwa. 
  
Kutokana na mtawanyiko wa watu, wengine walijikuta wametoka mbio kutoka Gongo la Mboto hadi Msasani bila kujijua, ni bahari tu ndio iliyowashitua kuwa wamefika ng'ambo ya jiji na hawawezi kuogelea kukimbia zaidi. Pia kuna watu walijikuta wamekimbilia kwenye miji mingine na kusahau sehemu ambazo jamaa zao wanaishi.

Cha kushangaza zaidi ni pale baadhi ya mbwa walipokutwa nao wamekimbilia chini ya uvungu wa vitanda vyumbani mwa watu (Hii imethibitishwa) labda kwa kuogopa kelele za milipuko au kusalimisha maisha yao. 
  
Sijajua kama kuna haja ya kuipa ushauri serikali kuhusiana na uhifadhi wa mabomu au wamekwisha pata funzo kwa sasa hasa ukizingatia tukio lingine la mabomu yale yaliyolipuka Mbagala miezi kadhaa iliyopita.

Picha hiyo hapo juu nimeihamisha kutoka kwenye mtandao wa Michuzi.
Pata picha zaidi kutoka kwa Michuzi

Wednesday 16 February 2011

Czech Doctors: Mass Resignations

It is likely health sector in Czech will collapse soon if strong measures will not place within a short time.
This is due to massive resignations of Czech doctors in protest for low salaries when they compare to other sectors which have less working hours as compared to Doctors.
So far, around 20% of all doctors have resigned, and much more are expected to resign in near future.
Czech has nearly 20,000 doctors.

Currently, the gross payment for Czech doctors which includes overtime, averages at USD 2,650 per months, that is before taxation.

The threat for resignation has been on pipeline since the end of last year, but probably it was not taken seriously by Czech government.

Low salaries is the fifth on the list of 13 reasons which made Czech doctors to resign, among others is financial mismanagement in hospitals and other you can read here

Czech has been faced with repeated doctors strike for various reasons like in 2005, private doctors had to show their angers following late re-imbursements from services they offered, and in Feb 2007 there was another protest against Czech health Insurance conduct.

As usual, the group of people who will be highly affected are ordinary people and not politicians who plays a key role in National decisions.

Tuesday 8 February 2011

Sababu ya Adimiko Langu

Yote ni maisha.

Kwa kipindi fulani nilikuwa nimeshindwa kuparaza blogu hii kwani nilifikwa na mkasa kidogo, wahenga wanasema ajali haina kinga.

Nilikuwa nimelazwa hospitalini kwa mara ya kwanza japo kwa siku moja baada ya kukumbwa na ajali. Kwa sasa nimesharuhusiwa na nipo nauguza vilivyobakia bakia nyumbani.

Tutaonana pindi nitakapokuwa na nafasi, kwani nimeshauriwa na daktari ati nipumzike,sijaelewa kama kublogu ni kazi au ni ruksa kama nimeambiwa kupumzika.

Yote kwa yote, leo niliguswa sana na mjadala wa bunge nikiwa siamini kuona wapinzani wakitetana kama vile ni maadui wakubwa!

Kila la heri kwenu nyote!

Wednesday 2 February 2011

Dar es Salaam, Tanzania

Leo nimekumbuka nyumbani!! 
 
Just enjoy a glimpse of Dar es Salaam City along the Zanzibar Ferry port, Tanzania

Tuesday 1 February 2011

What is the Meaning of This?!!!

Just imagine... this notice has been painted in the room where only adults use it... The bag for used clothes, is just there, and easily noticed, but ......
Does it mean, that people are irresponsible or they are uncivilised? 
  
Just look on this one below from another country.... The dustbin is just there, and rubbish are piled up just aside the dustbin ......
I got these two captions recently... I am still puzzled!