Member of EVRS

Sunday 31 October 2010

Miss World 2010: Miss USA, First Runner: Miss Botswana, Second Runner: Miss Venezuela

Mashindano ya Mrembo wa Dunia yaliyofanyika jana Sanya, nchini China yamemalizika kwa Mrembo wa Marekani, Alexandra Mills kuibuka mshindi, na kufuatiwa na Mrembo wa Botswana, Emma Wareus na nafasi ya tatu ilichukuliwa na Mrembo wa Venezuela, Adriana Vasini.  
  
Warembo wengine waliofanya vizuri katika mashindano hayo ni pamoja na Mrembo wa Kenya na wa Namibia  
   
Mrembo wa Tanzania alikwenda kushiriki katika mashindano hayo. Ila amepata cheti cha ushiriki kama walivyopata warembo wengine wote walioshiriki.  
    
Photo from missworld

Saturday 30 October 2010

Yemen: Seems to be the New Head-quarter of Al-Qaeda Now

Two parcels originating from Yemen were intercepted at Britain and Dubai while they were on their way to Chicago.  These bombs were targeted to the Jewish authorities.  
  
At Dubai, a bomb was found hidden in a printer and professionally, a closed circuit was connected to a mobile phone chip inside that printer.  
   
The parcels were sent using different internation carriers, UPS and FeDex companies. 

Read more details at this link

Friday 29 October 2010

Tafakari, Halafu Toa Jibu

Jamani, nilisema sitoi tena mambo ya uchaguzi, lakini kuna mtu amenichokoza na picha hii.

Natamani ningemjua aliyepiga au aliyeitoa hewani picha hii ili nimnukuu na kufuatilia wavuti au tovuti yake. 

Nahitimisha Habari za Kampeni za Uchaguzi 2010 Tanzania

Siku za kampeni za kisiasa Tanzania zinaelekea ukingoni.
Wasikilizaji tumefaidika sana katika kusikiliza sera mbalimbali za vyama vya kisiasa vinavyowania nafasi za kisiasa katika uchaguzi mkuu ujao. Sera nyingi zimekolezwa chumvi kupita kiasi.
Ahadi zisizo na kifani na zenye matumaini ya maendeleo kwa wananchi wote!
Yaani, kama mtoto aliyezaliwa leo angekuwa na ufahamu wa kutambua maneno yote yanayozungumzwa kwenye majukwaa ya kisiasa wakati huu, hakika angejiona ana bahati kubwa ya kuzaliwa kwenye nchi yenye neema sana. Ninafikiri angemshukuru sana aliyemleta katika dunia hii ya Tanzania!
Mbali ya ahadi nyingi ambazo zimeshindwa kutekelezwa kwa miaka 49 iliyopita ya uhuru wetu wa Tanganyika. Tumeshuhudia watu wakijigamba ya kuwa watazitekeleza kwa miaka 5 ijayo, hakika wengi wetu tumegundua kuwa kuna ka-ujuha Fulani vichwani mwa………
Kinachonishangaza ni mkanganyiko wa mawazo na sera za vyama vyetu, utakuta kuna chama hapo awali kilisema hakiwezi kutoa elimu ya bure, kwamba hiyo ni ndoto, wiki hii, mzito mmoja wa chama hicho hicho kaja na mpya ya kuwa watatoa elimu ya lazima, yaani ya bure hadi kidato cha nne!! Wanaoambiwa ni wananchi walewale, na makofi walipiga tena.
Wengine wanajiona ni bora kuliko wengine, na hata kujifananisha sijui na mawe au milima huku wenzao wakiwaita ni udongo au mfano wake!!!!
Wengine wanaanza kutuhumu kuibiwa kura, hata uchaguzi haujafika, na kuweka imani kwa watu kuwa kuna mpango wa wizi wa kura….
Wengine wanatoa picha kwenye vyombo vya habari kuonyesha kampeni zao za uchaguzi zinahudhuriwa na watu wengi, ukichunguza picha hizo, unakuta zimesanifiwa kwa kutumia mtindo wa kielektroniki… ha ha haaaa
Wengine wameibuka na kudai fidia za mabilioni wakidai wamekashfiwa katika mikutano ya kampeni za uchaguzi za vyama vingine….
Nina hakika baada ya tarehe 31 oktoba 2010, kuna watu hawataamini kitakachokuwa kimetokea.

Tuesday 26 October 2010

Women Tooth-Gap: Making People Crazy Now!

Photo above from msn specials
It is amazing how the world changes, it seems each feature in human body at one time become the point of attraction!

Long time ago, smiling with gaped tooth was considered a taboo, but now it is different, the beauty industry had just turned into different perceptions. Having a tooth-gap signify beauty!

Last month, on “America’s Next Top Model,” host Tyra Banks sent a 22-year-old contestant from Boise, Idaho, to the dentist to widen her gap.The beauty blogosphere has been buzzing ever since. (according to this source)


In some African countries, the tooth gap had high credibility for beauty and fertility. Some of the women had attempted to widen the gap just to attract their destinies according to the same source.

I am sure, very soon, dentists will turn their usual work into beauty-commercial services.

Read more in this link

Sunday 24 October 2010

Uchaguzi Tanzania 2010: Ni Heri au Kiama

Imebakia wiki moja tu kabla ya watanzania watumie haki yao ya kikatiba kuwachagua viongozi watakaoona wanawafaa. Ingawa sina hakika kama wengi wa wapiga kura huwa wanatafakari usemi huu.. wa kumchagua kiongozi atakayefaa, kwa maana nyingine ambaye atatimiza ndoto za jamii anayotaka kuiwakilisha.  
  
Sanduku la kura, ndio huwa linabeba siri yote ya nani kamchagua huyu, na yupi ana kura nyingi.
Kwa sisi watazamaji tunaona kijisanduku cheusi ambacho ni kama giza tu, tunasubiri kuja kutangaziwa ati kijicho bin Tamaa kashinda, na tunapiga makofi na kushangilia, yaani hatujui kwa nini tulimchagua zaidi ya kufuata upepo tu na kumeza ahadi chungu nzima bila kuangalia kama zina maslahi kwa wapiga kura.  
  
Watanzania wengi wamekuwa na hulka ya kuacha kupiga kura ati kwa kudai ni kupoteza wakati!!! Halafu wale wanaowaita ngumbaru wakipiga kura za kingumbaru na kuwashinda werevu wachache waliojitokeza kupiga kura, wale werevu ngumbaru wanakuja juu na kudai sio haki, hakushinda nk, ukiwauliza nyie mlimchagua nani, watadai kivuli (hawakupiga kura) sasa walitaka kiongozi awe hewa? Tena utakuta ambao hawakupiga kura ni wengi kuliko waliojitokeza.   Kwa nini wasiende kumuuliza huyo kivuli kwa nini hakushinda? Maana ndio chaguo lao.....   
   
Pia kuna ujinga fulani ambao watu husema .. ati ni heri ukutane na zimwi likujualo, ha ha haaa, yaani wanajua kuwa wanayemchagua kuwa ni boga tu, lakini wanaogopa kumchagua mtu mpya hata kama anaonekana yu safi kabisa. Ati wanaogopa mtafuno wake sijui utakuwaje!!  
 
Utakuta mgombea anahaidi kujenga daraja chini ya mto, na watu wanapiga makofi. Hata mgombea mwenyewe anacheka kuona haya majitu pambaf kabisa, daraja chini ya mto!!!!, yaani uchimbe chini ya mto uweke daraja, hata ukichukulia maana ya daraja haiji!  
  
Dhana ya watanzania kuogopa mabadiliko, haipo katika siasa tu, bali hata katika kufanya kazi za kimataifa, utakuta ukiwaambia njoo ujiendeleze hapa uje ujenge nchi yako baadaye kwa maarifa utakayoyapata huku, jamaa anaogopa, ati huko atapoteza kacheo kake, hata kama ni uchwara, atasingizia usalama, au hawezi kuwa mbali na mbuyu ulio jirani ya nyumba yake... yote hii ni kuogopa mabadiliko, na hivyo kila siku kukubali kuendelea kutafunwa na kazimwi kake.  
   
Ninafikiri watanzania wameweza kuwasikiliza wagombea mbalimbali wakimwaga sera zao, japo wanasiasa wajanja, wengi wamekwepa kuweka muda wa kuulizwa maswali kuhusiana na ahadi zao, ambapo nyingine ni za kufikirika tu.  
   
Mimi natoa ushauri kwa watanzania kuwa
  • Watambue kuwa kura ni siri ya mpigaji, na hakuna mtu yeyote atakayejua walimchagua nani
  • Wasiogope mabadiliko pale wanapoona yatawasaidia
  • Wawe na hulka ya kuwapima wagombea kwa yale wanayoahidi, na kama walikuwa wana nafasi hiyo kabla, wapimwe kwa yale waliyoyafanya na kama wataweza kutekeleza wanayo ahidi tena.
  • Wamchague mtu wanayefikiri ataleta maendeleo yanayoendana na eneo walilopo, sio mtu anasema atawajengea meli hapo, wakati eneo lipo kwenye sehemu ambayo hata maji ya vijito hakuna.
  • Waangalie rekodi ya uadilifu wa wagombea.
  • Watumie akili zao kutoa maamuzi na sio kuendeshwa kama punda na kubebeshwa mzigo usio na manufaa hata kidogo kwao, jaribu kufikiria punda anapobebeshwa mifuko ya sement au chumvi, unafikiri ina manufaa yoyote kwake?  
Nawatakia uchaguzi mwema hapo Jumapili ijayo. Msituangushe sisi ambao katiba yetu imetunyima uhuru wa kupiga kura.

Wednesday 20 October 2010

Here and There, Chicago

Eye Industry exhibition booths


This week, we had a meeting attended by more than 30,000 eye care teams from all over the world at Chicago, IL. It was an interesting experience! Something terrible to us was cold. ...
Green market at the heart of Chicago, masoko haya ni kama magulio ya huko kwetu nyumbani, kwani wakulima wanaleta mazao yao na kuyauza, wanayakuza bila kutumia mbolea wala virutubisho vya bandia. Lakini ... nyumbani si ndio muda wote tunatumia mbolea asili.....

Mihangaiko ya mitaani tu, usishangae mitaa kuwa mitupu, kibaridi si mchezo.


 Nilipita pita maeneo ya Cook County, ambapo Barack Obama alikuwa anaishi, na mtaa katika picha hii ya chini unaoitwa Ellis, kwa mbele kidogo, ndio kuna nyumba aliyokuwa anaishi Obama, kuna ulinzi mkali japo hauna mtu anayeishi katika nyumba hiyo, ilikuwa imepambwa na masanamu ya haloween!!
Sehemu hii ndio pekee nilipokuta walinzi wa jadi, au ukipenda community security, ambao walikuwa wapo wengi mtaa wa 51 ambako ndipo kuna nyumba ya Obama. Maeneo haya wanaishi watu wengi wenye asili ya Uafrika, ila .. duh, kuna sehemu nyingine, watu kaustaraabu wamekasahau.....
Bustani ya kupumzika Cook County, nje kidogo ya katikati ya jiji la Chicago, IL.

Sunday 17 October 2010

Will Come out Soon.

I have extreme busy schedule here at Chicago, IL, Scarse time to sleep, too many nyama choma and roast, too much desert receptions. Enormous sweet cookies, raw fish!!!, ma-salad, kama kambuzi ati..., kahawa ya barafu huku mmewasha heater ndani!!! Nyie watu wa huku mnapenda sana kumimina chakula ndani ya tumbo..... ''' He! halafu mnadai kunywa diet Coke, wakati cookies zina sukari kama asali!!... hii ni ..... n'bangue, kwa wale wanaojua hapo mmenipata!

I am optimistic, once I settle, I will be able to have fun with my posts. Let me enjoy Chicago first.

Being retina physian.... interesting.
Hey! Gotta many interested parties, scholarship available..., assisted programmes and funds on hand... any one interested pse!! Just have masters in ophthalmology first, then contact me, I mean for Rwanda and Tanzania. ASAP, expiring date just at the tip of my fingers. Hope it will not fall on damn deaf ears and blind eyes!!

Friday 15 October 2010

Bado nipo nipo!

Huu ndio usafiri wangu wa kila siku wakati nikielekea mitaani na sehemu nilizopangiwa kufanya kazi za abunuwasi.
Nilikuwa nikihisi wenzetu wanatoa huduma za hali ya juu, na hakuna kuchapia uongo kwa wagonjwa wao... lakini wapi bwana, wakichemsha wanapiga fiksi hizo...., halafu mgonjwa akitoka, wanakuambia, hapo kazi ilitushinda... alas!
Nilichogundua wana tumajungu, na kusagiana!
Wagonjwa wa macho, nilikuwa naona nyumbani wanapiga foleni ya mwaka, lakini na huku, watu wasubiri masaa 2-3 kumaliza, wagonjwa wakiombwa msamaha, wanadai hakuna shida, wenyeji wakitoka, utaona mtu anakuambia ati hao madokta ni bull-shit nk, duh.. kuwa mgeni mahali, unakuwa rafiki wa kila mtu




Nilipata wasaa wa kufika Staten Island, na pia kufika kwenye statue of Liberty, japo giza lilikuwa limeanza kuingia..... well, well, it was a greaqt experience to visit these sites  across Hudson  river
Picha hiyo hapo juu sio Shanghai au mji wowote wa China, bali mji huu upo New York, na unaitwa "China Town", Karibu 90% ya wafanyabiashara hapa ni wachina, bei za vitu zipo kwa yuan, na kuna kila kitu kinachopatikana China kuanzia vyakula, mavazi, hata na watu hapo karibu wote ni wachina, na kuna wengine hata kiingereza hawajui, lakini wapo na wanafanya biashara.......!!




Duka kubwa la apple ambalo liko chini ya ardhi, watu hapo....... kila mtu ananunua i-phone, i-pod, i-pad nk. Kununua unajipanga foleni kama nusu saa, mind you, that there sales people like 20 and they are very fast...


Kama kawaida, unapofanyia kazi au kupitisha muda wako mwingi, hukosi marafiki, wengine utadhani mlikuwa mnafahamiana siku nyingi....., hapa ni katika hospitali moja ya macho maarufu kwa tiba ya wagonjwa wenye shida ya retina katikati ya jiji la New York. Well, these were my colleagues, they are residents, on the left is from Montana state- US, Middle - from Portugal. We went along very well.....

Monday 11 October 2010

New York Slices


Time square at night

Museum near the Park - NY

Jumba la Makumbusho - NY

12 - 13th Century Chinese products

Below: Grand station for subway trains in NY

Wednesday 6 October 2010

At times....Out of Network. Kumradhi Wakuu

I am on the cruise to nearly extreme north and then to the extreme west. Accessing inernet and other communications is frequently interrupted or prohibited. But, whenever I get time...

Nipo kwenye harakati za safari, kwa muda nitakuwa kwenye mazingira ya kuzima simu, ati jamaa wanadai wakati wanaendesha vyombo vyao au ungo wa kizungu, hawataki abiria wawe wanawasiliana kwa simu.
Wanadai kelele za simu zinaingilia mitambo yao.

Nikiweka kituo mahali popote, nikaweza kuwasiliana nanyi marafiki zangu, nitakuwa nikikohoa.
Kwa sasa nasikiliza hotuba ya Odinga!!

Tuesday 5 October 2010

Ziara Fupi ya Arusha - Nairobi - Kigali kwa siku Moja


Last week I visited Arusha town, after more than 3 years without stepping my feet to this beautiful city.
It was dusty, and after walking about, I noted my shoes were powdered by vumbi!
I visited one of the shoe shiners ( Jamani hii kazi imekodiwa na wachagga), while waiting for my shoes to be ready, alas! I was given makata mbuga to wait while protecting my socks from dust.
Makata Mbuga, are local sandals, famously know as "Arusha to Moshi" by people living in this area. They are made from rejected or old car tyres. Maasai version of makata mbuga are more interesting!
The city  is beatiful and clean, at least to the areas I visited
Lakini.. when you go to Ngaramtoni, yaani ongeza sponji kwenye kiti, na chunga sana kichwa chako, kwani barabara ipo kwenye mashimo, na sio mashimo yapo kwenye baarabara.
Habari mpya nilikutana nayo njiani wakati Naelekea Namanga wakati wa asubuhi baada ya chai, kwani kuna baba mmoja wa kimasai, tulimkuta ana kijana mdogo wa kiume kama miaka 7 hivi kavalia sare za shule siku hiyo ya jumapili!!
Tulisimama, akasema, ero sopai!, nami nikajibu sopai orubaiyan, akaomba....saidia napeleka mutoto panado, yeye anasuka kuni boma ya ... ole parkw..., na mutoto yeye najua kabsaa, .. eeeh , tukamalizia kwa ashee, ashee nale. Naye akawahi kurudi kwa sangiki yake.
Kusema ukweli, huyo baba anajua umuhimu wa elimu, wikendi mtoto anarudi nyumbani, jumapili anawahi tena asubuhi, kwani shule ipo kama km 12 kutoka kwenye boma ya huyo baba, na aliposhukia ni porini..., kama kilomita 2-3 kufika shuleni kwao (Longido mjini).

Mchana, nilikuwa Nairobi, baada ya lunch, nilichukua taksi, kwa jinsi dereva alivyokuwa anaongea, na mate yanaruka kupitia geti la chini(Mwanya wa kutengeneza kwa kung'oa meno ya chini), hakika ni mluo, akadai pale nilipomkuta haparuhusiwi madereva wa kabila jingine, na hasa wakamba, ati wakienda kupaki pale ni nuksi, na kuna mkuu wa polisi fulani anawakingia kifua kwa ukorofi huo. Kwa kuwa alikuwa peke yake, akawa na wasiwasi watakuja kupaki, hivyo alinikimbiza airport kama mbio za langalanga, I had to ask him if he has helmet!!!, kwani mkanda niliona hautoshi, nikihofia kupata head injury kama atakutana na hump, kwani naweza kurushwa kwenye roof, anyway niliwahi airport, kwani nilikuwa karibu kuchelewa!!!

Usiku, nilifika Kigali, dereva wa taksi aliingia mitini, ati alisikia baridi pale airport na ndege yetu ilichelewa kwa dk 45!!, bahati nilipata usafiri wa mabasi yanayopaki karibu kabisa na airport ambayo yalikuwa hayana watu wengi, kwani nilikuwa na kimkoba kidogo tu, na kulikuwa hakuna taksi. Nikamaliza safari yangu kwa kupanda mabasi mawili hadi kufika kiotani kwangu, na yote yakiwa na makonda wanawake/wasichana, wakihangaika kupiga debe kila kituo! Ila wenyeji walikuwa wanayakwepa kwa kuwa yana ongezeko na pesa zaidi kidogo kuliko yale ya kawaida.

Sheeee

Sunday 3 October 2010

Super Husband Danger Akuku Passed Away

Mzee Ancentus Akuku Ogwela, famously known as Danger Akuku who surfaced in the media for a record of being married to around 130 wives had passed away today at the age of 94 years after suffering from hypertensive crisis and collapsed at his home.  
  
He was uncertain of number of children he had, but is said, that he left more than 160 children. 
  
Danger Akuku will be remebered not only for him being most famous polygamist, but also for building a school for his own children at Kisumu, Kenya.  
  
May his soul rest in eternal peace, Amen  

Tanzanian Festival - Kigali, Rwanda

Siku ya jumamosi, tarehe 2 oktoba 2010, umoja wa wanawake wa kitanzania waishio Rwanda, waliandaa vyakula vya asili ya Kitanzania ili kutunisha mfuko wao wa maendeleo. Shughuli hii ilifanyika kwenye hoteli mpya inaoendeshwa na Mtanzania kwa ubia iitwayo FOEYES PREMIER eneo la Bibare, jijini Kigali.
Kulisheheni vyakula mbalimbali ikiwepo supu ya makongoro, mtori, pilau la kibongo, vitumbua, samaki wa mpako, maandazi, chapati, aina zote za nyama choma isipokuwa kitimoto!, mihogo ya kuchemsha, kisamvu nk nk nk




Kwa wale wapenzi wa kinywaji, walifurahia bia za Tanzania, ambazo zimeanza kupatikana Kigali baada ya ufunguzi wa hoteli hii, na hakuna sehemu nyingine yoyote hapa Kigali unaweza kuzipata.
Mimi nilifunga kwa siku moja mahsusi ili niweze kufaidi Tanzanians Festival, lakini.... nafikiri walitayarisha double share, maana ... kilibaki ndugu.


Baada ya watu kushiba, ilikuwa ni saa ya kufukuza gout, kwa wale walioshindilia mbuzi huku wakiwa na matatizo ya gout!!!
Watu waliburudika na mduara na taarabu.

Kitu cha kufurahisha hapa, kila kitu kilikuwa kwenye utamaduni wa kitanzania, wafanyakazi karibu wote ni wanyarwanda, lakini walikuwa wanazungumza kiswahili vizuri, ikiwa ni pamoja na walinzi wa kampuni rasmi, wote waliokuwepo,   yaani unajisikia kama upo nyumbani.

Home sweet hooooooome!

Friday 1 October 2010

Stating Your Problems on T-Shirt is not an Excuse....

This man (James Johnson) is accused of slamming into the house steps while driving under the influence of alcohol.

This will be his fourth charge due to similar offence.

Interesting part, this man had worn a T shirt stating his problem....

Read more here