Member of EVRS

Friday 15 October 2010

Bado nipo nipo!

Huu ndio usafiri wangu wa kila siku wakati nikielekea mitaani na sehemu nilizopangiwa kufanya kazi za abunuwasi.
Nilikuwa nikihisi wenzetu wanatoa huduma za hali ya juu, na hakuna kuchapia uongo kwa wagonjwa wao... lakini wapi bwana, wakichemsha wanapiga fiksi hizo...., halafu mgonjwa akitoka, wanakuambia, hapo kazi ilitushinda... alas!
Nilichogundua wana tumajungu, na kusagiana!
Wagonjwa wa macho, nilikuwa naona nyumbani wanapiga foleni ya mwaka, lakini na huku, watu wasubiri masaa 2-3 kumaliza, wagonjwa wakiombwa msamaha, wanadai hakuna shida, wenyeji wakitoka, utaona mtu anakuambia ati hao madokta ni bull-shit nk, duh.. kuwa mgeni mahali, unakuwa rafiki wa kila mtu




Nilipata wasaa wa kufika Staten Island, na pia kufika kwenye statue of Liberty, japo giza lilikuwa limeanza kuingia..... well, well, it was a greaqt experience to visit these sites  across Hudson  river
Picha hiyo hapo juu sio Shanghai au mji wowote wa China, bali mji huu upo New York, na unaitwa "China Town", Karibu 90% ya wafanyabiashara hapa ni wachina, bei za vitu zipo kwa yuan, na kuna kila kitu kinachopatikana China kuanzia vyakula, mavazi, hata na watu hapo karibu wote ni wachina, na kuna wengine hata kiingereza hawajui, lakini wapo na wanafanya biashara.......!!




Duka kubwa la apple ambalo liko chini ya ardhi, watu hapo....... kila mtu ananunua i-phone, i-pod, i-pad nk. Kununua unajipanga foleni kama nusu saa, mind you, that there sales people like 20 and they are very fast...


Kama kawaida, unapofanyia kazi au kupitisha muda wako mwingi, hukosi marafiki, wengine utadhani mlikuwa mnafahamiana siku nyingi....., hapa ni katika hospitali moja ya macho maarufu kwa tiba ya wagonjwa wenye shida ya retina katikati ya jiji la New York. Well, these were my colleagues, they are residents, on the left is from Montana state- US, Middle - from Portugal. We went along very well.....

2 comments:

Simon Kitururu said...

Poa sana.Kusafiri bomba la shule!Tuko Pamoja Mkuu!

Yasinta Ngonyani said...

ni kweli kabisa kusafiri ni kujifunza mengi. Kama ule msemo usemao tembeo uone!!! Upendo Daima