Member of EVRS

Sunday 10 April 2011

Yusuph Makamba Ajiuzulu Ukatibu Mkuu wa CCM

Habari zilizojiri hivi karibuni zinasema Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi(CCM) Bw. Yusuph Makamba amejiuzulu wadhifa wake. Sio yeye peke yake, bali hata sekretarieti yake yote nayo pia imejiuzulu. 
Mpaka sasa hivi bado haijajulikana nani atateuliwa kushika nafasi yake.
Mwenyekiti wa CCM Mh. Jakaya Kikwete inasemekana amewataka wanachama wa CCM wawe watulivu wakati wakisubiri uteuzi mpya. Ameyasema hayo katika kikao cha CCM kinachoendelea huko Dodoma.  
   
Kujiuzulu kwa Makamba kulikuwa kunatarajiwa kwani alikuwa katika shutuma na lawama nzito juu yake kuhusiana hasa na kuporomoka kwa CCM katika uchaguzi mkuu uliopita kwani alihusishwa na kuleta mkanganyiko na makundi. Kuna baadhi ya wagombea walimhusisha na tuhuma za rushwa na upendeleo hasa wa kidini ambapo tuhuma hizo bado hajizathibitishwa.  
  
Habari zaidi zitapatikana muda si mrefu.

No comments: