Member of EVRS

Wednesday, 20 April 2011

Look here: Kigamboni, New City Plan

Being a prospective Kigamboni resident in Dar es Salaam....
 I was attracted by this master city plan....

Click here at kitururu's blog to see the .... plans

Tuesday, 19 April 2011

Jonathan Wins Nigerian Presidential Race


He is a winner, no doubts

Scoop more than 57% out of 20 contestants.

People from the North are angry for the South - South Corridor, because he was the president before, and now is tha president again ......

Friday, 15 April 2011

Muswada wa Marejeo ya Katiba ya Tanzania 2011 Waondolewa Bungeni

Kamati ya Bunge inayohusiana na masuala ya uundwaji wa sheria, imetoa mapendekezo ya kuongeza muda wa kupitia muswada wa sheria utakaohusu mabadiliko ya katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.

Sababu kubwa ni:
  • Kutoa muda zaidi wa kamati hiyo kupitia muswada huo
  • Kufanyia kazi mambo ambayo yameonyesha kuleta utata
  • Kuwapa muda zaidi wanachi wa Tanzania kutoa maoni zaidi
  • Kuandaa muswada kwa lugha ya kiswahili ili watu wauelewe zaidi kuliko kutafsiriwa na watu wachache
 
Spika Anne Makinda ameridhia, lakini ametoa tahadhari ya kuwa muswada huo haumilikiwa na chama chochote cha siasa, pia amewaasa watu wote kuupitia taratibu bila jazba wala kuleta fujo. Mwisho aliiagiza kamati kumpa ratiba ya shughuli za kurejea muswada huo, na kueleza lini watakuwa tayari kutoa muswada huo tena kwa lugha zote za kiswahili na kiingereza.
    
Hapo awali, muswada huu ulileta fadhaa na ghadhabu kwa baadhi ya watu wakiupinga kwani ulikuwa umekataza baadhi ya mambo kujadiliwa katika maoni ya marekebisho mapya yatakayopendekezwa.

Thursday, 14 April 2011

Anne Makinda: Bado Kanuni za Bunge Zinamkanganya

Kwa wale wanaofuatilia mijadala ya Binge la Tanzania kwenye runinga moja kwa moja, watakubaliana nami ya kuwa Bunge la sasa la Tanzania linaelekea kuyumba na kuendeshwa ndivyo sivyo. 
   
Chanzo kilichopo ni pamoja na Spika Anne Makinda kutokufahamu vizuri baadhi ya kanuni za uendeshaji wa Bunge la Tanzania, na wakati mwingine kuendesha mambo kwa "mazoea". 
Katika kikao cha Bunge kilichopita, kuna siku alikiri ya kuwa kuna baadhi ya kanuni hakuwa anazijua, hadi wabunge walipokuwa wananukuu vifungu fulani fulani, akajikuta kuwa naye alikuwa havijui.
Hayo ni matunda ya kuendesha Bunge kwa mazoea, ndio maana hata na yeye baada ya kukaa bungeni kwa zaidi ya miaka 30, bado hajui baadhi ya kanuni, achilia mbali ya kuwa alishawahi kuwa naibu spika! 
  
Jana wakati wa kikao cha Bunge aling'aka pale mbunge mmoja alipotaka mwongozo wa uteuzi wa wenyeviti wa Bunge, baada ya Bunge kukiuka uteuzi wa wagombea.
Mwishoni Spika ilibidi akubali kutengua kanuni hiyo iliyokiukwa ili wenyeviti hao waweze kuteuliwa na kufanya kazi baada ya kuonekana upungufu/ uvunjaji wa kanuni ya Bunge.

Pia kulikuwa na vurugu nyingine
Nisikumalizie uhondo, ingia hapa kwa Subi upate video ya vurugu Bungeni. Utabofya kwenye link aliyo onyesha, nina hakika utabaki mdomo wazi!!!

Monday, 11 April 2011

Mukama ateuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Mpya wa CCM

Hatimaye jina la mrithi wa Yusuph Makamba kama katibu mkuu wa CCM limetangazwa na mwenyekiti wa CCM, naye si mwingine bali ni Wilson Mukama (Pichani juu)
Jina lake limepitishwa na Kikao cha halmashauri kuu ya CCM huko Dodoma, na muda mfupi uliopita ndio jina hili likatangazwa rasmi.   
   
Naibu wake kwa upande wa Bara ni John Chiligati na kwa upande wa Visiwani ni Ali Vuai Ali.

Sunday, 10 April 2011

Yusuph Makamba Ajiuzulu Ukatibu Mkuu wa CCM

Habari zilizojiri hivi karibuni zinasema Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi(CCM) Bw. Yusuph Makamba amejiuzulu wadhifa wake. Sio yeye peke yake, bali hata sekretarieti yake yote nayo pia imejiuzulu. 
Mpaka sasa hivi bado haijajulikana nani atateuliwa kushika nafasi yake.
Mwenyekiti wa CCM Mh. Jakaya Kikwete inasemekana amewataka wanachama wa CCM wawe watulivu wakati wakisubiri uteuzi mpya. Ameyasema hayo katika kikao cha CCM kinachoendelea huko Dodoma.  
   
Kujiuzulu kwa Makamba kulikuwa kunatarajiwa kwani alikuwa katika shutuma na lawama nzito juu yake kuhusiana hasa na kuporomoka kwa CCM katika uchaguzi mkuu uliopita kwani alihusishwa na kuleta mkanganyiko na makundi. Kuna baadhi ya wagombea walimhusisha na tuhuma za rushwa na upendeleo hasa wa kidini ambapo tuhuma hizo bado hajizathibitishwa.  
  
Habari zaidi zitapatikana muda si mrefu.

Friday, 8 April 2011

Hellow Museveni! This is insanity

President Yoweri Museveni of Uganda has tendered a bill before the selective members of Parliament for endorsement of US $ 750 Million supplementary budget to buy 6 jet fighters from Russia. He said, money will be obtained from the Central Bank of Uganda. However, nobody within the bank is aware of the huge transaction plan.
Rosoboronexport, is the company which have signed a contract with Uganda to supply Su-30MK2s jet fighters. 
  
According to the Monitor, the members of parliament called to endorse the supplementary budget, were not aware of the agenda prior to meet the president, and he kept on referring the transactions without their knowledge, ........

It is further said, that the aim of buying the jet fighters is to protect Ugandan territory which is in danger of an attack.....
Political analysts are convinced that Museveni has observed what is happening in Libya, and realised that the same might occurs to him since he has been in power for more than 25 years and at the end of his current term, he will be cerebrating his 30+ years as president, and he seems that he would love to beat Gaddafi's record of 40+ years in power.
They concluded this, after the leaking news that he had signed another contract to buy anti-riot equipments, which of course will never be used to protect Uganda from al-shabaab offences!! 
 
Uganda need more money to invest on human welbeings (who are anyway tax payers, and the money is theirs) and environment than jet fighters, which might be used to protect the "chosen few". 

Thursday, 7 April 2011

Rwanda Leo Yaadhimisha Miaka 17 ya Mauaji ya Kimbari Dhidi ya Watutsi

Leo imetimia miaka 17 tangu mauaji ya Kimbari ya Rwanda kutokea.
Kwa miaka yote tangu mauaji hayo ya kikatili dhidi ya Watutsi yafanyike, tarehe kama ya leo watu hukumbuka matukio ya mwaka 1994 kwa hotuba na baadhi ya watu kutoa ushuhuda wa matukio ya wakati huo. Kwa ujumla huamsha hisia na uchungu kwa manusura, baadhi yao hupata mfadhaiko wa akili kiasi cha baadhi yao kulazimika kupelekwa hospitali kwa matibabu. 
  
Katika hotuba ya kitaifa siku ya leo, Rais wa Rwanda, Paul Kagame, katika machache aliyozungumza, hakuficha hisia zake na hasira kwa wale wanaoendelea kupinga mauaji hayo ya kimbari dhidi ya watutsi (Genocide against Tutsis), na pia aliyashutumu mataifa yanayoendelea kuwaficha watuhumiwa wakuu wa mauaji hayo ambao wamejificha katika baadhi ya nchi hususan za Ulaya, na kukataa kata kata kuwatoa kwa ajili ya kushitakiwa kisheria. Alitoa hisia yake ya kuwa nchi hizo zinaogopa kuwatoa kwa sababu zinaogopa ushahidi utakaotolewa na hao watuhumiwa, utadhihirisha ni jinsi gani nchi hizo zilishiriki katika kufanikisha mauaji ya Kimbari dhidi ya Watutsi wa Rwanda.  
  
Siku kama ya leo huwa ni mapumziko ya kitaifa, na shughuli zote za kikazi husimamishwa ikiwa ni pamoja na maduka kufungwa na shughuli zote za kibiashara kusimamishwa.  
 
Jinsi nilivyoiona siku ya leo, sikuona tofauti na siku nyingine za maadhimisho ya mauaji hayo hasa nikilinganisha na maadhimisho ya miaka iliyopita, kwani jiji la Kigali limepooza sana, na watu wachache wanaotembea barabarani, sura zao zinaonyesha huzuni kubwa.

Nakubaliana na msemo wao NEVER, NEVER... IT WILL NEVER HAPPEN..... NEVER AGAIN