Member of EVRS

Friday 6 April 2012

Kuenguliwa Kwa Lema, Ndio Mwanzo wa Ukurasa Mpya

Siasaaaaaaaa!
Kuenguliwa Ubunge kwa Godbless Lema kunaashiria mambo mengi, ya kuwa kuna uwezekano wa wabunge wengine nao kun'golewa ikiwa ni pamoja na wale waliopo kwenye baraza la mawaziri la sasa hivi. 
  
Iwapo ukitukana mtu wakati wa kampeni za ubunge wako unaweza kuenguliwa Ubunge hapo baadaye, basi kazi ipo. 
  
Mimi nafikiri tutarajie mengi tu kwenye kesi zinazoendelea. Halafu uchaguzi ukirudiwa, Chama fulani kitashinda.... Wakati huo huo mabilioni ya pesa yatapotea kwenye kampeni, huku dawa na vitendanishi katika hospitali hakuna. 
  
Kweli Bongo akili ipo.
Sitegemei sana mabadiliko ya atakayemrithi Lema, kwani watu wa Arusha hawajabadilika na Serikali yetu tukufu nayo haijabadilika. 
  
Ijumaa Kuu Njema!

1 comment:

José Ramón said...

Saludos desde
Creatividad e imaginación fotos de José Ramón