Member of EVRS

Wednesday 31 August 2011

Tips for Fuel Saving!

Step 1: Buy an adhesive tape
Step 2: Open the fuel gauge meter
Step 3: Pull the fuel lever to full tank position
Step 4: Cut adhesive tape and stick over the fuel gauge pointer
Step 5: Close the fuel gauge meter
Step 6: Enjoy the unlimited ride!

Friday 26 August 2011

Donald Trump and His New 100$ Millions' Private Jet

 Bilionea Donald Trump hivi karibuni alinunua ndege yake binafsi kutoka kwa Paul Allen kwa jumla ya dola za kimarekani kama milioni 100. Ndege hiyo aina ya Boeing 757 ni ya kisasa zaidi.
 Ina uwezo wa kuchukua kama watu 53. Na imepambwa kwa vitu vilivyopakawa rangi ya dhahabu ikiwa ni pamoja na mikanda ya usalama.
 Ina sehemu ya maongezi ya faragha au mkutano, kuna sehemu ya kupumzika, pia ina mfumo wa kisasa wa muziki na televisheni.
 Mbali ya hayo, ina sehemu ya jiko iliyotengenezwa kwa nakshi za mbao na masinki ya marumaru ya kahawia na mabomba yaliyopakawa utando wa dhahabu. Bafu na choo pia vimo....
Ndani ya ndege hii, kuna kitanda kikubwa cha kulala, ambapo Bw Donald akiwa anasafiri, anaweza kupumzika kwa amani.

Wanasema maisha ni mafupi, kama unazo, basi ni lazima ujipe furaha ukiwa katika Dunia hii, ambapo ni mapito tu ya watu!

For more information, click here, na ukitaka kuona video yake, basi bonyeza hapa

Tuesday 23 August 2011

Quotes From Warren Buffett


Price is what you pay. Value is what you get.

I don't look to jump over 7-foot bars: I look around for 1-foot bars that I can step over.

In the business world, the rearview mirror is always clearer than the windshield
  
It takes 20 years to build a reputation and five minutes to ruin it. If you think about that, you'll do things differently.  
 
Don't do what others say, just listen them and do what you feel good.

Monday 22 August 2011

Libya: End of Gadhafi's Regime?



Civialian greets Rebel fighters in Tripoli

Today at dawn: Libyan rebels seems to have captured the Libyan capital, Tripoli with little resistance.
There were few gunshots and throwing of shells from the Government militia, but this could not stop the rebels to move on and fights back.  
On their arrival at Tripoli, the rebels were cheered on by crowds hailing the end of Moammar Gadhafi's regime. 

It has been reported that two Gadhafi's son were captured by rebels.  

Get more news here

Friday 19 August 2011

Wazo la Ijumaa


Hakuna chochote zaidi ya kuwatakia mapumziko mema ya mwisho wa wiki :-)

Mount Kilimanjaro, the Pride of Tanzania

Wednesday 17 August 2011

Tanzia: Profesa Karashani Hatunaye tena

Taarifa ya kusikitisha imetufikia ya kuwa Prof. Karashani (Pichani juu) amefariki ghafla kwa mshtuko wa moyo usiku wa kuamkia jumapili nyumbani kwake Jijini Lusaka, nchini Zambia.

Mpaka mauti yanamkuta, Prof Karashani alikuwa mkuu wa Kitivo cha elimu ya anatomia (Anatomy) katika Chuo Kikuu cha Zambia (UNZA).
Katika safari yake ya kikazi, Prof Karashani alishawahi pia mkuu mkuu wa idara kama hiyo katika chuo kikuu cha Dar es Salaam kwenye kitivo cha tiba sehemu ya Muhimbili.

Sekta ya afya imempoteza nguli mmojawapo.

Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi, Amen.

Tuesday 16 August 2011

England Riots: When Epicenter of Civilisation Produces Tsunami Waves!

Despite several reasons given for the causes of London riots which later spreads to other cities such as social exclusions, spending cuts on welfare dependence, lack of employment, poor measures over technology and social networking, weak governing policies and opportunism. I still believe there is much more this riot has revealed, which include poor upbrough of youths in such a way they feel vandalism and social terror as something funny. 
 
I agree with the idea of Premier Cameron to find ways of reviving societal insight among young Britons following the riot in several cities of UK.   
  
When the retent youths asked what did they took during the riot or why they were involved in the riot, astonishing responses came out, some of them you cannot believe that they come from someone who is not under influence of brain tranquiliser!  
 
There was under 14 youth was held for snatching a bin
Another girl of almost similar age haked a handful of onions
16 years old boy, walk out with diappers for his neonate
Another girl when asked why she set fire on a shop, she replied that she did it for fun! Unbelievable
Another 16 years old boy is charged with a murder of 68 years old man, he has  another four bulglaries and violent behaviour charges!  
  
If nothing is gonna be done soon, the epicenter of civilisation will turn into disastrous tsunami of chaos and mad-society.

Monday 15 August 2011

Wananchi wa Kigamboni Waelekea Kuufukuzia Mbali Mradi wa Mji Mpya


Katika hali inayoonyesha kupungua kwa imani na kukata tama kuhusu ahadi ya ujenzi wa mji mpya wa Kigamboni, pia kuchoshwa na ahadi za serikali iliyopo madarakani, wananchi wa Kigamboni wamemuagiza mbunge wao Mhesh Dr. Faustine Ndugulile aufikishe ujumbe wao kwa waziri wa Ardhi, ustawi wa maliasili na maendeleo ya makazi ya kuwa wamechoshwa na subira ambayo hatima yake haijulikani. 

   
Hii ni kutokana na kuwa serikali ilisitisha shughuli zote za kuendeleza makazi na matumizi ya ardhi katika baadhi ya maeneo ya Kigamboni ili kupisha ujenzi wa mji mpya ambao unatarajiwa kujengwa eneo hilo la Kigamboni. Amri hii ya katazo ilitolewa tangu mwaka 2008 na ilikuwa imepangwa kuwa mpango wa ujenzi uwe umeanzwa ndani ya muda wa miaka 2 tangu ilipotolewa amri ya kusitisha shughuli zote za maendeleo. 
  
Kutokana na serikali kushindwa kuainisha ni lini kazi hiyo ya ujenzi wa mji mpya itaanza ikitanguliwa na kufanya uthamini wa mali za watakaoathirika, sehemu mbadala watakapokwenda kuishi ili kupisha ujenzi huo na muda wa kulipwa fidia. 
  
Kwa sababu serikali imekaa kimya kwa muda mrefu, huku wakazi wa eneo hili wakishindwa kuendeleza makazi, au kuuza maeneo yao wahamie kwingine, wameamua kumuagiza mbunge wao ampatie taarifa waziri Tibaijuka ya kuwa ifikapo tarehe 30 June 2012, kama Serikali haitakuja na mpango madhubuti wa kueleza kwa uhakika muda wa shughuli zote za upanuzi wa mji ukiwa na fidia, basi huo mradi wasiulete tena Kigamboni, na watafute sehemu nyingine kwa watu wasiojua maendeleo ni nini ndio wawapelekee. 
  
Mbunge wa Kigamboni akieleza kwa hisia kali leo jioni ndani ya Bunge wakati wa majadiliano ya hotuba ya makadirio ya wizara ya ardhi, aliainisha msimamo wa wananchi wake, na kusema atakuwa wa kwanza kuunga mkono hatua za “kuufukuzia” mbali mpango huo kama serikali itakuwa haijajipanga kuhusu mradi huo. Pia, aliionya wizara hiyo kwa tabia za kukiuka sheria za umiliki wa ardhi kwa kuvamia na kuyatwaa maeneo ya wananchi bila kuwasiliana na serikali za mitaa husika, na pia kuficha baadhi ya viwanja vya mradi na hivyo kusababisha mapori kwenye maeneo yaliyopimwa, ambapo vibaka hutumia maeneo hayo kufanya uhalifu wa wapiti njia na wakati mwingine kuvamia nyumba za wakazi. 
  
Mwisho aliomba wabunge wamuunge mkono katika kupinga kupitishwa kwa makadirio ya wizara hiyo kama haitatoa ufafanuzi wa uhakika kuhusu matatizo ya wakazi wa Kigamboni. 
 

Tuesday 9 August 2011

Humanised Animals!

Make your own story!

Photo from TN

Monday 8 August 2011

Vurugu Za Tottenham: Wa Kulaumiwa ni Nani?


Photo and English news from BBC
Watu wanaweza kujiuliza kwa nini mnamo kipindi cha mwisho wa wiki kulitokea Vurugu kaskazini mwa jiji la London katika eneo la Tottenham. 
  
Chanzo kikubwa ilikuwa ni mauaji ya mkazi mmoja wa eneo hilo ambayo yalifanywa na polisi tangu alhamisi ya wiki iliyopita. Inasemekana watu waliokuwa wanafuatilia sababu za kifo hicho katika kituo cha polisi hawakupata majibu ya aina yoyote au ya kuridhisha. Hivyo, waliamua kufanya maandamano ya amani kukizunguka kituo hicho.  
Wakaazi wa eneo hilo wanasema.. kwenye msafara wa mamba na kenge hawakosi. Maanadamano yaliyotarajiwa kuwa ya amani, yaligeuka kuwa ya vurugu, pale watu wachache waliaamua kuvamia maduka mbalimbali na kubomoa kisha kupora mali mbalimbali na kukimbia nazo.  
  
Baadhi ya mashuhuda walisema walikuwa wnawaona watu wakikimbia na seti za runinga, radio, vyombo vya elektroniki, blanketi, vyakula tena wengine wakitumia matoroli ya maduka waliyopora, na hakukuwa na hata askari wala gari la doria katika sehemu hiyo, na kwa hiyo wanaishutumu polisi kuwa iliachia kwa makusudi watu waendelee na vurugu hiyo.  
Lakini hakuna anayezungumzia polisi zaidi ya 30 waliojeruhiwa katika vurugu hizo!
   
Hata hivyo polisi wamepinga vikali ya kuwa waliachia waandamanaji waendelee na fujo! 
  
Kwa ujumla eneo hilo la Tottenham, ni maarufu kwa wahamiaji wanaotoka sehemu mbalimbali duniani hususan Afrika, na ambao wameshapewa uraia wa Uingereza, na wengi wao ni maskini, ambao wanaishi kwa msaada wa posho za kutokuwa na kazi, na wengine walikuwa wanafaidi posho zaidi kwa kuzaa watoto kwa wingi, kiasi kwamba ilifikia wakati walikuwa wanapata posho karibu sawa au zaidi ya wafanyakazi wa kawaida. Kwa kawaida posho hizi zimekuwa zikiongezeka kila mkaazi anapopata mtoto mwingine, japo serikali ya sasa imeanza kuzipunguza posho hizo ukizingatia ya kuwa "watu wasiotaka kufanya kazi" wamekuwa wakiongezeka. Punguzo hili hakika linawakera wakazi hao waliokuwa hawapendi kufanya kazi. 
  

Friday 5 August 2011

Tuesday 2 August 2011

Indonesia: Matibabu kwa Njia ya Mshtuo wa Umeme (Treatment using Electric shock)

Watu wa Indonesia wamekuwa wanatumia njia ya kujilaza kwenye njia za reli ili wapate mshtuo wa umeme kwa nia ya kupata matibabu ya maradhi mbalimbali hasa yanayohusiana na uchovu (Relaxing spa treatment). 
  
Wanachotarajia ni kupata mshtuo mdogo wa nguvu za umeme kutoka kwenye reli hizo hasa njia hiyo inapotumika na zile treni za umeme zilizounganishwa kwa waya za juu. 
Inasemekana wakati mwingine unahitaji kukaa kwa muda wa karibu saa moja kwenye reli za uvuguvugu, maana yake ni lazima ulale juani ili kuweza kupata mshtuo huo. Waliojaribu, wanasema kuna wakati inaogofya kwani mshtuo wa umeme (electric shock) unaweza kuwa na nguvu kidoogo kiasi cha kuleta msisimko ule mtu anaoupata akishika transistor.  
  
Matibabu haya yamekuwa yakikatizwa mara nyingine na treni zinazokuja kwenye njia hizo na kuwalazimu watu kutimua mbio (kukimbia) ili wasije wakagongwa.  
   
Shirika la reli la Indonesia limejitahidi kuzuia watu bila mafanikio na kufikia hatua ya kuweka vibao vya tahadhari likiwaonya watu wanaojilaza kwenye reli ya kuwa kufanya hivyo ni kosa la jinai.  
  
Hii ni changamoto kwa Tz..... umeme kwa matumizi ya kawaida tu ni kwa mbinde, sasa......

Picha kutoka Aol Travel