Member of EVRS

Friday, 29 July 2011

Tanzania: Kuanza Kutegemea Mgao wa Mbalamwezi Wakati wa Usiku!

Suala la upatikanaji wa umeme, Watanzania inabidi waendelee kuishi kwa matumaini… 

  
Kampuni inayozalisha gesi asilia kutoka visiwa vya Songosongo, Songas imekiri kuwa haina uwezo wa kuzalisha gesi ya kuendesha mtambo mpya ulionunuliwa na Tanesco wa kuzalisha umeme wa megawati 100 kwa kutumia gesi asilia. 
   
Kampuni hiyo imesema kwa sasa inazalisha gesi kwa kiwango cha ukomo wa juu, na haiwezi kuongeza hadi itakapofanya upanuzi wa mitambo yake ya kuzalisha gesi ikiwa ni pamoja na kubadili bomba la kusafirisha gesi kuelekea Dar es Salaam. Shughuli hii inatarajiwa kukamilika baada ya miaka 2. Kwa maana hiyo, hata hizo megawati za ziada kutoka Tanesco zitapatikana kuanzia mwaka 2013. Hii ina maana huo mtambo ambao Tanesco ilikimbilia kuununua haraka haraka utakaa bila kazi hadi mwaka 2013!!!!! 
 
Hii inanikumbusha hotuba za mbunge wa CHADEMA na waziri kivuli wa Nishati na Madini, John Mnyika. Pia na ile ya mwenyekiti wa kamati ya nishati na madini, January Makamba (CCM), ambao walionyesha shaka kubwa kwa mipango ya Tanesco katika kuzalisha umeme huku wakiwa hawajajipanga kujua ni wapi watapata nyenzo za kuendesha hatua zao za dharura. 
  
Sasa ukweli umeanza kujionyesha kuwa mipango ya hawa wenzetu ni kweli ilikuwa ni ya “zima moto” kwa maana zote mbili za kufanya mambo kidharura ambapo mara nyingi watu hawafikirii sana zaidi ya kuuzima moto haraka kabla haujaharibu zaidi, na pili kufanya mchezo wa kiini macho kuwapumbaza watu kuwa umeme waja hivi karibuni kupunguza moto wa hasira za watu na wabunge kuhusiano na mgao mkubwa giza… 
 
Lakini…. Walikuta wabunge karibu wote bila kujali itikadi zao za kisiasa, walikuwa tayari ni moto usioweza kupozwa kwa mbinu ya ghiliba. 
  
Watanzania endeleeni kuishi kwa matumaini mkitegemea mgao wa mbalamwezi, kwani hata hizo taa za mafuta ya taa mtashindwa kuzitumia baada ya bei ya mafuta ya taa nayo kupandishwa. Siku mkipata umeme kwa siku nzima inabidi mshangae 

Sunday, 24 July 2011

Mauaji ya Norway: Ukatili Dhidi ya Haki ya Kuishi

Anders Behring Breivik (Pichani juu), ambaye ni raia wa Norway ameitikisa dunia wiki hii kwa kufanya mauaji ya kikatili ya karibu watu 100 kwa siku moja katika mji mkuu wa Norway, Oslo. 
  
Sababu kubwa za kufanya mauaji hayo bado zipo kwenye uchunguzi mkali unaofanywa na Serikali ya Norway. Mtu huyu alikamatwa siku hiyohiyo aliyofanya mauaji ya kutisha na kinyama, kwani aliwashambulia kwa risasi vijana waliokuwa katika mkutano wa mafunzo ya kisisasa wanaounga mkono chama kinachotawala Norway. Inadaiwa siku ya kufanya shambulio hilo, alikuwa amevaa nguo kama askari.
Mtu huyu, pia anahusishwa na kutega bomu lililolipuka karibu na ofisi kuu za Serikali mjini Oslo. Siku ya tukio hili la kutisha, maiti 7 zilipatikana karibu na eneo lilipolipuka bomu hilo, na ilikuwa inahofiwa kuwa huenda kuna baadhi ya watu wanaweza kuwa wamefukiwa na kifusi cha jengo lililobomoka kutokana na bomu lililolipuka.  
  
Tukio hili linasikitisha sana, na haieleweki huyu jamaa kama alishirikiana na mtu yeyote, japo alipohojiwa alidai yeye akushirikiana na mtu au kikundo chochote kutekeleza azma yake hii mbaya sana.  
  
Tunaombea amani na utulivu katika nchi ya Norway tukiwa na matumaini ya kuwa tukio kama hili halitarudiwa tena!  

Friday, 22 July 2011

Friday Humour!

One afternoon a lawyer was riding in his limousine when he saw two men along the roadside eating grass.
Disturbed, he ordered his driver to stop and he got out to investigate.
He asked one man, 'Why are you eating grass?'
'We don't have any money for food,' the poor

man replied. 'We have to eat grass.'
'Well, then, you can come with me to my house and I'll feed you,' the lawyer said.
'But sir, I have a wife and two children with me. They are over there, under that tree.'
'Bring them along,' the lawyer replied.
Turning to the other poor man he stated, 'You come with us, also..'
The second man, in a pitiful voice, then said, 'But Sir, I also have a wife and SIX children with me!'
'Bring them all, as well,' the lawyer answered
They all entered the car, which was no easy task, even for a car as large as the limousine was.
Once underway, one of the poor fellows turned to the lawyer and said, 'Sir, you are too kind.'
'Thank you for taking all of us with you.'
The lawyer replied, 'Glad to do it.
You'll really love my place..

The grass is almost a foot high.'

What do you think now, was he too kind or too exploitant?!!!!

Tuesday, 19 July 2011

Mzaha kwa Tanesco!

Utani mwingine bwana.....

Ati kwa sababu nyaya za umeme za Tanzania hazipitishi umeme kwa sababu ya mgao, kwa hiyo kwa sasa hazina la kufanya zaidi ya kujitafutia michezo ili kupitisha muda zikishirikiana na nguzo.

Mojawapo ya michezo inazofanya ambayo ni ya kitoto ni kuruka kamba kama unavyoona katika opicha hiyo hapo juu :-)

Monday, 18 July 2011

Give Your Week a Smile

Smile is just a smile. It always increase facial beauties!
It also make your life more meaningful!

Photo from FPs

Japan Beats USA to clinch 2011 Women World Cup

Few minutes ago, USA has proven that today they were not in better shape to score through penalties after missing 3 out of 4 penalty shots and lost the game to Japan who scored 3 out of 4 penalty shots. Therefore Japan were crowned the Queens of 2011 FIFA women world cup winners after winning the final game by penalties 3 - 1 against USA.

Japanese player, Kumagai was the scorer of the winning goal after beating USA goalie Solo.

Up to the end of regular time, the score was 1 - 1, at extra time Japan equalise for the second time in dying minutes of  this period forcing the game winners to be decided by penalties.

Awards given to individual players

Best player Solo - USA
Best Goalie Solo -USA
Golden boot - Sawa - Japan
Golden ball Sawa - Japan

Friday, 15 July 2011

Nice Weekend

I have nothing to write... Just wishes you a nice weekend!

Thursday, 14 July 2011

Rostam Aziz Kujiuzulu Ubunge na Ujumbe wa NEC: Hotuba Kamili


Rostam Aziz, ambaye ni mbunge wa Igunga, au aliyekuwa mbunge wa Igunga kama amekubaliwa kujiuzulu, jana kwnye muda wa saa 7 mchana alitangaza kujiuzulu nafasi zake zote za kisiasa alizozipata akiwa ndani ya CCM na kubakia kuwa mwanachama wa kawaida.
Alitaja sababu nyingi lakini kubwa ni kuwa amechoka na siasa za uchwara na tuhuma zisizo na ushahidi ambazo zimekuwa zikielekezwa kwake kwa muda mrefu. 
  
Hotuba yake kamili inapatikana hapa 
Mbali ya kutoa sababu hizo, alijivunia mafanikio aliyoyapata kwa kipindi cha miaka 18 aliyokuwa mbunge, mara baada ya kushinda uchaguzi mdogo kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa Igunga Charles Kabeho. 
  
Kuna mabo kadhaa wa kadha yaliyojitokeza katika mkutano huo aliouita wa kuongea na wazee wa Igunga.

Kwangu naona kama alichelewa mno kutoa uamuzi huu, na hivyo kuendelea kupakwa madongo kwa tuhuma mbalimbali alizohusishwa nazo ikiwamo ya kampuni ya kufua umeme ya Richmond na baadaye Dowans (ambayo ilikuwa inasemekana ilikuwa ikitumia anuani ya posta na abarua pepe ya huyu mheshimiwa mstaafu), na pia kuna nyaraka mbalimbali za mawasiliano kati ya Tanesco na Dowans ambazo zilikuwa zinalitaja jina lake katika masuala ya makubaliano katika mktaba tata uliowekwa kati ta ya Tanesco na Dowans. 
  
Ingekuwa busara mheshimiwa huyu angechukua uamuzi wa uwajibikaji kama alivyofanya aliyekuwa mkuu wa IMF au Mzee Mwinyi wakati ule alipokuwa waziri wa mambo ya ndani. 
 
Nina matumaini mwenyekiti wake atakubaliana na uamuzi wa kada huyu ili kujenga imani kwa serikali yake kuwa ni sikivu na inayowajibika kisheria kwa sasa. 
  
Mengi tunawaachia wanasiasa na wanachi waamue....