Member of EVRS

Wednesday 14 March 2012

Jiolojia: Afrika kugawanyika na Kuwa Mabara Mawili!

Wanasayansi wa jeolojia ambao wamekuwa wanafanya utafiti wa namna bahari inavyotokea katikati ya nchi kavu hivi karibuni wamegundua mvutano mkubwa wa sumaku katika bonde la Afar nchini Ethiopia. 
 
Mvutano huu wa sumaku ndio unaosemekana kuwa chanzo cha mkondo wa bahari kutokea mahali. Na mara nyingi hufanya kuwa tofauti ya nguvu za kisumaku katika tabaka la udongo, hii ni kutokana na miamba moto kusogea juu karibu na uso wa ardhi na kisha kupoa. Inapotokea mvutano wa kisumaku kutokea, miamba hii huanza kutoa nguvu za kisumaku kuelekea upande mwingine kuliko ilivyokuwa awali na hivyo kukinzana na miamba ya awali, na hivyo kuchochea miamba kusigana na kuachanana hivyo kutengeneza mkondo mpya wa bahari. 
 
Mara nyingi mivutano kama hii huonekana kwenye maeneo ya bahari kuu. 
  
Iwapo msukumo huu wa kisumaku utaendelea, basi kuna uwezekano wa bara la Afrika kugawanyika katika sehemu mbili zikitengwa na bahari. 
  
Ili kuweza kuwa na ufa inakadiriwa kuwa itaweza kupita miaka kama milioni 2, na kuweza kuacha nafasi ya mkondo wa bahari, inakadiriwa itahitajika kama miaka milioni 2 mingine ipite.  
Kwa hiyo watakaoshuhudia bahari hiyo, ni wale watakaokuwa wanaishi duniani mika akam milioni 4 ijayo.
  
Mimi sina utaalamu wa aina yoyote ya jiolojia, Kama unayaamini haya, basi habari ndiyo hiyo, inapatikana hapa pia 

No comments: