Member of EVRS

Tuesday, 5 October 2010

Ziara Fupi ya Arusha - Nairobi - Kigali kwa siku Moja


Last week I visited Arusha town, after more than 3 years without stepping my feet to this beautiful city.
It was dusty, and after walking about, I noted my shoes were powdered by vumbi!
I visited one of the shoe shiners ( Jamani hii kazi imekodiwa na wachagga), while waiting for my shoes to be ready, alas! I was given makata mbuga to wait while protecting my socks from dust.
Makata Mbuga, are local sandals, famously know as "Arusha to Moshi" by people living in this area. They are made from rejected or old car tyres. Maasai version of makata mbuga are more interesting!
The city  is beatiful and clean, at least to the areas I visited
Lakini.. when you go to Ngaramtoni, yaani ongeza sponji kwenye kiti, na chunga sana kichwa chako, kwani barabara ipo kwenye mashimo, na sio mashimo yapo kwenye baarabara.
Habari mpya nilikutana nayo njiani wakati Naelekea Namanga wakati wa asubuhi baada ya chai, kwani kuna baba mmoja wa kimasai, tulimkuta ana kijana mdogo wa kiume kama miaka 7 hivi kavalia sare za shule siku hiyo ya jumapili!!
Tulisimama, akasema, ero sopai!, nami nikajibu sopai orubaiyan, akaomba....saidia napeleka mutoto panado, yeye anasuka kuni boma ya ... ole parkw..., na mutoto yeye najua kabsaa, .. eeeh , tukamalizia kwa ashee, ashee nale. Naye akawahi kurudi kwa sangiki yake.
Kusema ukweli, huyo baba anajua umuhimu wa elimu, wikendi mtoto anarudi nyumbani, jumapili anawahi tena asubuhi, kwani shule ipo kama km 12 kutoka kwenye boma ya huyo baba, na aliposhukia ni porini..., kama kilomita 2-3 kufika shuleni kwao (Longido mjini).

Mchana, nilikuwa Nairobi, baada ya lunch, nilichukua taksi, kwa jinsi dereva alivyokuwa anaongea, na mate yanaruka kupitia geti la chini(Mwanya wa kutengeneza kwa kung'oa meno ya chini), hakika ni mluo, akadai pale nilipomkuta haparuhusiwi madereva wa kabila jingine, na hasa wakamba, ati wakienda kupaki pale ni nuksi, na kuna mkuu wa polisi fulani anawakingia kifua kwa ukorofi huo. Kwa kuwa alikuwa peke yake, akawa na wasiwasi watakuja kupaki, hivyo alinikimbiza airport kama mbio za langalanga, I had to ask him if he has helmet!!!, kwani mkanda niliona hautoshi, nikihofia kupata head injury kama atakutana na hump, kwani naweza kurushwa kwenye roof, anyway niliwahi airport, kwani nilikuwa karibu kuchelewa!!!

Usiku, nilifika Kigali, dereva wa taksi aliingia mitini, ati alisikia baridi pale airport na ndege yetu ilichelewa kwa dk 45!!, bahati nilipata usafiri wa mabasi yanayopaki karibu kabisa na airport ambayo yalikuwa hayana watu wengi, kwani nilikuwa na kimkoba kidogo tu, na kulikuwa hakuna taksi. Nikamaliza safari yangu kwa kupanda mabasi mawili hadi kufika kiotani kwangu, na yote yakiwa na makonda wanawake/wasichana, wakihangaika kupiga debe kila kituo! Ila wenyeji walikuwa wanayakwepa kwa kuwa yana ongezeko na pesa zaidi kidogo kuliko yale ya kawaida.

Sheeee

Sunday, 3 October 2010

Super Husband Danger Akuku Passed Away

Mzee Ancentus Akuku Ogwela, famously known as Danger Akuku who surfaced in the media for a record of being married to around 130 wives had passed away today at the age of 94 years after suffering from hypertensive crisis and collapsed at his home.  
  
He was uncertain of number of children he had, but is said, that he left more than 160 children. 
  
Danger Akuku will be remebered not only for him being most famous polygamist, but also for building a school for his own children at Kisumu, Kenya.  
  
May his soul rest in eternal peace, Amen  

Tanzanian Festival - Kigali, Rwanda

Siku ya jumamosi, tarehe 2 oktoba 2010, umoja wa wanawake wa kitanzania waishio Rwanda, waliandaa vyakula vya asili ya Kitanzania ili kutunisha mfuko wao wa maendeleo. Shughuli hii ilifanyika kwenye hoteli mpya inaoendeshwa na Mtanzania kwa ubia iitwayo FOEYES PREMIER eneo la Bibare, jijini Kigali.
Kulisheheni vyakula mbalimbali ikiwepo supu ya makongoro, mtori, pilau la kibongo, vitumbua, samaki wa mpako, maandazi, chapati, aina zote za nyama choma isipokuwa kitimoto!, mihogo ya kuchemsha, kisamvu nk nk nk




Kwa wale wapenzi wa kinywaji, walifurahia bia za Tanzania, ambazo zimeanza kupatikana Kigali baada ya ufunguzi wa hoteli hii, na hakuna sehemu nyingine yoyote hapa Kigali unaweza kuzipata.
Mimi nilifunga kwa siku moja mahsusi ili niweze kufaidi Tanzanians Festival, lakini.... nafikiri walitayarisha double share, maana ... kilibaki ndugu.


Baada ya watu kushiba, ilikuwa ni saa ya kufukuza gout, kwa wale walioshindilia mbuzi huku wakiwa na matatizo ya gout!!!
Watu waliburudika na mduara na taarabu.

Kitu cha kufurahisha hapa, kila kitu kilikuwa kwenye utamaduni wa kitanzania, wafanyakazi karibu wote ni wanyarwanda, lakini walikuwa wanazungumza kiswahili vizuri, ikiwa ni pamoja na walinzi wa kampuni rasmi, wote waliokuwepo,   yaani unajisikia kama upo nyumbani.

Home sweet hooooooome!

Friday, 1 October 2010

Stating Your Problems on T-Shirt is not an Excuse....

This man (James Johnson) is accused of slamming into the house steps while driving under the influence of alcohol.

This will be his fourth charge due to similar offence.

Interesting part, this man had worn a T shirt stating his problem....

Read more here

Thursday, 30 September 2010

Tuesday, 28 September 2010

Monday, 27 September 2010

Kenya Airways: Nao Wamo Kwa Ndege za Mitumba


 Nilikuwa kimya kwa siku kadhaa, kwani nilikuwa mimekabiliwa na majukumu yanayohusu mipango ya maendeleo na utoaji huduma za macho, mpango huu unahusisha juhudi binafsi za wananchi wazalendo na wazawa katika ukanda wa Afrika Mashariki, na kwa kuanzia, Kenya ndio imekuwa ya kwanza kuratibu mpango huu kwa nchi shirikishi za umoja huu wa kanda ya Afrika Mashariki.
Kwa kuwa nilikabiliwa na zaidi ya masaa 40 bila ya kulala kutokana na usafiri kuanza saa 6 usiku na kuondoka usiku wa manane ilhali mkutano ulikuwa unaanza saa 2 asubuhi hadi saa 2 usiku, na baada ya hapo kuandika muhtasari.. hakika siwezi kusema zaidi........



kusafiri, ni kuona mengi na pia kujifunza mengi. Hapo jana wakati narejea Kigali, nilipokuwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta, Nairobi, niliona ndege kwa mbali, nikadhani ni ya KLM, lakini kwa kuwa nimezoea kuona madege ya KLM ambayo huja huku, nikashangaa kwa nini safari hii wameleta ndege ndogo, tena jioni.. ..... wakati huwa zinatua huku usiku na kuondoka usiku huo huo..... nikawa na maswali...


Kusoma jina la ndege likawa halifanani na rangi ya ndege niliyoizoea!, nilihisi bado nina usingizi, na hivyo rangi zikawa zinanichanganya. Nilipata moyo baada ya kuona kuna baadhi ya wasafiri wenzangu nao walikuwa wakishangaa kama mimi. Wengine walikuwa wakikenua meno na kucheka, kwani nao naona walikuwa wanshangaa hizo rangi za ndege kuwa ni za KLM wakati shirika linaloimiliki ni Kenya Airways

Tukutane tena wakati mwingine, kwani safari hii ilinifurahisha kwa mengi ambayo iliniwezesha kukaa miji mitatu, kwenye nchi tatu tofauti kwa siku moja!!

Friday, 24 September 2010

Google translator Ruins Swahili-English Meaning

Many people have been laughing when reviewing or translating swahili words into English by using google translator...
I did not pay critical attention regarding these translations until recently when I tried to translate what I had written using google translator.

What came out of it... ugh!....senseless meaning, in fact, if you know well swahili language, you may think something is wrong with your computer or your eyes :-)

It is my hope that google company will review swahili vocabularly and put more appropriate words to enable appropriate translation.