Member of EVRS

Showing posts with label yapungua. Show all posts
Showing posts with label yapungua. Show all posts

Thursday, 19 January 2012

Rwanda Yapunguza Kodi ya Nishati ya Mafuta Kupunguza Makali ya Mfumuko wa Bei

Wakati mfumuko wa bei unaelekea kupanda hapa Rwanda, na hivyo kuelekea kupandisha bei za bidhaa mbalimbali za vyakula na matumizi mengine. Serikali ya Rwanda imeamua kupunguza tozo ya kodi kwa mafuta kwa asilimia 6% . Taarifa hii ya punguzo ilitolewa na wazara ya Biashara na Viwanda.
 
Hali hii imesababisha kushuka mara moja kwa bei ya mafuta kutoka Faranga za Rwanda 1,000 kwa lita moja ya mafuta ya petroli na dizeli hadi Faranga 940. Hii ni sawa na punguzo la asilimia 6% kwa kila lita inayonunuliwa.  Bei elekezi ilitolewa na wizara hiyo ikitegemea bei ya mafuta ya rejareja haitazidi Faranga za Rwanda 940 kwa lita.
 
Baada ya kutangazwa bei hii mpya, vituo vyote vilishusha bei na hakukuwa na tatizo lolote la vituo kuacha kuuza mafuta kama inavyokuwa Kenya na Tanzania. 
 
Hii ndio serikali inayojali mustakabali na uchumi wa wananchi wake.