Member of EVRS

Showing posts with label Tanzania Taifa Queens. Show all posts
Showing posts with label Tanzania Taifa Queens. Show all posts

Friday, 16 September 2011

Hatimaye! Tanzania yapata medali yake Mashindano ya Afrika

Timu ya taifa ya mpira wa pete, Taifa Queens, hapo juzi iliipatia medali Tanzania kutoka katika mashindano ya Afrika, baada ya kuifunga timu ya akina dada wa Botswana kwa 43 - 35 na hivyo kuchukua medali ya fedha katika mashindano hayo.
Waliochukua medali ya dhahabu ni Uganda, na ya shaba ni Zambia.

Timu ya Tanzania, ilipoteza michezo 2 kati ya 8 iliyocheza, na ilifungwa na timu za Uganda 52-41 na Zambia 46-42 pekee, ambazo zote hizi ndio zilizofanikiwa kutwaa medali katika mchezo huu.

Hata hivyo Tanzania waliwazidi Zambia kwa idadi ya magoli, kwani walikuwa waanalingana kwa alama.

Michezo waliyocheza:

Waliwafunga
Kenya 36 - 35
Ghana 94 - 24
Mozambique 92 - 8
Zimbabwe 38 - 27
South Africa 32 - 29
Botswana 43 - 35

Tunaipongeza timu ya Taifa Queens kwa kutuondolea fedheha ya muda mrefu.

Picha kutoka Star Africa