Mwananmziki mkongwe na maarufu nchini Tanzania, Ramadhani Mtoro Ongala au maarufu kama Dokta Remmy amefariki dunia usiku wa kuamkia leo.
Remmy alikuwa akisumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa kisukari ambao ulisababishwa alazwe mara kadhaa hospitalini ikiwa ni pamoja na hospitali ya taifa ya Muhimbili. Inasemekana amefariki kwa matatizo hayo hayo ya kisukari.
Remmy atakumbukwa kwa mengi ikiwa ni pamoja na kuwa mshindi wa pili kwa sura mbaya Tanzania japo alilalamika ya kuwa kaonewa kwani aliamini ya kuwa yeye ana sura mbaya kuliko watu wote waliokuwa wanaishi Tanzania wakati huo!!!!!
Pia kuna nyimbo kadhaa alizoimba ambazo watu watatzikumbuka ikiwa ni pamoja na wimbo wa KIFO.
Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi
