Member of EVRS

Showing posts with label Norway gun attack. Show all posts
Showing posts with label Norway gun attack. Show all posts

Sunday, 24 July 2011

Mauaji ya Norway: Ukatili Dhidi ya Haki ya Kuishi

Anders Behring Breivik (Pichani juu), ambaye ni raia wa Norway ameitikisa dunia wiki hii kwa kufanya mauaji ya kikatili ya karibu watu 100 kwa siku moja katika mji mkuu wa Norway, Oslo. 
  
Sababu kubwa za kufanya mauaji hayo bado zipo kwenye uchunguzi mkali unaofanywa na Serikali ya Norway. Mtu huyu alikamatwa siku hiyohiyo aliyofanya mauaji ya kutisha na kinyama, kwani aliwashambulia kwa risasi vijana waliokuwa katika mkutano wa mafunzo ya kisisasa wanaounga mkono chama kinachotawala Norway. Inadaiwa siku ya kufanya shambulio hilo, alikuwa amevaa nguo kama askari.
Mtu huyu, pia anahusishwa na kutega bomu lililolipuka karibu na ofisi kuu za Serikali mjini Oslo. Siku ya tukio hili la kutisha, maiti 7 zilipatikana karibu na eneo lilipolipuka bomu hilo, na ilikuwa inahofiwa kuwa huenda kuna baadhi ya watu wanaweza kuwa wamefukiwa na kifusi cha jengo lililobomoka kutokana na bomu lililolipuka.  
  
Tukio hili linasikitisha sana, na haieleweki huyu jamaa kama alishirikiana na mtu yeyote, japo alipohojiwa alidai yeye akushirikiana na mtu au kikundo chochote kutekeleza azma yake hii mbaya sana.  
  
Tunaombea amani na utulivu katika nchi ya Norway tukiwa na matumaini ya kuwa tukio kama hili halitarudiwa tena!