Member of EVRS

Wednesday 30 June 2010

Tuepukane na Ufinyu wa Kufikiria

Bado ile habari niliyoiona kwenye runinga juzi iliyohusu watoto wa shule ya msingi huko Mkoani Tanga ya kutokuvaa viatu wakienda shuleni bado inanigonga kichwa!!

Yaani shule nzima ... mwanafunzi mmoja tu ndio alikutwa amevaa viatu, kati ya mamia ya wanafunzi... yaani miguu miwili tu ndio ilikuwa imefunikwa kwa viatu, ha ha haaa, yaani hapo najaribu kuongeza idadi ya kuhesabu, japo nikisema miguu miwili nimevuka moja...

Kikubwa zaidi ni pale msamaria mwema mmoja kutoka Kenya, alipopata habari za awali, ambazo zilitolewa na mwandishi wa habari siku za nyuma, alikuja kutoa msaada wa viatu jozi 50 kwa shule hiyo, kama njia ya kuwasaidia watoto kuvaa viatu.

Yaelekea hilo hilo tatizo ni la siku nyingi, kwani naibu waziri wa masuala ya elimu nk, alikuwa mmoja wa wageni walioenda kupokea msaada huo, alisema wazi ya kuwa mkuu aliyetangulia hapo alikweka sheria ya kuwa wattot wote ni lazima wanunuliwe viatu vya shule, lakini alipohamishwa, viatu navyo vikahama.

Sababu ya kutokuvaa viatu inachekesha, ha ha haaaa...., eti wenyeji wana imani ya kuwa uvaaji wa viatu huleta sugu kwenye miguu, he he heeee
Hivi kipi kinaleta sugu zaidi, kupiga peku au kuvaa viatu viavyokutosha?!

Kuna sehemu za mkoa wa Tanga ni maarufu kwa kuwa na funza wengi, tena wanakula miguu haooo,........ utakuta watoto wadogo miguu imevimba sana, na watu wazima miguu ikiwa imekwenda tenge, mtu anaenda mbele, miguu inaeleekea kulia na kushoto, kiasi kwamba unashindwa kujua anaelekea wapi......

Jamani visingizio visivyo na maana viachwe, watoto wanunuliwe viatu alaaaaaa....

Tuesday 29 June 2010

Gari ya Ubalozi wa Tanzania Burundi Yalipuliwa kwa Bomu

Katika harakati za uchaguzi wa urais Burundi jana, watu wasiojulikana walirusha bomu la kutupa kwa mkono mjini Bujumbura na kulipuka na kusababisha kuharibika kwa gari la ubalozi wa Tanzania Burundi. Watu hao walikuwa katika gari ya kiraia walitokomea haraka sana baada ya kurusha bomu hilo.

Hakuna mtu aliyejeruhiwa na hakukuwa na taarifa rasmi kutoka katika ofisi ya ubalozi wa Tanzania mjini Bujumbura.

Kwa kawaida maeneo haya ya maziwa makuu, unapokaribia uchaguzi, visa vya kurusha mabomu ya aina hii hujitokeza hasa Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Inasemekanan mitaa ya Bujumbura jana ilikuwa na watu wachache sana.

Huwa siwaelewi watu wanaosubiri kwenye matukio kama haya kuanzisha vurugu ambazo hazina tija

Monday 28 June 2010

Mbinu nyingine Kwenye Ajira ya Watoto

Kumekuwa na ongezeko la ajira kwa watoto duniani.
Jitihada za kutokomeza tatizo hii inaelekea bado haijapata mafanikio makubwa.

Umuhimu wa kupiga vita ajira kwa watoto ni kwamba inawasaidia kupata muda wa kujifunza na kuweza kuwa wazalishaji mali hapo watakapokuwa wanajitegemea. Kuwakatishia fursa hii ni kuwanyima haki ya kimsingi katika maisha yao ya baadaye, na pia huchangia kuwaharibia fursa na utashi wao katika kupanga maisha yao ya baadaye.

Kwa sasa kuna aina nyingine ya ajira kwa watoto, watu wengi wameishaiona lakini labda hawajaitilia maananani au hawajatambua kwamba ni janja ya watu kuwatumia watoto katika ajira zisizo rasmi.

Jana wakati naenda na kutoka madhabahuni, nikiwa kwenye usafiri, niliona mama aliyekuwa na watoto mapacha wenye umri kama wa miezi 3 ambao walionekana kuwa na afya njema, na wakiwa wamevaa vyema. Tatizo lilikuwa ni kwamba alikuwa amewalaza pembeni ya barabara ya waenda kwa miguu chini ya kivuli kiduchu, na kwa sasa ni msimu wa kiangazi, kwa hiyo vumbi lilikuwa ni kali mno likiwatimkia hao vichanga. Toka saa 3 asubuhi nilipopita kwa mara ya kwanza na saa 6 adhuhuri nilipokuwa nikirudi walikuwa wameanikwa chini!

Sababu kubwa ya kuwaanika watoto hao hivyo ilikuwa ni kupiga mizinga (kuomba) kwa wapita njia waliokuwa wakielekea na kutoka kanisani.

Kwangu mimi naona ni sehemu ya ajira kwa watoto, kwani ni mara nyingi utakuta akina babu na bibi wakitembea mitaani na watoto wadogo na kuwashindisha njaa, na kuwaacha watoto hao wakiwa wachafu na kuchakaa kabisa kwa makusudi ili kiwe chambo cha kupewa misaada.

Ninawachukulia wanaofanya hivi kuwa ni wachoyo na wasio na huruma hata chembe. Wanapaswa kuelimishwa, na kama wanajifanya sugu, ni vizuri wachukuliwe hatua kama wale ambao huwaajiri watoto kufanya kazi.

Sunday 27 June 2010

I Got It Right! Ghana are in Quarter Final

Yesterday I predicted that Ghana fans and African fans in general will enjoy this weekend by seeing Ghana seeding a place to quarter final of FIFA 2010 World cup in South Africa.

Indeed they managed to cross over by beating USA 2 - 1, but it was not an easy task, as Americans as opponents were too strong to be beaten. Probably Americans should blame themselves by taking longer time to study Ghana's game and ended by finding themselves behind by a goal scored just in 5 minutes by Prince Boateng. The secong goal was scored early on extra time by Asamoah Gyan.

Both goals from Ghanaian side were fantastic.

The next game, Ghana will face Uruguay, that match will be tough, but I am optimistic to see a new record where for the first time African team will qualify for Semi-final.

Cheers Black Stars. Many fans are cheering you especially from Africa.

Photo: From BBC

Friday 25 June 2010

Furahia wikiendi na Ushindi wa Ghana


Nawatakia wikiendi njema na furaha tele kwa kuiombea Ghana ishinde mechi ya kesho dhidi ya Marekani katika uwanja wa Royal Bafokeng (Pichani juu).
Afrika hatuna chaguo lingione zaidi ya Ghana.
Nina imani tutatoka na kicheko he he heeee.

Thursday 24 June 2010

Italy Stormed Out of World Cup 2010 Competitions

Bad day for Giants reigning world champions, the Italian team, as they are wiped out of world cup 2010 tournament. They were knocked out by Slovakia by 3 -2 goals.

They got out of competition with 2 points only. Good memmories they had 4 years ago had just faded like a thin smoke in air.

This 2010 world cup had come with many surprises. Many Giant teams had really struggled to qualify for the next stage, African teams have done badly, and South American teams have shined out.

Italy has to be restructured and get ready for 2014 world cup in Brazil. With the current team they will not reach far.

Who is to be blamed......... Jabulani ball! or ....

Italians fans are very much disappointed (including their African fans)

Tuesday 22 June 2010

Who is More Strategic and Cleverer


Among these "beggars", who will you opt to assist the daily bread?
Must be the one who is most clever!
Enjoy your day

Monday 21 June 2010

Je, Wajua Haya?

Nafikiri wafahamu ya kuwa watu wengi duniani wanatumia zaidi mkono wa kulia kwa shughuli mbalimbali kuliko wa kushoto.

Je unajua ya kuwa watu wengi hupenda kubeba mikoba au mabegi yao katika bega la kushoto?

Na je wajua ya kuwa watu wanapokaa mahali na kusikiliza kitu kwa makini au kuwa katika mawazo fulani, huwa kichwa hakikai wima, yaani hupindisha kidogo shingo yao upande mmojawapo?

Je unajua ni kwa sababu gani?

Kama hujui nakupa mwaka mzima wa kutafakari, mie nitatoa jibu tarehe na mwezi kama wa leo, siku ya Jumanne mwaka kesho.

Nakutakia jumatatu njema

Thursday 17 June 2010

Somalia: Watching World cup means Death Penalty!

Watching 2010 FIFA world cup in Somalia means you are liable to death penalty!

Last saturday in Mogadishu, 2 people were killed while watching world cup. They were stormed by militants people and gunned down.

It is said extremist groups they think world cup will pre-occupy people's minds and they will fail to assist radical groups to overthrow the goverment, which after all is weak government.

read here

Hii ni ajabu kabisa kwa watu kuwa na msimamo wa namna hii, itakumbukwa miezi michache iliyopita, kundi la al-shabbaab lilipiga marufuku vituo vyote vya radio Mogadishu kupiga muziki wa aina yoyote katika matangazo yao, ilibidi baadhi ya vituo kuweka milio ya wanyama na risasi kabla ya kutangaza habari kama kionjo.

Sasa na kitendo cha kuua watu watakaoangalia kome la dunia 2010 ni ukatili kama sio kuchanganyikiwa.

Tuesday 15 June 2010

American Lawyer Denied Bail in Rwanda

Prof.Peter Erlinder (in pink prisoner dress) who was arrested in Kigali, Rwanda and charged for genocidal denial through his speeches and publications, has been denied bail out as he requested to be considered in huanitarian grounds, where he is intending to travel to USA for appropriate treatment to his ill/risky healthy conditions as he brought papers showing that he was diagnosed to have brain, skin and heart problems which may turn into cancer.
Read more information in English here

Inadaiwa Mmarekani huyu ambaye pia ni mwanasheria na pia ni profesa, alipoingia Rwanda alikuwa anapinga uwepo wa mauaji ya Kimbari - Rwanda, kimsingi kukana mauaji hayo hapa Rwanda ni kosa la jinai, na ikithibitishwa una imani hiyo, unachukuliwa kama mtu ambaye unachochea mauaji kama hayo na adhabu yake ni kali.

Mzungu huyu anadai alipimwa Marekani na kugundulika ana uvimbe kwenye ubongo, pia ana matatizo ya moyo na ngozi ambayo yanaweza kumsababishia kupata saratani ambayo hata hivyo haikufafanuliwa. Mahakama pia iliambiwa ya kuwa alikuwa kwenye harakati za kuandika historia mpya ya mauaji ya kimbari ya 1994, na kudaiwa kuwa alikuwa anataka kupotosha ukweli wa mauaji hayo.

Mtuhumiwa huyu pia anadai anapata mateso ya kulala ndani ya selo kwa sababu ya kelele za mbu, hivyo analazimika kuweka karatasi ya chooni (toilet paper) masikioni kuziba ili asisikie kelele za mbu!, maana yake kuwa chandarua hakitoshi, bali anataka mbu nao wanyamaze :-)

Hivyo, aliomba aachiwe kwa dhamani ki-ubinadamu ili aende Marekani akapate matibabu sahihi! Nami nafikiri pia aepuke kelele za vuvuzela za mbu wa Rwanda.

Wiki hii shauri lake litasikilizwa tena ili kama atastahili kupewa dhamana.

Sunday 13 June 2010

Jabulani Ball: Will Be Remembered in World Cup


Today is the third day of the FIFA 2010 World Cup.

Up to this time, we have witnessed 7 fixtures producing 3 ties and 4 wins.

England will not forget the moment when the jabulani ball slipped off the hand of goalie Green and help USA to equalise.
Other teams that will not forget the jabulani includes Algeria when one of Algeria player was sent off after turning the jabulani into handball rather than football game. Eventually Algeria was overpowered and lost the game to Slovenia.

Serbia also suffered a defeat by Ghana through a penaly kick following a hand jabulani by a serbian player.

We expect much surprises in this year FIFA/Coca Cola World Cup 2010 in South Africa.

Friday 11 June 2010

World Cup In Africa

It is half time for the FIFA 2010 World cup between South Africa and Mexico. Score is 0-0

Many people are nervous, of course including my self for many reasons

The world cup is played for the first time in Africa

Host country South Africa,

I live in Africa

I am an African

I was born in Africa
I grew up in Africa
I have spent much of my life time in Africa
I have visited South Africa before, and now I feel as I am South African.
All the best for South Africa

Wednesday 9 June 2010

Rwanda Kuanza kutumia Bangi katika Matibabu. (Rwanda to Use Marijuana for Treatment Purposes)

The Rwanda Ministry of Health has forwarded a bill to parliament that seeks to legalize the use of marijuana and other narcotics to be used strictly for medical purposes.

The minister, Dr. Richard Sezibera promised MPs that: “The medicine will thus be available and correctly utilised" as pain relievers, especially in treating the problems related to the behavioural problems.
Members of Parliament unanimously endorsed the bill without any objection

Huo ndio ukweli, Bangi imeidhinishwa kutumika kwa shughuli za matibabu hasa ya kutuliza maumivu kwa watu walioshindikana kitabia, na sio kwa ajili nyingine yeyote.

Hapa nawakumbuka ndugu zangu wa Iringa ambao hula bangi kama mboga ya majani ya kawaida, lakini sihusishi ulaji wa bangi hii na tabia ya kujinyonga..... :-(

Na pia nawakumbuka ndugu zetu wa Mara ambao ni maarufu kwa kulima bangi, ila sijui wao huwa wanaitumia kwa shughuli gani, ingawa na ukanda huo kwa kupenda kuuana kwa sababu za ki.#*.. :-((

Tanzania: Ranked High Among Peaceful Countries in Africa

Tanzania, the Mwalimu Nyerere's motherland has been ranked 8th most peaceful country in Africa by Global Peace Index (GPI) released yesterday 8th June 2010. Botswana, Tunisia and Mozambique are the top for African countries.

The GPI designers define peace as the absence of violence, with the survey looking at several qualitative and quantitative indicators of external and internal measures to maintain peace.
These include a country’s crime rates, political instability, and level of organised crime besides external measures like a country’s relations with its neighbours.

The new ranks has New Zealand as the most peaceful country in the world, while Iceland and Japan holds 2nd and 3rd places.

On the bottom there is Afghanistan which is trailed by Somalia and Iraq. Somalia is the worst peaceful country in Africa while Iraq is the worst overall in the world.

Tuesday 8 June 2010

RwandAir Roars


Photo and Source: New times

Rwandair, a company which was established in 2002 is striving hard to achieve great successes in air transport industry.

Recently had acquire a new Boeing 737-500 which has a capacity of taking 110 on board including crews.

They expect to get another similar aircraft by August this year. And yet... they have secured a loan which will enable them to buy 2 more Boeing 737-800 series towards the end of next year.

They want to compete on the west Africa market which now is dominated by Kenya airways and Ethiopian airlines. Also they are planning to establish daily flights to Johanesburg.

It should be remembered that late last year, RwandAir, acquired its first fleet of two CRJ200s aircrafts, By which they manage to establish direct flights from Kigali to Dar-es Salaam which has better services if you compare with many aged airliners in the region.

Mimi nachukulia maendeleo ya Rwandair kama ni changamoto kwa nchi nyingine, wajue penye nia pana njia. Na hakuna kisichowezekana.

Congrats RwandAir express.

Monday 7 June 2010

Mixed Weekend for Tanzania Football Teams

Taifa Stars (Tanzania) with blue jersey, they lost 1 - 0 to Amavubi stars (Rwanda) on the final game for CHAN finals qualifications.
Taifa stars outshined Rwanda, however they bowed to Rwanda through surprise shot in the first half which secure Rwanda place in CHAN finals. This goal left Tanzanian's goalie puzzled.

It was painful moment when the final whistle blown.
Tanzania is expecting to play Brazil on 7th June 2010 at Dar es Salaam, just a day after this match with Rwanda.

On the other side, this weekend has been good for the Tanzanian women national football team (Twiga Stars) when they secure their place for African Football championship finals which will be done shortly after the world cup in South Africa. They won by aggregate of 11 - 4.

Also within this weekend, The Copa Coca-Cola cup, Tanzania's under 17's team won 11- 0 against Malawi.

We wish all the best for Tanzanian Football team to beat Brazil in less than 24 hours from now.

Friday 4 June 2010

Enjoy your Weekend

I just want to wish you all of you a nice weekend.

I am gathering energy to cheer Taifa Stars during their return match with Amavubi Stars for the CHAN qualification.

The match will be held here in Kigali, Rwanda on Sunday 6th June 2010.

Every one is talking about this match here....

Cheers

Kudhibiti Uhalifu: Tanzania Yapaswa Kujifunza Kutoka Kwa Rwanda

Tukio la hivi karibuni la watu kuchoma moto kituo cha polisi huko Mkoani Kilimanjaro ni la kusikitisha sana, ukipenda waweza kuliita la kuudhi sana.

Sababu kubwa ya uchomaji wa kituo hicho cha polisi kwangu mimi siielewi, kwani taarifa zinajikanganya.

Kituoni humo walikuwepo watuhumiwa waliokuwa wanadaiwa kumteka na kumuua mtoto kwa shughuli za kafara, lakini kimsingi tuhuma hizo hazikuwa sahihi, kwani mtoto alipatikana siku iliyofuata akiwa Moshi, tena mzima na buheri wa afya!

Tukio ambalo ni la aibu, ni kuona kuwa polisi wa Tanzania hawako au hawakuwekwa katika mazingara ya kuwa imara kuweza kudhibiti wahalifu wawapo vituoni mwa polisi, kwani vituo vingi ni majengo tu, na polisi wenyewe mbali ya kuwa ni waoga, lakini pia hawana vifaa vya kujilinda kwa matukio ya uvamizi kama huo.

Lakini pia mfumo wa nchi yetu umelitelekeza jeshi la polisi wakati matukio ya uhalifu ni mengi.

Kwa mtizamo wangu ningeishauri serikali yetu kuweza kuiga mfano wa Rwanda, ambao hulitumia jeshi la wananchi wa Rwanda kushiriki katika ulinzi wa mali na usalama wa watu sehemu mbalimbali hasa nyakati za usiku, ambapo hufanya doria wakiwa wana silaha za moto za kujilinda dhidi ya waalifu na waleta vurugu.

Utakuta wanazunguka mitaani usiku, tena kwa mpango maalumu ambapo hata ukiwashambulia, huwezi kuwapata wote kwani hawaendi kiholela kama kuku. Na wanapita sehemu zote zenye mikusanyiko ya watu kama sehemu za starehe, supermarkets, makazi ya watu, hospitali kubwa na maeneo ya masoko.

Kwa Tanzania, mbali ya kuwa polisi hawatoshelezi maeneo yote, lakini jeshi hilo limeachiwa pekee jukumu la kuangalia usalama wa ndani ya nchi, ikiwa ni pamoja na kudhibiti watekaji wa magari wakati wa usiku kwenye mapori, na wakati huo huo jeshi la wananchi wapo majumbani wamelala, na hivyo kuwapa fursa kwa baadhi yao kushiriki katika uhalifu, au kupiga wananchi bila sababu za msingi.

Tunapaswa kuondoa dhana ya kuwa wanajeshi kazi yao ni kwenye vita tu, bali katika kipindi hiki cha "utulivu kwa jina" watumike katika kudhibiti matukio ya uhalifu hasa maeneo ya mipakani sehemu za Kigoma na Kagera ambako wezi hutoka nchi za jirani wakiwa na silaha nyingine za kivita na kuendesha uhalifu kwetu, na pia mijini maeneo ambayo yamekithiri kwa visa vya uporaji na kushambulia wananchi.
Kwa mantiki hii kutasaidia kuongeza amani na usalama, na pia wanajeshi watapata heshima na hadhi kwa kutimiza madhumuni ya kulinda wananchi na mali zao.

Nina hakika hili linawezekana

Tuesday 1 June 2010

Just at Your Glance

Part of spectrum of the vitreo-retinal surgeons (Members of Europen Vitreo-retinal surgeons Society) from all over the world when they met sometimes last year for refreshing course in Germany.

A lot of innovations were just at the finger tips of colleagues.

South Africa was lucky, to have 5 out of 7 Africans who participated in this refreshing course in the field of Ophthalmology. Tanzania and Zimbabwe were the other two countries represented.

Sounds difficult terminologies, this shows how complex this field is......

I always smile, no matter ......